Thursday, February 28, 2019

NAIBU WAZIRI IKUPA AWAOMBA WADAU KUWASAIDIA WALEMAVU VIFAA SAIDIZI


Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu nayeshughulikia watu wenye ulemavu, Mhe. Stella Ikupa ametoa wito kwa wadau kuendelea kutoa msaada wa vifaa saidizi kwa watu wenye ulemavu kwa kuwa hili ni hitaji endelevu kwa watu hao.

Mhe. Ikupa ameyasema hayo jana Februari 27, 2019 wakati akizungumza na viongozi na watendaji wa Serikali wilayani Busega mkoani Simiyu wakati akiwa katika ziara yake ya kikazi wilayani humo.

Amewashukuru viongozi wa Wilaya ya Busega kwa namna inavyowasaidia watu wenye ulemavu katika kuwapatia vifaa saidizi huku akibainisha kuwa Serikali inaendelea kufanya jitihada za kuwatafutia na kuwapatia watu wenye ulemavu vifaa hivyo kwa kadri vitakavyopatikana.

“Napenda kuwashukuru viongozi wa Busega kwa namna wanavyowasaidia watu wenye ulemavu kupata vifaa saidizi kama fimbo nyeupe kwa wasioona, baiskeli na viungo bandia kwa walemavu wa viungo, mafuta kwa wenye ualbino, lakini niwaombe wadau waendelee kuwasaidia kwa kuwa hili ni hitaji endelevu katika kuishi kwao.” alisema Mhe. Ikupa.

Katika hatua nyingine Mhe. Naibu Waziri amesisitiza Kamati za watu wenye ulemavu kupewa miongozo ya namna ya kuziendesha kamati hizo, ili ziweze kutimiza majukumu yake ipasavyo na kuzitaka kutoa taarifa kuhusu fursa na masuala mbalimbali yanayowahusu walemavu katika maeneo yao.

Vile vile Mhe. Ikupa amesema Serikali inatarajia kuanzisha mfuko wa watu wenye ulemavu ambao utakuwa ukishughulikia masuala mbalimbali ya watu wenye ulemavu ikiwa ni pamoja na kutoa ruzuku kwa vyama vya walemavu.

Akitoa taarifa Mkuu wa Wilaya ya Busega, Mhe. Tano Mwera, amesema Serikali wilayani imetoa baiskeli 17 kwa watu wenye ulemavu wa viungo, zaidi ya fimbo nyeupe 50 kwa wasioona, mafuta kwa watu wenye ualbino na Halmashauri imeandaa mpango maalum wa Mfuko wa Bima ya Afya(CHF) iliyoboreshwa kwa ajili ya huduma za afya kwa walemavu.

Kwa upande wao watu wenye ulemavu wameiomba Serikali na wadau kuendelea kuwapa msaada wa vifaa saidizi , kupewa elimu ya kuunda vikundi na kuandaa maandiko ya miradi na kutoa semina elekezi kwa kamati za watu wenye ulemavu.

“Mahitaji ya walemavu bado ni makubwa tunaomba wadau mbalimbali waendelee kutukumbuka kutupa msaada wa vifaa saidizi kama fimbo nyeupe kwa wasioona, viungo bandia na baiskeli kwa walemavu wa viungo lakini na mafuta kwa wenzetu wenye ualbino” alisema Katibu wa  SHIVYAWATA Wilaya ya Busega, Makasi Egonjo.

“Tunaishukuru Serikali kwa kutusaidia kwenye mahitaji yetu mengi lakini tunaendelea kuomba wasichoke kutusaidia, tunaomba maafisa ustawi wa jamii wawafikie watu wenye ulemavu mpaka waliopo vijijini ili tuwe na elimu kuhusu mambo yanayotuhusu na fursa za mikopo na ujasiriamali” alisema Mwenyekiti wa Chama cha Wasioona, John Daniel

Naye Mwakilishi wa Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga amemhakikishia Naiba waziri Ikupa kuwa Mkoa wa Simiyu utaendelea kufanyia kazi maelekezo yote yaliyotolewa katika ziara yake na kuhakikisha walemavu wanashirikishwa na kufikiwa katika fursa mbalimbali.

Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia walemavu, Mhe. Stella Ikupa amehitimisha ziara yake ya siku tatu mkoani Simiyu Febrauari 27, 2019 ambapo alipata nafasi ya kuzungumza na  viongozi wa serikali, watu wenye ulemavu na kukagua mradi wa kitalu nyumba katika Halmashauri zote sita za Mkoa wa Simiyu.
MWISHO
Katibu wa  Shirikisho la Vyama vya Watu wenye ulemavu (SHIVYAWTA) Wilaya ya Busega, Makasi Egonjo akiwasilisha taarifa ya watu wenye ulemavu kwa Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia walemavu, Mhe. Stella Ikupa, wakati wa ziara yake Wilayani humo Februari 27, 2019
Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia walemavu, Mhe. Stella Ikupa, akizungumza na viongozi wa Serikali na watu wenye ulemavu  wilayani Busega, wakati wa ziara yake Wilayani humo Februari 27, 2019.
 Mwenyekiti wa Chama cha Wasioona, John Daniel akiwasilisha hoja kwa Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia walemavu, Mhe. Stella Ikupa, wakati wa ziara yake Wilayani humo Februari 27, 2019. 
Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia walemavu, Mhe. Stella Ikupa, akizungumza jambo na viongozi wa Serikali na watu wenye ulemavu  wilayani Busega, wakati wa ziara yake Wilayani humo Februari 27, 2019.
 Mwakilishi wa Mkuu wa mkoa wa Simiyu, Mhe. Athony Mtaka ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga akizungumza na viongozi na watu wenye ulemavu wilayani Busega, wakati wa ziara ya Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia walemavu, Mhe. Stella Ikupa, Wilayani humo Februari 27, 2019.
Mkuu wa Wilaya ya Busega, Mhe. Tano Mwera akiwasilisha taarifa ya wilaya kwa Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia walemavu, Mhe. Stella Ikupa, wakati wa ziara yake Wilayani humo Februari 27, 2019.
 Baadhi ya Wakuu wa Idara wa Halmashauri ya Wilaya ya Busega wakifuatilia kati ya viongozi wa watendaji wa wilaya hiyo, watu wenye ulemavu na Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia walemavu, Mhe. Stella Ikupa, wakati wa ziara yake Wilayani humo Februari 27, 2019.




Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia walemavu, Mhe. Stella Ikupa akiwaaga baadhi ya viongozi na watendaji wa serikali pamoja na watu wenye ulemavu wilayani Busega(baadhi hawapo pichani) mara baada ya kukamilisha ziara yake wilayani humo,  Februari 27, 2019




Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia walemavu, Mhe. Stella Ikupa(wa pili kushoto) alipotembelea Ofisi za CCM Wilaya, wakati wa ziara yake ya kikazi wilayani humo, Februari 27, 2019.
Baadhi ya viongozi na watendaji wa serikali pamoja na watu wenye ulemavu wilayani Busega wakimsikiliza Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia walemavu, Mhe. Stella Ikupa, wakati alipotembelea Kitalu nyumba katika ziara yake wilayani humo Februari 27, 2019.

DC BARIADI: WALEMAVU WATASHIRIKISHWA KATIKA FURSA ZOTE ZA KIUCHUMI

Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga amesema Serikali wilayani humo itaendelea kuhakikisha watu wenye ulemavu wanashirikishwa katika fursa za kiuchumi ili waweze kujikwamua kiuchumi na kuondokana na utegemezi.


Kiswaga ameyasema hayo wakati wa ziara ya Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia watu wenye Ulemavu, Mhe. Stella Ikupa Wilayani Bariadi, ambayo ililenga kujionea utekelezaji wa mradi wa kitalu nyumba na masuala mbalimbali ya watu wenye ulemavu.

Amesema katika mradi wa kitalu nyumba ambao utahusisha vijana 100 atahakikisha vijana wenye ulemavu wanashirikishwa kupata elimu ya ujenzi wa kitalu nyumba na kilimo cha kisasa chenye tija kupitia mradi huo ili waweze kujiajiri na kujipatia kipato.

Aidha, katika mradi wa ushonaji unaotarajiwa kuanza kutekelezwa hivi karibuni katika Halmashauri ya Mji wa Bariadi  atakahikisha sehemu ya washiriki katika miradi huo ni watu wenye ulemavu.

“Tunatarajia kuanza mradi wa ushonaji hapa Bariadi Mjini na tayari tuna vyerehani 50 kwa  hiyo tutahakikisha watu wenye ulemavu wamejumuishwa ili nao wanufaike na mradi huu ambao utawasaidia wananchi kupata kipato na Halmashauri kupata chanzo cha mapato pia” alisema Kiswaga.

Kwa upande wao watu wenye ulemavu pamoja na kuishukuru serikali kwa kushughulikia  changamoto zinazowakabili wameomba Serikali kuendelea kuboresha mazingira ya kujifunzia kwa watu wenye ulemavu na kuongeza walimu wa elimu maalum.

Vile vile wameomba watu wenye ulemavu wapewe kipaumbele katika suala la ajira na mafunzo mbalimbali yakiwepo ya Jeshi la Kujenga Taifa ili nao wawe sehemu ya kutegemewa katika jamii badala ya kuwa tegemezi.

