Friday, November 22, 2019

DKT BANA AOMBA WIZARA YA FEDHA KUWEZESHA UJENZI WA MABWENI IFM KAMPASI YA SIMIYU


Mwenyekiti wa Baraza la Uongozi la Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM) Balozi Dkt. Benson Bana ameiomba Wizara ya Fedha na Mipango kuwezesha ujenzi wa mabweni kwa wanafunzi  takribani 500 wanaotarajiwa kudahiliwa mwezi Machi, 2020 katika Kampasi ya Kanda ya Ziwa ya  Chuo hicho Mkoani Simiyu, ili kuwaondolea adha ya kupanga mitaani.

Dkt. Bana ametoa ombi hilo kwa Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt.Ashatu Kijaji alipofanya ziara Novemba 21, 2019 kuona maendeleo ya ujenzi wa kampasi hiyo  kijiji cha Sapiwi wilayani Bariadi Mkoani Simiyu.

Dkt. Bana amesema kutokana na ongezeko la wanafunzi wanaoomba udahili wa masomo, Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM), kimeanzisha Kampasi ya Kanda ya Ziwa iliyopo Kijiji cha Sapiwi wilayani Bariadi Simiyu, ambapo mwezi Machi 2020 wanafunzi takribani 1000 wanatarajiwa kuanza masomo.

“Ili tuweze kufikia malengo yetu tunaomba mabweni ya kuhimili angalau wanafunzi 500 tu, Mhe. Naibu Waziri tunaomba kuwezeshwa kujenga mabweni haya mengine utuachie tutafanya, tusipofanikiwa hili Mhe. Naibu Waziri, juhudi za Mhe. Mkuu wa Mkoa na viongozi wenzake zinaweza kuishai mahali ambapo si pazuri,” alisema Dkt. Bana.

Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt.Ashatu Kijaji amesema Serikali inatambua juhudi za Mkoa wa Simiyu katika elimu na kuahidi kujenga mabweni yenye uwezo wa kuchukua wanafunzi 500 kama alivyoomba Mwenyekiti wa Baraza la Uongozi wa Chuo, ili wanafunzi watakaodahiliwa wapate malazi hususani wanafunzi wa kike.

“Hizi changamoto mlizozitaja na hasa hili la mabweni kwa ajili ya watoto wetu linafanyiwa kazi kwa haraka na ujenzi wa mabweni ya watoto 500 mpaka tutakapofika mwezi Machi inawezekana,” alisema Dkt.  Kijaji.

Naye Mkuu wa mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka ameushukuru uongozi wa Chuo cha IFM kwa uamuzi wa kujenga Kampasi mpya Simiyu na kuamua kuifungua mwaka 2020 ambapo amesema kuwepo kwa chuo hicho kutachangia kuongeza mwamko wa elimu katika mkoa wa Simiyu, huku akiwaalika wawekezaji kuwekeza katika huduma mbalimbali katika kampasi hiyo.

Kwa upande wake Makamu Mkuu wa Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM), Prof.Tadeo Satta amewashukuru viongozi wa Mkoa wa Simiyu kwa namna walivyowezesha kupata eneo la ujenzi lenye ukubwa wa ekari 30 ambalo lilitolewa bure na pia walivyosaidia katika hatua ya ujenzi ambapo wametoa wataalam kusaidia kusimamia ujenzi na kupelekea ujenzi kwenda kwa kasi.

Ameongeza kuwa majengo yanayotarajiwa kujengwa katika kampasi ya Simiyu ni jengo la utawala, maktaba, madarasa, maabara ya kompyuta, hosteli za wanafunzi, nyumba za wafanya kazi, kafteria na holi kwa ajili ya mikutano; ambapo kwa awamu ya kwanza ujenzi ulianza mwezi Julai 2019 mpaka sasa jengo la utawala lenye ghorofa moja limefikia asilimia 62 na madarasa yamefikia asilimia 92.
MWISHO



Katibu Tawala Msaidizi sehemu ya Miundombinu katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mashaka Luhamba (mbele) akiwaongoza  Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt.Ashatu Kijaji (mwenye ushungi), Viongozi na Wajumbe wa Baraza la Uongozi la Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM)  na viongozi wa mkoa wa Simiyu, kutembelea majengo  ya Kampasi ya Kanda ya Ziwa ya  Chuo cha Usimamizi  wa Fedha IFM(Simiyu), wakati wa ziara ya Naibu Waziri Kijaji Novemba 21, 2019 katika kampasi hiyo inayojengwa Kijiji cha Sapiwi wilayani Bariadi Mkoani Simiyu, aliyofanya  kwa lengo la kuona maendeleo ya ujenzi.

