Monday, November 25, 2019

WANANCHI SIMIYU WASHAURIWA KUFANYA MAZOEZI, KUACHA ULAJI USIOFAA KUZUIA MAGONJWA YASIYOAMBUKIZA


Mganga Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Dkt. Festo Dugange ametoa wito kwa wananchi mkoani Simiyu kujenga utamaduni wa kufanya mazoezi na kuacha ulaji usiofaa kwa kuacha kutumia vyakula vyenye sukari, mafuta na chumvi nyingi na nafaka zilizokobolewa kwa lengo la kudhibiti magonjwa yasiyoambukiza yakiwemo kisukari, shinikizo la juu la damu na saratani.

Dkt Dugange ameyasema hayo Novemba 22, 2019 wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya kudhibiti na kuzuia magonjwa yasiyoambukiza, ambayo ilizinduliwa rasmi kimkoa Novemba 22, 2019 katika Uwanja wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi.

“ Asilimia 43 ya wagonjwa wanaotibiwa katika vituo vya kutolea huduma za afya wana matatizo yanayotokana na  magonjwa yasiyo ya kuambukiza, kutofanya mazoezi kunachangia kwa asilimia 60 magonjwa yasiyoambukiza, hivyo ni vema wananchi wakafanya mazoezi na kuepuka ulaji usiofaa ili kudhibiti magonjwa haya,” alisema Dkt. Dugange.

Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bw. Jumanne Sagini amewataka watumishi wa idara ya afya mkoani hapa, kuwafikishia wananchi elimu ya kujikinga na magonjwa yasiyoambukiza na kutoa ushauri kwa mtu mmoja mmoja kuhusu umuhimu wa kufanya mazoezi, lishe bora na madhara ya kutumia vilevi kupita kiasi.

Aidha, Sagini amesisitiza wataalam wa afya kuelimisha jamii namna ya kutambua magonjwa yasiyoambukiza kupitia upimaji na kufuatilia watu wenye magonjwa sugu yasiyoambukiza.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga amesema atashirikiana na viongozi wengine kusimamia ufanyaji wa mazoezi ya viungo ikiwemo utekelezaji wa agizo la Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan la kufanya mazoezi Jumamosi ya pili ya kila mwezi ili kuwahamasisha wananchi kudhibiti magonjwa yasiyoambukiza.

“Tutakachokifanya sasa hivi ni kugawa vituo vya mazoezi ya mara kwa mara kulingana na kanda kwa kuwa mji unakuwa, lakini pia tutaweka viongozi kwa kila kanda, ili kila inapofika Jumamosi ya pili mwezi viongozi wanakuja na watu wao tunajumuika pamoja katika mazoezi,”alisema Kiswaga.

Kwa upande wao watumishi walioshiriki katika mazoezi hayo wamewashukuru viongozi wa Mkoa kwa kuhamasisha watumishi na wananchi kushiriki mazoezi haya, kwa sababu wanatumia muda mwingi kazini wakiwa wamekaa hali inayoweza kuchangia wao kupata magonjwa yasiyoambukiza, hivyo wakaomba utaratibu huo uwe endelevu na waahihidi kushiriki kila wakati ili kujikinga na magonjwa yasiyoambukiza.

“Watumishi wengi tumekuwa tukijihusisha  zaidi na shughuli zetu za kikazi tunasahau na wakati mwingine tunashindwa  kufanya mazoezi ambayo ni muhimu kwa afya zetu na ufanisi wa kazi zetu, ninashukuru viongozi wetu kuandaa na kufanikisha zoezi hili na sisi kama watumishi tunaahidi kuwa suala hili litakuwa endelevu,” alisema Marko Igenge mtumishi idara ya afya.

Kampeni ya kudhibiti na kuzuia magonjwa ilizinduliwa rasmi kimkoa Novemba 22, 2019 katika Uwanja wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi na utaratibu wa kufanya mazoezi ya viungo utaendelea kufanyika kila Jumamosi ya pili katika kila mwezi.
MWISHO

Baadhi ya viongozi, watumishi wa umma na taasisi binafsi  na wananchi wakifanya mazoezi ya viungo katika uzinduzi wa Kampeni ya kudhibiti na kuzuia magonjwa yasiyoambukiza  ambayo ilizinduliwa rasmi kimkoa Novemba 22, 2019.katika Uwanja wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi.
Baadhi ya viongozi, watumishi wa umma na taasisi binafsi  na wananchi wakifanya mazoezi ya viungo katika uzinduzi wa Kampeni ya kudhibiti na kuzuia magonjwa yasiyoambukiza  ambayo ilizinduliwa rasmi kimkoa Novemba 22, 2019.katika Uwanja wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi.

