Saturday, June 9, 2018

VIONGOZI MKOANI SIMIYU WAASWA KUZUNGUMZA LUGHA MOJA KUHUSU HAKI ZA WANANCHI

Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana UVCCM Taifa Kheri James  amewaasa  viongozi wa dini ,chama na Serikali kutotofautiana lugha kuhusu haki za wananchi katika kukomesha dhuluma na pia wawakemee wanaokwamisha juhudi za Serikali katika kuwaletea maendeleo wananchi.

James amesema hayo katika futari iliyoandaliwa na Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Anthony Mtaka katika viwanja vya ofisi ya mkoa, na kuhudhuriwa na waumini wa Dini ya Kiislamu wakiongozwa na Shekh Mahamudu Kalokola ,viongozi wa madhehebu mbalimbali na viongozi wa chama na serikali ,ikiwa ni desturi yake kila mwaka kujumuika pamoja katika kipindi cha mfungo mtukufu wa Ramadhan.

“Maendeleo yanayofanywa sasa ni kwa ajili ya watu wote sisi kama viongozi tunao wajibu wa kushiriki ili tuweze kuhakikisha kuwa yanafikiwa kwa wakati, viongozi wa dini, chama na Serikali tusitofautiane lugha katika kutetea haki za wananchi, tuhakikishe tunasimamia wananchi wetu wanapata haki na dhuluma inakomeshwa” alisema James.

James amesema viongozi wa madhehebu ya dini wana mchango mkubwa kwa  Serikali katika kuhimiza maendeleo kupitia makanisa na misikiti ,hivyo ni vema kuendelea kuliombea taifa kudumisha amani pasipo kutofautiana na chama na Serikali.

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe.Anthony Mtaka amewashukuru viongozi wa dini kwa namna wanavyoshirikiana na Serikali katika masuala mbalimbali , huku akiwaomba kuendelea kusaidia katika malezi ya watoto hasa katika mkakati wa mkoa wa kuinua kiwango cha ufaulu madarasa la mitihani,  ambapo Kidato cha nne na darasa la saba wapo katika kambi za Kitaaluma.

“Watoto wetu wa kidato cha nne na darasa la saba wako katika kambi za kitaaluma kwa ajili ya kujiandaa na mitihani ya Taifa, sisi kama Serikali tumetoa nafasi ya kama nusu saa kwa watoto kushiriki ibada kila siku katika kambi hizo, tunaomba viongozi wetu wa dini mfike kwa ajili ya kuwausia na kuwasisitiza kusoma kwa kuwa tunahitaji watoto wetu wafanye vizuri “ alisema.

Shekhe  wa Mkoa wa Simiyu Mahamudu Kalokola ameishukuru Viongozi wa Serikali Mkoani humo wakiongozwa na Mkuu wa Mkoa, Mhe. Anthony Mtaka kwa namna wanavyoshirikiana na Madhehebu yote ya dini naye akaahidi kuendelea kushirikiana na  Serikali katika Nyanja mbalimbali za maendeleo.
Naye Mkuu wa Wilaya ya Kongwa Mhe. Deo Ndejembi ambaye yupo SIMIYU na viongozi wa vikundi vya vijana Kongwa kwa lengo la kujifunza Simiyu ilivyofanikiwa kwa miradi ya vijana, akiwa katika futari hiyo amesema Simiyu  imejipambanua vema katika masuala ya vijana hususani katika uzalishaji mdogo mdogo jambo ambalo liwawafanya waje kujifunza ili waweze kuwasaidia vijana wa Kongwa kuanzisha miradi endelevu na yenye tija.
MWISHO


Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana UVCCM Taifa Kheri James akizungumza na Viongozi wa Dini, Waumini wa  Kiislamu, Viongozi wa Chama naSerikali Mkoani Simiyu, katika shughuli fupi ya futari iliyoaandaliwa na Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka  kwa makundi tajwa Mjini Bariadi,
 Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka akizungumza na Viongozi wa Dini, Waumini wa Kiislamu, Viongozi wa Chama na Serikali Mkoani Simiyu, katika shughuli fupi ya futari aliyoiandaa kwa makundi tajwa  Mjini Bariadi,

 Shekhe  wa Mkoa wa Simiyu Mahamudu Kalokola akizungumza na Viongozi wa Dini, Waumini wa  Kiislamu, Viongozi wa Chama na Serikali Mkoani Simiyu, baada ya shughuli fupi ya futari iliyoaandaliwa na Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka kwa makunditajwa,  Mjini Bariadi. 
Katibu Tawala Mkoa wa Simiyu, Bw. Jumanne Sagini akitambulisha viongozi na makundi ya watu mbalimbali walioshiriki futari iliyoandaliwa na Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka  kwa ajili ya Viongozi wa Dini, Waumini wa  Kiislamu, Viongozi wa Chama na Serikali Mkoani humo, Mjini Bariadi.


Kutoka kushoto Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Simiyu, Mhe. Enock Yakobo,  Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka na Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana UVCCM Taifa Kheri James wakifurahia jambo baada ya  shughuli fupi ya futari iliyoandaliwa na  Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka  kwa ajili ya Viongozi wa Dini, Waumini wa  Kiislamu, Viongozi wa Chama na Serikali Mkoani humo, Mjini Bariadi.
Mkuu wa Wilaya ya Kongwa Mhe. Deo Ndejembi akizungumza na Viongozi wa Dini, Waumini wa  Kiislamu, Viongozi wa Chama na Serikali Mkoani Simiyu, baada ya shughuli  fupi ya futari iliyoandaliwa na Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka   kwa makundi tajwa Mjini Bariadi.


