Thursday, October 31, 2019

NAIBU WAZIRI IKUPA APONGEZA UBUNIFU WA KAMBI ZA KITAALUMA SIMIYU


Na Stella Kalinga, Simiyu RS
Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, anayeshughulikia masuala ya watu wenye ulemavu, Mhe. Stella Ikupa, amefunga rasmi kambi ya kitaaluma kwa wanafunzi wa kidato cha nne Mkoani Simiyu, ambapo amewapongeza viongozi wa mkoa wakiongozwa na Mkuu wa Mkoa huo, Mhe. Anthony Mtaka kwa ubunifu huo ambao utawasaidia wanafunzi hao kufanya vizuri katika mitihani yao.

Naibu Waziri Ikupa ameyasema hayo Oktoba 30, 2019 wakati wa kuhitimisha kambi ya kitaaluma ya wanafunzi wa kidato cha nne ambayo imefanyika kwa muda wa siku 60 katika Shule ya sekondari Simiyu na Chuo cha Ualimu Bariadi Mjini Bariadi, kwa lengo la kuwaandaa na mtihani wa Taifa unaotarajia kufanyika kuanzia Novemba 04, 2014.

“Nampongeza Mkuu wa Mkoa kwa ubunifu mkubwa wa kuandaa kambi hizi kwani, naamini wanafunzi mmejifunza mambo mengi  na mtafanya vizuri katika mtihani wenu, ningeshauri watu  wengine waige jambo hili, niwakumbushe wanafunzi mtakaoanza mtihani wenu Novemba 4, 2019, kumuomba Mungu ili awaongoze kipindi chote cha mitihani,” alisema Ikupa.

 Aidha, Ikupa amesema Serikali imeendelea kuboresha sekta ya elimu nchi kwa kuongeza bajeti katika shule, kujenga madarasa, na anaamini kuwa itaendelea kutatua changamoto ya walimu  katika mkoa wa Simiyu, na nchini kwa ujumla.       

Mkuu wa Mkoa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka amesema uongozi wa Mkoa, walimu, wazazi na wadau wote wa elimu mkoani humo wamefanya uwekezaji mkubwa kwa wanafunzi wote waliokuwa katika kambi za kitaaluma na kupitia kazi nzuri iliyofanywa na walimu anaamini kwamba watafanya vizuri katika mtihani wa Taifa utakaoanza  Novemba 4, 2019. 

 Ameongeza Serikali mkoani Simiyu itaendelea kuwapa motisha walimu, wanafunzi na shule  zote zitakazofanya vizuri katika mitihani ya Kitaifa, huku akiahidi kuwalinda walimu wote, ambapo ameahidi  kuwa kuanzia Desemba Mosi, 2019 viongozi wa mkoa watawatembelea walimu katika Halmashauri zote na kuzungumza nao.

Mkurugenzi wa Idara ya Habari- MAELEZO na Msemaji Mkuu wa Serikali, Dkt. Hassan Abbas amewaomba wadau kuendelea kuunga mkono kambi hizi ili waweze kutimiza ndoto zao huku akibainisha kuwa kupitia kambi hizo watapatikana viongozi mahiri wa baadaye.

Katibu Mkuu, Chama cha Walimu Tanzania, Deus Seif amesema walimu wana imani na Serikali na wameamua kufanya kazi yao kwa bidii na wanaiomba Serikali kuendelea kushughulikia changamoto mbalimbali zinazowakabili ikiwemo kupandishwa madaraja na mishahara kwa wakati na malipo ya fedha za likizo na malimbikizo ya mishahara.

Naye Afisa Elimu wa Mkoa, Mwl. Ernest Hinju amesema tangu kambi hizi zianze mwaka 2016 zimesaidia kuongeza kiwango cha  ufaulu katika matokeo ya darasa la saba, kidato cha nne na kidato cha sita, ambapo kwa kidato cha nne  mwaka 2017 ufaulu ulikuwa 70.68% na mwaka 2019, ufaulu umekuwa 86.46%.                

Naye Diana Boniphace mwanafunzi kutoka Shule ya sekondari Kidinda amesema, “kupitia kambi hii wanafunzi tumejifunza mambo mengi kupitia kwa walimu mahiri na kiwango cha ufaulu kimeongezeka tofauti na tulivyoingia hivyo tunaahidi kuwa tutafanya vizuri katika mtihani wa Taifa tutakaoanza Novemba 04, 2019.”

