Friday, October 14, 2016

RAIS SHEIN : SERIKALI IMEJIPANGA KUKUSANYA MAPATO NA KUPUNGUZA MISAADA YA WAHISANI



Na Stella Kalinga
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt. Ali Mohamed Shein amesema Serikali imejipanga  kukusanya  na kutumia Mapato na rasiliamali zake  kwa maendeleo ya wananchi ili kupunguza na hatimaye kuondokana na kupewa misaada ya wahisani.

Rais Shein amesema hayo leo wakati alipowahutubia  na wananchi wa Mkoa wa Simiyu na Taifa kwa ujumla kwenye  maadhimisho ya  Kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru,  Kumbukumbu ya kifo cha Baba wa Taifa, mwl. Julius K. Nyerere na Wiki ya vijana, yaliyofanyika kitaifa Mkoani Simiyu.

Rais Shein amesema Serikali haiko tayari kukubali misaada ya baadhi ya wahisani ambao wamekuwa wakitoa na kuambatanisha na masharti yasiyotekelezeka  ambayo yapo wa ajili ya kuharibu mipango ya maendeleo.

Aidha, Rais Shein amesema ili kufikia azma hiyo Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar zimejidhatiti kuimarisha uwajibikaji kwa watumishi wa umma, kubana mianya yote ya rushwa na upotevu wa mapato na fedha zitakazookolewa zitaelekezwa katika shughuli za kiuchumi na huduma za jamii.

Sanjali na hilo Mhe. Dkt. Shein ametoa pongezi kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli kwa kazi nzuri anayoifanya ya kusimamia uchumi wa nchi na kupambana na watu wenye tamaa na lengo la kuhujumu uchumi.

Dkt. Shein amesema juhudi hizo za Serikali zina nia ya kuleta mabadiliko ya kiuchumi na kijamii ambapo alizitaka Mamlaka ya Mapato Tanzania(TRA) na Bodi ya Mapato Zanzibar kuwajibika ipasavyo katika ukusanyaji wa mapato.

“Tumeanza kuwawajibisha watumishi wasio waadilifu wapo waliotangazwa na ambao hawajatangazwa, bado tunaendelea kuwachunguza wengine “alisema Rais Shein.

Naye Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Ajira, Kazi, Vijana na Wenye ulemavu , Mhe. Jenista Mhagama amesema  Mwenge wa uhuru mwaka 2016 umebaini ubadhilifu na udanganyifu katika miradi ya maendeleo katika Halmashauri saba nchini, hivyo akaelekeza hatua stahiki kwa mujibu wa Sheria kanuni na taratibu za Utumishi wa Umma zichukuliwe kwa watakaobainika kuwa chanzo cha ubadhilifu huo.

Katika kutekeleza Kauli mbiu ya Mbio za Mwenge wa Uhuru, mwaka 2016, “Vijana ni nguvu kazi ya Taifa; Washirikishwe na kuwezeshwa” Mhe.Mhagama amesema mikoa ya Simiyu, Njombe,Mwanza, Ruvuma, Mbeya na Mtwara imetekeleza agizo la Serikali la kuhakikisha vijana wote nchini wanawezeshwa kwa kuwapa mitaji na kuwajengea uwezo wa kuendesha miradi mbalimbali.

Akitoa salamu za Mkoa, Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe. Anthony Mtaka amesema mkoa wake umedhamiria kuwawezesha vijana kujiairi kwa kutumia fursa zilizopo ikiwemo kuanzisha viwanda vidogo vidogo kwa kila wilaya chini ya Kauli Mbiu “Wilaya moja bidhaa moja”, ambapo hadi sasa Wilaya ya Maswa ina kiwanda cha kuzalisha chaki na Meatu kiwanda cha kusindika maziwa.

Maadhimisho ya  Kilele cha Mbio za Mbio za Mwenge wa Uhuru na Kumbukumbu ya kifo cha Baba wa Taifa mwaka 2016 yalitanguliwa na Ibada ya Kumuombea Hayati Baba wa Taifa iliyofanyika katika Kanisa Katoliki la Mtakatifu Yohana Mjini Bariadi, ambapo Askofu wa Jimbo la Shinyanga,  Liberatus Sangu amewaasa Watanzania kumuenzi Baba wa Taifa kwa  kupinga rushwa, ubaguzi na kudumisha amani na utulivu nchini.


