Sunday, April 28, 2019

RC MTAKA: KAMBI ZA KITAALUMA SIMIYU ZITAKUWA ENDELEVU


Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka amesema Kambi za Kitaaluma mkoani Simiyu kwa wanafunzi wa darasa la saba, kidato cha nne na kidato cha Sita, ambayo ni madarasa yanayofanya Mitihani ya Taifa ya kuhitimu elimu ya Msingi na Sekondari zitakuwa endelevu.

Mtaka amesema hayo Aprili 28, 2019 wakati akihitimisha Kambi ya Kitaaluma kwa wanafunzi wa kidato cha sita iliyofanyika kwa takribani mwezi mmoja katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa, iliyohusisha wanafunzi 1166 kutoka katika shule 12 mkoani hapa.

Amesema Mkoa utaendelea kufanya jitihada na kuboresha zaidi kambi hizo huku akieleza kuwa ameshawaelekeza Wakurugenzi wa Halmashauri zote mkoani humo kutenga fedha kwa ajili ya motisha kwa walimu na wanafunzi watakaokuwa wakifanya vizuri.

“Kambi za kitaaluma  zitaendelea kuwepo katika kipindi chote nitakacho kuwepo na tutaendelea kuboresha; mwaka huu nimewaambia Wakurugenzi ni lazima kila Halmashauri itenge fedha kwa ajili ya motisha katika elimu, motisha kwa walimu na wanafunzi wanaofanya vizuri” alisema Mtaka.
Katika hatua nyingine Mtaka amewashukuru walimu, wanafunzi na wadau mbalimbali waliochangia kufanikisha kambi ya kidato cha sita, huku akiwasisitiza wanafunzi wa hao kuendeleza juhudi walizozionesha wakiwa kambini na kutumia mbinu walizopewa na walimu mahiri ili waweze kufanya vizuri mitihani yao ya mwisho.
Naye Mchungaji wa Kanisa la Waadventista Wasabato kutoka Jijini Mwanza, Nicodemo Ntabindi amewaonya wanafunzi wa Kidato cha sita kutojihusisha na masuala ya mapenzi badala yake wajikite katika masomo tu kwa sasa ili waweze kufikia ndoto zao.

Kwa upande wao wanafunzi waliokuwepo katika kambi hiyo ya Kitaaluma wamesema kambi hiyo imekuwa msaada kwa wanafunzi kwa kuwa imechangia kuwasaidia kupata ufumbuzi wa mada ngumu zilizokuwa zinawapa shida na kuahidi kufanya vizuri katika mtihani wa Taifa kutokana na namna walivyoandaliwa vema.

“Tunashukuru uwepo wa kambi hii maana imetusaidia kupata maarifa ya namna ya kujibu maswali kwenye mitihani, lakini tumeweza kusaidiwa na walimu kutatua mada ngumu ambazo zilikuwa zinatushinda, ninaamini kwa namna tulivyoandaliwa hatutamuangusha Mkuu wetu wa Mkoa” alisema mwanafunzi Farida Omary.

“Kambi hizi hazijafanyika popote hapa nchini tunamshukuru sana Mkuu wa Mkoa kwa kuja na wazo la kuwa na kambi kwa sababu tumejifunza mengi, tumekutana na wenzetu wa shule mbalimbali hapa mkoani kwetu na tukapata maarifa ambayo awali hatukuwa nayo, tuna imani tufanya vizuri “ alisema mwanafunzi Casto Nyakarungu.

