Saturday, November 30, 2019

RAS SIMIYU AZINDUA UTAFITI WA MATUMIZI YA SIMU KATIKA KUONGEZA ULIPAJI KODI ZA MAJENGO


Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bw. Jumanne Sagini amezindua rasmi utafiti unaohusu matumizi ya simu za mikononi katika kuongeza ulipaji kodi za majengo nchini Tanzania, PIERI 20355 ambao utafanyika kuanzia Novemba 28, 2019 hadi 30 Juni 2020 katika Halmashauri ya Mji wa Bariadi na Halmashauri ya Wilaya ya Busega.

Akizindua utafiti huo Novemba 28, 2019 mjini Bariadi Sagini amewataka Wakurugenzi wa Halmashauri hizo kutoa ushirikiano unaotakiwa kwa watafiti ili kuwawezesha kufanya kazi yao kwa ufanisi na kupata matokeo sahihi.

 “ Wakurugenzi katika Halmashauri ya Mji wa Bariadi na Busega, hakikisheni mnatoa ushirikiano katika utafiti kwani majengo yanayolipiwa kodi ya majengo yapo kwenye maeneo yenu na wamiliki wa majengo hayo pia wapo katika maeneo yenu,” alisema Sagini.
Sagini amewaahidi watafiti ushirikiano mkubwa ili utafiti ufanyike kama ilivyokusudiwa kwa lengo la kuongeza mapato yatokanayo na kodi ya majengo huku akiwaomba watafiti hao  kuendeleza kushirikiano na mkoa wa Simiyu katika tafiti mbalimbali kwa maendeleo ya Mkoa, wananchi na Taifa kwa ujumla.

Akiwasilisha taarifa ya utambulisho wa utafiti huo Mhadhiri Mwandamizi wa Chuo Kikuu Mzumbe na Mtafiti Mwandamizi wa Utafiti huu, Dkt.Francis Mwaijande, amesema Matokeo ya utafiti huu yatawezesha mamlaka za maamuzi ziweze kutoa maamuzi kwa kuzingatia taarifa zilizifanyiwa utafiti na hivyo kuwa na maamuzi ya kuongeza ufanisi kwenye ukusanyaji kodi.

Ameongeza kuwa matokeo ya utafiti huu yanatarajiwa kuongeza mapato yatokanayo na kodi za majengo kwa Serikali kwa kuhamasisha ulipaji kodi kwa kutumia simu zao za mkononi kwa njia ya meseji.
Utafiti unaohusu matumizi ya simu za mikononi katika kuongeza ulipaji kodi za majengo nchini Tanzania, PIERI 20355 unafanyika kwa lengo la kutafuta Ushahidi wa kitaaluma ili kuainisha kipi kinaweza kuongeza ulipaji kodi kwa kufuata sheria.
MWISHO
 Katibu Tawala wa Mkoa, Bw. Jumanne Sagini akizungumza na watafiti wanaofanya utafiti kuhusu unaohusu matumizi ya simu za mikononi katika kuongeza ulipaji kodi za majengo nchini Tanzania, PIERI 20355 katika mikoa ya Simiyu na Shinyanga wakati wa utambulisho wa utafiti mjini Bariadi  Novemba 28, 2019
 Watafiti wanaofanya utafiti kuhusu unaohusu matumizi ya simu za mikononi katika kuongeza ulipaji kodi za majengo nchini Tanzania, PIERI 20355 katika Mikoa ya Simiyu na Shinyanga, wakimsikiliza Katibu Tawala wa Mkoa, Bw. Jumanne Sagini wakati akizungumza nao katika  utambulisho wa utafiti mjini Bariadi  Novemba 28,  2019. 




Katibu Tawala wa Mkoa, Bw. Jumanne Sagini akizungumza na watafiti wanaofanya utafiti kuhusu unaohusu matumizi ya simu za mikononi katika kuongeza ulipaji kodi za majengo nchini Tanzania, PIERI 20355 wakati wa utambulisho wa utafiti mjini Bariadi  Novemba 28, 2019.

 
 Katibu Tawala wa Mkoa, Bw. Jumanne Sagini(katikati mbele)  akiwa katika picha ya pamoja na watafiti wanaofanya utafiti kuhusu matumizi ya simu za mikononi katika kuongeza ulipaji kodi za majengo nchini Tanzania, PIERI 20355 wakati wa utambulisho wa utafiti mjini Bariadi  Novemba 28, 2019.



 Mhadhiri Mwandamizi wa Chuo Kikuu Mzumbe na Mtafiti Mwandamizi wa Utafiti huu, Dkt.Francis Mwaijande akiwasilisha taarifa kwa Katibu Tawala wa Mkoa, Bw. Jumanne Sagini wakati wa utambulisho wa utafiti huo mjini Bariadi  Novemba 28, 2019. 


 


Katibu Tawala wa Mkoa, Bw. Jumanne Sagini akizungumza na watafiti wanaofanya utafiti kuhusu unaohusu matumizi ya simu za mikononi katika kuongeza ulipaji kodi za majengo nchini Tanzania, PIERI 20355 katika mikoa ya Simiyu na Shinyanga wakati wa utambulisho wa utafiti mjini Bariadi  Novemba 28, 2019.