“Tunaishukuru Serikali kutusaidia kutatua changamoto mbalimbali lakini tunaendelea kuiomba iboreshe mazingira ya kujifunzia kwa watoto wenye ulemavu kwa kuongeza madarasa na wataalam wa lugha ya alama, ili nao wapate haki yao ya msingi ya elimu bora”alisema Alex Benedicto Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Wasiosikia

Akijibu baadhi ya changamoto za watu wenye ulemavu, Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia watu wenye Ulemavu, Mhe. Stella Ikupa amesema Serikali imeendelea kuajiri watu wenye ulemavu katika kada mbalimbali huku akitoa wito kwa Halmashauri kuweka mikakati ya kutafuta wataalam wa lugha ya alama ili waweze kuwasaidia walemavu wasiosikia kuwasiliana.

Kuhusu miundombinu Mhe. Ikupa ametoa wito kwa taasisi zinazoendelea kujenga majengo zizingatie ujenzi wa miundombinu rafiki kwa watu wenye ulemavu na kwa upande wa majengo ya zamani taasisi zione namna ya kufanya marekebisho madogo ili ziweze kufikika kirahisi na watu enye ulemavu katika kupata huduma.

Naibu Waziri Stella Ikupa akiwa wilayani Bariadi amezungumza na viongozi wa Serikali na watu wenye ulemavu pamoja na kutembelea mradi wa Kitalu nyumba ili kujionea utekelezaji.

MWISHO




Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia watu wenye Ulemavu, Mhe. Stella Ikupa akipokelewa na baadhi ya viongozi wa Wilaya ya Bariadi kuelekea kwenye kikao kuzungumza na viongozi hao na watu wenye ulemavu Mjini Bariadi, wakati akiwa katika ziara yake ya kikazi  Wilayani humo, Feburuari 2019.



Kiongozi wa Chama cha Watu wenye ulemavu wa kusikia, Alex Benson  akichangia hoja katika kikao cha Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia watu wenye Ulemavu, Mhe. Stella Ikupa na viongozi wa Serikali na watu wenye ulemavu Mjini Bariadi, wakati akiwa katika ziara yake ya kikazi  Wilayani humo, Feburuari 2019.

Katibu wa SHIVYAWATA Wilaya ya Bariadi, Zizi Kubilu akiwasilisha taarifa ya walemavu  kwa Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia watu wenye Ulemavu, Mhe. Stella Ikupa na viongozi wa Serikali na watu wenye ulemavu Mjini Bariadi, wakati akiwa katika ziara yake ya kikazi  Wilayani humo, Feburuari 2019.
Mkalimani wa lugha ya alama(mbele kulia) akiwatafsiria baadhi ya watu wenye ulemavu wa kusikia hotuba ya Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia watu wenye Ulemavu, Mhe. Stella Ikupa, wakati  akizungumza na  viongozi wa Serikali na watu wenye ulemavu Mjini Bariadi, alipokuwa katika ziara yake ya kikazi  Wilayani humo, Feburuari 2019.
Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga akiwasilisha taarifa ya Wilaya kuhusu watu wenye ulemavu kwa Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia watu wenye Ulemavu, Mhe. Stella Ikupa, wakati akiwa  katika ziara yake ya kikazi  Wilayani humo, Feburuari 2019.
Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia watu wenye Ulemavu, Mhe. Stella Ikupa(aliyepo kwenye gari) akizungumza na viongozi wa Serikali na watu wenye ulemavu wilayani Meatu  baada ya kutembelea Kitalu nyumba kilichopo Nyakabindi , wakati akiwa katika ziara yake ya kikazi  Wilayani Bariadi, Feburuari 2019.
Baadhi ya viongozi na watu wenye ulemavu Wilaya ya Bariadi wakipewa maelezo juu kilimo kinavyofanyika katika Kitalu nyumba kilichopo Nyakabindi
Baadhi ya wakuu wa idara halmashauri ya Wilaya ya Bariadi na Mji wa Bariadi wakifuatilia kikao cha Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia watu wenye Ulemavu, Mhe. Stella Ikupa(hayupo pichani ) na viongozi wa Serikali na watu wenye ulemavu wilayani Bariadi, wakati akiwa katika ziara yake ya kikazi  Wilayani Bariadi, Feburuari 2019




SERIKALI KUZINDUA MFUKO WA WATU WENYE ULEMAVU


Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia watu wenye ulemavu, Mhe. Stella Ikupa amesema Serikali inatarajia kuzindua rasmi mfuko wa watu wenye ulemavu ambao utakuwa ukishughulikia masuala mbalimbali ya watu wenye ulemavu ikiwemo kutoa ruzuku kwa vyama vya watu wenye ulemavu.

Mhe. Ikupa ameyasema hayo wakati akizungumza na viongozi na watendaji wa Serikali na  watu wenye ulemavu wakati akiwa katika ziara ya kikazi wilayani humo, Februari 26,2019.