Katika kambi hii Ofisi ya Mkuu wa mkoa wa Simiyu, imetoa shilingi milioni 12 kwa ajili ya motisha kwa walimu waliokuwa wakifundisha kambini hapo na imeahidi kutoa shilingi milioni nne kwa mwanafunzi atakayepata ‘division one, pointi tatu’ na kuwa miongoni mwa wanafunzi kumi bora Kitaifa.
MWISHO
Mkuu wa Mkoa.wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka akizungumza na wanafunzi wa Kidato Cha Sita Mkoani humo, wakati wa kufunga Kambi ya Kitaaluma kwa wanafunzi hao, iliyofanyika kwa takribani mwezi mmoja katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa na kuhitimishwa Aprili 28, 2019.
Baadhi ya wanafunzi wa Kidato Cha Sita Mkoani Simiyu wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa huo, Mhe. Anthony Mtaka (hayupo pichani) alipokuwa akizungumza nao wakati wa kufunga Kambi ya Kitaaluma ya Wanafunzi hao, iliyofanyika kwa takribani mwezi mmoja katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa na kuhitimishwa Aprili 28, 2019 na Mkuu wa Mkoa huo.
Aliyekuwa mlezi(Patron) wa kambi ya kitaaluma ya kidato cha sita kwa wanafunzi wa kidato cha Sita mkoani Simiyu, Mwl.Pimbili Chalya kutoka Mwandoya, akitoa tathmini ya kambi hiyo , iliyofanyika kwa takribani mwezi mmoja katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa na kuhitimishwa Aprili 28, 2019 na Mkuu wa Mkoa huo, Mhe. Anthony Mtaka.
Joseph Mathias Mwanafunzi kutoka Shule ya Sekondari Bariadi akitoa tathmini ya kambi ya kitaaluma ya kidato cha sita mkoani Simiyu, iliyofanyika kwa takribani mwezi mmoja katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa na kuhitimishwa Aprili 28, 2019 na Mkuu wa Mkoa huo, Mhe. Anthony Mtaka.
Mwanafunzi wa kidato cha Sita Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa, akitoa burudani ya wimbo, wakati wa kufunga Kambi ya Kitaaluma kwa wanafunzi hao, iliyofanyika kwa takribani mwezi mmoja katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa na kuhitimishwa Aprili 28, 2019 na Mkuu wa Mkoa huo, Mhe. Anthony Mtaka.


 Mchungaji wa Kanisa la Waadventista Wasabato kutoka Mkoani Mwanza, Nicodemo Ntabindi akizungumza na wanafunzi wa Kidato Cha Sita Mkoani Simiyu, wakati wa kufunga Kambi ya Kitaaluma kwa wanafunzi hao, iliyofanyika kwa takribani mwezi mmoja katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa na kuhitimishwa Aprili 28, 2019 na Mkuu wa Mkoa huo, Mhe. Anthony Mtaka.


 Mwalimu Dennis Wasagara ambaye pia ni mzazi akizungumza na wanafunzi wa Kidato Cha Sita Mkoani Simiyu, wakati wa kufunga Kambi ya Kitaaluma kwa wanafunzi hao, iliyofanyika kwa takribani mwezi mmoja katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa na kuhitimishwa Aprili 28, 2019 na Mkuu wa Mkoa huo, Mhe. Anthony Mtaka.


Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa, Mwl. Kuyunga Jackson akitoa tathmini ya kambi ya kitaaluma ya kidato cha sita mkoani Simiyu, wakati wa kufunga kambi hiyo , iliyofanyika kwa takribani mwezi mmoja katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa na kuhitimishwa Aprili 28, 2019 na Mkuu wa Mkoa huo, Mhe. Anthony Mtaka.
Mchungaji wa Kanisa la Waadventista Wasabato kutoka Mkoani Mwanza, Nicodemo Ntabindi (wa pili kushoto) akiongoza maombi kwa ajili ya wanafunzi wa kidato cha sita mkoani Simiyu wanaotarajia kuanza Mtihani wao wa taifa Mei 06, 2019 wakati wa kufunga Kambi ya Kitaaluma kwa wanafunzi hao, iliyofanyika kwa takribani mwezi mmoja katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa na kuhitimishwa Aprili 28, 2019 na Mkuu wa Mkoa huo, Mhe. Anthony Mtaka.
Wakuu wa Shule za Sekondari za Kidato cha Sita mkoani Simiyu, wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa huo, Mhe. Anthony Mtaka (hayupo pichani) alipokuwa akizungumza nao  pamoja na wanafunzi wa kidato cha sita , wakati wa kufunga Kambi ya Kitaaluma ya Wanafunzi hao, iliyofanyika kwa takribani mwezi mmoja katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa na kuhitimishwa Aprili 28, 2019 na Mkuu wa Mkoa huo.




