Sunday, October 9, 2016

WAZIRI MHAGAMA ATOA MAAGIZO KWA HALMASHAURI NCHINI

Na Stella Kalinga

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu sera, bunge, kazi, ajira na wenye ulemavu Jenista Mhagama ameziagiza halmashauri zote nchini ambazo hazijatenga maeneo kwa ajili ya vijana kufanya hivyo mara moja.

Mbali na hilo Mhagama ameziagiza halmashauri nchi nzima kuhakikisha zinafungua na kuanzisha SACCOS za Vijana na kuzisimamia ili vijana wapate mikopo yenye masharti nafuu, ikiwa pamoja na kuhakikisha zinatenga asilimia 5 ya mapato ya ndani kama inavyotakiwa.

Waziri Mhagama alitoa maagizo hayo leo Mkoani Simiyu wakati akiongea na mamia ya wananchi na vijana wa Mkoa huo mjini Bariadi katika ufunguzi wa maadhimisho ya wiki ya vijana Kitaifa yanayofanyika mkoani hapa.

Mhagama amesema kuwa mpaka sasa ni halmashauri 72 zimeshatenga hekari 84037 kati 185 kwa ajili ya vijana katika shughuli za kilimo, ufugaji na kibiashara, ili kuweza kujiletea maendeleo ya kiuchumi.

“ ..kupitia maadhimisho haya ninaagiza halmashauri zote nchini ambazo zinafahamu bado hazijatenga maeneo haya kuhakikisha wanatenga mara moja…na kuwapatia vijana kwa ajili ya kufanya shughuli hizo” Alisema Waziri

Aidha Waziri huyo aliongeza kuwa bado kuna halmashauri nchini zimeshindwa kutekeleza maagizo ya serikali ya kuanzisha SACCOS za Vijana, ambapo mpaka sasa ni halmashauri 113 tu ambazo zimeanzisha SACCOS hizo kati ya 185, huku zikiwa zimetenga jumla ya shilingi Bilioni.3.9 kwa mwaka wa fedha 2016/17 na akazitaka halmashauri zingine kuanzisha SACCOS hizo na kutenga fedha za Vijana mara moja.

Awali akimkaribisha Waziri huyo Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe. Anthony Mtaka amesema kuwa mkoa huo umeanza kutekeleza kwa vitendo agizo la Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt John Pombe Magufuli la kuifanya Tanzania kuwa ya viwanda kwa kuanzisha viwanda viwili vidogo; kiwanda cha kutengeneza chaki kilichopo wilaya ya Maswa na  cha kusindika Maziwa kilichopo Meatu.

Mtaka amesema Serikali mkoani humo imedhamiria kuufanya mkoa huo kuwa wa mfano na kuwa miongoni mwa mikoa mitano ya kutumainiwa kibiashara ambao viongozi mbalimbali wataenda kujifunza namna unavyotekeleza.

Hata hivyo Waziri Mhagama alimpongeza Mkuu wa mkoa huyo na kusema kuwa amekuwa kiongozi wa kwanza kutekeleza agizo la Rais, na kumuahidi kuwa ofisi ya Waziri Mkuu iko tayari kusaidia juhudi hizo hata kwa kutoa fedha za kuwawezesha vijana.

Kwa upande wake Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia wenye ulemavu amewataka Wakuu wa mikoa , wakuu wa wilaya na wakurugenzi wa Halmashauri kote nchini  kuwa chachu  na kiungo muhimu katika  kuandaa na kutekeleza mikakati ya kutokomeza unyanyapaa na vitendo vya ukatili,  wanavyofanyiwa watu wenye ualbino ili nao waweze kufanya shughuli za maendeleo bila uoga kama ilivyo kwa baadhi yao.