Mkuu wa Wilaya ya Bariadi  Mhe. Festo Kiswaga  akizungumza na Viongozi wa Dini, Waumini wa  Kiislamu, Viongozi wa Chama naSerikali Mkoani Simiyu,baada ya shughuli fupi ya futari iliyoaandaliwa na Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka  kwa Mjini Bariadi, kwa ajili ya makundi tajwa.
Baadhi ya Waumini wa Dini ya Kiislamu Mkoani Simiyu wakipata futari iliyoandaliwa na Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka  kwa ajili ya Viongozi wa Dini, Waumini wa  Kiislamu, Viongozi wa Chama na Serikali Mkoani humo, Mjini Bariadi
Baadhi ya Waumini wa Dini ya Kiislamu Mkoani Simiyu wakimsikiliza Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana UVCCM Taifa Kheri James wakati wa shughuli ya futari iliyoandaliwa na Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka  kwa ajili ya Viongozi wa Dini, Waumini wa  Kiislamu, Viongozi wa Chama na Serikali Mkoani humo, Mjini Bariadi.
Baadhi ya Waumini wa Dini ya Kiislamu Mkoani Simiyu wakipata futari iliyoandaliwa na Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka  kwa ajili ya Viongozi wa Dini, Waumini wa  Kiislamu, Viongozi wa Chama na Serikali Mkoani humo, Mjini Bariadi.

Friday, June 8, 2018

KONGWA WAFANYA ZIARA MKOANI SIMIYU KUTEMBELEA MIRADI YA VIJANA ILI KUJIFUNZA


Viongozi kutoka Wilaya ya Kongwa Mkoani Dodoma wakiongozwa na Mkuu wa Wilaya hiyo, Mhe. Deo Ndejembi pamoja na baadhi ya viongozi wa vikundi vya vijana wilayani humo wamefanya ziara Mkoani Simiyu ili kujifunza namna vikundi vya vijana vinavyotekeleza miradi yake.

Timu hiyo imefanya ziara ya siku mbili hadi Juni 08, 2018  katika miradi inayotekelezwa na vijana kwa kushirikiana na Halmashauri ambayo ni Kiwanda cha Chaki,  Kiwanda cha kutengeneza bidhaa za ngozi wilayani Maswa na Mradi wa kiwanda cha kusindika maziwa wilayani Meatu.

Mkuu wa wilaya ya Kongwa amesema wameamua kuja Simiyu kwa kuwa vikundi vyake vimeonekana vikifanya vizuri katika miradi yake, hivyo wamewaleta vijana wao ili wapate uzoefu na ari itawasukuma kubuni miradi yao na kujua namna bora ya kuiendesha.

"Tumeona tuje tujifunze kutoka Simiyu maana mkoa wa Simiyu umeonesha mfano wa namna vikundi vya vijana vinavyotakiwa kutekeleza miradi yake, tumeona kwenye vyombo vya habari na kwingineko mkipata sifa nyingi kutokana na miradi yenu kuonesha matokeo, nia yetu vijana waje waone wajifunze wapate hasira ya kufanya kitu cha kwao" alisema Ndejembi.

Ndejembi amesema ni matamanio yake kuona vijana wa Kongwa wanaanzisha miradi ya viwanda kama ilivyo kwa Maswa na Meatu kwa kuwa wilaya hiyo ndiyo inayofanya vizuri katika kilimo na ufugaji Mkoani Dodoma ambapo uzalishaji wa malighafi ya viwanda hivyo uko vizuri pia.

Ameongeza kuwa baada ya ziara hiyo vijana wake wamejifunza hivyo watakapofika wilayani Kongwa wataenda kufanya miradi ambayo itakuwa ya mfano na endelevu kwa kuwa tayari wana wafadhili waliokubali kutoa fedha kwa ajili ya kuanzisha miradi hiyo.

Naye Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa, Dkt. Omary Nkullo amesema Halmashauri itahakikisha inatoa fedha kuwawezesha vijana kutekeleza miradi yao na itawasimamia ili waweze kufikia ndoto zao.

Akizungumza kwa niaba ya vijana kutoka Kongwa waliofika Simiyu kujifunza, Bw. Zamoyoni George amesema kuja kwao Simiyu hakutakuwa bure bali itakuwa chachu ya kuanzisha miradi endelevu na yenye tija ambayo hata vijana wa Simiyu wataenda kujifunza kwao.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Maswa, Mhe. Dkt. Seif Shekalaghe amewapongeza wilaya ya Kongwa kuona umuhimu wa kujifunza na kuwashauri kuwa fedha wakazozitoa kwa vijana kupitia asilimia tano za mapato ya Halmashauri, zielekezwe kutekeleza miradi ambayo italeta tija na kurejesha fedha za Halmashauri kwa wakati.

Aidha, Dkt. Shekalaghe amesema  Maswa itaendelea kuboresha ubora na biashara ya chaki (MASWA CHALKS)  na kuomba Wilaya ya Kongwa kuanza kununua Chaki za Maswa na kutumia katika shule zake, huku akisisitiza timu hiyo ya Kongwa pia kwenda kutangaza bidhaa za Ngozi zinazozalishwa Kijiji cha Senani wilayani humo.