 Mhadhiri Mwandamizi wa Chuo Kikuu Mzumbe na Mtafiti Mwandamizi wa Utafiti huu, Dkt.Francis Mwaijande akiwa katika picha ya pamoja na  Katibu Tawala wa Mkoa, Bw. Jumanne Sagini mara baada ya utambulisho wa utafiti kuhusu matumizi ya simu za mikononi katika kuongeza ulipaji kodi za majengo nchini Tanzania, PIERI 20355 mjini Bariadi  Novemba 28, 2019. 
 Katibu Tawala wa Mkoa, Bw. Jumanne Sagini akifurahia jambo na mmoja wa watafiti wanaofanya  utafiti kuhusu matumizi ya simu za mikononi katika kuongeza ulipaji kodi za majengo nchini Tanzania, PIERI 20355 katika mikoa ya Simiyu na Shinyanga, mara baada ya utambulisho wa utafiti huo mjini Bariadi  Novemba 28, 2019. 
Katibu Tawala wa Mkoa, Bw. Jumanne Sagini akiagana na mmoja wa watafiti wanaofanya  utafiti kuhusu matumizi ya simu za mikononi katika kuongeza ulipaji kodi za majengo nchini Tanzania, PIERI 20355 katika mikoa ya Simiyu na Shinyanga, mara baada ya utambulisho wa utafiti huo mjini Bariadi  Novemba 28, 2019.


MASWA YAZINDUA MFUKO WA WALIMU KUWASAIDIA KUPATA MIKOPO YENYE RIBA NAFUU

Wilaya ya Maswa imezindua mfuko wa walimu kwa lengo la kuwasaidia walimu ambao hawana sifa za kukopesheka katika taasisi zingine za fedha ili waweze kupata mikopo kwa riba nafuu.
Mfuko huo umezinduliwa na Katibu wa Chama cha Walimu nchini, Mwl. Deus Seif wakati wa hafla ya kuwapongeza walimu zaidi ya 1400 wa shule za msingi 123 za wilaya hiyo kwa kuwezesha wilaya kufanya vizuri kwenye Matokeo ya darasa la saba na kuongeza ufaulu  kutoka asilimia 34.9 mwaka 2013 hadi kufikia asilimia 88.73 mwaka 2019.
Akizungumza na mamia ya walimu walioshiriki katika uzinduzi huo, Seif amewaasa walimu kutambua thamani waliyopewa na viongozi wa wilaya na mkoa kwa kuendelea kuwajibika kwa uadilifu mkubwa.
“ Nitoe wito kwa walimu wenzangu ambao si waadilifu wabadilike, wale watoro waache utoro, ambao ni walevi wache ulevi wafundishe watoto; lakini wazazi na ninyi mtusaidie kuhimiza watoto wawe na mahudhurio mazuri shuleni ili walimu waweze kufanya kazi yao vizuri,” alisema Seif.
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa, Dkt. Fredrick Sagamiko amesema hadi sasa mfuko huo umeingiziwa kiasi cha shilingi milioni 15 na halmashauri na baadaye wadau kuongeza kiasi cha shilingi milioni 15 na kuufanya mfuko huo kuwa na jumla ya shilingi milioni 30.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Antony Mtaka amewataka walimu kuacha tabia ya kukopa fedha katika taasisi nyingine za fedha hususani za binafsi zenye riba kubwa ambazo huwalazimu kuweka kadi zao za benki kama rehani, huku akishauri Benki ya walimu kuja na huduma zinazojibu changamoto za walimu ikiwemo kutoa mikopo kwa riba nafuu
Kwa upande wake Katibu wa CWT ameipongeza Wilaya ya Maswa kwa kuona haja kuwapongeza walimu na ya kuwasaidia walimu kwa kutoa mikopo yenye riba nafuu kupitia mfuko huo, ambapo CWT pia imeunga mkono juhudi Wilaya kwa kuchangia kiasi cha shilingi milioni Nane (8).
Wilaya hiyo pia imetoa zawadi ya majiko ya gesi 101 kama zawadi kwa shule hizo ili kuwawezesha walimu kupata chai asubuhi wakiwa shuleni na kuwapunguza walimu muda wa kwenda kutafuta huduma hiyo nje ya maeneo ya shule.
Mkuu wa Wilaya ya Maswa, Dkt. Seif Shekalaghe amesema mwaka 2018 Wilaya ilitoa majiko ya gesi kwa  shule 20 zilizofanya vizuri hivyo, majiko hayo yanatolewa kwa shule 101 ambazo hazikupata awali, pamoja na zawadi ya majiko shule zilizofanya vizuri zimepewa fedha taslimu shilingi 500,000.
Katika uzinduzi huo pia ilifanyika harambee kwa ajili ya kuchangia ujenzi wa nyumba nne za walimu ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kukabiliana na changamoto ya upungufu wa nyumba za walimu
MWISHO



Katibu wa CWT Taifa, Mwl.Deus Seif (kulia) na viongozi wengine wa mkoa wa Simiyu wakiwa wameshika mfano wa hundi ya shilingi milioni 15 ambayo imetolewa na Halmashauri ya Wilaya ya Maswa kwa ajili ya kuanzisha mfuko wa walimu uliozinduliwa rasmi Novemba 29, 2019 Mjini Maswa. 

 Kutoka kulia Mkuu wa Wilaya ya Maswa, Dkt. Seif Shekalaghe, Katibu wa CWT Taifa, Mwl.Deus Seif na Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Antony Mtaka wakikata keki kuashiria uzinduzi wa Mfuko wa walimu, Novemba 29, 2019 katika  hafla ya kuwapongeza walimu wa shule za msingi 123 wilayani Maswa kwa kuwezesha wilaya kufanya vizuri kwenye Matokeo ya darasa la saba na kuongeza ufaulu  kutoka asilimia 34.9 mwaka 2013 hadi kufikia asilimia 88.73 mwaka 2019.


 Kutoka kulia Mkuu wa Wilaya ya Maswa, Dkt. Seif Shekalaghe na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa, Dkt. Fredricka Sagamiko(kushoto) wakipokea hudni ya shilingi milioni nane kutoka kwa Katibu wa CWT Taifa, Mwl.Deus Seif(kulia) zilizotolewa an chama hicho kuchangia Mfuko wa walimu uliozinduliwa rasmi Novemba 29, 2019 mjini Maswa.