Amesema taratibu zote zimekamilika na sasa iko katika hatua za mwisho ili mfuko huo uweze kuzinduliwa huku akibainisha kuwa Baraza la Ushauri kwa watu wenye Ulemavu Taifa nalo litazinduliwa hivi karibuni kwa kuwa tayari Mwenyekiti wa Baraza hilo ameshateuliwa na Rais wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli.

“Tayari tumeshapata Mwenyekiti wa lile Baraza la Ushauri kwa watu wenye ulemavu ambaye ameteuliwa na Mhe. Rais na tunaamini muda si mrefu lile baraza litazinduliwa na litaendelea kufanya kazi kwa mujibu wa sheria” alisema Naibu Waziri Ikupa.

Katika hatua nyingine Mhe. Ikupa amepongeza viongozi wa Wilaya ya Meatu kwa namna wanavyoshughulikia masuala ya watu wenye ulemavu na wakati huo huo akawapongeza watu wenye ulemavu wilayani humo kutumia vema fedha za mikopo wanazopata kutokana asilimia mbili za mapato ya ndani ya Halmashauri kwa kuanzisha shughuli za ujasiriamali.

Aidha, ametoa wito kwa watu wenye ulemavu kujitokeza kwa wingi kuomba mikopo hiyo ambayo haina riba ili waweze kuanzisha shughuli za ujasiriamali zitakazowasaidia kujikwamua kiuchumi na kuondokana na utegemezi.

Mkuu wa Wilaya ya Meatu, Dkt. Joseph Chilongani amesema Halmashauri ya Wilaya hiyo imetenga takribani shilingi milioni Sabini kwa ajili ya kuwawezesha kiuchumi watu wenye ulemavu na akatoa wito kwao kujitokeza kuomba mikopo ili iwasaidie kuanzisha shughuli za kuwaingizia kipato.

Kwa upande wao watu wenye ulemavu wameiomba Serikali kwa kushirikiana na wadau mbalimbali kusaidia katika utatuzi wa changamoto mbalimbali zinazowakabili ikiwa ni pamoja na ukosefu vifaa saidizi kwa watu wenye ulemavu na kutengeneza mazingira wezeshi shuleni kwa wanafunzi wenye ulemavu.

“ Tunaomba Serikali yetu kwa kushirikiana na wadau itusaidie kupata nyenzo saidizi kama fimbo nyeupe kwa wasioona, viungo bandia na baiskeli za miguu mitatu kwa walemavu wa viungo” alisema Ndimila Luyoja Katibu wa SHIVYAWATA wilaya ya Meatu.

“ Tunaomba vifaa saidizi vya kukuza maandishi kwa wanafunzi  wenye ualbino na pia walimu wawape nafasi ya kukaa mbele madarasani ili waweze kuona vizuri kama wanafunzi wengine kwa sababu wasipopata nafasi hiyo watashindwa kuona vizuri ubaoni kutokana na wao kuwa na uoni hafifu”Mwenyekiti wa Chama cha Watu wenye ualbino Meatu.

Naye Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Festo Kiswaga amesema Serikali mkoani humo itaendelea kutoa kipaumbele kwa watu wenye uelemavu ambapo amesema wataendelea kujumuishwa katika agenda ya ujenzi wa uchumi wa viwanda kufikia uchumi wa kati mkoani humo.

Akiwa Wilayani Meatu, Mhe. Naibu Waziri amezungumza na viongozi, watu wenye ulemavu, kuona kazi mbalimbali za watu wenye ulemavu na kutembelea mradi wa Kitalu nyumba ili kujionea utekelezaji wake.
MWISHO



Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia watu wenye Ulemavu, Mhe. Stella Ikupa(katikati) akizungumza na viongozi na watendaji wa Wilaya ya Meatu pamoja na watu wenyeulemavu wakati akiwa katika ziara yake ya kikazi wilayani humo, Februari 26, 2019.
Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia watu wenye Ulemavu, Mhe. Stella Ikupa(wa tatu kulia) akiangalia baadhi ya kazi za wajasiriamali wenye ulemavu , wakati akiwa katika ziara yake ya kikazi wilayani humo, Februari 26, 2019.
Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia watu wenye Ulemavu, Mhe. Stella Ikupa(aliyeshika mkeka kushoto) akiangalia baadhi ya kazi za wajasiriamali wenye ulemavu , wakati akiwa katika ziara yake ya kikazi wilayani humo, Februari 26, 2019.