Mkurugenzi wa Wilaya ya Meatu, Bw. Fabian Manoza akitoa maelezo juu ya  kiwanda cha maziwa amesema Halmashauri ina mpango wa kukipanua kiwanda hicho na Benki ya Maendeleo ya Kilimo imekubali kutoa mkopo wa shilingi bilioni 6 kwa ajili ya upanuzi wa kiwanda hicho na kuboresha teknolojia ya uzalishaji ili kifikie uwezo wa kuzalisha lita 15,000 kwa siku kutoka lita 800 za sasa.

Mkoa wa Simiyu ni mkoa uliojipambanua kama mkoa wa Viwanda kupitia Falsafa yake ya “Wilaya Moja Bidhaa Moja Kiwanda Kimoja” ambapo umedhamiria kujenga uchumi wa viwanda kwa kutumia malighafi yake inapatikana hapa nchini.

Mkuu wa Wilaya ya Maswa, Mhe. Dkt. Seif Shekalaghe (katikati)akitoa maelezo kwa Mkuu wa Wilaya ya Kongwa, Mhe. Deo Ndejembi na baadhi ya vijana kutoka Kongwa waliofika kutembelea kiwanda cha chaki wilayani humo, wakati wa ziara yao ya kutembelea miradi ya vijana Mkoani Simiyu kwa lengo la kujifunza.
Mkuu wa Wilaya ya Maswa, Mhe. Dkt. Seif Shekalaghe(kulia) akimuonesha  Mkuu wa Wilaya ya Kongwa, Mhe. Deo Ndejembi kiatu kilichotengenezwa na Kikundi cha Vijana Senani wilayani Maswa, wakati wa ziara ya Viongozi na Vijana wa Wilaya ya Kongwa kutembelea miradi ya vijana Mkoani Simiyu kwa lengo la kujifunza.
Mkuu wa Wilaya ya Kongwa, Mhe. Deo Ndejembi (kushoto) akiangalia chupa ya maziwa yanayosindikwa wilayani Meatu, baada ya kutembelea Kiwanda cha kusindika maziwa ‘Meatu Milk’ wakati wa Ziara yake na vijana wa Wilaya ya Kongwa ya kutembelea miradi ya vijana Mkoani Simiyu kwa lengo la kujifunza.
Mkurugenzi Mtendaji wa Wilaya ya Meatu, Bw. Fabian Manoza akimkabidhi Mkuu wa Wilaya ya Kongwa, Mhe. Deo Ndejembi zawadi ya maziwa, mara baada ya kutembelea Kiwanda cha Kusindika Maziwa wilayani humo,  wakati wa Ziara yake na vijana wa Wilaya ya Kongwa ya kutembelea miradi ya vijana Mkoani Simiyu kwa lengo la kujifunza.
Mmoja wa Vijana kutoka kikundi cha Maswa Family akitoa maelezo kwa Mkuu wa Wilaya ya Kongwa, Mhe. Deo Ndejembi na baadhi ya vijana kutoka Kongwa(wa tatu kulia) waliofika kutembelea kiwanda cha chaki wilayani humo, wakati wa ziara yao ya kutembelea miradi ya vijana Mkoani Simiyu kwa lengo la kujifunza
Mkuu wa Wilaya ya Kongwa, Mhe. Deo Ndejembi (wa pili kulia) akiuliza jambo wakati alipotembea eneo la kufungashia chaki wakati alipotembelea kiwanda cha chaki wilayani Maswa, wakati wa ziara yao ya kutembelea miradi ya vijana Mkoani Simiyu kwa lengo la kujifunza.
Mkuu wa Wilaya ya Kongwa, Mhe. Deo Ndejembi (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Maswa, Mhe. Dkt. Seif Shekalaghe(kushoto) na Mkuu wa Wilaya ya Meatu, Mhe.Dkt. Joseph Chilongani mara baada ya kumaliza ziara yake pamoja na viongozi wa Vijana wa wilaya ya Kongwa iliyokuwa na lengo la kutembelea miradi ya vijana Mkoani Simiyu kwa lengo la kujifunza.
Vijana kutoka Wilaya ya Kongwa wakipata maelezo ya hatua mbalimbali za utengenezaji wa viatu walipotembelea kiwanda cha kutengeneza bidhaa za ngozi kilichopo Kijiji cha  Senani wilayani Maswa, wakati wa ziara yao ya kutembelea miradi ya vijana Mkoani Simiyu kwa lengo la kujifunza, (kulia) Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Kongwa, Dkt. Omary Nkullo.
Mkuu wa Wilaya ya Kongwa, Mhe. Deo Ndejembi (kushoto) akizungumza na Viongozi wa Kikundi cha Vijana Senani wilayani Maswa (hawapo pichani) wakati wa ziara ya Viongozi na Vijana wa Wilaya ya Kongwa ya kutembelea miradi ya vijana Mkoani Simiyu kwa lengo la kujifunza.
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Meatu, Bw. Fabian Manoza(kulia) akitoa maelezo kwa Mkuu wa Wilaya ya Kongwa, Mhe. Deo Ndejembi(kushoto) na baadhi ya vijana kutoka Kongwa waliofika kutembelea kiwanda cha maziwa(Meatu Milk) wilayani humo, wakati wa ziara yao ya kutembelea miradi ya vijana Mkoani Simiyu kwa lengo la kujifunza.
Vijana kutoka Wilaya ya Kongwa wakipata maelezo ya hatua mbalimbali za utengenezaji wa viatu walipotembelea kiwanda cha kutengeneza bidhaa za ngozi kilichopo Kijiji cha  Senani wilayani Maswa, wakati wa ziara yao ya kutembelea miradi ya vijana Mkoani Simiyu kwa lengo la kujifunza, (wa pili kulia) Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Kongwa, Dkt. Omary Nkullo.
Mkuu wa Wilaya ya Kongwa, Mhe. Deo Ndejembi (wa pili kushoto) akizungumza na Mkuu wa Wilaya ya Meatu, Mhe. Dkt. Joseph Chilongani (kulia) wakati wa Ziara yake na vijana wa Wilaya ya Kongwa ya kutembelea miradi ya vijana Mkoani Simiyu kwa lengo la kujifunza.