Baadhi ya wanafunzi wa kidato cha sita mkoani Simiyu wakiimba wimbo wa kuwapongeza viongozi, walimu na wanafunzi wenzao mkoani humo kwa kufanikisha Kambi ya Kitaaluma ya Wanafunzi hao, iliyofanyika kwa takribani mwezi mmoja katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa na kuhitimishwa Aprili 28, 2019 na Mkuu wa Mkoa huo.

Baadhi ya wanafunzi wa Kidato Cha Sita Mkoani Simiyu wakinyosha mikonoyao juu kukubali kuwa watafanya vizuri mara baada ya kuhojiwa na  Mkuu wa Mkoa huo, Mhe. Anthony Mtaka (hayupo pichani) ikiwa wako tayari kufanya vizuri  alipokuwa akizungumza nao wakati wa kufunga Kambi ya Kitaaluma ya Wanafunzi hao, iliyofanyika kwa takribani mwezi mmoja katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa na kuhitimishwa Aprili 28, 2019 .
Vijana wa Skauti wakimvisha skafu Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka  kabla ya Mkuu huyo wa Mkoa kuhitimisha Kambi ya Kitaaluma ya Wanafunzi wa Kidato cha Sita Aprili 28, 2019  , iliyofanyika kwa takribani mwezi mmoja katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa.




 Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka akimkabidhi cheti cha shukrani Katibu wa Klabu ya Waandishi wa Habari Mkoa wa Simiyu,  Bw. Samwel Mwanga, ikiwa ni kutambua mchango wa waandishi wa habari katika kuripoti habari za Kambi ya Kitaaluma ya Wanafunzi wa Kidato cha Sita, iliyofanyika kwa takribani mwezi mmoja katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa na kuhitimishwa Aprili 28, 2019.




Mmoja wa walimu mahiri akitoa tathmini ya kambi ya kitaaluma ya kidato cha sita mkoani Simiyu wakati wa kufunga kambi hiyo , iliyofanyika kwa takribani mwezi mmoja katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa na kuhitimishwa Aprili 28, 2019 na Mkuu wa Mkoa huo, Mhe. Anthony Mtaka.
Wanafunzi wa Kidato cha Sita mkoani Simiyu, wakiwa katika maombi maalum wakati wa kufunga kambi ya kitaaluma kwa wanafunzi hao , iliyofanyika kwa takribani mwezi mmoja katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa na kuhitimishwa Aprili 28, 2019 na Mkuu wa Mkoa huo, Mhe. Anthony Mtaka.




 Mkuu wa Mkoa.wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka akizungumza na wanafunzi wa Kidato Cha Sita Mkoani humo, wakati wa kufunga Kambi ya Kitaaluma kwa wanafunzi hao, iliyofanyika kwa takribani mwezi mmoja katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa na kuhitimishwa Aprili 28, 2019.
Baadhi ya wanafunzi wa Kidato Cha Sita Mkoani Simiyu wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa huo, Mhe. Anthony Mtaka (hayupo pichani) alipokuwa akizungumza nao wakati wa kufunga Kambi ya Kitaaluma ya Wanafunzi hao, iliyofanyika kwa takribani mwezi mmoja katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa na kuhitimishwa Aprili 28, 2019 na Mkuu wa Mkoa huo.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka akimkabidhi cheti cha pongezi kwa mmoja wa walimu Mwl. Makame Makame ikiwa ni kutambua mchango wake katika kuwafundisha wanafunzi kwenye Kambi ya Kitaaluma ya Wanafunzi wa Kidato cha Sita, iliyofanyika kwa takribani mwezi mmoja katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa na kuhitimishwa Aprili 28, 2019.