Wiki ya vijana itahitimishwa pamoja na Mbio za Mwenge wa Uhuru na Kumbukumbu ya Kifo cha Baba wa Taifa Mwl. Julius Kambarage Nyerere, tarehe 14 Oktoba, 2016 Mjini Bariadi Mkoani Simiyu.
Waziri wa nchi ofisi ya Waziri Mkuu sera, bunge, kazi, ajira na wenye ulemavu Jenista Mhagama (wa tano kushoto) viongozi mbalimbali ngazi ya taifa na Mkoa wakipokea maandamano ya vijana katika Uzinduzi wa Wiki ya Vijana,  Uwanja wa Sabasaba Mjni Bariadi.
Baadhi ya Vijana wa Mkoa wa Simiyu wakionesha mabango yenye jumbe mbalimbali kwa Waziri wa nchi ofisi ya Waziri Mkuu sera, bunge, kazi, ajira na wenye ulemavu Jenista Mhagama ambaye alikuwa mgeni rasmi katika Uzinduzi wa Wiki ya Vijana Mjini Bariadi.
Waziri wa nchi ofisi ya Waziri Mkuu sera, bunge, kazi, ajira na wenye ulemavu Jenista Mhagama, akivishwa skafu na vijana wa skauti wa Mkoa wa Simiyu baada ya kupokea maandamano ya amani ya vijana katika Uzinduzi wa Wiki ya Vijana,  Uwanja wa Sabasaba Mjni Bariadi.


Kikundi cha Brass Band cha Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) Mgulani Dar es Salaam wakiwaongoza vijana katika maandamano ya amani kuelekea uwanja wa Sabasaba Mjini Bariadi ambapo wiki ya vijana imezinduliwa rasmi leo
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka akizungumza kabla ya kumkaribisha Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu sera, bunge, kazi, ajira na wenye ulemavu Mhe.Jenista Mhagama (Mb), azungumze na Vijana na Wananchi wa Mkoa huo wakati wa Uzinduzi wa Wiki ya Vijana kitaifa mwaka 2016, Mjini Bariadi.
Vijana wa Halaiki wakiwa na mabango yenye jumbe mbalimbali katika katika maandamano ya amani kuelekea uwanja wa Sabasaba Mjini Bariadi ambapo wiki ya vijana imezinduliwa rasmi leo.



Waziri wa nchi ofisi ya Waziri Mkuu sera, bunge, kazi, ajira na wenye ulemavu Jenista Mhagama, akizungumza na Vijana na Wananchi wa Mkoa wa Simiyu wakati wa Uzinduzi wa Wiki ya Vijana kitaifa mwaka 2016, Mjini Bariadi.
Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu , anayeshughulikia wenye ulemavu Mhe. Dkt. Abdallah Possi akizungumza na Vijana na Wananchi wa Mkoa wa Simiyu wakati wa Uzinduzi wa Wiki ya Vijana kitaifa mwaka 2016, Mjini Bariadi.
Baadhi ya Vijana wa Mkoa wa Simiyu wakielekea uwanja wa Sabasaba,Mjini Bariadi mahali ulipofanyika Uzinduzi wa Wiki ya Vijana kitaifa mwaka 2016.
Baadhi ya Vijana wa Mkoa wa Simiyu wakielekea uwanja wa Sabasaba,Mjini Bariadi mahali ulipofanyika Uzinduzi wa Wiki ya Vijana kitaifa mwaka 2016
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka (mbele) akiwaongoza viongozi wa Wizara ya Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu sera, bunge, kazi, ajira na wenye ulemavu kuimba pamoja na Kwaya ya Walimu wa Bariadi iliyotoa burudani wakati wa Uzinduzi wa Wiki ya Vijana kitaifa mwaka 2016, Mjini Bariadi.Kutoka kushoto (wa tatu) Waziri Jenista Mhagama, (wa tano) Naibu Waziri Anthony Mavunde na (wa sita) Naibu Waziri Abdallah Possi.