Mkuu wa Wilaya ya Meatu, Mhe. Dkt. Joseph Chilongani akimkaribisha Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia watu wenye Ulemavu, Mhe. Stella Ikupa mara baada ya kuwasili Mjini Mwanhuzi Meatu wakati akiwa katika ziara yake ya kikazi wilayani humo, Februari 26, 2019.
Mwenyekiti wa SHIVYAWATA  Wilaya ya Meatu ambaye pia ni mlemavu wa macho, Bw. Charles Hilu akiwasilisha changamoto za watu wenye ulemavu kwa  Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia watu wenye Ulemavu, Mhe. Stella Ikupa (wa pili kulia) wakati akiwa katika ziara yake ya kikazi wilayani humo, Februari 26, 2019.
Baadhi ya watoto wenye ulemavu wa kusikia wilayani Meatu wakifuatilia hotuba ya Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia watu wenye Ulemavu, Mhe. Stella Ikupa(hayupo pichani) kwa usaidizi wa Mkalimani wa lugha ya alama, wakati wa  ziara ya kikazi ya kiongozi huyo wilayani humo, Februari 26, 2019.
Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia watu wenye Ulemavu, Mhe. Stella Ikupa akitoka katika Kitalu Nyumba(Green House)  kilichopo Mwanhuzi Wilayani Meatu mara baada ya kukikagua, wakati akiwa katika ziara yake ya kikazi wilayani humo, Februari 26, 2019.
Afisa Kilimo wa Wilaya ya Meatu Bw. Thomas Shilabu akitoa maelezo juu ya mfumo wa umwagiliaji  uliowekwa katika Mradi wa Kitalu nyumba (green house) unaotekelezwa na Vijana ;  kwa Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia watu wenye Ulemavu, Mhe. Stella Ikupa wakati akiwa katika ziara yake ya kikazi wilayani humo, Februari 26, 2019.
Mbunge wa Viti maalum Mkoa wa Simiyu (CCM) Mhe. Leah Komanya akizungumza katika kikao cha Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia watu wenye Ulemavu, Mhe. Stella Ikupa na viongozi wa Wilaya ya Meatu, wakati wa ziara ya kikazi ya Naibu Waziri huyo  wilayani humo, Februari 26, 2019.
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Meatu, Mhe. Pius Machungwa akizungumza katika kikao cha Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia watu wenye Ulemavu, Mhe. Stella Ikupa na viongozi wa Wilaya ya Meatu na watu wenye ulemavu, wakati wa ziara ya kikazi ya Naibu Waziri huyo  wilayani humo, Februari 26, 2019.
Baadhi ya Viongozi na watu wenye ulemavu wilayani Meatu wakiwa katika kikao na Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia watu wenye Ulemavu, Mhe. Stella Ikupa , wakati wa ziara ya kikazi ya Naibu Waziri huyo  wilayani humo, Februari 26, 2019.
Mwakilishi wa  Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Anthony Mtaka, ambaye ni Mkuu wa Wilaya ya Bariadi , Mhe. Festo Kiswaga akizungumza na viongozi wa wilaya ya Meatu na baadhi ya watu wenye ulemavu katika kikao cha Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia watu wenye Ulemavu, Mhe. Stella Ikupa , wakati wa ziara ya kikazi ya Naibu Waziri huyo  wilayani humo, Februari 26, 2019.
Baadhi ya Viongozi na watu wenye ulemavu wilayani Meatu wakiwa katika kikao na Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia watu wenye Ulemavu, Mhe. Stella Ikupa , wakati wa ziara ya kikazi ya Naibu Waziri huyo  wilayani humo, Februari 26, 2019
Baadhi ya Viongozi na watu wenye ulemavu wilayani Meatu wakiwa katika Kitalu nyumba kilichopo Mwanhuzi wakati  Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia watu wenye Ulemavu, Mhe. Stella Ikupa  alipotembelea kujionea utekelezaji wa Mradi wa Kitalu Nyumba katika ziara ya kikazi wilayani humo, Februari 26, 2019.
Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia watu wenye Ulemavu, Mhe. Stella Ikupa (katikati) akizungumza naviongozi wa Wilaya ya Meatu, mara baada ya kuwasili wilayani humo kwa ziara ya kikazi, Februari 26, 2019. 

Tuesday, February 26, 2019

NAIBU WAZIRI IKUPA: KILIMO SI SHUGHULI YA WAZEE


Naibu waziri Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia watu wenye ulemavu, Mhe.  Stella  Ikupa  amewashauri Vijana nchini, kuondokana na dhana ya kuwa shughuli za kilimo ni za Wazee na badala yake watumie vitalu nyumba kujifunza kilimo chenye tija na hatimaye waweze kujikwamua  kiuchumi.

Ikupa ametoa ushauri huo wilayani Maswa wakati alipowatembelea  Vijana katika kitalu nyumba katika kata ya Binza  akiwa katika ziara yake wilayani humo Mkoani Simiyu Februari 25, 2019.