Jumla ya Miradi  1,342 yenye thamani ya shilingi bilioni 498.8 imewekewa mawe ya Msingi  na mingine kuzinduliwa na Mwenge wa uhuru mwaka 2016 na kuanza kutoa huduma kwa wananchi, Mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka 2017 zitazinduliwa katika Mkoa wa Katavi na kuhitimishwa katika Mkoa wa Mjini Magharibi 
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt. Ali Mohamed Shein akipokea Mwenge wa Uhuru kutoka kwa Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka 2016, Ndg. George Mbijima  wakati wa sherehe za Kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru,  Kumbukumbu ya kifo cha Baba wa Taifa, mwl. Julius K. Nyerere na Wiki ya vijana, zilizofanyika kitaifa Mkoani Simiyu
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt. Ali Mohamed Shein akipanda katika jukwaa maalum kwa ajili ya kupokea Mwenge wa uhuru kutoka wa Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru, Mwaka 2016, Ndg. George Mbijima.


Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt. Ali Mohamed Shein akiwahutubia  na wananchi wa Mkoa wa Simiyu wakati wa sherehe za Kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru,  Kumbukumbu ya kifo cha Baba wa Taifa, mwl. Julius K. Nyerere na Wiki ya vijana, zilizofanyika kitaifa Mkoani Simiyu
Wakimbiza Mwenge Kitaifa wakielekea kumkabidhi Mwenge wa Uhuru wa uhuru Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt. Ali Mohamed Shein.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Ajira, Kazi, Vijana na Wenye ulemavu , Mhe. Jenista Mhagama akizungumza  na wananchi wa Mkoa wa Simiyu wakati wa sherehe za Kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru,  Kumbukumbu ya kifo cha Baba wa Taifa, mwl. Julius K. Nyerere na Wiki ya vijana, zilizofanyika kitaifa Mkoani Simiyu.
Waziri wa Kazi,Uwezeshaji, Vijana, Wazee,Wanawake na Watoto wa Zanzibar , Mhe. Moudline Castico akizungumza  na wananchi wa Mkoa wa Simiyu wakati wa Maadhimsho ya  Kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru,  Kumbukumbu ya kifo cha Baba wa Taifa, mwl. Julius K. Nyerere na Wiki ya vijana, yaliyofanyika kitaifa Mkoani Simiyu.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe. Anthony Mtaka akitoa salamu za mkoa kwenye maadhimisho ya Kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru,  Kumbukumbu ya kifo cha Baba wa Taifa, mwl. Julius K. Nyerere na Wiki ya vijana, yaliyofanyika kitaifa Mkoani Simiyu
: Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt. Ali Mohamed Shein akiwa katika picha ya pamoja na  Viongzi wa mkoa wa Simiyu

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt. Ali Mohamed Shein akiwa katika picha ya pamoja na, Mawaziri wenye dhamana ya Vijana Zanzibar (kushoto) na Jamhuri ya Muungano (kulia) ,Wakimbiza Mwenge Kitaifa, Mkuu wa Mkoa wa Simiyu (pili kushoto), Mwenyekiti wa CCM mkoa, Dkt.Titus Kamani na Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Festo Kiswaga(mstari wa pili kushoto)

Vijana wa Halaiki wakionesha maumbo ya vitu mbalimali katika onesho lao maalum wakati wa maadhimisho ya Kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru,  Kumbukumbu ya kifo cha Baba wa Taifa, Mwl. Julius K. Nyerere na Wiki ya vijana, yaliyofanyika kitaifa Mkoani Simiyu.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt. Ali Mohamed Shein akiwa katika picha ya pamoja na  viongozi wa Dini walishiriki katika maadhimisho ya Kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru,  Kumbukumbu ya kifo cha Baba wa Taifa, Mwl. Julius K. Nyerere na Wiki ya vijana, yaliyofanyika kitaifa Mkoani Simiyu

Vijana wa Halaiki wakionesha maumbo ya vitu mbalimali katika onesho lao maalum wakati wa maadhimisho ya Kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru,  Kumbukumbu ya kifo cha Baba wa Taifa, Mwl. Julius K. Nyerere na Wiki ya vijana, yaliyofanyika kitaifa Mkoani Simiyu.