Kambi ya Kitaaluma iliyohitimishwa Oktoba 30, 2019 ilihusisha wanafunzi 1512 ambao walikuwa na ufaulu hafifu(daraja sifuri), wanafunzi waliofanya vizuri katika mtihani wa Mkoa(Mock) na wanafunzi kutoka shule  zenye wanafunzi chini ya 30 na wamekaa kambini siku 60.
MWISHO

Baadhi ya wanafunzi wa kidato cha nne Mkoani Simiyu wakiwa katika picha ya pamoja na Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, anayeshughulikia masuala ya watu wenye ulemavu, Mhe. Stella Ikupa, mara baada ya kambi ya kitaaluma ya siku 60 kwa wanafunzi hao kuhitimishwa Oktoba 30, 2019 Mjini Bariadi.
\
Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, anayeshughulikia masuala ya watu wenye ulemavu, Mhe. Stella Ikupa, akizungumza na walimu pamoja na wanafunzi wa kidato cha nne mkoani Simiyu, wakati wa kufunga  kambi ya kitaaluma ya siku 60 Oktoba 30, 2019 Mjini Bariadi.
Baadhi ya wanafunzi wa Kidato cha nne kutoka shule mbalimbali mkoani Simiyu, wakimsikiliza Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, anayeshughulikia masuala ya watu wenye ulemavu, Mhe. Stella Ikupa, wakati wa kufunga  kambi yao ya kitaaluma ya siku 60 Oktoba 30, 2019 Mjini Bariadi.
Kutoka kulia Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, anayeshughulikia masuala ya watu wenye ulemavu, Mhe. Stella Ikupa,Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka, Katibu Tawala Mkoa, Bw. Jumanne Sagini, Afisa Elimu Mkoa, Ernest Hinju na Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga wakifurahia jambo, wakati wa kufunga  kambi ya kitaaluma ya siku 60 kwa wanafunzi wa kidato cha nne Oktoba 30, 2019 Mjini Bariadi.
Baadhi ya wanafunzi wa kidato cha nne Mkoani Simiyu wakishangilia jambo wakati wa hafla ya kufunga kambi ya kitaaluma ya siku 60 kwa wananfunzi wao ambayo imehitimishwa na Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, anayeshughulikia masuala ya watu wenye ulemavu, Mhe. Stella Ikupa, Oktoba 30, 2019 Mjini Bariadi.

Baadhi ya wanafunzi Kidato cha nne kutoka shule mbalimbali mkoani Simiyu wakicheza na kufurahi na Mkuu wa Mkoa huo, Mhe. Anthony Mtaka mara baada ya kufunga  kambi ya kitaaluma ya siku 60 Oktoba 30, 2019 Mjini Bariadi.
Baadhi ya viongozi wakifuatilia kitu wakati wa kufunga kambi ya kitaaluma ya siku 60 kwa wanafunzi wa kidato cha nne Oktoba 30, 2019 Mjini Bariadi , kutoka kulia walioketi mbele, Msemaji Mkuu wa Serikali, Dkt Hassan Abbas, Katibu wa CWT Taifa, Mwl. Deus Seif na Mbunge la Afrika Mashariki, Mhe. Happyness Lugiko.

Baadhi ya walimu mahiri  waliofundisha kambi ya kitaaluma ya kidato cha nne wakishangilia jambo wakati wa hafla ya kufunga kambi ya kitaaluma ya siku 60 kwa wanafunzi wao ambayo imehitimishwa na Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, anayeshughulikia masuala ya watu wenye ulemavu, Mhe. Stella Ikupa, Oktoba 30, 2019 Mjini Bariadi.
Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Simiyu, Mhe. Enock Yakobo akitoa salamu za Chama,  wakati wa hafla ya kufunga kambi ya kitaaluma ya siku 60 kwa wanafunzi wao ambayo imehitimishwa na Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, anayeshughulikia masuala ya watu wenye ulemavu, Mhe. Stella Ikupa, Oktoba 30, 2019 Mjini Bariadi.
Sheikh wa Mkoa wa Simiyu, Mahamoud Kalokola akitoa dua wakati wa hafla ya kufunga kambi ya kitaaluma ya siku 60 kwa wanafunzi wao ambayo imehitimishwa na Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, anayeshughulikia masuala ya watu wenye ulemavu, Mhe. Stella Ikupa, Oktoba 30, 2019 Mjini Bariadi.
Mmoja wa wanafunzi wa kidato cha nne walio kuwa katika kambi ya kitaaluma mkoani Simiyu, ambayo imehitimishwa  Oktoba 30, 2019 Mjini Bariadi akitoa  ushuhuda wa namna kambi zilivyomsaidia kuongeza ufaulu wake mbele ya wanafunzi wenzake, walimu na viongozi mbalimbali.