 Baadhi ya walimu kutoka shule mbaimbali wilayani Maswa wakishangilia jambo wakati wa hafla ya kuwapongeza walimu wa shule za msingi 123 wilayani Maswa kwa kuwezesha wilaya kufanya vizuri kwenye Matokeo ya darasa la saba na kuongeza ufaulu  kutoka asilimia 34.9 mwaka 2013 hadi kufikia asilimia 88.73 mwaka 2019 ambayo imefanyika Novemba 29, 2019 mjini Maswa.


 Mmoja wa Wakurugenzi katika Benki ya Walimu akitoa maelezo kwa viongozi wa Mkoa wa Simiyu juu ya namna benki hiyo itakavyounga mkono mfuko wa walimu wilayani maswa uliozinduliwa rasmi Novemba 29, 2019 Mjini Maswa.


 Mmoja wa Walimu akipokea zawadi ya jiko la gesi iliyotolewa na  Halmashauri ya Wilaya ya Maswa kwa kila shule kwa ajili ya kutumia kupikia chai asubuhi wakiwa shuleni, katika  hafla ya kuwapongeza walimu wa shule za msingi 123 wilayani Maswa kwa kuwezesha wilaya kufanya vizuri kwenye Matokeo ya darasa la saba na kuongeza ufaulu  kutoka asilimia 34.9 mwaka 2013 hadi kufikia asilimia 88.73 mwaka 2019 ambayo imefanyika Novemba 29, 2019 mjini Maswa.



Mkuu wa Mkoa wa Simiyu. Mhe. Anthony Mtaka (kushoto) akiteta jambo na Katibu wa CWT Taifa, Mwl.Deus Seif katika  hafla ya kuwapongeza walimu wa shule za msingi 123 wilayani Maswa kwa kuwezesha wilaya kufanya vizuri kwenye Matokeo ya darasa la saba na kuongeza ufaulu  kutoka asilimia 34.9 mwaka 2013 hadi kufikia asilimia 88.73 mwaka 2019.
 Baadhi ya Maafisa Elimu Kata wakifutailia matukio katika  hafla ya kuwapongeza walimu wa shule za msingi 123 wilayani Maswa kwa kuwezesha wilaya kufanya vizuri kwenye Matokeo ya darasa la saba na kuongeza ufaulu  kutoka asilimia 34.9 mwaka 2013 hadi kufikia asilimia 88.73 mwaka 2019, hafla iliyofanyika  Novemba 29, 2019 mjini Maswa. 


Baadhi ya walimu wa shule za msingi wilayani Maswa, wakifutailia matukio katika  hafla ya kuwapongeza walimu wa shule za msingi 123 wilayani Maswa kwa kuwezesha wilaya kufanya vizuri kwenye Matokeo ya darasa la saba na kuongeza ufaulu  kutoka asilimia 34.9 mwaka 2013 hadi kufikia asilimia 88.73 mwaka 2019, hafla iliyofanyika  Novemba 29, 2019 mjini Maswa. 

 Baadhi ya viongozi na wadau wa elimu wakicheza wimbo maalum uliondaliwa na kwaya ya walimu Maswa wakati wa hafla ya kuwapongeza walimu wa shule za msingi 123 wilayani Maswa kwa kuwezesha wilaya kufanya vizuri kwenye Matokeo ya darasa la saba na kuongeza ufaulu  kutoka asilimia 34.9 mwaka 2013 hadi kufikia asilimia 88.73 mwaka 2019, hafla iliyofanyika  Novemba 29, 2019 mjini Maswa. 


 Baadhi ya viongozi wa Chama na  Serikali mkoa wa Simiyu na viongozi wa CWT na wakifutailia matukio katika  hafla ya kuwapongeza walimu wa shule za msingi 123 wilayani Maswa kwa kuwezesha wilaya kufanya vizuri kwenye Matokeo ya darasa la saba na kuongeza ufaulu  kutoka asilimia 34.9 mwaka 2013 hadi kufikia asilimia 88.73 mwaka 2019, hafla iliyofanyika  Novemba 29, 2019 mjini Maswa. 


 Baadhi ya viongozi wa Chama na  Serikali mkoa wa Simiyu na viongozi wa CWT na wakiwa katika  picha ya pamoja baada ya kuhitimishwa kwa hafla ya kuwapongeza walimu wa shule za msingi 123 wilayani Maswa kwa kuwezesha wilaya kufanya vizuri kwenye Matokeo ya darasa la saba na kuongeza ufaulu  kutoka asilimia 34.9 mwaka 2013 hadi kufikia asilimia 88.73 mwaka 2019, hafla iliyofanyika  Novemba 29, 2019 mjini Maswa. 


 Majiko 101 yaliyotolewa na Halmashauri ya wilaya ya Maswa kwa ajili ya shule za msingi kwa ajili ya kupikia chai asubuhi, katika hafla ya kuwapongeza walimu wa shule za msingi 123 wilayani Maswa kwa kuwezesha wilaya kufanya vizuri kwenye Matokeo ya darasa la saba na kuongeza ufaulu  kutoka asilimia 34.9 mwaka 2013 hadi kufikia asilimia 88.73 mwaka 2019, hafla iliyofanyika  Novemba 29, 2019 mjini Maswa. 


 Katibu wa CWT Taifa, Mwl.Deus Seif akizungumza na walimu wa shule a msingi wilayani maswa(hawapo pichani), katika hafla ya kuwapongeza walimu wa shule za msingi 123 wilayani Maswa kwa kuwezesha wilaya kufanya vizuri kwenye Matokeo ya darasa la saba na kuongeza ufaulu  kutoka asilimia 34.9 mwaka 2013 hadi kufikia asilimia 88.73 mwaka 2019, hafla iliyofanyika  Novemba 29, 2019 mjini Maswa. 