Vijana wa Halaiki wakionesha maumbo ya vitu mbalimali katika onesho lao maalum wakati wa maadhimisho ya Kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru,  Kumbukumbu ya kifo cha Baba wa Taifa, Mwl. Julius K. Nyerere na Wiki ya vijana, yaliyofanyika kitaifa Mkoani Simiyu.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Ajira, Kazi, Vijana na Wenye ulemavu , Mhe. Jenista Mhagama akitoa maelezo ya utangulizi kwa  Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt. Ali Mohamed Shein kabla ya kutembelea mabanda ya maonesho ya vijana.

 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt. Ali Mohamed Shein akipewa maelezo na kijana kutoka kikundi cha Meatu Milk alipotembelea Banda la Vijana wa Meatu mkoani Simiyu wanaosindika maziwa.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt. Ali Mohamed Shein akipewa maelezo na kijana mgunduzi wa teknolojia ya umwagiliaji wa matone alipotembelea mabanda ya vijana, Uwanja wa SABASABA mjin Bariadi.

Askofu wa Jimbo Kuu la Shinyanga, Liberatus Sangu akiwa katika picha ya pamoja na Mapadri na Viongozi wa Serikali walioshiriki Ibada Maalum ya Kumuombea Baba wa Taifa Mwl.Julius K.Nyerere iliyofanyika katika Kanisa Katoliki la Mtakatifu Yohana Mjini Bariadi.
Askofu wa Jimbo Kuu la Shinyanga, Liberatus Sangu akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi wa madhehebu mbalimbali  walioshiriki Ibada Maalum ya Kumuombea Baba wa Taifa Mwl.Julius K.Nyerere iliyofanyika katika Kanisa Katoliki la Mtakatifu Yohana Mjini Bariadi.


Askofu wa Jimbo Kuu la Shinyanga, Liberatus Sangu akitoa dua ya kumuombea Baba wa Taifa Mwl.Julius K.Nyerere kwenye maadhimisho ya Kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru,  Kumbukumbu ya kifo cha Baba wa Taifa, Mwl. Julius K. Nyerere na Wiki ya vijana, yaliyofanyika kitaifa Mkoani Simiyu.

Askofu wa Jimbo Kuu la Shinyanga, Liberatus Sangu na Mapadri wakiwa katika Ibada Maalum ya Kumuombea Baba wa Taifa Mwl.Julius K.Nyerere iliyofanyika katika Kanisa Katoliki la Mtakatifu Yohana Mjini Bariadi.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe. Anthony Mtaka akiwatambulisha viongozi wa Serikali (hawapo pichani)walioshiriki katika Ibada Maalum ya Kumuombea Baba wa Taifa Mwl.Julius K.Nyerere iliyofanyika katika Kanisa Katoliki la Mtakatifu Yohana Mjini Bariadi.



Askofu wa Jimbo Kuu la Shinyanga, Liberatus akiongoza  Ibada Maalum ya Kumuombea Baba wa Taifa Mwl.Julius K.Nyerere iliyofanyika katika Kanisa Katoliki la Mtakatifu Yohana Mjini Bariadi.

Baadhi ya Waumini walioshiriki Ibada Maalum ya Kumuombea Baba wa Taifa Mwl.Julius K.Nyerere iliyofanyika katika Kanisa Katoliki la Mtakatifu Yohana Mjini Bariadi

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Ajira, Kazi, Vijana na Wenye ulemavu , Mhe. Jenista Mhagama akitoa salamu za Serikali walioshiriki katika Ibada Maalum ya Kumuombea Baba wa Taifa Mwl.Julius K.Nyerere iliyofanyika katika Kanisa Katoliki la Mtakatifu Yohana Mjini Bariadi.