Makamu Mkuu wa Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM), Prof. Tadeo Satta(wa tatu kulia) akitoa maelezo kwa Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt.Ashatu Kijaji (mwenye ushungi), juu ya ujenzi wa majengo mbalimbali unaoendelea katika Kampasi ya Kanda ya Ziwa ya  Chuo hicho, wakati wa ziara ya Naibu Waziri Kijaji Novemba 21, 2019 katika kampasi hiyo Kijiji cha Sapiwi wilayani Bariadi Mkoani Simiyu, aliyofanya kwa lengo la kuona maendeleo ya ujenzi.

Makamu Mkuu wa Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM), Prof. Tadeo Satta(wa pili kushoto) akitoa maelezo kwa Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt.Ashatu Kijaji (mwenye ushungi katikati), juu ya ujenzi wa majengo mbalimbali unaoendelea katika Kampasi ya Kanda ya Ziwa ya  Chuo hicho, wakati wa ziara ya Naibu Waziri Kijaji Novemba 21, 2019 katika kampasi hiyo Kijiji cha  Sapiwi wilayani Bariadi Mkoani Simiyu aliyofanya kwa lengola kuona maendeleo ya ujenzi.


Kutoka kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka akifurahia jambo na Mwenyekiti wa Baraza la uongozi la Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM), Mhe. Balozi Dkt. Benson Bana na Makamu Mkuu wa Chuo hicho, Prof. Tadeo Satta, mara baada ya mazungumzo kati yake na wajumbe wa Baraza la Uongozi wa  Chuo cha usimamizi wa Fedha (IFM) walipomtembela ofisini kwake Novemba 21, 2019 siku ya ziara ya Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt.Ashatu Kijaji (hayupo pichani) mkoani Simiyu ya kutembelea Kampasi ya Kanda ya Ziwa katika Kijiji cha Sapiwi wilayani Bariadi.
Sehemu ya jengo la Utawala katika Kampasi ya Kanda ya Ziwa ya  Chuo cha usimamizi wa Fedha (IFM) katika Kijiji cha Sapiwi wilayani Bariadi Mkoani Simiyu, ambayo ujenzi wake umefikia asilimi 62 na ikitarajiwa kukamilika.
 Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt.Ashatu Kijaji akizungumza na Viongozi na Wajumbe wa Baraza la Uongozi la Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM)  na viongozi wa mkoa wa Simiyu(baadhi hawapo pichani), kabla ya  kutembelea majengo  ya Kampasi ya Kanda ya Ziwa ya  Chuo cha Usimamizi  wa Fedha IFM(Simiyu), wakati wa ziara yake katika kampasi hiyo inayojengwa Kata ya Sapiwi wilayani Bariadi Mkoani Simiyu, aliyofanya  kwa lengo la kuona maendeleo ya ujenzi huo.


Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka (wa tano kulia) akiwa katika picha ya pamoja na wajumbe wa Baraza la Uongozi la Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM) mara baada ya mazungumzo kati yake na wajumbe wa Baraza la Uongozi la Chuo cha usimamizi wa Fedha (IFM) walipomtembela ofisini kwake Novemba 21, 2019 siku ya ziara ya Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt.Ashatu Kijaji (hayupo pichani) mkoani Simiyu ya kutembelea Kampasi ya Kanda ya Ziwa ya Chuo hicho  katika Kata ya Sapiwi wilayani Bariadi.