Katibu wa CWT Taifa, Mwl.Deus Seif akimshukuru Mbunge wa Maswa mashariki na Naibu Waziri wa Madini, Mhe. Stanslaus Nyongo kwa kukubaki kuchangia ujenzi wa nyumba za walimu wilayani Maswa, katika hafla ya kuwapongeza walimu wa shule za msingi 123 wilayani Maswa kwa kuwezesha wilaya kufanya vizuri kwenye Matokeo ya darasa la saba na kuongeza ufaulu  kutoka asilimia 34.9 mwaka 2013 hadi kufikia asilimia 88.73 mwaka 2019, hafla iliyofanyika  Novemba 29, 2019 mjini Maswa.
 Mmoja wa Walimu akipokea zawadi ya jiko la gesi iliyotolewa na  Halmashauri ya Wilaya ya Maswa kwa kila shule kwa ajili ya kutumia kupikia chai asubuhi wakiwa shuleni, katika  hafla ya kuwapongeza walimu wa shule za msingi 123 wilayani Maswa kwa kuwezesha wilaya kufanya vizuri kwenye Matokeo ya darasa la saba na kuongeza ufaulu  kutoka asilimia 34.9 mwaka 2013 hadi kufikia asilimia 88.73 mwaka 2019 ambayo imefanyika Novemba 29, 2019 mjini Maswa.
 Baadhi ya walimu wa shule za msingi wilayani Maswa, wakifutailia matukio katika  hafla ya kuwapongeza walimu wa shule za msingi 123 wilayani Maswa kwa kuwezesha wilaya kufanya vizuri kwenye Matokeo ya darasa la saba na kuongeza ufaulu  kutoka asilimia 34.9 mwaka 2013 hadi kufikia asilimia 88.73 mwaka 2019, hafla iliyofanyika  Novemba 29, 2019 mjini Maswa.

Baadhi ya walimu wa shule za msingi wilayani Maswa, wakifutailia matukio katika  hafla ya kuwapongeza walimu wa shule za msingi 123 wilayani Maswa kwa kuwezesha wilaya kufanya vizuri kwenye Matokeo ya darasa la saba na kuongeza ufaulu  kutoka asilimia 34.9 mwaka 2013 hadi kufikia asilimia 88.73 mwaka 2019, hafla iliyofanyika  Novemba 29, 2019 mjini Maswa.

 Baadhi ya walimu wa shule za msingi wilayani Maswa, wakifutailia matukio katika  hafla ya kuwapongeza walimu wa shule za msingi 123 wilayani Maswa kwa kuwezesha wilaya kufanya vizuri kwenye Matokeo ya darasa la saba na kuongeza ufaulu  kutoka asilimia 34.9 mwaka 2013 hadi kufikia asilimia 88.73 mwaka 2019, hafla iliyofanyika  Novemba 29, 2019 mjini Maswa. 
Kutoka kulia Mkuu wa Wilaya ya Maswa, Dkt. Seif Shekalaghe, Katibu wa CWT Taifa, Mwl.Deus Seif na Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Antony Mtaka wakiteta jambo katika  hafla ya kuwapongeza walimu wa shule za msingi 123 wilayani Maswa kwa kuwezesha wilaya kufanya vizuri kwenye Matokeo ya darasa la saba na kuongeza ufaulu  kutoka asilimia 34.9 mwaka 2013 hadi kufikia asilimia 88.73 mwaka 2019, hafla iliyofanyika  Novemba 29, 2019 mjini Maswa.

CWT KUJENGA KIWANDA CHA MIKATE LISHE SIMIYU


Chama cha Walimu Tanzania (CWT) kinatarajia kujenga kiwanda cha mikate lishe kupitia kampuni yao inayosimamia Maendeleo ya Walimu ya biashara (TDCL), katika eneo la Ng’hami wilayani Maswa mkoani Simiyu.

Akimkabidhi  Katibu wa Chama cha Walimu Nchini, Mwl. Deus Seif hati ya kiwanja chenye ukubwa wa hekari mbili (2), Mkuu wa Wilaya ya Maswa, Dkt. Seif Shekalaghe amesema wilaya imetoa kiwanja hicho bure, ikiwa ni moja ya njia ya kuhamasisha uwekezaji katika sekta ya viwanda ambapo kumhakikishia upatikanaji wa malighafi ya kiwanda hicho (viazi lishe)
“Tumejipanga kuzalisha viazi lishe vya kutosha vitavyotumika kama malighafi ya kiwanda hiki na tayari wakulima wamepewa mbegu za viazi hivyo, niendelee kuwakaribisha CWT wilayani Maswa, kama kuna uwekezaji mwingine mnahitaji kufanya karibuni, hata kama ni tawi la benki yenu ile ya walimu tunawakaribisha sana,” alisema Dkt. Shekalaghe.
Kwa upande wake Mkuu wa mkoa wa Simiyu amesema kukamilika kwa kiwanda hicho kutasaidia kupunguza tatizo la ukosefu wa lishe ambalo limekuwa ni changamoto kwa  Mkoa wa Simiyu.
Aidha, Mtaka amesisitiza Mkuu wa Wilaya, Mkurugenzi wa Halmashautri na wataalam wa kilimo wahakikishe mbegu ya viazi lishe inapatikana kwa wingi ili wananchi wanapohitaji waipate
Katibu wa Chama cha Walimu Tanzania(CWT) Taifa, Mwl. Deus Seif amesema chama hicho kinaunga mkono sera ya Tanzania ya Viwanda huku akibainisha kuwa ujenzi wa kiwanda hicho utaenda haraka kwa kuwa tayari kampuni ya CWT inayosimamia miradi imeshaanza kulifanyia kazi suala hilo.
Ameongeza kuwa pamoja na kujenga kiwanda cha mikate lishe, chama hicho pia kinatarajia kuchukua uwakala katika Kiwanda cha Chaki cha Maswa ili kusambaza chaki zinazozalishwa wilayani humo katika shule zote nchini.
MWISHO



 Mkuu wa Wilaya ya Maswa, Mhe. Dkt. Seif Shekalaghe (mwenye tai kushoto) akimkabidhi Katibu wa Chama cha Walimu Tanzania, Mwl. Deus Seif(mwenye suti nyeusi kulia) hati ya kiwanja chenye ukubwa wa hekari mbili (2) kilichopo Ng’hami wilayani humo  ambacho Halmashauri imekitoa bure kwa CWT kwa ajili ya kujenga kiwanda cha mikate lishe.