Friday, April 26, 2019

KATIBU MTENDAJI NECTA AWAASA KIDATO CHA SITA KUTOJIHUSHA NA UDANGANYIFU MTIHANI WA TAIFA


Katibu MTENDAJI wa Baraza la Taifa la Mitihani Tanzania (NECTA) amewataka wanafunzi wa kidato cha sita nchini, wanaotarajia kufanya mtihani wao wa mwisho mapema mwezi Mei, 2019 kuepuka aina yoyote ya udanganyifu kwenye mtihani huo.

Dkt. Msonde ameyasema hayo wakati akiongea na wanafunzi wa kidato cha sita mkoani Simiyu waliopo kwenye kambi ya kitaaluma katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa, ambayo inayohusisha wanafunzi 1166 kutoka shule 12 zikiwemo 10 za umma na mbili za binafsi zenye kidato cha sita.

"Niwatake msifanye asilani habari yoyote ya udanganyifu kwenye mtihani wenu, mkifanya hayo tu kwanza yatawafanya mshindwe lakini pili tutakaponusa tu harufu yoyote ya udanganyifu tutawafutia matokeo"alisema Dkt. Msonde.

Wakati huo huo Dot. msonde amewataka wanafunzi hao kuondokana na dhana kwamba mtihani wa Taifa ni mgumu hali inayopelekea kuwa na homa ya mtihani(hofu), badala yake wajiamini na wajiandae vema kwa kuzingatia waliyofundishwa na walimu wao.

Pamoja na hayo amewapongeza viongozi wa mkoa wa Simiyu kwa ubunifu wao wa kuanzisha kambi za kitaaluma hatua inayopelekea mkoa huo kupiga hatua ya katika ufaulu wa mitihani ya kidato cha sita na kidato cha nne.

Awali akimkaribisha Katibu Mtendaji wa NECTA,  Afisa Elimu mkoa wa Simiyu, Mwl. Ernest Hinju amesema kuwa awali mkoa ulikuwa na ufaulu mbaya lakini kupitia kambi ufaulu umepanda kuanzia matokeo ya kidato cha sita kutoka nafasi ya 26 mwaka 2017 hadi nafasi ya 10 mwaka 2018 na kidato cha nne kutoka nafasi ya 11 mwaka 2017 hadi nafasi ya 9 mwaka 2018.

Akiongea kwa niaba ya walimu mkuu wa shule ya sekondari ya wasichana Maswa Mwl. Kuyunga Jackson amesema kuwa vijana wa kidato cha sita Simiyu wamepikwa vizuri kitaaluma hivyo matarajio yao ni kuingia tatu bora kitaifa.

Katika hatua nyingine wanafunzi waliopo kambini hapo wamesema kuwa ujio wa katibu mtendaji NECTA umekuwa chachu ya ufaulu wao na kuahidi kuyafanyia kazi yale yote aliyoyaeleza ikiwemo kuepuka udanganyifu pamoja na kuondoa homa ya mtihani.

"Tunakushukuru Sana kwa ujio wako umetujenga na kutuondolea hofu ya mtihani, tutafanyia kazi uliyotueleza, tunakuhakikishia hatutajihusisha na udanganyifu wowote kwa sababu walimu wametuandaa vizuri na  tunajua udanganyifu unaweza kusababisha tusifikie ndoto zetu; tutazingatia yote tuliyofundishwa na walimu wetu" alisema Julieth John.
MWISHO

Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani la Taifa(NECTA), Dkt. Charles Msonde akizungumza na wanafunzi wa Kidato Cha Sita mkoani Simiyu walio katika kambi ya Kitaaluma katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa, wakati alipotembelea kambi hiyo Aprili 25,2019.
Baadhi ya Wanafunzi wa Kidato Cha Sita mkoani Simiyu wakimsikiliza Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani la Taifa(NECTA), Dkt. Charles Msonde (hayupo pichani) wakati alipowatembelea katika kambi ya Kitaaluma inayoendelea katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa, Aprili 25, 2019.
Afisa Elimu wa Mkoa wa Simiyu, Mwl. Ernest Hinju akizungumza kabla ya kumkaribisha Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani la Taifa(NECTA), Dkt. Charles Msonde azungumze na wanafunzi wa Kidato Cha Sita mkoani Simiyu, walio katika kambi ya Kitaaluma katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa  Aprili 25, 2019.
Mwanafunzi wa Kidato cha Sita Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa,  Julieth John akitoa shukrani kwa Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani la Taifa(NECTA), Dkt. Charles Msonde alipowatembelea Wanafunzi wa Kidato Cha Sita Mkoani Simiyu, Aprili 25, 2019  katika kambi ya Kitaaluma Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa
PICHA 4:-Mwanafunzi wa Kidato Cha Sita Shule ya Sekondari Simba wa Yuda,  Innocent Leonard  akitoa shukrani kwa Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani la Taiga(NECTA), Dkt. Charles Msonde alipowatembelea Wanafunzi wa Kidato Cha Sita Mkoani Simiyu, Aprili 25, 2019  katika kambi ya Kitaaluma Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa.
Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa, Mwl. Kuyunga Jackson akizungumza kwa niaba ya walimu wakati wa ziara ya Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani la Taifa(NECTA), Dkt. Charles Msonde katika kambi ya Kitaaluma kwa Wanafunzi wa KIDATO Cha Sita katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa, Aprili 25, 2019. 
Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani la Taifa(NECTA), Dkt. Charles Msonde(katikati kwa walioketi) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Maafisa wa Idara ya Elimu Mkoa wa Simiyu, walimu  wanafunzi wa Kidato Cha Sita mkoani Simiyu, Mara baada ya kuhitimisha ziara yake katika kambi ya Kitaaluma ya Wanafunzi wa Kidato cha Sita inayoendelea katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa.
Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani la Taifa(NECTA), Dkt. Charles Msonde (katikati kwa walioketi)akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Maafisa wa Idara ya Elimu Mkoa wa Simiyu, walimu  wanafunzi wa Kidato Cha Sita mkoani Simiyu, Mara baada ya kuhitimisha ziara yake katika kambi ya Kitaaluma ya Wanafunzi wa Kidato cha Sita inayoendelea katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa.
Picha 7:-Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani la Taifa(NECTA), Dkt. Charles Msonde(wa nne kulia) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Maafisa wa Idara ya Elimu Mkoa wa Simiyu, walimu mahiri wanaowafundisha wanafunzi wa Kidato Cha Sita katikankambibya Kitaaluma ya Wanafunzi wa Kidato Cha Sita mkoani Simiyu, Mara baada ya kutembelea kambi  hiyo Aprili 25, 2019 ambayo inayoendelea katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa.
Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani la Taifa(NECTA), Dkt. Charles Msonde(kushoto) akiteta jambo na Afisa Elimu wa Mkoa wa Simiyu, Mwl. Ernest Hinju wakati alipowatembeleawanafunzi wa kidato cha sita Simiyu katika kambi ya Kitaaluma inayoendelea katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa, Aprili 25, 2019.






RAS SIMIYU AWATAKA WAGANGA WAKUU, MAAFISA LISHE KUWASILISHA MPANGO KAZI WA LISHE


Katibu Tawala Mkoa wa Simiyu, Bw. Jumanne Sagini amewaagiza Maafisa Lishe na waganga wakuu wa wilaya mkoani hapa kufikia mwisho wa mwezi huu wa Aprili 2019, wawasilishe mpango kazi wa lishe unaoainisha lishe inayoweza kuandaliwa kwa kutumia vyakula vinavyopatikana katika mazingira ya mkoa huu, ili waweze kutoa elimu ya lishe bora kwa wananchi na kukabiliana na utapiamlo.

Sagini ameyasema hayo katika katika kikao cha Kamati ya Lishe Mkoa na Kamati tendaji  ya Mkoa ya uendeshaji wa mradi wa lishe wa Right Start Initiative, kilichofanyika Aprili 25, 2019 Mjini Bariadi.
Katibu Tawala wa Mkoa, Bw. Jumanne Sagini akizungumza na wajumbe wa Kamati ya Lishe mkoa na wadau wa lishe katika kikao cha Kamati ya Lishe Mkoa na Kamati tendaji  ya Mkoa ya uendeshaji wa mradi wa lishe wa Right Start Initiative, kilichofanyika Aprili 25, 2019 Mjini Bariadi.