Waziri wa nchi ofisi ya Waziri Mkuu sera, bunge, kazi, ajira na wenye ulemavu Jenista Mhagama na viongozi wengine wakicheza pamoja na msanii Alphonce Seme  (Mzee wa Madodoso) wakati wa Uzinduzi wa Wiki ya Vijana kitaifa mwaka 2016, Mjini Bariadi.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka (wa saba kushoto) na viongozi wengine wa kitaifa na kimataifa wakiimba pamoja na Kwaya ya Walimu wa Bariadi iliyotoa burudani wakati wa Uzinduzi wa Wiki ya Vijana kitaifa mwaka 2016, Mjini Bariadi.

Katibu Tawala Mkoa wa Simiyu, Jumanne Sagini akitambulisha viongozi wa Kitaifa na Kimataifa (hawapo pichani) walioshiri katika uzinduzi wa wiki ya Vijana Mkoni Simiyu.
Mkurugenzi wa Idara ya Vijana kutoka Wizara ya nchi ofisi ya Waziri Mkuu sera, bunge, kazi, ajira na wenye ulemavu , Jemasi Kajugusi akizungumza na Vijana na Wananchi wa  wa Mkoa wa Simiyu wakati wa Uzinduzi wa Wiki ya Vijana kitaifa mwaka 2016, Mjini Bariadi.

Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Shirika la linaloshughulikia idadi ya watu duniani, Christina Mwanukuzi akiwasilisha salamu za Mkurugenzi huyo kwa Vijana na Wananchi wa Mkoa wa Simiyu wakati wa Uzinduzi wa Wiki ya Vijana kitaifa mwaka 2016, Mjini Bariadi.

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka akiimba wimbo wa mkoa huo na Vijana wa Halaiki waliotoa burudani wakati wa Uzinduzi wa Wiki ya Vijana kitaifa mwaka 2016, Mjini Bariadi.

Vijana wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) wakitoa burudani ya nyimbo wakati wa Uzinduzi wa Wiki ya Vijana kitaifa mwaka 2016, Mjini Bariadi.

Mwakilishi wa Vijana Diana Rose Lyimo akisalimiana na viongozi mara baada ya kuwasilisha maaazimio ya vijana wakati wa Uzinduzi wa Wiki ya Vijana kitaifa mwaka 2016, Mjini Bariadi.
Amosi Manyama Mwakilishi wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki-Moon akitoa salamu za Katibu Mkuu huyo kwa Vijana na Wananchi wa Mkoa wa Simiyu wakati wa Uzinduzi wa Wiki ya Vijana kitaifa mwaka 2016, Mjini Bariadi.

Waziri wa nchi ofisi ya Waziri Mkuu sera, bunge, kazi, ajira na wenye ulemavu Jenista Mhagama akipewa maelezo na Maafisa wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi NEC alipotembelea banda la tume hiyo wakati wa Uzinduzi wa Wiki ya Vijana kitaifa mwaka 2016, Mjini Bariadi

Waziri wa nchi ofisi ya Waziri Mkuu sera, bunge, kazi, ajira na wenye ulemavu Jenista Mhagama akipewa maelezo na Kijana mgunduzi juu ya kifaa alichokigundua kinachotumika kupima mwendokasi wa magari, alipotembelea banda la Vijana hao wakati wa Uzinduzi wa Wiki ya Vijana kitaifa mwaka 2016, Mjini Bariadi
Wasanii wa Kikundi cha burudani cha BASEKI cha Mjini Bariadi wakitoa burudani wakati wa Uzinduzi wa Wiki ya Vijana kitaifa mwaka 2016, Mjini Bariadi.


: Viongozi wa kimkoa, kitaifa na kimataifa wakiimba pamoja na Kwaya ya Walimu wa Bariadi iliyotoa burudani wakati wa Uzinduzi wa Wiki ya Vijana kitaifa mwaka 2016, Mjini Bariadi.
Kikundi cha Brass Band kutoka Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) Mgulani wakiwaogoza vijana wa mkoa wa Simiyu katika  maandamano ya amani yaliyofanywa kuelekea uwanja wa Sabasaba Mjini Bariadi, katika Uzinduzi wa Wiki ya Vijana kitaifa mwaka 2016.






0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!