 Mkuu wa Wilaya ya Maswa, Mhe. Dkt. Seif Shekalaghe (kulia) akiwaongoza viongozi mbalimbali kwenda katika kiwanja chenye ukubwa wa hekari mbili (2) kilichopo Ng’hami wilayani humo , kilichotolewa bure na Halmashauri kwa CWT kwa ajili ya kujenga kiwanda cha mikate lishe kabla ya makabidhiano ya hati ya kiwanda hicho kati yake na Katibu wa Chama cha Walimu Tanzania, Mwl. Deus Seif Novemba 29, 2019.


 Mkuu wa Wilaya ya Maswa, Mhe. Dkt. Seif Shekalaghe  akitoa maelezo kwa viongozi mbalimbali katika kiwanja chenye ukubwa wa hekari mbili (2) kilichopo Ng’hami wilayani humo , kilichotolewa bure na Halmashauri kwa CWT kwa ajili ya kujenga kiwanda cha mikate lishe kabla ya makabidhiano ya hati ya kiwanja hicho  kati yake na Katibu wa Chama cha Walimu Tanzania, Mwl. Deus Seif Novemba 29, 2019.


 Mkuu wa mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka akizungumza kabla ya makabidhiano ya hati ya kiwanja chenye ukubwa wa hekari mbili (2) kilichopo Ng’hami wilayani Maswa , kilichotolewa bure na Halmashauri kwa CWT kwa ajili ya kujenga kiwanda cha mikate lishe kabla ya makabidhiano ya hati ya kiwanja hicho  kati  Mkuu wa Wilaya ya Maswa, Dkt. Seif Shekalaghe na Katibu M wa Chama cha Walimu Tanzania, Mwl. Deus Seif Novemba 29, 2019.  


 Katibu wa Chama cha Walimu Tanzania, Mwl. Deus Seif akizungumza na viongozi mbalimbali wa Mkoa wa Simiyu, kabla ya makabidhiano ya hati ya kiwanja chenye ukubwa wa hekari mbili (2) kilichopo Ng’hami wilayani Maswa , kilichotolewa bure na Halmashauri kwa CWT kwa ajili ya kujenga kiwanda cha mikate lishe,  kabla ya makabidhiano ya hati ya kiwanja hicho  kati yake na Mkuu wa Wilaya ya Maswa, Dkt. Seif Shekalaghe Novemba 29, 2019.


 Mkuu wa Wilaya ya Maswa, Mhe. Dkt. Seif Shekalaghe (mwenye tai kushoto) akimkabidhi Katibu wa Chama cha Walimu Tanzania, Mwl. Deus Seif(mwenye suti nyeusi kulia) hati ya kiwanja chenye ukubwa wa hekari mbili (2) kilichopo Ng’hami wilayani humo  ambacho Halmashauri imekitoa bure kwa CWT kwa ajili ya kujenga kiwanda cha mikate lishe.


Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Simiyu, Mhe. Enock Yakobo akizungumza akizungumza kabla ya makabidhiano ya hati ya kiwanja chenye ukubwa wa hekari mbili (2) kilichopo Ng’hami wilayani Maswa , kilichotolewa bure na Halmashauri kwa CWT kwa ajili ya kujenga kiwanda cha mikate lishe kabla ya makabidhiano ya hati ya kiwanja hicho  kati  Mkuu wa Wilaya ya Maswa, Dkt. Seif Shekalaghe na Katibu wa Chama cha Walimu Tanzania, Mwl. Deus Seif Novemba 29, 2019


Monday, November 25, 2019

MWEKEZAJI KUTOKA MALAYSIA ANATARAJIA KUWEKEZA MRADI WA DOLA BILIONI 2.5 PORI LA AKIBA LA KIJERESHI SIMIYU

Mwekezaji Azhar Malik kutoka Nchini Malaysia ameonesha nia ya kuwekeza kiasi cha Dola za kimarekani bilioni 2.5 katika mradi mkubwa eneo la pori la akiba la Kijereshi na Ziwa Victoria wilaya ya Busega Mkoani Simiyu, sehemu ya uwekezaji huo ikiwa ni katika ujenzi wa hoteli ya kitalii, usafirishaji, utamaduni na maeneo mengine yatakayoimarisha utalii na kutoa ajira kwa wananchi.

Mwekezaji ambaye amefuatana na Balozi wa Tanzania nchini Malaysia, Mhe. Dkt. Ramadhan Dau amesema ikiwa kila kitu kitaenda kama kilivyopangwa ikiwemo mradi huo unatarajiwa kuanza kutekelezwa kuanzia mwezi Januari 2020, huku akisisitiza kuwa utatekelezwa bila kuathiri ikolojia na mazingira ya uhifadhi.

“Nashukuru kwa ushirikiano nilioupata kwa viongozi wa Mkoa wa Simiyu, pia namshukuru Balozi Dau kwa namna alivyolisimamia jambo hili tangu likiwa wazo mpaka sasa tunapoelekea kwenye utekelezaji niwaahidi tu kuwa pale pande zote zitakapofanya maamuzi mikataba ikisainiwa kwa mujibu wa sheria, mwakani mwezi Januari tutaanza utekelezaji,”alisema Malik

Kwa upande wake Balozi wa Tanzania nchini Malaysia, Mhe. Dkt. Ramadhan Dau amepongeza uongozi wa Chama na Serikali kwa utayari walioonesha, akisisitiza ushirikiano wa viongozi hao na taasisi zote za Serikali zinazohusika, ili mambo yote muhimu yanayohitajika kufanikisha uwekezaji huo yafanyike mapema  kuanzia mwezi Januari kazi ianze.