IKUPA amesema Vijana wanapaswa  kuachana na dhana potofu kuwa kilimo ni shughuli inayopaswa kufanywa na Wazee, badala yake watumie fursa za mafunzo ya kilimo na wakawe mabalozi ndani ya jamii kuwa kilimo kinaweza kuwapatia ajira na kipato.

“ Kilimo kinaweza kuwatoa vijana kutoka mahali fulani kikawapeleka mahali pengine tena wakawa na uwezo mzuri kifedha kuliko hata wale walioajiriwa katika kazi za maofisini, niwashauri vijana muione fursa kupitia vitalu nyumba ondoeni dhana kwamba eti kilimo ni kazi ya wazee si kweli” alisema.

Ameongeza kuwa vijana wanayo nafasi ya kupata mikopo kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Vijana kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu na Halmashauri zao hivyo wachangamkie fursa hiyo kupata mikopo itakayowawezesha kuendeleza shughuli zao za uzalishaji ikiwemo kilimo kupitia vitalu nyumba.

Katika hatua nyingine Mhe. Ikupa amesema ni vema Halmashauri zikazingatia masuala ya watu wenye ulemavu katika mipango ya bajeti zao ili ziweze kusaidia katika utatuzi wa baadhi ya changamoto za watu wenye ulemavu.

Aidha, amesisitiza umuhimu wa kuwatumia wakalimani wa lugha ya alama ili waweze kusaidia mawasiliano kati ya walemavu wa kusikia na makundi mbalimbali ya watu ikiwemo viongozi.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Maswa, Mhe. Dkt. Seif Shekalaghe amekiri kupokea maelekezo yote yaliyotolewa na Mhe. Naibu Waziri Ikupa na kumhakikishia kuwa watu wenye ulemavu watalindwa, watashirikishwa katika fursa mbalimbali ikiwa ni pamoja na mradi wa Kitalu nyumba.

Nao baadhi ya vijana wanaojihusisha na utekelzaji wa mradi wa Kitalu nyumba katika Kata ya Sola wameishukuru Serikali na kuomba ipanue wigo wa kuwafikia vijana kupitia mradi huu ili vijana wengi waweze kufikiwa mpaka ngazi ya Kata.

“ Mimi ninaishukuru Serikali yetu kwa kutuletea mradi wa kitalu nyumba, tumeshajifunza namna ya kutengeneza vitalu nyumba, kilimo bora chenye tija kupitia mradi huu, tunaomba mradi upelekwe mpaka ngazi ya kata ili vijana wengi waweze kunufaika  zaidi” alisema Rachel Paulo mkazi wa Sola Maswa.

Naibu Waziri Ikupa, anaendelea na ziara yake Mkoani Simiyu ambayo itahitimishwa tarehe 27 Februari 2019, akiwa wilayani Maswa Naibu waziri ametembelea kitalu nyumba kilichopo Sola na kuzungumza na viongozi wa Serikali na watu wenye ulemavu.
MWISHO


Baadhi ya Viongozi wilayani Maswa na wananchi wa Kata ya Sola wakisikiliza Naibu waziri Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia watu wenye ulemavu, Mhe.  Stella  Ikupa (hayupo pichani), wakati akizungumza nao mara baada ya kutembelea na kuona utekelezaji wa Mradi wa kitalu nyumba katika Kata ya Sola Wilayani Maswa, Februari, 25, 2019.
Mkuu wa Wilaya ya Maswa, Dkt. Seif Shekalaghe akimkaribisha Naibu waziri Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia watu wenye ulemavu, Mhe.  Stella  Ikupa  mara baada ya kuwasili wilayani humo ka ajili ya ziara ya kikazi Februari 25, 2019.
 Sehemu ya kitalu nyumba katika Kata ya Sola Wilayani Maswa


Baadhi ya viongozi, watendaji na watu wenye ulemavu wakimsikiliza Naibu waziri Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia watu wenye ulemavu, Mhe.  Stella  Ikupa (hayupo pichani) mara baada ya kuwasili wilayani humo ka ajili ya ziara ya kikazi Februari 25, 2019.
Mwakilishi wa Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka ambaye ni Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe.  Festo akizungumza na baadhi ya viongozi, watendaji na watu wenye ulemavu wilayani Maswa wakati wa Ziara yake ya kikazi Februari 25, 2019.
Naibu waziri Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia watu wenye ulemavu, Mhe.  Stella  Ikupa akizungumza jambo na Mkuu wa Wilaya ya Maswa, Mhe. Dkt. Seif Shekalaghe wakati wa Ziara yake ya kikazi wilaya ya Maswa mkoani Simiyu Februari 25, 2019.

NAIBU WAZIRI IKUPA ATOA WITO KWA WENYE ULEMAVU KUJIUNGA NA CHF ILIYOBORESHWA


Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia  masuala ya watu wenye  ulemavu, Mhe.Stella Ikupa  ametoa wito kwa viongozi wa vyama vya watu wenye  ulemavu, kuwahamasisha wanachama wao kujiunga na  mfuko  wa afya ya jamii (CHF )ulioboreshwa ili waweze kupata uhakika wa matibabu.