Baadhi ya viongozi, watumishi wa umma na taasisi binafsi  na wananchi wakifanya mazoezi ya viungo katika uzinduzi wa Kampeni ya kudhibiti na kuzuia magonjwa yasiyoambukiza  ambayo ilizinduliwa rasmi kimkoa Novemba 22, 2019.katika Uwanja wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi.


Baadhi ya viongozi, watumishi wa umma na wananchi wakifanya mazoezi ya viungo katika uzinduzi wa Kampeni ya kudhibiti na kuzuia magonjwa yasiyoambukiza  ambayo ilizinduliwa rasmi kimkoa Novemba 22, 2019.katika Uwanja wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi.
Baadhi ya viongozi, watumishi wa umma na taasisi binafsi  na wananchi wakifanya mazoezi ya viungo katika uzinduzi wa Kampeni ya kudhibiti na kuzuia magonjwa yasiyoambukiza  ambayo ilizinduliwa rasmi kimkoa Novemba 22, 2019.katika Uwanja wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi.
Baadhi ya viongozi, watumishi wa umma na taasisi binafsi  na wananchi wakifanya mazoezi ya viungo katika uzinduzi wa Kampeni ya kudhibiti na kuzuia magonjwa yasiyoambukiza  ambayo ilizinduliwa rasmi kimkoa Novemba 22, 2019.katika Uwanja wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi.

.

Wachezaji wa timu ya Ofisi ya Mkuu wa Mkoa waSimiyu(wenye jezi za zambarau) na timu ya Hospitali ya Rufaa ya Mkoa(wenye jezi nyeupe) wakicheza mechi ya kirafiki wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya kudhibiti na kuzuia magonjwa yasiyoambukiza  ambayo ilizinduliwa rasmi kimkoa Novemba 22, 2019.katika Uwanja wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi.

Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bw. Jumanne Sagini akizungumza na watumishi wa umma na wananchi, wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya kudhibiti na kuzuia magonjwa yasiyoambukiza  ambayo ilizinduliwa rasmi kimkoa Novemba 22, 2019.katika Uwanja wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi.

Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga akizungumza na watumishi wa umma na wananchi, wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya kudhibiti na kuzuia magonjwa yasiyoambukiza  ambayo ilizinduliwa rasmi kimkoa Novemba 22, 2019.katika Uwanja wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi.




Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bw. Jumanne Sagini(mwenye fulana ya mistari)  akiwa katika picha ya pamoja na wachezaji wa timu ya Ofisi ya Mkuu wa Mkoa waSimiyu kabla ya mechi ya kirafiki iliyochezwa kati ya timu hiyo na timu ya Hospitali ya Rufaa ya Mkoa, wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya kudhibiti na kuzuia magonjwa yasiyoambukiza  ambayo ilizinduliwa rasmi kimkoa Novemba 22, 2019.katika Uwanja wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi.



Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bw. Jumanne Sagini(mwenye fulana ya mistari)  akiwa katika picha ya pamoja na wachezaji wa timu ya Hospitali ya Rufaa ya Mkoa kabla ya mechi ya kirafiki iliyochezwa kati ya timu hiyo na timu ya Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya kudhibiti na kuzuia magonjwa yasiyoambukiza  ambayo ilizinduliwa rasmi kimkoa Novemba 22, 2019.katika Uwanja wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi.
Wachezaji wa timu ya Ofisi ya Mkuu wa Mkoa waSimiyu(wenye jezi za zambarau) na timu ya Hospitali ya Rufaa ya Mkoa(wenye jezi nyeupe) wakicheza mechi ya kirafiki wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya kudhibiti na kuzuia magonjwa yasiyoambukiza  ambayo ilizinduliwa rasmi kimkoa Novemba 22, 2019.katika Uwanja wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi.




Baadhi ya viongozi, watumishi wa umma na taasisi binafsi  na wananchi wakifanya mazoezi ya viungo katika uzinduzi wa Kampeni ya kudhibiti na kuzuia magonjwa yasiyoambukiza  ambayo ilizinduliwa rasmi kimkoa Novemba 22, 2019.katika Uwanja wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi.

0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!