“Kwa kasi na namna tulivyoanza lile lengo tulilojiwekea kwamba ikifika Januari 2020 mambo yote yanayohusiana na taratibu na  kusaini mikataba, yanapaswa yawe yamekamilika na wataalam waje site (eneo la mradi) waanze survey (utafiti) watengeneze master plan(mpango kabambe), ili kabla ya mwezi Juni 2020 hili jambo liwe limeanza,” alisema Balozi Dau.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe. Anthony Mtaka amesema Uwekezaji huu utaupambanua Mkoa wa Simiyu, Kanda ya Ziwa na kuupambanua utalii kwenye uso wa dunia, ambapo amebainisha kuwa mradi huu utajibu mahitaji mengi kwenye ajira na kukua kwa maendeleo ya ukanda huo.
Kwa upande wao Wizara ya Maliasili na Utalii na Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori (TAWA) wameahidi kutoa ushirikiano ili kuhakikisha mradi huu unafanikiwa.
Mradi huu wa uwekezaji katika sekta ya utalii wilayani Busega utatekelezwa kwa awamu, ambapo awamu ya kwanza inatarajiwa kugharimu takribani dola bilioni 500 na mpaka kukamilika kwake utagharimu dola za Kimarekani bilioni 2.5.
MWISHO

Mwekezaji kutoka nchini Malaysia, Bw. Azhar  Malik(kulia) akiwasilisha taarifa yake ya uwekezaji katika sekta ya Utalii kwenye Pori la Akiba la Kijereshi  wilayani Busega kwa viongozi wa Mkoa wa Simiyu na watendaji kutoka Wizara ya Maliasili na Utalii, wakati wa Ziara yake jana akiwa amefuatana na Balozi wa Tanzania nchini Malaysia, Dkt. Ramadhan Dau aliyofanya kwa lengo la kuangalia mazingira ya uwekezaji
 Balozi wa Tanzania nchini Malaysia, Dkt. Ramadhan Dau akizungumza na viongozi wa mkoa wa Simiyu baada ya kuwasili mjini Bariadi akiwa na Malik(kulia) ambaye amekubali kuwekeza katika mradi mkubwa kwenye sekta ya utalii katika Pori la Akiba la Kijereshi wilayani Busega utakaojumuisha ujenzi wa hoteli ya kitalii, usafirishaji na maeneo mengine yenye kutoa ajira kwa wananchi wakati wa ziara yake jana mkoani Simiyu,


Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka (wa tatu kulia) akisisitiza jambo wakati wa ziara ya Balozi wa Tanzania nchini Malaysia, Dkt. Ramadhan Dau akiwa amefuatana na Mwekezaji kutoka nchini Malaysia, Bw. Azhar  Malik ambaye amekubali kuwekeza katika mradi mkubwa kwenye sekta ya utalii katika Pori la Akiba la Kijereshi  wilayani Busega utakaojumuisha ujenzi wa hoteli ya kitalii, usafirishaji na maeneo mengine yenye kutoa ajira kwa wananchi mkoani Simiyu.

Mkuu wa Wilaya ya Busega, Mhe. Tano Mwera (kulia) akitoa neon la shukrani mara baada ya kumalizika kwa  ziara ya Balozi wa Tanzania nchini Malaysia, Dkt. Ramadhan Dau akifuatana  na Mwekezaji kutoka nchini Malaysia, Bw. Azhar  Malik ambaye amekubali kuwekeza katika mradi mkubwa kwenye sekta ya utalii katika Pori la Akiba la Kijereshi  wilayani Busega utakaojumuisha ujenzi wa hoteli ya kitalii, usafirishaji na maeneo mengine yenye kutoa ajira kwa wananchi mkoani Simiyu.
Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bw. Jumanne Sagini akifafanua jambo katika kikao kati ya viongozi wa mkoa, Balozi wa Tanzania nchini Malaysia, Dkt. Ramadhan Dau  na Mwekezaji kutoka nchini Malaysia, Bw. Azhar  Malik ambaye amekubali kuwekeza katika mradi mkubwa kwenye sekta ya utalii katika Pori la Akiba la Kijereshi  wilayani Busega utakaojumuisha ujenzi wa hoteli ya kitalii, usafirishaji na maeneo mengine yenye kutoa ajira kwa wananchi mkoani Simiyu

 Balozi wa Tanzania nchini Malaysia, Dkt. Ramadhan Dau(wa tano kulia) akizungumza na viongozi wa mkoa wa Simiyu baada ya kuwasili mjini Bariadi akiwa na Mwekezaji kutoka Malaysia Azhar Malik(wa pili kushoto), ambaye amekubali kuwekeza katika mradi mkubwa kwenye sekta ya utalii katika Pori la Akiba la Kijereshi wilayani Busega utakaojumuisha ujenzi wa hoteli ya kitalii, usafirishaji na maeneo mengine kwenye Utalii yenye kutoa ajira kwa wananchi wakati wa ziara yake jana mkoani Simiyu.