IKUPA ametoa wito huo  wilayani Itilima  katika ziara yake wakati akizungumza na viongozi wa Wilaya, Viongozi wa Vyama vya wenye ulemavu na  baadhi ya wenye ulemavu wenyewe wakati wa ziara yake wilayani humo Februari 25, 2019, ambayo ililenga kukagua utekelezaji wa maelekezo ya Serikali ikiwa ni pamoja na mradi wa Kitalu nyumba na masuala mbalimbali yahusuyo wenye walemavu.

Amesema ni vema viongozi wa vyama na wenye ulemavu wakapena taarifa na kuhamasishani kujiunga na mfuko wa Afya ya Jamii(CHF) ulioboreshwa, ili wapewe vitambulisho waweze kutibiwa kirahisi.

“Mkijiunga na CHF iliyoboreshwa mkapata kadi mtakuwa na uwezo wa kutibiwa muda wowote, kwa hiyo peaneni hizo taarifa mjiunge watu mnaofahamiana muweze kupewa hivyo vitambulisho mpate kutibiwa kirahisi wakati tukiwa tunasubiri ile bima ya afya kwa kila Mtanzania” alisema Mhe. Ikupa.

Katika hatua nyingine amewaagiza maafisa Ustawi wa jamii na maendeleo ya jamii kutoa elimu vijijini kwa  watu wenye  ulemavu kuhusiana na  uundwaji wa vikundi na namna ya kutekeleza miradi mbalimbali.

Mkuu wa Wilaya ya Itilima,Mhe.  Benson Kilangi  akizungumzia utekelezaji wa mradi wa kitalu nyumba amesema katika awamu ya kwanza jumla ya vijana 20 wamepata mafunzo ya utengenezaji wa vitalu nyumba na kufundishwa stadi mbalimbali za kuendesha kilimo biashara na kuongeza mnyororo wa thamani.

Naye Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Festo Kiswaga amesema  miradi ya vitalu katika Mkoa wa Simiyu itatekelezwa kwa viwango na kwa malengo yaliyokusudiwa, huku akibainisha kuwa vitasaidia kuongeza kipato kwa wananchi katika mkoa  na kuwa sehemu ya wananchi kujifunza kilimo bora.

Kwa upande wao viongozi pamoja na watu wenye ulemavu walioshiriki katika ziara hiyo wamemwomba Mhe. Naibu Waziri kushughulikia baadhi ya changamoto zinazowakabili katika maeneo yao.

“Ninaomba Serikali itusaidie tuweze kupata wakalimani wa lugha ya alama ili na sisi walemavu wa kusikia tuweze kupata ujumbe unaokuwa unawasilishwa na viongozi wetu kwenye mikutano na ziara kama hii ya leo hii itatusaidia sana” alisema Mhandi Ntobi Mwenyekiti wa Chama cha Walemavu wasiosikia Mkoa wa Simiyu.

“NaombaWataalam waje watutembelee kwenye vijiji vyetu na kwenye vyama vyetu watusaidie kutupa elimu ya namna ya kuunda vikundi na namna ya kufanya shughuli zinazoweza kutuongezea kipato” Bw. Seni Jitabo mlemavu wa viungo Mkazi wa Zagayu wilayani Itilima.