Makamu Mkuu wa Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM), Prof. Tadeo Satta akizungumza na baadhi ya wananchi wa Kata ya Sapiwi waliofika kumsikiliza Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt.Ashatu Kijaji ambaye alitembelea Kampasi ya Kanda ya Ziwa ya Chuo hicho  katika Kata ya Sapiwi wilayani Bariadi. Novemba 21, 2019 kuona maendeleo ya ujenzi wa kampasi hiyo ambayo inatarajiwa kuanza kufunguliwa Machi 2020.
Makamu Mkuu wa Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM), Prof. Tadeo Satta akitoa maelezo kwa Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt.Ashatu Kijaji (mwenye ushungi), juu ya ujenzi wa majengo mbalimbali unaoendelea katika Kampasi ya Kanda ya Ziwa ya  Chuo hicho, wakati wa ziara ya Naibu Waziri Kijaji Novemba 21, 2019 katika kampasi hiyo Kata ya Sapiwi wilayani Bariadi Mkoani Simiyu, aliyofanya kwa lengo la kuona maendeleo ya ujenzi.
Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Simiyu, Mhe. Enock Yakobo akizungumza na baadhi ya wananchi wa Kata ya Sapiwi waliofika kumsikiliza Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt.Ashatu Kijaji ambaye alitembelea Kampasi ya Kanda ya Ziwa ya Chuo hicho  katika Kata ya Sapiwi wilayani Bariadi. Novemba 21, 2019 kuona maendeleo ya ujenzi wa kampasi hiyo ambayo inatarajiwa kufunguliwa Machi 2020.
Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Simiyu, Mhe. Enock Yakobo akizungumza na baadhi ya wananchi wa Kata ya Sapiwi waliofika kumsikiliza Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt.Ashatu Kijaji ambaye alitembelea Kampasi ya Kanda ya Ziwa ya Chuo hicho  katika Kata ya Sapiwi wilayani Bariadi. Novemba 21, 2019 kuona maendeleo ya ujenzi wa kampasi hiyo ambayo inatarajiwa kufunguliwa Machi 2020.

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka (wa tatu  kushoto) akizungumza na wajumbe wa Baraza la Uongozi la Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM) walipomtembela ofisini kwake Novemba 21, 2019 siku ya ziara ya Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt.Ashatu Kijaji (hayupo pichani) mkoani Simiyu ya kutembelea Kampasi ya Kanda ya Ziwa ya Chuo hicho  katika Kata ya Sapiwi wilayani Bariadi.

Diwani wa Kata ya Sapiwi akizungumza na baadhi ya wananchi wa Kata ya Sapiwi waliofika kumsikiliza Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt.Ashatu Kijaji ambaye alitembelea Kampasi ya Kanda ya Ziwa ya Chuo hicho  katika Kata ya Sapiwi wilayani Bariadi. Novemba 21, 2019 kuona maendeleo ya ujenzi wa kampasi hiyo ambayo inatarajiwa kufunguliwa Machi 2020.

Katibu Tawala Msaidizi sehemu ya Miundombinu katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mashaka Luhamba (mbele kushoto) akiwaongoza  Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt.Ashatu Kijaji (mwenye ushungi), Viongozi na Wajumbe wa Baraza la Uongozi la Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM)  na viongozi wa mkoa wa Simiyu, kutembelea majengo  ya Kampasi ya Kanda ya Ziwa ya  Chuo cha Usimamizi  wa Fedha IFM(Simiyu), wakati wa ziara ya Naibu Waziri Kijaji Novemba 21, 2019 katika kampasi hiyo inayojengwa Kata ya Sapiwi wilayani Bariadi Mkoani Simiyu, aliyofanya  kwa lengo la kuona maendeleo ya ujenzi.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka  akizungumza na baadhi ya wananchi wa Kata ya Sapiwi waliofika kumsikiliza Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt.Ashatu Kijaji ambaye alitembelea Kampasi ya Kanda ya Ziwa ya Chuo hicho  katika Kata ya Sapiwi wilayani Bariadi. Novemba 21, 2019 kuona maendeleo ya ujenzi wa kampasi hiyo ambayo inatarajiwa kufunguliwa Machi 2020.

Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt.Ashatu Kijaji(kushoto)  akiteta jambo na Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka  mara baada ya kuhitimisha ziara yake katika Kampasi ya Kanda ya Ziwa ya Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM) katika Kata ya Sapiwi wilayani Bariadi. Novemba 21, 2019 kuona maendeleo ya ujenzi wa kampasi hiyo ambayo inatarajiwa kufunguliwa Machi 2020


Katibu Tawala Msaidizi sehemu ya Miundombinu katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mashaka Luhamba (mbele) akiwaongoza  Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt.Ashatu Kijaji (mwenye ushungi), Viongozi na Wajumbe wa Bodi ya Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM)  na viongozi wa mkoa wa Simiyu, kutembelea majengo  ya Kampasi ya Kanda ya Ziwa ya  Chuo cha Usimamizi  wa Fedha IFM(Simiyu), wakati wa ziara ya Naibu Waziri Kijaji Novemba 21, 2019 katika kampasi hiyo inayojengwa Kata ya Sapiwi wilayani Bariadi Mkoani Simiyu, aliyofanya  kwa lengo la kuona maendeleo ya ujenzi.