Mkuu wa  Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka akifungua  kikao kati ya viongozi wa mkoa, Balozi wa Tanzania nchini Malaysia, Dkt. Ramadhan Dau  na Mwekezaji kutoka nchini Malaysia, Bw. Azhar  Malik ambaye amekubali kuwekeza katika mradi mkubwa kwenye sekta ya utalii katika Pori la Akiba la Kijereshi  wilayani Busega utakaojumuisha ujenzi wa hoteli ya kitalii, usafirishaji na maeneo mengine kwenye Utalii yenye kutoa ajira kwa wananchi  wilayani Busega mkoani Simiyu.
Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bw. Jumanne Sagini (kulia) akizungumza na Balozi wa Tanzania nchini Malaysia, Dkt. Ramadhan Dau (katikati) na Mwekezaji kutoka nchini Malaysia, Bw. Azhar  Malik(kushoto) mara baada  ya kuwapokea katika Uwanja wa Ndege wa Mwanza  jana, kwa ajili ya kuanza ziara ya kuangalia mazingira ya uwekezaji katika sekta ya utalii mkoani Simiyu.
Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bw. Jumanne Sagini (kulia) akizungumza na Balozi wa Tanzania nchini Malaysia, Dkt. Ramadhan Dau (katikati) na Mwekezaji kutoka nchini Malaysia, Bw. Azhar  Malik(kushoto) mara baada  ya kuwapokea katika Uwanja wa Ndege wa Mwanza  jana, kwa ajili ya kuanza ziara ya kuangalia mazingira ya uwekezaji katika sekta ya utalii mkoani Simiyu.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka(kulia) akiteta jambo na Mwekezaji kutoka nchini Malaysia, Bw. Azhar  Malik wakati wa ziara yake katika Pori la Akiba la kijereshi wilayai Busega  jana ambapo amekubai kuwekeza katika mradi mkubwa utakaohusisha ujenzi wa hoteli ya kitalii, usafirishaji na maeneo mengine ya kuinua utalii na ajira kwa wananchi.
Balozi wa Tanzania nchini Malaysia, Dkt. Ramadhan Dau (katikati) akifurahia jambo na baadhi ya viongozi wa Mkoa wa Simiyu, wataalam kutoka Wizara ya Maliasili na Utalii na Mwekezaji kutoka nchini Malaysia, Bw. Azhar  Malik(kushoto)mara baada ya ziara ya balozi na mwekezaji huyo katika Pori la Akiba la Kijereshi wilayani Busega  jana,  iliyofanyika kwa lengo la kuangalia mazingira ya uwekezaji katika sekta ya utalii.

Balozi wa Tanzania nchini Malaysia, Dkt. Ramadhan Dau (katikati) akifurahia jambo na baadhi ya viongozi wa Mkoa wa Simiyu, wataalam kutoka Wizara ya Maliasili na Utalii na Mwekezaji kutoka nchini Malaysia, Bw. Azhar  Malik(kushoto)mara baada ya ziara ya balozi na mwekezaji huyo katika Pori la Akiba la Kijereshi wilayani Busega  jana,  iliyofanyika kwa lengo la kuangalia mazingira ya uwekezaji katika sekta ya utalii.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka  na viongozi wengine wakifurahia jambo wakati wakiagana na Balozi wa Tanzania nchini Malaysia, Dkt. Ramadhan Dau (wa tatu kulia) Mwekezaji kutoka nchini Malaysia, Bw. Azhar  Malik,mara baada ya ziara ya balozi na mwekezaji huyo katika Pori la Akiba la Kijereshi wilayani Busega  jana,  iliyofanyika kwa lengo la kuangalia mazingira ya uwekezaji katika sekta ya utalii.
Mkurugenzi wa Utalii kutoka wizara ya maliasili na utalii akieleza mchango wa wizara hiyo katika kufanikisha mradi utakaotekelezwa na Mwekezaji kutoka nchini Malaysia, Bw. Azhar  Malik, katika Pori la Akiba la Kijereshi wilayani Busega  jana ambapo amekubali kuwekeza katika mradi mkubwa utakaohusisha ujenzi wa hoteli ya kitalii, usafirishaji na maeneo mengine ya kuinua utalii na ajira kwa wananchi.
Kutoka kushoto Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bw. Jumanne Sagini, Mwekezaji kutoka nchini Malaysia, Bw. Azhar  Malik na Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka wakimsikiliza :- Balozi wa Tanzania nchini Malaysia, Dkt. Ramadhan Dau, wakati wa ziara yake katika Pori la Akiba la kijereshi wilayani Busega  jana ambapo amekubali kuwekeza katika mradi mkubwa utakaohusisha ujenzi wa hoteli ya kitalii, usafirishaji na maeneo mengine ya kuinua utalii na ajira kwa wananchi.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka  na viongozi wengine wakifurahia jambo wakati wakiagana na Balozi wa Tanzania nchini Malaysia, Dkt. Ramadhan Dau (wa tatu kulia) Mwekezaji kutoka nchini Malaysia, Bw. Azhar  Malik,mara baada ya ziara ya balozi na mwekezaji huyo katika Pori la Akiba la kijereshi wilayani Busega  jana,  iliyofanyika kwa lengo la kuangalia mazingira ya uwekezaji katika sekta ya utalii.


Baadhi ya wataalam wakifuatilia uwasilishaji wa taarifa ya Mwekezaji kutoka nchini Malaysia, Bw. Azhar  Malik(hayupo pichani), katika sekta ya Utalii kwenye Pori la Akiba la Kijereshi  wilayani Busega aliyoiwasilisha kwa viongozi wa Mkoa wa Simiyu na watendaji kutoka Wizara ya Maliasili na Utalii, wakati wa Ziara yake jana akiwa amefuatana na Balozi wa Tanzania nchini Malaysia, Dkt. Ramadhan Dau aliyofanya kwa lengo la kuangalia mazingira ya uwekezaji.

Mwekezaji kutoka nchini Malaysia, Bw. Azhar  Malik(kulia) akiwasilisha taarifa yake ya uwekezaji katika sekta ya Utalii kwenye Pori la Akiba la Kijereshi  wilayani Busega kwa viongozi wa Mkoa wa Simiyu na watendaji kutoka Wizara ya Maliasili na Utalii, wakati wa Ziara yake jana akiwa amefuatana na Balozi wa Tanzania nchini Malaysia, Dkt. Ramadhan Dau aliyofanya kwa lengo la kuangalia mazingira ya uwekezaji .