Kikundi cha Burudani cha SAKWE kutoka Wilaya ya Bariadi wakitoa burudani kwenye kwenye maadhimisho ya Kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru,  Kumbukumbu ya kifo cha Baba wa Taifa, Mwl. Julius K. Nyerere na Wiki ya vijana, yaliyofanyika kitaifa Mkoani Simiyu.


Kwaya kutoka Kanisa la Kotoliki Mjini Bariadi wakiimba wimbo maalum wa Hayati Baba wa Taifa wakati wa ibada ya kumbukumbu ya kifo chake kilichotokea mika 17 iliyopita.


Thursday, October 13, 2016

RAIS WA ZANZIBAR MHE. DKT. ALI MOHAMED SHEIN AWASILI SIMIYU

Na Stella Kalinga
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi , Mhe. Dkt. Ali Mohamed Shein amewasili Mjini Bariadi jioni hii kwa ajili ya Maadhimisho ya kilele cha mbio za Mwenge wa Uhuru, Kumbukumbu ya Kifo cha Baba wa Taifa na Wiki ya Vijana yatakayofanyika kitaifa kesho tarehe 14 Oktoba, 2016 Mjini, Bariadi mkoani hapa.

Mhe. Rais wa Zanzibar ndiye atakayekuwa mgeni rasmi katika kilele cha mbio za Mwenge wa Uhuru, Kumbukumbu ya Kifo cha Baba wa Taifa na Wiki ya Vijana, tukio ambalo ni la kihistoria kwa mkoa wa Simiyu.


Rais Shein amepokelewa na viongozi mbalimbali wa mkoa huo wakiwemo viongozi wa Chama na Serikali pamoja na wananchi wa Mjini Bariadi.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi , Mhe. Dkt. Ali Mohamed Shein akipewa heshima na vijana wa Skauti Mkoa wa Simiyu mara baada ya kupokelewa Ikulu ndogo Mjini Bariadi.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi , Mhe. Dkt. Ali Mohamed Shein (wa pili kushoto) akiwa amevalishwa skafu na vijana wa Skauti Mkoa wa Simiyu mara baada ya kupokelewa Ikulu ndogo Mjini Bariadi,  ishara ya kumkaribisha, (kushoto) Mkuu wa Mkoa, Mhe. Anthony Mtaka.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi , Mhe. Dkt. Ali Mohamed Shein akisalimiana na baadhi ya viongozi, watumishi na wananchi wa Mkoa wa Simiyu mara baada ya kupokelewa Ikulu ndogo Mjini Bariadi.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi , Mhe. Dkt. Ali Mohamed Shein akisalimiana na baadhi ya viongozi, watumishi na wananchi wa Mkoa wa Simiyu mara baada ya kupokelewa Ikulu ndogo Mjini Bariadi.

VIJANA WAASWA KUACHA KULALAMIKA

Na Stella Kalinga
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Wenye ulemavu Mhe. Jenista Mhagama amewataka vijana kuacha kuilalamikia Serikali na badala yake  wachukue hatua za utekelezaji.

Waziri Mhagama aliyasema hayo jana katika ufunguzi wa Kongamano la Vijana Mkoa wa Simiyu lililofanyika Mjini Bariadi kwa lengo la kujadili Nafasi ya Vijana katika Maendeleo ya Uchumi wa Viwanda nchini.

 Waziri Mhagama amesema vijana wanapaswa kuacha kukaa vijiweni na wabuni miradi mbalimbali ya maendeleo ili Serikali iwawezeshe kwa kuwapatia mikopo ya kuendeleza Miradi hiyo kama walivyofanya vijana wa Wilaya ya Meatu na Maswa Mkoani Simiyu, ambao walipewa mikopo na wizara  na kuanzisha kiwanda cha chaki na maziwa.

“ Vijana acheni kulalamika , onyesheni uwezo wenu Serikali iko tayari kuwaunga mkono; tumetoa mkopo wa shilingi 38,000,000 kwa vijana wa Maswa waliokuwa tayari wameshafungua kiwanda cha kutengeneza chaki, Meatu walipewa shilingi 31,000,000 wamefungua kiwanda cha kusindika maziwa, Simiyu wameweza na mikoa mingine chukueni hatua” alisema Mhagama.