Thursday, June 7, 2018

MKUU WA MAJESHI AHAMASISHA VIJANA KUJIUNGA JKT KUPATA STADI ZA KAZI ZIWASAIDIE KUJIAJIRI


Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi  Jenerali Venance Mabeyo amewahamasisha vijana kujiunga na Jeshi la Kujenga Taifa ili waweze kupata stadi za ufundi na hatimaye wajiajiri badala ya kutegemea kuajiriwa na Serikali.

Jenerali Mabeyo ametoa ushauri huo wakati alipokutana na Mkuu wa Mkoa wa Simiyu na Wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Simiyu mjini Bariadi Juni 07, 2018.
Mabeyo amesema vyombo vya habari vinapaswa kuwahamasisha vijana kujiunga na Jeshi la Kujenga Taifa ili waweze kupata stadi za ufundi na hatimaye wajiajiri na hivyo waondokane na dhana ya kuajiriwa  .

“Vijana tunaowachukua JKT ni kwa ajili ya kuwapa elimu na stadi za kazi ili hata kijana akikosa nafasi katika vyombo vya Ulinzi na Usalama anaweza kurudi kijijini akafanya vitu vya maendeleo, mimi nadhani watu wanahamasishana vibaya kuwa kila anayekwenda JKT lazima aajiriwe,  ipo haja ya kubadili mtazamo” alisema Jenerali Mabeyo

“Jeshi linachukua vijana elfu ishirini kwa mafunzo, wanaochukuliwa na vyombo vya ulinzi na usalama hawazidi vijana 2000 sasa hawa wengine 18,000 wanaenda wapi, kama mawazo yatakuwa ni kwenda JKT ili kuajiriwa hatutafanikiwa lakini kama watakwenda JKT kujifunza stadi za kazi kuwasaidia ili ziwasaidie kujiajiri na kubadili maisha yao tutafanikiwa sana” alisisitiza

Katika hatua nyingine Jenerali Mabeyo ametoa pongezi kwa  juhudi zinazofanywa na Mkoa wa Simiyu katika mkakati wa Kilimo cha Umwagiliaji ili kuwa na ziada ya chakula cha kutosha.

“Suala la umwagiliaji halikuwepo katika fikra za watu wengi, walio wengi wanategemea mvua na isiponyesha hawalimi na  maisha yanakuwa duni  wanaanza kuilalamikia Serikali, lakini sisi hapa tunayo maji ya Ziwa Victoria, Mkuu wa Mkoa nawapongeza sana kwa juhudi zinazofanywa katika kilimo cha Umwagiliaji, zitasaidia kuwatoa wananchi kwenye ufukara” amesema  Mabeyo.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Anthony Mtaka amesema mkoa huo umeweka malengo ya kujitosheleza kwa chakula na kupitia mkakati wa kuwa na mradi wa kilimo cha umwagiliaji katika bonde la Mwamanyili wilayani Busega, ambapo amebainisha kuwa Benki ya Maendeleo ya Kilimo imeahidi kutoa shilingi bilioni 12kwa ajili ya mradi huo.

“ Lengo letu kama mkoa ni kuifanya wilaya ya Busega kuwa eneo ambalo linafanya vizuri katika kilimo cha umwagiliaji kwa kuwa lina maji ya uhakika ya Ziwa Victoria, Benki ya Kilimo wameahidi kutupa shilingi bilioni 12 kwa ajili ya mradi wa Kilimo cha Umwagiliaji wa Mwamanyil” alisema Mtaka.

Akizungumzia suala la elimu Mtaka amesema mkoa huo umejipanga kiushindani ambapo madarasa ya mitihani. yatakuwa na makambi ya kitaaluma  ambazo zitawakutanisha wanafunzi kwa ajili ya kupitia maeneo yaliyo magumu ili waweze kujiandaa na mitihani ya Kitaifa.
Mkuu wa Majeshi nchini, Jenerali Venance Mabeyo akizungumza na Viongozi wa Mkoa wa Simiyu wakati alipomtembelea Mkuu wa Mkoa huo, Mhe. Anthony Mtaka Ofisini kwake Juni 07, Mjini Bariadi.


Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka  akitoa taarifa fupi ya mkoa kwa Mkuu wa Majeshi hapa nchini Jenerali Venance Mabeyo (kulia)  wakati alipomtembelea ofisini kwakeJuni 07, 2018 Mjini Bariadi na kuzungumza na Kamati ya Ulinzi n aUsalama ya Mkoa.

