Thursday, September 20, 2018

WAZAZI WAASWA KUWALEA WATOTO KATIKA MAADILI MEMA, KUWAEPUSHA NA DAWA ZAKULEVYA, MAAMBUKIZI YA VVU

Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera ,Bunge Kazi,Vijana ,Ajira na Walemavu  Mhe. Anthony Mavunde ametoa wito kwa  Wazazi nchini  kuwalea watoto wao  katika maadili mema ili kuwaepusha na  matumizi ya dawa za kulevya na Maambukizi ya   Virusi Vya Ukimwi.


Ushauri huo ameutoa  wakati akifungua makambi ya siku saba ya Kanisa la Waadventisa Wasabato mkoani SIMIYU, katika Uwanja wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi.

Mavunde amesema malezi ya watoto ni jambo muhimu sana hasa katika kizazi cha hivyo watoto wakikosa malezi bora katika umri walio nao ni rahisi kutumbukia katika makundi yasiyofaa yakiwemo ya matumizi ya dawa za kulevya na hivyo kukosa nguvu kazi ya Taifa.

“Kwa mujibu wa takwimu Tanzani kila siku watu 200 wanapat maambukizi mapya ya VVU katika watu 200 watu 80 ni vijana katika hao vijana 80 asilimia 80 ni watoto wa kike, hivyo tuendelee kuelemisha  na kuliandaa hili kundi kubwa la Vijana katika malezi bora ili wawe nguvu kazi ya kuleta tija katika Taifa letu” alisema.

Ameongeza kuwa ili watu waweze kuondokana na umaskini ni lazima wafanye kazi hivyo akatoa wito kwa Viongozi, waumini wa Kanisa la Waadventisa Wasabato na wananchi wote kufanya kazi kwa staha, uadilifu na malengo ili waweze kufanikiwa kiuchumi.

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka amesema makambi hayo ni sehemu ya Maandalizi ya Mkutano mkubwa wa Chama cha Wanataaluma na Wajasiriamali Waadventista Wasabato (ATAPE) unatarajiwa kufanyika mwaka 2019 mkoani humo.

Aidha, Mtaka alitumia fursa hiyo kuwaeleza wananchi kuwa mwaka 2019 kutakuwa na matukio makubwa matatu ambayo yataitambulisha Simiyu ambayo ni mkutano huo wa ATAPE, Mkutano wa Madaktari wa Nchi nzima na Maonesho ya Nanenane ya Kimataifa.

Katika hatua nyingine amewahimiza wananchi kujifunza masuala ya Ujasiriamali na kuwakaribisha katika Maonesho ya Viwanda Vidogo SIDO yatakayofanyika Kitaifa mwaka huu 2018 kuanzia tarehe 24 hadi 28 Oktoba, 2018 katika Viwanja vya Nyakabindi.

Awali akitoa somo kuhusu masuala ya Ujasiriamali, Mchungaji Joshua Njuguna aliwasisitiza waumini wote kuwa siyo mpango wa Mungu mtu yeyote awe maskini , akawaasa kufanya kazi ili kuutafuta utajiri  hivyo akawataka wazitafute fursa za kupata utajiri  na kufanya kazi kwa bidii.

Pia Naibu Waziri MAVUNDE  ameahidi kuchangia jumla ya mifuko 100 ya saruji kwa ajili ya kuwaunga mkono WAUMINI HAO katika  ujenzi wa Hospitali ya Kanisa  katika eneo la Pasiasi jijini Mwanza.