Awali akizungumza kabla ya kumkaribisha Waziri Mhagama Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe. Anthony Mtaka alisema mkoa wake kupitia kauli mbiu ya “Wilaya moja bidhaa moja”umedhamiria kuzalisha bidhaa ambazo malighafi yake yanapatikana hapa nchini.

Mtaka alisema katika kutimiza azma ya Kila wilaya kuzalisha bidhaa moja wilaya ya Maswa imeanza kutengeneza chaki, Meatu kusindika maziwa na wilaya ya Itilima, Busega na Bariadi zinaendelea kubuni na kuendeleza mradi.  

Pamoja na kuzalisha chaki na maziwa mkoa kwa kushirikiana na wadau wengine unajipanga kuanzisha kiwanda cha kuzalisha mahitaji yatokanayo na pamba kama vile bandeji, pamba za masikioni, pamba za hospitali kwa kuwa Mkoa huo ni wa tatu kwa uzalishaji wa pamba nchini.

Aidha, Mkoa una mkakati wa kuziongezea thamani bidhaa zote zitokanazo na kilimo na mifugo kama  vile mazao ya nafaka na mikunde, ngozi na nyama ambapo kwa upande wa mifugo maziwa tayari yameshaanza kusindikwa Wilaya ya Meatu.

Akizungumza katika Kongamano hilo  Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Tafiti za Sera za kiuchumi na Kijamii (ESFR) ametoa wito kwa vijana kufanya kazi kwa bidii kwa kuwa fursa zipo katika nyanja mbalimbali ili watimize wajibu wao katika kubuni miradi hususani viwanda vidogo vidogo.

Kongamano la vijana Mkoani Simiyu lilihusisha vijana kutoka idara na taasisi mbalimbali,vyuo vikuu, vikundi vya wajasiriamali kutoka sehemu mbalimbali nchini ambapo mada mbalimbali ziliwasilishwa ikiwa ni pamoja na Mageuzi ya kiuchumi yanayohitajika kuboresha maisha ya vijana, Fursa za Vijana katika Uchumi wa Viwanda, umuhimu wa viwanda vidogo vidogo katika maendeleo ya viwanda nchini, fursa mpya katika kilimo Biashara na kadhalika.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe. Anthony Mtaka akiwa amesimama katikati ya mabango ya Chaki za Maswa na Maziwa ya Meatu bidhaa ambazo zinazalishwa chini ya Kauli mbiu ya Mkoa huo ya “Wilaya moja bidhaa moja”
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Wenye ulemavu Mhe. Jenista Mhagama akipokea zawadi ya mafuta kutoka kwa kijana mjasiriamali kutoka Mkoa wa Lindi.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Wenye ulemavu Mhe. Jenista Mhagama akisalimiana na viongozi wa Mkoa wa Simiyu kabla ya kuanza Kongamano la Vijana wa Mkoa huo.
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Tafiti za Sera za kiuchumi na Kijamii (ESFR) Dkt. Tausi Kida akitoa mada kwa washiriki wa kongamano la Vijana wa Mkoa wa Simiyu (hawapo pichani).
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe. Anthony Mtaka (wa tatu kushoto) na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Wenye ulemavu Mhe. Jenista Mhagama (wa nne kushoto) wakiteta jambo kabla ya Kongamano la Vijana wa Mkoa huo kufunguliwa.
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Tafiti za Sera za kiuchumi na Kijamii (ESFR) Dkt. Tausi Kida na Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe. Anthony Mtaka wakifuatilia hotuba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Wenye ulemavu Mhe. Jenista Mhagama ufunguzi wa Kongamano la Vijana wa Mkoa wa Simiyu
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Wenye ulemavu Mhe. Jenista Mhagama akizungumza na vijana wa mkoa wa Simiyu katika kongamano la mkoa la vijana hao.
Mkuu wa Wilaya ya Masw, Mhe. Dkt. Seif Shekalaghe akiwakaribisha washiriki wa Kongamano la Vijana Mkoa wa Simiyu lililofanyika Mjini Bariadi kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi (Mwenyeji) , Mhe. Festo Kiswaga.
Baadhi ya washiriki wa kongamano la Vijana Mkoa wa Simiyu wakfuatilia mada mbalimbali zilizokuwa zikiwasilishwa.
Kutoka kulia Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Tafiti za Sera za kiuchumi na Kijamii (ESFR) Dkt. Tausi Kida, Waziri Jenista Mhagama, Mwakilishi wa Katibu Mkuu UN, Amoni Manyama, Naibu Waziri Kazi, Vijana na Ajira, Anthony Mavunde na Mmoja wa Wawasilisha mada.    
Baadhi ya washiriki wa kongamano la Vijana Mkoa wa Simiyu wakfuatilia mada mbalimbali zilizokuwa zikiwasilishwa.