Naibu Waziri Ikupa, anaendelea na ziara yake Mkoani Simiyu ambayo itahitimishwa 27 Februari 2019, akiwa wilayani Itilima Naibu waziri ametembelea kitalu nyumba kilichopo Lagangabilili na kituo cha maarifa ya jamii Kanadi, ambako amejionea shughuli mbalimbali za uzalishaji zinazofanywa na vijana.
MWISHO
Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi,Ajira na Wenye Ulemavu anayeshughulikia walemavu, Mhe. Stella Ikupa akizungumza jambo na Bw. Mhandi Ntobi ambaye ni Mwenyekiti wa Chama cha Watu wasiosikia Mkoa wa Simiyu, wakati akiwa katika ziara yake Wilayani Itilima Mkoani Simiyu, Februari 25, 2019.
 Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi,Ajira na Wenye Ulemavu anayeshughulikia walemavu, Mhe. Stella Ikupa akizungumza na viongozi wa Mkoa wa Simiyu( hawapo pichani) mara baad ya kuwasilis Mjini Bariadi kwa ajili ya ziara yake mkoani humo, Februari 25, 2019.
 Mbunge wa Jimbo la Bariadi, Mhe. Andrew Chenge akimweleza jambo Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi,Ajira na Wenye Ulemavu anayeshughulikia walemavu, Mhe. Stella Ikupa( wa pili kulia) alipotembea Ofisi za CCM Mkoa wa Simiyu wakati wa ziara yake Mkoani Simiyu, Februari 25, 2019.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi,Ajira na Wenye Ulemavu anayeshughulikia walemavu, Mhe. Stella Ikupa( katikati kwa walioketi) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya viongozi wa Mkoa wa Simiyu na watumishi wa Mifuko ya Hifadhi ya Jamii Mkoani Simiyu(NSSF na PSSSF) mara baada ya kutembelea ofisi za mifuko hiyo wakati wa ziara yake mkoani Simiyu , Februari 25, 2019.
Bw. Seni Jitabo ambaye ni mlemavu wa Viungo akiwasilisha baadhi ya changamoto kwa Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi,Ajira na Wenye Ulemavu anayeshughulikia walemavu, Mhe. Stella Ikupa(hayupo pichani) wakati wa ziara yake Mkoani Simiyu, Februari 25, 2019
Mwenyekiti wa Chama cha Watu wenye ualbino , akiwasilisha baadhi ya changamoto za kundi hilo kwa Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi,Ajira na Wenye Ulemavu anayeshughulikia walemavu, Mhe. Stella Ikupa(hayupo pichani) wakati wa ziara yake Mkoani Simiyu, Februari 25, 2019
Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi,Ajira na Wenye Ulemavu anayeshughulikia walemavu, Mhe. Stella Ikupa akipokea zawadi ya sabuni kutoka kwa Afisa Vijana wa Wilaya ya Itilima ambaye alimkabidhi kwa niaba ya viongozi wa Wilaya hiyo wakati wa ziara yake Mkoani Simiyu, Februari 25, 2019
Moja ya Kitalu nyumba(green house) ikatika kata ya Lagangabilili wilayani Itilima, kilichotembelewa na  Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi,Ajira na Wenye Ulemavu anayeshughulikia walemavu, Mhe. Stella Ikupa wakati wa ziara yake.
Baadhi ya viongozi , watendaji na watu wenye ulemavu wakimsikiliza Mkuu wa Wilaya ya Itilima, Mhe. Benson Kilangi akitoa taarifa ya Wilaya Februari 25, 2019  kwa Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi,Ajira na Wenye Ulemavu anayeshughulikia walemavu, Mhe. Stella Ikupa,ambaye yupo ziarani mkoani Simiyu.
Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi,Ajira na Wenye Ulemavu anayeshughulikia walemavu, Mhe. Stella Ikupa(aliyeketi) akipewa maelezo ya namna sabuni za WIZA zinavyotengenezwa, wakati alipotembelea kiwanda hicho kilichopo Kata ya Kanadi wakati waziara yake wilaya ya Itilima mkoani Simiyu Februari 25, 2019.
 Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi,Ajira na Wenye Ulemavu anayeshughulikia walemavu, Mhe. Stella Ikupa akielekea katika Kiwanda cha kutengeneza sabani za WIZA zinazotengenezwa katika Kata ya Kanadi wakati ziara yake Wilaya ya Itilima mkoani Simiyu Februari 25, 2019. 


Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi,Ajira na Wenye Ulemavu anayeshughulikia walemavu, Mhe. Stella Ikupa(aliyeketi) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Viongozi wa Wilaya ya Itilima, mara baada ya kukamilisha ziara yake wilayani humo Februari 25, 2019.
Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi,Ajira na Wenye Ulemavu anayeshughulikia walemavu, Mhe. Stella Ikupa(aliyeketi katikati )akiwa katika picha ya pamoja na wana kikundi wanaojihusisha na utengenezaji wa sabuni za WIZA zinazotengenezwa katika Kata ya Kanadi wakati  wa ziara yake Wilaya ya Itilima mkoani Simiyu Februari 25, 2019.
 Sehemu ya Jengo la Kiwanda cha Sabuni Itilima kilichopo Kanadi
Viongozi wa Wilaya ya Itilima wakimkaribisha Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi,Ajira na Wenye Ulemavu anayeshughulikia walemavu, Mhe. Stella Ikupa kwa ajili ya kuanza ziara wilayani humo, Februari 25, 2019.
 Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi,Ajira na Wenye Ulemavu anayeshughulikia walemavu, Mhe. Stella Ikupa katika picha ya pamoja na wanafunzi wa shule ya sekondari Kanadi  wilayani Itilima, wakati  wa ziara yake Wilaya ya Itilima mkoani Simiyu Februari 25, 2019



Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi,Ajira na Wenye Ulemavu anayeshughulikia walemavu, Mhe. Stella Ikupa katika picha ya pamoja na wanafunzi wa shule ya sekondari Kanadi  wilayani Itilima, wakati  wa ziara yake Wilaya ya Itilima mkoani Simiyu Februari 25, 2019

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!