Baadhi ya Wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Simiyu na baadhi ya maafisa wa Jeshi  walioongozana na Mkuu wa Majeshi hapa Nchini wakati alipomtembelea Mkuu wa mkoa wa   Simiyu, wakimsikiliza Mkuu huyo majeshi Mjini Bariadi alipozungumza na viongozi wa mkoa wa Simiyu.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka  akimtambulisha Mkuu wa Majeshi hapa nchini Jenerali Venance Mabeyo viongozi mbalimbali wa mkoa huo waliofika kumpokea mara baada ya kuwasili mjini Bariadi Juni 07, 2018.
Mkuu wa Majeshi hapa nchini Jenerali Venance Mabeyo akisalimiana na Mkuu wa Wilaya ya Bariadi Mhe. Festo Kiswaga mara baada ya kuwasili Mjini Bariadi wakati alipomtembelea Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka Juni 07, 2018.
Mkuu wa Majeshi hapa nchini Jenerali Venance Mabeyo akisaini kitabu cha wageni katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, mara baada ya kuwasili Mjini Bariadi  Mkoani Simiyu Juni 07, 2018,(kulia) Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka.


Mkuu wa Majeshi hapa nchini Jenerali Venance Mabeyo ( wa nne kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa Mkoa wa Simiyu mara baada ya kumaliza mazungumzo  na viongozi hao  Mjini Bariadi, ,Juni 07, 2018.
Baadhi ya Wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Simiyu na baadhi ya maafisa wa Jeshi  walioongozana na Mkuu wa Majeshi hapa Nchini wakati alipomtembelea Mkuu wa Mkoa huo Mhe.Anthony Mtaka  Mjini Bariadi, wakimsikiliza Mkuu huyo majeshi Bariadi alipozungumza na viongozi wa mkoa wa Simiyu.
Kutoka kushoto Mkuu wa Wilaya ya Bariadi Mhe. Festo Kiswaga, Mkuu wa Majeshi hapa nchini Jenerali Venance Mabeyo na Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka  wakifurahia jambo wakati Mkuu huyo wa Majeshi alipomaliza kuzungumza na viongozi wa Mkoa huo Mjini Bariadi Juni 07, 2018.
Mkuu wa Majeshi hapa nchini Jenerali Venance Mabeyo akisalimiana na Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Simiyu, ACP  Boniventure Mushongi mara baada ya kuwasili Mjini Bariadi  Mkoani Simiyu Juni 07, 2018.

Mkuu wa Majeshi hapa nchini Jenerali Venance Mabeyo (kushoto) na Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka  wakiteta jambo baada ya Mkuu huyo wa Majeshi kuzungumza na viongozi Mkoani humo Juni 07, 2018.

Monday, June 4, 2018

WAGANGA WAFAWIDHI WATAKAOSHINDWA KUSIMAMIA VITUO VYAO KUVULIWA MADARAKA

Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu Jumanne Sagini amewaagiza Waganga Wakuu wa Wilaya kuwaondoa katika nafasi za usimamizi wa zahanati na vituo vya afya ,waganga wafawidhi watakaoshindwa kusimamia vituo vyao kufika vigezo vilivyowekwa katika utoaji huduma za afya kwa wananchi kupitia mpango wa malipo kwa ufanisi (RBF).

Agizo hilo amelitoa wakati wa kikao chake na Wakurugenzi wa Halmashauri, Waganga Wakuu wa wilaya, Timu ya Usimamizi wa Huduma za Afya Mkoa(RHMT), waganga wafawidhi wa zahanati na vituo vya afya lengo likiwa ni kujadili matokeo ya Mpango wa Malipo kwa ufanisi (RBF) kwa kipindi cha Mwezi Januari-Machi 2018 na masuala mbalimbali yahusuyo Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya ikiwepo Mfuko wa Afya ya Jamii ulioboreshwa.

“Waganga na Wauguzi wafawidhi tumewaita hapa tunataka mabadiliko kwenye utendaji wenu, vituo vyenu wote viende kwenye Alama A, kinyume na hapo Waganga Wakuu wa Wilaya wawavue madaraka na Waganga wakuu wa Wilaya wasipofanya  hivyo Wakurugenzi washughulikieni wao” alisema Sagini.

Amesema kutotekeleza majukumu yao vizuri ikiwa ni pamoja na kushindwa kusimamia suala la ujazwaji wa  takwimu sahihi kwa wakati,  kunasababisha Vituo vyao kutopata fedha za mpango huo (RBF)  ambazo hutolewa kwa vituo vinavyofanya vizuri,  ambapo vituo hivyo vikizipata zitasaidia kuboresha miundombinu ya Afya na ununuzi wa dawa na vifaa tiba.

Ameongeza kuwa  Timu za Usimamizi wa Huduma za Afya Wilaya (CHMT) zinapaswa kufanya ufuatiliaji na usimamizi katika Vituo vya kutolea huduma na kuhakikisha mapungufu yote yanayojitokeza yanafanyiwa kazi ili vituo vyote vitoe huduma kwa ufanisi na kupata fedha kulingana mwongozo wa Mpango wa RBF ambazo zitasaidia kuboresha huduma kwenye vituo.

Katika hatua nyingine Sagini amewataka Waganga wakuu wa Wilaya na Waganga Wafawidhi wa Vituo vya kutolea huduma za Afya kuwasilisha taarifa za wagonjwa wanaopata huduma kupitia Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya  kwa wakati kama maelekezo yanavyowataka kufanya ili kuondoa usumbufu usio wa lazima.

Nao Wasimamizi wa Vituo baada ya maelekezo ya Katibu Tawala wa Mkoa wamekiri kuwa watabadilika na kuhakikisha vituo vyao vinafanya vizuri na kufikia alama A ili kuwawezesha kupata fedha kupitia Mpango wa Malipo kwa Ufanisi(RBF) zitakazowasaidia kuboresha huduma za afya katika vituo vyao.