Ufunguzi wa makambi umehudhuriwa na waumini mbalimbali kutoka mikoa mbalimbali hapa nchini, lengo likiwa ni kujifunza neno la Mungu, kutoa elimu ya ujasiriamali, mafunzo ya ndoa na malezi ya watoto na  kuliombea Taifa. 
MWISHO

Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera ,Bunge Kazi,Vijana ,Ajira na Walemavu  Mhe. Anthony Mavunde(mwenye miwani), Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka wakikagua gwaride la Vijana Kanisa la Waadventista Wasabato katika ufunguzi wa makambi Mjini Bariadi, Septemba 18, 2018.
Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera ,Bunge Kazi,Vijana, Ajira na Walemavu  Mhe. Anthony Mavunde akivisha skafu na  Vijana Kanisa la Waadventista Wasabato kabla ya ufunguzi wa makambi Mjini Bariadi, Septemba 18, 2018 ambao alikuwa mgeni rasmi.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka(mwenye skafu kulia)  akiimba pamoja na  Waimbaji wa Kwaya ya Kanisa la Waadventista Wasabato(SDA) Kurasini, katika ufunguzi wa makambi ya Kanisa hilo yanayofanyika Mjini Bariadi, Septemba 18, 2018 .
Baadhi ya waumini wa Kanisa la Waadventista Wasabato(SDA) wakifuatilia hotuba ya Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera ,Bunge Kazi,Vijana ,Ajira na Walemavu  Mhe. Anthony Mavunde katika ufunguzi wa makambi yanayofanyika  Mjini Bariadi, Septemba 18, 2018
Waimbaji wa Kwaya ya Kanisa la Waadventista Wasabato(SDA) wakiimba katika ufunguzi wa makambi ya Kanisa hilo yanayofanyika  Mjini Bariadi, Septemba 18, 2018.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka (wa pili kushoto) Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera ,Bunge Kazi,Vijana ,Ajira na Walemavu  Mhe. Anthony Mavunde(wa tatu kilia) na viongozi wengine wa Serikali na Kanisa la Waadventista Wasabato(SDA), wakifuatilia mafundisho katika ufunguzi wa makambi ya Kanisa hilo Septemba 18, 2018 ambayo yanafanyika  Mjini Bariadi
Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera ,Bunge Kazi,Vijana ,Ajira na Walemavu  Mhe. Anthony Mavunde akizungumza na Viongozi na waumini wa Kanisa la Waadventista Wasabato(SDA), wakati akifungua makambi ya Kanisa hilo Septemba 18, 2018 ambayo yanafanyika  Mjini Bariadi.

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka akizungumza na Viongozi na waumini wa Kanisa la Waadventista Wasabato(SDA), katika ufunguzi wa makambi ya Kanisa hilo Septemba 18, 2018 ambayo yanafanyika  Mjini Bariadi.
Mchungaji wa Kanisa la Waadiventista Wasabato kutoka Nchini Kenya Joshua Njuguna Kenya akitoa mafundisho, katika ufunguzi wa makambi ya Kanisa hilo Septemba 18, 2018 ambayo yanafanyika  Mjini Bariadi.
Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera ,Bunge Kazi,Vijana ,Ajira na Walemavu  Mhe. Anthony Mavunde (mwenye miwani) akipokea zawadi kutoka kwa wawakilishi wa wakina mama wa Kanisa la Waadventista Wasabato(SDA), katika ufunguzi wa makambi ya Kanisa hilo Septemba 18, 2018 ambayo yanafanyika  Mjini Bariadi.
Mkuu wa Wilaya ya Maswa, Mhe. Dkt. Seif Shekalaghe akipokea zawadi kutoka kwa wawakilishi wa wakina mama wa Kanisa la Waadventista Wasabato(SDA), katika ufunguzi wa makambi ya Kanisa hilo Septemba 18, 2018 ambayo yanafanyika  Mjini Bariadi.
Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga akipokea zawadi kutoka kwa wawakilishi wa wakina mama wa Kanisa la Waadventista Wasabato(SDA), katika ufunguzi wa makambi ya Kanisa hilo Septemba 18, 2018 ambayo yanafanyika  Mjini Bariadi

Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera ,Bunge Kazi,Vijana ,Ajira na Walemavu  Mhe. Anthony Mavunde( wa pili kushoto ) akisalimiana na mmoja wa Viongozi wa ATAPE mkoa wa Simiyu, Eng. Paul Jidayi mara tu alipowasili Uwanja wa Halmashauri ya Mji Bariadi kufungua makambi ya Kanisa la Waadiventista Wasabato(SDA) , Septemba 18, 2018.


0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!