Tuesday, October 11, 2016

WAZIRI MHAGAMA AFUNGUA KIWANDA CHA CHAKI SIMIYU

Na Stella Kalinga
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Wenye ulemavu Mhe. Jenista Mhagama amefungua kiwanda cha kutengeza chaki kinachoendeshwa na kikundi cha Vijana cha Maswa Family kilichopo wilayani Maswa Mkoani Simiyu.

Akizungumza na wananchi wa Wilaya ya Maswa waliyojitokeza kushuhudia zoezi hilo la ufunguzi, Mhagama amempongeza Mkuu wa Mkoa huo Mhe. Anthony Mtaka na watendaji ngazi ya Mkoa na wilaya waliowasaidia vijana hao kuendeleza wazo lao na kufikia hatua waliyopo sasa, hali iliyowatengenezea ajira na kuwapatia kipato.

Waziri Mhagama amewataka vijana hao kufanya kazi kwa bidii, kutoingiza masuala ya kisisasa na maslahi binafsi katika uendeshaji wa mradi ili waweze kufikia malengo yao.

 Katika kuunga mkono juhudi za Kikundi hicho cha Maswa Family Waziri Mhagama ameahidi kuwa Wizara yake itawapatia mkopo wa shilingi 30,000,000 ili ziweze kuwasaidia kuongeza mtaji na uzalishaji.

Awali akizungumza kabla ya kumkaribisha Waziri huyo, Mkuu wa Mkoa huo amesema Serikali mkoani humo imejipanga kuonesha kuwa Watanzania wana uwezo wa kutengeneza vya kwao kwa kutumia malighafi za hapa nchini.

Mtaka amesema Mkoa wake ni wa kutekeleza hivyo viongozi wake wamejipanga kutekeleza ili kufikia azma ya kuwa miongoni mwa mikoa mitano inayotumaini kiuchumi hapa nchini,  badala ya  kufungua semina, warsha na makongamano ya wajasiriamali ambayo hayawasaidii wanachi katika kuinua uchumi wao.

Naye Waziri Mhagama ametangaza rasmi kuwa kiongozi yeyote asimualike katika kufungua warsha, semina na makongamano ya ujasiriamali badala yake wamuite kufungua na kuona utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo kwa vijana kama alivyofanya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu.

“Kwa hali hiyo naomba nitangaze rasmi sasa na ninaamini ujumbe huu utafika nchi nzima kuwa,   kiongozi yeyote tangu wewe Mhe Mkuu wa Mkoa umeamua kufanya maamuzi haya,  asinialike kufungua kongamano wala warsha, kuanzia leo nialikwe kuyafanya kama haya uliyoyafanya kwenye  Mkoa wa Simiyu na wilaya ya Maswa” alisema Mhagama.

Kwa upande wake Naibu Waziri wa nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana na Ajira Mhe Anthony Mavunde ambaye ametangaza kuwa balozi wa Chaki zinazotengezwa Maswa(MASWA CHALKS) amewataka vijana kutimiza wajibu wao kwa kujishughulisha na kuacha kulamu Serikali.

Naye Mbunge wa Jimbo la Maswa Mashariki Mhe. Stanslaus Nyongo amesema yeye pamoja na mbunge mwenzake wa Jimbo la Maswa Magharibi, Mhe. Mashimba Ndaki watasimamia na kuhakikisha mafungu yote yanayotolewa kwa ajili ya wanawake na vijana wa Maswa yanawafikia na kuwanufaisha.

Kiwanda cha kuzalisha chaki cha Maswa kimegharimu zaidi ya milioni 37 na kinaweza kuzalisha katoni 128 kwa siku, ambapo zaidi ya shule za Msingi na Sekondari 600 za mkoa wa Simiyu na za mikoa ya jirani zinaweza kunufaika na kiwanda hiki.


Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Wenye ulemavu Mhe. Jenista Mhagama akimwaga uji ulioandaliwa kwa ajili kutengeneza chaki juu ya mashine alipotembelea kiwanda cha kutengeneza chaki wilayani Maswa

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Wenye ulemavu Mhe. Jenista Mhagama akiangalia namna chaki zinavyotengenezwa na kutolewa katika mashine alipotembelea kiwanda cha kutengeneza chaki Maswa.


Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Wenye ulemavu Mhe. Jenista Mhagama akiangalia chaki zilizotengenezwa alipotembelea kiwanda cha kutengeneza chaki Maswa.


Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Wenye ulemavu Mhe. Jenista Mhagama akizungumza na wananchi wa Wilaya ya Maswa mara baada ya kufungua kiwanda cha chaki cha Vijana wilaya hiyo.

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka akizungumza na wananchi wa Wilaya ya Maswa mara baada ya Waziri Jenista Mhagama kufungua kiwanda cha chaki wilayani  humo


Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Ajira na Vijana Mhe. Anthony Mavunde(kulia) akizungumza na wananchi wa Wilaya ya Maswa mara baada ya Waziri Jenista Mhagama kufungua kiwanda cha chaki wilayani humo.
.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Wenye ulemavu Mhe. Jenista Mhagama akisalimiana na viongozi wa Wilaya ya Maswa kabla ya kufungua kiwanda cha kutengeneza chaki wilayani humo.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Wenye ulemavu Mhe. Jenista Mhagama akisaini kitabu cha wageni katika Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa kabla ya kufungua kiwanda cha kutengeneza chaki wilayani humo.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Wenye ulemavu Mhe. Jenista Mhagama (wa pili kushoto waliokaa) akiwa katika picha ya pamoja na vijana wa Maswa Family, viongozi wa Chama na Serikali ngazi ya Mkoa na Wilaya ya Maswa baada ya  kufungua kiwanda cha kutengeneza chaki wilayani Maswa.

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka (kushoto)  akicheza muziki na vijana wa Maswa Family mara baada ya Waziri Jenista Mhagama kufungua kiwanda chao cha chaki wilayani  humo.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Wenye ulemavu Mhe. Jenista Mhagama akisalimiana na Mbunge wa Maswa Magharibi, Mhe. Mashimba Ndaki kabla ya kwenda kufungua kiwanda cha kutengeneza chaki wilayani humo.
Vijana wa Maswa Family wakifurahia jambo baada ya kiwanda chao cha chaki kufunguliwa rasmi na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Wenye ulemavu Mhe. Jenista Mhagama.




0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!