Wednesday, October 12, 2016

WAZIRI MHAGAMA AZINDUA KIWANDA CHA KUSINDIKA MAZIWA MEATU SIMIYU



Na Stella Kalinga
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Wenye ulemavu Mhe. Jenista Mhagama amefungua kiwanda cha kusindika maziwa kinachoendeshwa na  kikundi cha Vijana wa Meatu kilichopo wilayani humo Mkoa wa Simiyu.

Akizungumza na Vijana hao wanaosindika maziwa ya Meatu (MEATU MILK), Waziri Mhagama amewataka kuutunza mradi huo ili uwe mradi mkubwa wa kuwaingizia mapato wao na Serikali kwa ujumla. 

Mhagama amesema kwa kadri mradi huo utakavyokuwa mkubwa ndivyo wafugaji wa Wilaya ya Meatu na Mkoa wa Simiyu kwa ujumla watakavyonufaika kwa kupata soko la uhakika la maziwa.

Aidha, Waziri huyo amewataka Viongozi wote wa wilaya kuunga mkono juhudi zilizofanywa na Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka za kuwatengenezea  vijana mazingira mazuri ya kutekeleza shughuli mbalimbali za maendeleo yao, ikiwa ni pamoja na kushughulikia upatikanaji wa mitaji na mafunzo ya kuwajengea uwezo.

Wakati huo huo Waziri Mhagama ameahidi  kuwa Ofisi yake itatoa mkopo wa shilingi 30,000,000 kwa lengo la kuwasaidia vijana hao kuongeza uzalishaji ili kupanua soko la maziwa yao ndani na nje ya Mkoa.

“Mhe. Mkuu wa Mkoa Ofisi ya Waziri Mkuu itawapa mkopo vijana wa “Meatu Milk”ili wapanue uzalishaji; Wizara yangu itatoa mikopo kwa vijana walio tayari kutekeleza ikiwa ni pamoja na kuanzisha viwanda vidogo vidogo vitakavyowasaidia kuwapa ajira na kujikwamua kwenye umaskini” alisema Mhagama.

Akizungumza na wananchi wa wilaya ya Meatu kabla ya kumkaribisha Waziri Mhagama Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka amesema Mkoa huo umejipanga kuzalisha bidhaa mbalimbali kwa kutumia malighafi zinazopatikana hapa nchini.

“Tumejichagua kuwa pacha wa Mhe. Rais katika kutekeleza Ilani ya Chama cha Mapinduzi kwa Vitendo na tumedhamiria kuwa miongoni mwa mikoa mitano inayofanya vizuri katika uchumi”, alisema Mtaka.

Akiwasilisha taarifa ya mradi kwa niaba ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Meatu  kwa Mhe. Waziri, kiongozi wa kikundi cha Meatu Milk Lightness Benedicto amesema Halmashauri imewapa mtaji na kuwajengea uwezo kwenye teknolojia za usindikaji, ufungishaji wa bidhaa za maziwa pamoja na elimu ya ujasiriamali.


Naye Mbunge wa Jimbo la Meatu, Mhe. Salum Mbuzi ameahidi kuwaongezea mtaji wa shilingi 5,000,000 vijana hao pamoja na kuwasaidia kukutafuta soko la uhakika kwa maziwa watakayosindika.