“ Nimesikitishwa sana na Halmashauri yetu kukosa fedha za RBF kiasi kilichotajwa na mratibu kwa sababu ya baadhi ya watendaji kutotimiza wajibu wao, mimi ninaona haya yote yako ndani ya uwezo wetu, kuanzia sasa tunapaswa kutimiza wajibu wetu na tuhakikishe taarifa zote zinazopelekwa wilayani zinajazwa kwa usahihi na kwa wakati” alisema Godfrey Pascal kutoka Zahanati ya Nkololo.

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Meatu, Bw.Fabian Manoza amesema ipo haja ya kuwajengea uwezo na kutoa mafunzo ya menejimenti ya takwimu  kwa wasimamizi wa vituo vya kutolea huduma za Afya, ili waweze  kukusanya takwimu zinazotakiwa kwa mujibu wa mwongozo wa Mpango wa RBF hatimaye vituo vyao vipate alama nzuri na fedha zitazowasaidia kuboresha huduma.

Kwa upande wake Meneja wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya Mkoa wa Simiyu Jarlath Mushashu ameziomba Halmashauri zote Mkoani Simiyu kulipa deni ambalo Mfuko huo unazidai lililofikia shilingi milioni 78, ili kuuwezesha mfuko huo kutoa huduma za matibabu kwa wanachama na wategemezi wao kama inavyotakiwa.

Wakati huo huo Mushashu amewaomba Wakurugenzi wa Halmashauri kuwasilisha kwa wakati michango ya watumishi ya Bima ya Afya hususani watumishi wanaolipwa kwa kutumia mapato ya ndani ya Halmashauri.
MWISHO
Katibu Tawala Mkoa wa Simiyu, Bw.Jumanne Sagini akifungua kikao kazi cha Viongozi na Watendaji wa Idara ya Afya Mkoani humo chenye lengo la kujadili matokeo ya Mpango wa Malipo kwa ufanisi (RBF) kwa kipindi cha Mwezi Januari-Machi 2018 na masuala mbalimbali yahusuyo Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya ikiwepo Mfuko wa Afya ya Jamii ulioboreshwa.
 Meneja wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya Mkoa wa Simiyu Jarlath Mushashu akiwasilisha taarifa ya Mfuko huo katika kikao kazi cha Viongozi na Watendaji wa Idara ya Afya Mkoani humo chenye lengo la kujadili matokeo ya Mpango wa Malipo kwa ufanisi (RBF) kwa kipindi cha Mwezi Januari-Machi 2018 na masuala mbalimbali yahusuyo Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya ikiwepo Mfuko wa Afya ya Jamii ulioboreshwa. 

Mratibu wa Mpango wa Malipo kwa Ufanisi, Mkoa wa Simiyu Bw.Oscar Tenganamba akiwasilisha taarifa ya mpango huo katika kikao kazi cha Viongozi na Watendaji wa Idara ya Afya Mkoani humo chenye lengo la kujadili matokeo ya Mpango wa Malipo kwa ufanisi (RBF) kwa kipindi cha Mwezi Januari-Machi 2018 na masuala mbalimbali yahusuyo Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya ikiwepo Mfuko wa Afya ya Jamii ulioboreshwa. 

Katibu Tawala Mkoa akimkabidhi Muuguzi Mfawidhi wa Zahanati ya Nyangokolwa, Bi. Nuriath Mtumbi  Mjini Bariadi, fedha taslimu kiasi cha shilingi 185,000/= zilizotolewa na wajumbe wa kikao cha Viongozi na Watendaji wa Idara ya Afya Mkoani humo chenye lengo la kujadili matokeo ya Mpango wa Malipo kwa ufanisi (RBF) kwa kipindi cha Mwezi Januari-Machi 2018 na masuala mbalimbali yahusuyo Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya, kumpongeza kwa usimamizi mzuri wa kituo chake.
Baadhi ya Viongozi na Watendaji wa Idara ya Afya Mkoani Simiyuwakimsikiliza Katibu Tawla wa Mkoa wa Simiyu, Bw.Jumanne Sagini katika kikao kilicholenga kujadili matokeo ya Mpango wa Malipo kwa ufanisi (RBF) kwa kipindi cha Mwezi Januari-Machi 2018 na masuala mbalimbali yahusuyo Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya ikiwepo Mfuko wa Afya ya Jamii ulioboreshwa. 