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka (wa tatu kulia) akisisitiza jambo wakati wa ziara ya Balozi wa Tanzania nchini Malaysia, Dkt. Ramadhan Dau akiwa amefuatana na Mwekezaji kutoka nchini Malaysia, Bw. Azhar  Malik ambaye amekubali kuwekeza katika mradi mkubwa kwenye sekta ya utalii katika Pori la Akiba la Kijereshi  wilayani Busega utakaojumuisha ujenzi wa hoteli ya kitalii, usafirishaji na maeneo mengine yenye kutoa ajira kwa wananchi mkoani Simiyu.
Baadhi ya wataalam wakifuatilia uwasilishaji wa taarifa ya Mwekezaji kutoka nchini Malaysia, Bw. Azhar  Malik(hayupo pichani) , katika sekta ya Utalii kwenye Pori la Akiba la Kijereshi  wilayani Busega aliyoiwasilisha kwa viongozi wa Mkoa wa Simiyu na watendaji kutoka Wizara ya Maliasili na Utalii, wakati wa Ziara yake jana akiwa amefuatana na Balozi wa Tanzania nchini Malaysia, Dkt. Ramadhan Dau aliyofanya kwa lengo la kuangalia mazingira ya uwekezaji .
Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bw. Jumanne Sagini akifafanua jambo (wa tatu kushoto) wakati wa ziara ya Balozi wa Tanzania nchini Malaysia, Dkt. Ramadhan Dau akiwa amefuatana na Mwekezaji kutoka nchini Malaysia, Bw. Azhar  Malik ambaye amekubali kuwekeza katika mradi mkubwa kwenye sekta ya utalii katika Pori la Akiba la Kijereshi  wilayani Busega utakaojumuisha ujenzi wa hoteli ya kitalii, usafirishaji na maeneo mengine yenye kutoa ajira kwa wananchi mkoani Simiyu.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka  na viongozi wengine wakifurahia jambo wakati wakiagana na Balozi wa Tanzania nchini Malaysia, Dkt. Ramadhan Dau (wa tatu kulia) Mwekezaji kutoka nchini Malaysia, Bw. Azhar  Malik,mara baada ya ziara ya balozi na mwekezaji huyo katika Pori la Akiba la kijereshi wilayani Busega  jana,  iliyofanyika kwa lengo la kuangalia mazingira ya uwekezaji katika sekta ya utalii.
Kutoka kushoto Mwekezaji kutoka nchini Malaysia, Bw. Azhar  Malik, Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka, Balozi wa Tanzania nchini Malaysia, Dkt. Ramadhan Dau na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Simiyu, Mhe. Enock Yakobo wakiteta jambo wakati wa ziara ya Balozi na Mwekezaji huyo , ambaye amekubali kuwekeza katika mradi mkubwa kwenye sekta ya utalii katika Pori la Akiba la Kijereshi  wilayani Busega utakaojumuisha ujenzi wa hoteli ya kitalii, usafirishaji na maeneo mengine yenye kutoa ajira kwa wananchi mkoani Simiyu.
Kutoka kushoto Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bw. Jumanne Sagini, Balozi wa Tanzania nchini Malaysia, Dkt. Ramadhan Dau na Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka, wakifuatilia uwasilishaji wa taarifa ya Mwekezaji kutoka nchini Malaysia, Bw. Azhar  Malik(hayupo pichani) , katika sekta ya Utalii kwenye Pori la Akiba la Kijereshi  wilayani Busega aliyoiwasilisha kwa viongozi wa Mkoa wa Simiyu na watendaji kutoka Wizara ya Maliasili na Utalii, wakati wa Ziara yake jana akiwa amefuatana na Balozi wa Tanzania nchini Malaysia, Dkt. Ramadhan Dau.

Baadhi ya viongozi wakifuatilia uwasilishaji wa taarifa ya Mwekezaji kutoka nchini Malaysia, Bw. Azhar  Malik(hayupo pichani) ,amabye amekubali kuwekeza katika sekta ya Utalii kwenye Pori la Akiba la Kijereshi  wilayani Busega aliyoiwasilisha kwa viongozi wa Mkoa wa Simiyu na watendaji kutoka Wizara ya Maliasili na Utalii, wakati wa Ziara yake jana akiwa amefuatana na Balozi wa Tanzania nchini Malaysia, Dkt. Ramadhan Dau(kulia).
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka (wa tatu kulia) akisisitiza jambo wakati wa ziara ya Balozi wa Tanzania nchini Malaysia, Dkt. Ramadhan Dau akiwa amefuatana na Mwekezaji kutoka nchini Malaysia, Bw. Azhar  Malik ambaye amekubali kuwekeza katika mradi mkubwa kwenye sekta ya utalii katika Pori la Akiba la Kijereshi  wilayani Busega utakaojumuisha ujenzi wa hoteli ya kitalii, usafirishaji na maeneo mengine yenye kutoa ajira kwa wananchi mkoani Simiyu.
Katibu Tawala Mkoa wa Simiyu, Bw. Jumanne Sagini (kulia) akizungumza na akizungumza na Balozi wa Tanzania nchini Malaysia, Dkt. Ramadhan Dau (wa pili kulia) na Mwekezaji kutoka nchini Malaysia, Bw. Azhar  Malik(kushoto) mara baada  ya kuwapokea katika Uwanja wa Ndege wa Mwanza  jana, kwa ajili ya kuanza ziara ya kuangalia mazingira ya uwekezaji katika sekta ya utalii mkoani Simiyu, wengine ni wataalam walioambatana na mwekezaji huyo.

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!