Jengo la Maktaba katika Kampasi ya Kanda ya Ziwa ya  Chuo cha usimamizi wa Fedha (IFM) katika Kata ya Sapiwi wilayani Bariadi Mkoani Simiyu, ambalo liko katika hatua ya ukamilishaji  ikitarajiwa kukamilika kabla ya Machi 2020.


Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka akiwa ameongozana na  Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt.Ashatu Kijaji (mwenye ushungi), Viongozi na Wajumbe wa Baraza la Uongozi la Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM)  na viongozi wa mkoa wa Simiyu, kutembelea majengo  ya Kampasi ya Kanda ya Ziwa ya  Chuo cha Usimamizi  wa Fedha IFM(Simiyu), wakati wa ziara ya Naibu Waziri Kijaji Novemba 21, 2019 katika kampasi hiyo inayojengwa Kata ya Sapiwi wilayani Bariadi Mkoani Simiyu, aliyofanya  kwa lengo la kuona maendeleo ya ujenzi.


Makamu Mkuu wa Chuo cha Usimamizi wa Chuo(IFM), Prof. Tadeo Satta  na viongozi wengine wakiwasikiliza baadhi ya wananchi wa Kata ya Sapiwi ambao walikuwa wakiwasilisha hoja zao kwa Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt.Ashatu Kijaji (mwenye ushungi katikati) ambaye alitembelea Kampasi ya Kanda ya Ziwa ya Chuo hicho  katika Kata ya Sapiwi wilayani Bariadi. Novemba 21, 2019 kuona maendeleo ya ujenzi wa kampasi hiyo ambayo inatarajiwa kufunguliwa Machi 2020.


Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka(kushoto) akifurahia jambo na Mwenyekiti wa Baraza la Uongozi la Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM), Mhe. Balozi Dkt. Benson Bana wakati wajumbe wa bodi hiyo, walipomtembela ofisini kwake Novemba 21, 2019 siku ya ziara ya Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt.Ashatu Kijaji (hayupo pichani) mkoani Simiyu ya kutembelea Kampasi ya Kanda ya Ziwa katika Kata ya Sapiwi wilayani Bariadi.


Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt.Ashatu Kijaji akizungumza na baadhi ya wananchi wa Kata ya Sapiwi waliofika kumsikiliza wakati wa ziara yake  katika Kampasi ya Kanda ya Ziwa ya Chuo hicho,  Kata ya Sapiwi wilayani Bariadi Novemba 21, 2019 kuona maendeleo ya ujenzi wa kampasi hiyo ambayo inatarajiwa kufunguliwa Machi 2020.

Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt.Ashatu Kijaji akisaini kitabu cha wageni katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu mara baada ya kuwasili Mjini Bariadi kwa ajili ya ziara yake katika Kampasi ya Kanda ya Ziwa ya Chuo hicho,  Kata ya Sapiwi wilayani Bariadi Novemba 21, 2019 kuona maendeleo ya ujenzi wa kampasi hiyo ambayo inatarajiwa kufunguliwa Machi 2020.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka akitoa salamu za Mkoa kwa Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt.Ashatu Kijaji (wa pili kushoto) mara baada ya kuwasili Mjini Bariadi kwa ajili ya ziara yake katika Kampasi ya Kanda ya Ziwa ya Chuo hicho, Kata ya Sapiwi wilayani Bariadi  Novemba 21, 2019 kuona maendeleo ya ujenzi wa kampasi hiyo ambayo inatarajiwa kufunguliwa Machi 2020.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka (kulia) akiagana na baadhi ya wajumbe wa Bodi ya Wajumbe wa Baraza la Uongozi la Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM), mara baada ya mazungumzo kati yake na wajumbe hao walipomtembelea ofisini kwake Novemba 21, 2019 siku ya ziara ya Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt.Ashatu Kijaji (hayupo pichani) mkoani Simiyu ya kutembelea Kampasi ya Kanda ya Ziwa ya Chuo hicho katika Kata ya Sapiwi wilayani Bariadi.


0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!