Mradi wa kiwanda cha kusindika maziwa Meatu wenye vijna 18 hadi sasa umegharimu jumla ya shilingi 34,903,000 kati ya hizo shilingi 10,000,000 ni michango ya wanachama kutoka kwenye gawio la fedha za mkopo uliotolewa na Wizara yenye dhamana na vijana,shilingi 24,903,000 ni mkopo kutoka kwenye 5% ya mapato ya ndani ya Halmashauri.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Wenye ulemavu Mhe. Jenista Mhagama akikata utepe kabla ya kuzindua kiwanda cha kusindika maziwa wilayani Meatu.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Wenye ulemavu Mhe. Jenista Mhagama (wa pili kushoto), akipewa maelezo na vijana wa kikundi cha Meatu Milk wanaojishugulisha na usindikaji wa maziwa kabla ya kuweka jiwe la uzinduzi katika kiwanda cha kusindika Maziwa Meatu.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Wenye ulemavu Mhe. Jenista Mhagama, akiweka jiwe la uzinduzi katika kiwanda cha kusindika Maziwa wilaya ya Meatu, Mkoani Simiyu.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Wenye ulemavu Mhe. Jenista Mhagama, akipewa maelezo na vijana wa kikundi cha Meatu Milk wanaojishugulisha na usindikaji wa maziwa kabla ya kuweka jiwe la uzinduzi katika kiwanda cha kusindika Maziwa Meatu.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Wenye ulemavu Mhe. Jenista Mhagama akimkabidhi zawadi ya maziwa Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka mara baada ya kuzindua kiwanda cha kusindika maziwa Meatu

Baadhi ya viongozi wa Wilaya Meatu, mkoa wa Simiyu na viongzi wa kitaifa wakisikiliza taarifa kutoka kwa kiogozi wa Vijana wanaojishughulisha na usindikaji wa maziwa (hayupo pichani)  wilayani Meatu .


Naibu Waziri wa kazi, Vijana na Ajira, Mhe. Antony Mavunde(kulia) akizungumza na Vijana na wananchi wa Meatu baada ya  Waziri Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Wenye ulemavu Mhe. Jenista Mhagama  kuzindua kiwanda cha maziwa Meatu.

Naibu Waziri wa kazi, Vijana na Ajira, Mhe. Antony Mavunde akipokea gudulia la maziwa kutoka kwa Waziri Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Wenye ulemavu Mhe. Jenista Mhagama mara baada ya kuzindua kiwanda cha maziwa Meatu.
Baadhi ya viongozi wa Wilaya Meatu, mkoa wa Simiyu na viongozi wa kitaifa wakicheza muziki ishara ya kufurahia uzinduzi wa Kiwanda cha Maziwa wilayani Meatu.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu  Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Wenye ulemavu Mhe. Jenista Mhagama (waliokaa) wa nne) akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa wilaya ya Maswa, Mkoa wa Simiyu, na Vijana wa Meatu Milk.
Waziri Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Wenye ulemavu Mhe. Jenista Mhagama, akimkabidhi zawadi ya Maziwa Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya Meatu, Mhe. Pius machungwa  mara baada ya kuzindua kiwanda cha maziwa Meatu.


Mbunge wa Jimbo la Meatu, Mhe. Salum Mbuzi akipokea zawadi ya maziwa kutoka kwa Waziri Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Wenye ulemavu Mhe. Jenista Mhagama mara baada ya kuzindua kiwanda cha maziwa Meatu.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Wenye ulemavu Mhe. Jenista Mhagama akizungumza na vijana na wananchi wa Meatu mara baada ya kuzindua kiwanda cha kusindika maziwa wilayani  humo.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Wenye ulemavu Mhe. Jenista Mhagama akimkabidhi zawadi ya maziwa Waziri wa Kazi, Uwezeshaji, Wazee, Vijana, Wanawake na Watoto Zanzibar, Mhe. Maudline Castico mara baada ya kuzindua kiwanda cha maziwa Meatu



Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Meatu Mhe. Fabian Manoza akipokea zawadi ya  maziwa kutoka kwa Waziri Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Wenye ulemavu Mhe. Jenista Mhagama mara baada ya kuzindua kiwanda cha maziwa Meatu

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!