Baadhi ya Viongozi na Watendaji wa Idara ya Afya Mkoani Simiyuwakimsikiliza Katibu Tawla wa Mkoa wa Simiyu, Bw.Jumanne Sagini katika kikao kilicholenga kujadili matokeo ya Mpango wa Malipo kwa ufanisi (RBF) kwa kipindi cha Mwezi Januari-Machi 2018 na masuala mbalimbali yahusuyo Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya ikiwepo Mfuko wa Afya ya Jamii ulioboreshwa.
Mganga Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Dkt.Mageda Kihulya  akizungumza Viongozi na Watendaji wa Idara ya Afya Mkoani humo katika kikao kilicholengakujadili matokeo ya Mpango wa Malipo kwa ufanisi (RBF) kwa kipindi cha Mwezi Januari-Machi 2018 na masuala mbalimbali yahusuyo Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya ikiwepo Mfuko wa Afya ya Jamii ulioboreshwa.
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Itilima, Bw. Mariano Mwanyigu akichangia hoja katika kikao kazi cha Viongozi na Watendaji wa Idara ya Afya Mkoani Simiyu chenye lengo la kujadili matokeo ya Mpango wa Malipo kwa ufanisi (RBF) kwa kipindi cha Mwezi Januari-Machi 2018 na masuala mbalimbali yahusuyo Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya ikiwepo Mfuko wa Afya ya Jamii ulioboreshwa.
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Meatu, Bw. Fabian Manoza akichangia hoja katika kikao kazi cha Viongozi na Watendaji wa Idara ya Afya Mkoani Simiyu chenye lengo la kujadili matokeo ya Mpango wa Malipo kwa ufanisi (RBF) kwa kipindi cha Mwezi Januari-Machi 2018 na masuala mbalimbali yahusuyo Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya ikiwepo Mfuko wa Afya ya Jamii ulioboreshwa. 
Mganga Mfawidhi wa Kituo cha kutolea huduma za Afya akichangia hoja katika kikao kazi cha Viongozi na Watendaji wa Idara ya Afya Mkoani Simiyu chenye lengo la kujadili matokeo ya Mpango wa Malipo kwa ufanisi (RBF) kwa kipindi cha Mwezi Januari-Machi 2018 na masuala mbalimbali yahusuyo Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya ikiwepo Mfuko wa Afya ya Jamii ulioboreshwa.
 Mkaguzi Mkuu wa ndani Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Bw.Mika Mollel akichangia hoja katika kikao kazi cha Viongozi na Watendaji wa Idara ya Afya Mkoani humo, chenye lengo la kujadili matokeo ya Mpango wa Malipo kwa ufanisi (RBF) kwa kipindi cha Mwezi Januari-Machi 2018 na masuala mbalimbali yahusuyo Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya ikiwepo Mfuko wa Afya ya Jamii ulioboreshwa. 
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Busega, Bw. Anderson Njiginya akichangia hoja katika kikao kazi cha Viongozi na Watendaji wa Idara ya Afya Mkoani Simiyu chenye lengo la kujadili matokeo ya Mpango wa Malipo kwa ufanisi (RBF) kwa kipindi cha Mwezi Januari-Machi 2018 na masuala mbalimbali yahusuyo Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya ikiwepo Mfuko wa Afya ya Jamii ulioboreshwa.

SIMIYU YAKABIDHIWA ZAHANATI NA SHIRIKA LA LIFE MINISTRY


Shirika la Kikristo la Life Ministry limekabidhi Zahanati kwa Uongozi wa Mkoa wa Simiyu ambayo imejengwa katika Kijiji cha Itubukilo wilayani Bariadi.

Akisoma taarifa ya makabidhiano ya zahanati hiyo mbele ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka, Mkurugenzi wa Life Ministry Tanzania, Bw. Dismas Shekalaghe amesema shirika hilo lilipokea zahanati hiyo kutoka kwa wananchi ambao walianza kujenga kwa nguvu zao na kuifikisha hatua ya renta, hadi kufikia hatua za ukamilishaji wa zahanati hiyo Shirika la Life Ministry limetoa kiasi cha Shilingi milioni 71.

Amesema pamoja na zahanati hiyo, shirika hilo limefanya mengi mkoani Simiyu ikiwa ni apamoja na kutoa vifaa tiba Hospitali Teule ya Mkoa vyenye thamani ya shilingi milioni 40, huduma za macho na kutoa miwani bure, kutoa baiskeli zaidi ya 20 kwa walemavu, kugawa vifaa mbalimbali kwa makundi mbalimbali wakiwemo watoto wenye ualbino, kuwezesha vikundi vya bustani zaidi ya 40 katika kilimo cha umwagiliaji kwa njia ya matone na kuchimba visima virefu 12 vyenye thamani ya shilingi milioni 300.

Akizungumza mara baada ya makabidhiano hayo, Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka ameishukuru Life Ministry kwa msaada wa zahanati hiyo na kuwahakikishia kuwa mara tu itakapokamilika Serikali itahakikisha Zahanati hiyo inafanya kazi na itapeleka watoa huduma za afya ili wananchi waanze kupata huduma.

"Niwakikishie tu kuwa Serikali itahakikisha Zahanati hii inafanya kazi kwa kuleta wataalam na bahati nzuri Serikali imekubali kuajiri watu wa Sekta ya Afya" alisema Mtaka.

Mtaka amesema Taasisi za Dini zimekuwa zikiunga mkono kazi mbalimbali zinazofanywa na Serikali katika kuwaletea wananchi maendeleo na akaiomba Life Ministry kuendelea kusaidia katika ujenzi wa Vituo vya kutolea huduma za Afya, ili kusaidia uboreshaji wa huduma za Afya mkoani Simiyu, kwa kuwa mkoa huo una uhitaji  mkubwa wa vituo vya afya.

" Mkoa wetu tuna asilimia chini ya 40 ya vituo vya Afya, Kama ni jambo ambalo litakuwa ndani ya uwezo wa Taasisi ningeomba muendelee kutusaidia kwenye sekta ya Afya; zipo juhudi za Serikali katika uimarishaji wa sekta ya Afya hususani kwenye ujenzi wa Zahanati, Vituo vya Afya na Hospitali lakini washirika kama Taasisi za Dini bado tunawahitaji kwa kuwa mmekuwa mkono wa pili kwenye kuunga mkono juhudi za Serikali" alisisitiza.

Akizungumza kwa niaba ya Wananchi wa Itubukilo, Diwani wa Kata ya Itubukilo Mhe. Mayanda Makenzi akiishuku Life Ministry kwa kukamilisha ujenzi wa zahanati hiyo ambayo amesema itawaondolea adha wananchi wake kutembea mwendo mrefu kufuata huduma za Afya.