Msemaji Mkuu wa Serikali, Dkt Hassan Abbas(kulia) na Katibu wa CWT Taifa, Mwl. Deus Seif wakiteta jambo wakati wa hafla ya kufunga kambi ya kitaaluma ya siku 60 kwa wanafunzi wao ambayo imehitimishwa na Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, anayeshughulikia masuala ya watu wenye ulemavu, Mhe. Stella Ikupa, Oktoba 30, 2019 Mjini Bariadi.
Baadhi ya wanafunzi wa kidato cha nne mkoani Simiyu wakimvika skafu Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, anayeshughulikia masuala ya watu wenye ulemavu, Mhe. Stella Ikupa, ambaye alikuwa Mgeni rasmi katika ufungaji wa kambi ya kitaaluma kwa wanafunzi wa kidato cha nne Oktoba 30, 2019 Mjini Bariadi.

Baadhi ya viongozi wakicheza pamoja na waimbaji wa kwaya ya walimu Bariadi, wakati wa hafla ya kufunga kambi ya kitaaluma ya siku 60 kwa wanafunzi wao ambayo imehitimishwa na Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, anayeshughulikia masuala ya watu wenye ulemavu, Mhe. Stella Ikupa, Oktoba 30, 2019 Mjini Bariadi.
Baadhi ya wanafunzi wa kidato cha nne Mkoani Simiyu wakiwa katika picha ya pamoja na Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, anayeshughulikia masuala ya watu wenye ulemavu, Mhe. Stella Ikupa, mara baada ya kambi ya kitaaluma ya siku 60 kwa wanafunzi hao kuhitimishwa Oktoba 30, 2019 Mjini Bariadi.

Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, anayeshughulikia masuala ya watu wenye ulemavu, Mhe. Stella Ikupa(wa pili kushoto) akizungumza na walimu pamoja na wanafunzi wa kidato cha nne mkoani Simiyu, wakati wa kufunga  kambi ya kitaaluma ya siku 60 Oktoba 30, 2019 Mjini Bariadi.
Mbunge la Afrika Mashariki, Mhe. Happyness Lugiko , akipokea cheti cha shukrani ya kuchangi kambi ya kitaaluma mkoani Simiyu, wakati wa hafla ya kufunga kambi ya kitaaluma ya siku 60 kwa wanafunzi wao ambayo imehitimishwa na Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, anayeshughulikia masuala ya watu wenye ulemavu, Mhe. Stella Ikupa, Oktoba 30, 2019 Mjini Bariadi.


Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka (kushoto) akiteta jambo na na Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, anayeshughulikia masuala ya watu wenye ulemavu, Mhe. Stella Ikupa, wakati wa kufunga  kambi ya kitaaluma ya siku 60 Oktoba 30, 2019 Mjini Bariadi.

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka akizungumza na walimu pamoja na wanafunzi wa kidato cha nne mkoani Simiyu, wakati wa kufunga  kambi ya kitaaluma ya siku 60 Oktoba 30, 2019 Mjini Bariadi
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka akizungumza na walimu pamoja na wanafunzi wa kidato cha nne mkoani Simiyu, wakati wa kufunga  kambi ya kitaaluma ya siku 60 Oktoba 30, 2019 Mjini Bariadi.

Kutoka Kushoto Katibu Tawala wa Mkoa, Bw. Jumanne Sagini, Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka wakimsikiliza Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, anayeshughulikia masuala ya watu wenye ulemavu, Mhe. Stella Ikupa mara baada ya kufika katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, kabla ya hafla ya kufunga kambi ya kitaaluma ya siku 60 kwa wanafunzi wa kidato cha nne ambayo imehitimishwa na Naibu Waziri huyo,  Oktoba 30, 2019 Mjini Bariadi.
Katibu wa CWT Taifa, Mwl. Deus Seif akizungumza na viongozi wa Mkoa na Simiyu na viongozi wengine, mara baada ya kufika katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, kabla ya hafla ya kufunga kambi ya kitaaluma ya siku 60 kwa wanafunzi wa kidato cha nne ambayo imehitimishwa na Naibu Waziri huyo,  Oktoba 30, 2019 Mjini Bariadi.
Baadhi ya viongozi walioshiriki katika halfa ya kufunga kambi ya kitaaluma ya siku 60 kwa wanafunzi wa kidato cha nne mkoani Simiyu wakifuatilia masuala mbalimbali katika hafla hiyo iliyofanyika Oktoba 30, 2019.



0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!