Friday, May 31, 2019

RC MTAKA AWAHAKIKISHIA USHIRIKIANO WA SERIKALI WAUMINI, VIONGOZI WA MADHEHEBU YA DINI

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka amewahakikishia waumini na viongozi wa madhehebu ya dini mkoani hapa kuwa viongozi wa serikali wako pamoja nao na wataendelea kushirikiana na kila watakapo wahitaji .

Mtaka ameyasema hayo jana Mei 30, 2019 katika futari aliyoiandaa kwa waumini na viongozi wa madhehebu ya Kiislam katika Viwanja vya Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mjini Bariadi.

“Ndugu zangu waislam mliopo hapa naomba muamini kabisa kwamba viongozi wa mkoa na viongozi wote wa Serikali kwenye maeneo yetu  ndani ya mkoa wa Simiyu wako pamoja na ninyi; kwa jambo lolote, eneo lolote ambalo mngehitaji ushirikiano kwenye mkoa wetu sisi tuko tayari kuunga mkono” alisema Mtaka.

Aidha, ameshauri viongozi wa BAKWATA Mkoa wa Simiyu kuomba kuandaa tukio moja kubwa la Kitaifa kufanyika Mkoani Simiyu kama ambavyo yamekuwa yakifanyika katika mikoa mingine na akaahidi kushirikiana na viongozi hao endapo watakuwa tayari kuandaa tukio lolote.

Katika hatua nyingine Mtaka ametoa wito pia kwa viongozi wa Madhehebu ya Kiislam kutengeneza mazingira mazuri kwa vijana na kuwafundisha ikiwa ni njia moja wapo ya kuwaandaa kushiriki katika mashindano ya kuhifadhi Quran ili Mkoa wa Simiyu na nchi kwa ujumla iweze kuwakilishwa vema katika mashindano hayo.

Sambamba na hilo amewashukuru viongozi wa dini kwa kuendelea kuiombea nchi, viongozi wake, kuombea amani, umoja na mshikamano miongoni mwa Watanzania ambapo amebainisha kuwa Serikali inatambua mchango wa Taasisi za dini katika nchi na kwa namna viongozi wa dini wanavyoshirikiana na Serikali katika masuala na mtukio mbalimbali.

Kwa upande wake Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mahamoud Kalokola amemshukuru Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka kwa namna anavyoenzi waislam na akatoa wito kwa watu wengine kuiga mfano wake kwa kuwa kila anyefanya hivyo anapata thawabu yake kwa Mwenyezi Mungu.

Ameongeza kuwa tendo hilo la kufuturisha linawakusanya watu pamoja walio waislam na wasio waislam jambo ambalo linadumisha umoja, upendo, ushirikiano na mshikamano kwa wote bila kujali tofauti ya dini zao.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga amempongeza Mkuu wa mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka ambao nao watajipanga kufanya jambo hili ili nao waweze kupata baraka za Mwenyezi Mungu.

Huu umekuwa ni utaratibu kwa Mkuu wa mkoa wa Simiyu, kuandaa furati kwa waumini viongozi wa madhehebu ya dini ya Kiisla, ambayo pia huwahusisha viongozi wengine wa chama na Serikali wakati wa mfungo wa mwezi Mtukufu wa Ramadhani.
MWISHO




Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka (kushoto) akiteta jambo na Sheikh wa Mkoa wa Simiyu, Mahamoud Kalokola  mara baada ya futari iliyoandaliwa kwa ajili ya waumini wa madhehebu ya Kiislam na viongozi wengine jana Mei 30, 2019.

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka akizungumza na waumini wa madhehebu ya Kiislam na viongozi mbalimbali walioshiriki katika futari aliyoindaa Mei 30, 2019.
Baadhi ya waumini wa madhehebu ya Kiislam na viongozi mbalimbali walioshiriki katika futari aliyoandaliwa  na Mkuu wa mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka kwa ajili yao, Mei 30, 2019.
Baadhi ya waumini wa madhehebu ya Kiislam na viongozi mbalimbali walioshiriki katika futari aliyoandaliwa  na Mkuu wa mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka kwa ajili yao, Mei 30, 2019.
Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga akizungumza na waumini wa madhehebu ya Kiislam na viongozi mbalimbali walioshiriki katika futari aliyoindaa kwa ajili yao, Mkuu wa mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka kwa ajili ya waumini wa madhehebu ya Kiislam na viongozi wengine jana Mei 30, 2019.
Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bw. Jumanne Sagini (kulia) akiteta jambo na Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga baada ya futari aliyoandaliwa  na Mkuu wa mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka kwa ajili ya waumini wa madhehebu ya Kiislam na viongozi wengine jana Mei 30, 2019.
Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bw. Jumanne Sagini akizungumza na waumini wa madhehebu ya Kiislam na viongozi mbalimbali walioshiriki katika futari aliyoindaa kwa ajili yao, Mkuu wa mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka kwa ajili ya waumini wa madhehebu ya Kiislam na viongozi wengine jana Mei 30, 2019.
Baadhi ya waumini wa madhehebu ya Kiislam na viongozi wa Chama na Serikali wakishiriki futari iliyoandaliwa kwa ajili ya na Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka jana Mei 30, 2019.
Baadhi ya waumini wa madhehebu ya Kiislam na viongozi wa Chama na Serikali wakishiriki futari iliyoandaliwa kwa ajili ya na Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka jana Mei 30, 2019.
Mwakilishi wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Simiyu akizungumza na waumini wa madhehebu ya Kiislam na viongozi mbalimbali walioshiriki katika futari aliyoindaa kwa ajili yao, Mkuu wa mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka kwa ajili ya waumini wa madhehebu ya Kiislam na viongozi wengine jana Mei 30, 2019.

0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!