Naye Diwani wa Viti Maalum Mhe. Juliana Lucas amesema ukamilishaji wa zahanati hiyo utawasaidia sana wananchi kupata huduma karibu hususani wanawake ambao watapata huduma za afya ya uzazi na kupata msaada wa karibu wakati wa kujifungua na hivyo kupunguza vifo vya wakina mama na watoto.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi, Bw. Abdallah Malela amesema Zahanati hiyo ya Itubukilo itafunguliwa rasmi na kuanza kutoa huduma Julai Mosi, 2018.

MWISHO


Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka akikata utepe kuashiria kupokea Zahanati iliyojengwa na Shirika la Life Ministry katika Kijiji cha Itubukilo Wilayani Bariadi  ambayo ilikabidhiwa rasmi kwa Serikali na Shirika hilo Juni 03, 2018.
Mkuu wa Mkoawa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka akifurahia jambo na Viongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi, Viongozi wa Life Ministry naViongozi wa madhehebu ya Kikristo baada ya makabidhiano ya Zahanati ya Itubukilo kati ya Serikali na Shirika la Life Ministry ambayo imejengwa na Shilika hilo, Juni 03, 2018. 
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka(wa pili kulia) akiteta jambo na Mkurugenzi wa Life Ministry Tanzania, Bw. Dismas Shekalaghe(kushoto) na Mwenyekiti wa Bodi ya Life Ministry Tanzania, Mhandisi. Kapuulya Musomba (katikati) wakati wa hafla ya makabidhiano ya Zahanati iliyojengwa na Shirika hilo katika Kijiji cha Itubukilo wilayani Bariadi.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka na baadhi ya viongozi wa madhehebu ya dini ya Kikristo wakitoka kukagua jengo la Zahanati iliyojengwa na Shirika la Life Ministry Tanzania katika Kijiji cha Itubukilo wilayani Bariadi ambayo ilikqbidhiwarasmi Juni 03, 2018 kwa Serikali ya Mkoa.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Utubukilo wilayani Bariadi wakati wa hafla ya makabidhiano ya Zahanati iiliyojengwa na Life Ministry Tanzania Juni 03, 2018.
Mkurugenzi wa Life Ministry Tanzania, Bw. Dismas Shekalaghe(kushoto) akiwasilisha taarifa ya ujenzi wa Zahanati ya Itubukilo ambayo imejengwa na shirika hilo la Kikristo na kukabidhiwa kwa Serikali Juni 03, 2018.
Diwani wa Kata ya Itubukilo, Mhe. Mayanda Makenzi akizungumza na wananchi Kijiji cha Utubukilo wilayani Bariadi wakati wa hafla ya makabidhiano ya Zahanati iliyojengwa na Life Ministry Tanzania Juni 03, 2018.
Kutoka kushoto Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, mheAnthony Mtaka, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi, Bw. Abdallah Malela na Katibu wa CCM Wilaya ya Bariadi wakiteta jambo wakati wa makabidhiano ya Zahanati ya Itubukilo na Shrika la Life Ministry.
Viongozi wa Shirika la Life Ministry na viongozi wa Chama na Serikali wa Wilaya ya Bariadi na Mkoa wa Simiyu wakiwa katika picha ya Pamoja mara baada ya hafla ya makabidhiano ya Zahanati katika Shirika Hilo na Serikali ambayo imejengwa katika Kata ya Itubukilo Wilayani Bariadi.
Baadhi ya viongozi wa madhehebu ya Kikristo na wataalam wa Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi, wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka wakati akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Itubukilo katika hafla ya makabidhiano ya Zahanati iliyojengwa na Shirika la Life Ministry Juni 03, 2018.
Diwani wa Viti Maalum, Mhe. Juliana Lucas akimkabidhi  Mwenyekiti wa Bodi ya Life Ministry Tanzania, Mhandisi. Kapuulya Musomba zawadi ya Kitenge kwa niaba ya waananchi wa Itubukilo kama ishara ya kumshukuru kwa kuruhusu Shirika hilo Kujenga Zahanati ya Itubukilo wilayani Bariadi katika hafla ya makabidhiano ya Zahanati hiyo.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka(kushoto) akiteta jambo na Mkurugenzi wa Life Ministry Tanzania, Bw. Dismas Shekalaghe(kulia) na Mwenyekiti wa Bodi ya Life Ministry Tanzania, Mhandisi. Kapuulya Musomba (katikati) baada ya hafla ya makabidhiano ya Zahanati iliyojengwa na Shirika hilo katika Kijiji cha Itubukilo wilayani Bariadi, Juni 03, 2018.
Diwani wa Viti Maalum, Mhe. Juliana Lucas akimkabidhi  Mkuu wa Mkoa wa Simiyu. Mhe. Anthony  Mtaka zawadi ya Kitenge kwa niaba ya wananchi wa Itubukilo kama ishara ya kumshukuru kwa namna anavyopigania maendeleo ya wananchi wake  wakati wa makabidhiano ya Zahanati ya Itubukilo wilayani Bariadi iliyojengwa na Shirika la Kikristo la Life Ministry.
Baadhi ya viongozi wa madhehebu ya Kikristo, wataalam wa Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi na Wajumbe kutoka Shirika la Life Ministry wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka wakati akizungumza na wananchi wa Kijiji chaItubukilo katika hafla ya makabidhiano ya Zahanati iliyojengwa na Shirika la Life Ministry Juni 03, 2018. 

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!