Mganga Mkuu wa Mkoa, Dkt. Mageda Kihulya  akizungumza na wajumbe wa Kamati ya Lishe mkoa na wadau wa lishe katika kikao cha Kamati ya Lishe Mkoa na Kamati tendaji  ya Mkoa ya uendeshaji wa mradi wa lishe wa Right Start Initiative, kilichofanyika Aprili 25, 2019 Mjini Bariadi.
Afisa Lishe Mkoa wa Simiyu, Dkt. Chacha Magige akiwasilisha taarifa ya lishe ya mkoa katika kikao cha Kamati ya Lishe Mkoa na Kamati tendaji  ya Mkoa ya uendeshaji wa mradi wa lishe wa Right Start Initiative, kilichofanyika Aprili 25, 2019 Mjini Bariadi.
Dkt.Sylvester Nandi kutoka Shirika lisilo la Kiserikali la Nutrition International akiwasilisha taarifa yake katika kikao cha Kamati ya Lishe Mkoa na Kamati tendaji  ya Mkoa ya uendeshaji wa mradi wa lishe wa Right Start Initiative, kilichofanyika Aprili 25, 2019 Mjini Bariadi.
Afisa Mradi wa Right Start Initiative kutoka AMREF Bi. Yasinta Bahati akiwasilisha taarifa ya mradi huo kwa wajumbe wa kikao cha Kamati ya Lishe Mkoa na Kamati tendaji  ya Mkoa ya uendeshaji wa mradi wa lishe wa Right Start Initiative, kilichofanyika Aprili 25, 2019 Mjini Bariadi.
Mtaalam kutoka Programu ya USAID  Boresha Afya akiwasilisha taarifa ya mradi huo kwa wajumbe wa kikao cha Kamati ya Lishe Mkoa na Kamati tendaji  ya Mkoa ya uendeshaji wa mradi wa lishe wa Right Start Initiative, kilichofanyika Aprili 25, 2019 Mjini Bariadi.
Mganga Mkuu wa Wilaya ya Meatu, Dkt...... akichangia jambo katika kikao cha Kamati ya Lishe Mkoa na Kamati tendaji  ya Mkoa ya uendeshaji wa mradi wa lishe wa Right Start Initiative, kilichofanyika Aprili 25, 2019 Mjini Bariadi..
Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bw. Jumanne Sagini(katikati  walioketi) akiwa katika picha ya pamoja na wajumbe wa Kamati ya Lishe mkoa na wadau wa lishe baada ya  kikao cha Kamati ya Lishe Mkoa na Kamati tendaji  ya Mkoa ya uendeshaji wa mradi wa lishe wa Right Start Initiative, kilichofanyika Aprili 25, 2019 Mjini Bariadi.
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Kikristo (CCT) Mkoa wa Simiyu, Mchungaji Martin Nketo akichangia hoja katika kikao cha Kamati ya Lishe Mkoa na Kamati tendaji  ya Mkoa ya uendeshaji wa mradi wa lishe wa Right Start Initiative, kilichofanyika Aprili 25, 2019 Mjini Bariadi.
Sheikh wa Mkoa wa Simiyu, Mahamoud Kalokola akichangia hoja katika kikao cha Kamati ya Lishe Mkoa na Kamati tendaji  ya Mkoa ya uendeshaji wa mradi wa lishe wa Right Start Initiative, kilichofanyika Aprili 25, 2019 Mjini Bariadi.
Baadhi ya wajumbe wa Kamati ya Lishe mkoa na wadau wa lishe wakiwa katika  kikao cha Kamati ya Lishe Mkoa na Kamati tendaji  ya Mkoa ya uendeshaji wa mradi wa lishe wa Right Start Initiative, kilichofanyika Aprili 25, 2019 Mjini Bariadi.
Meneja Mradi CUAMM, Bi. FortHappiness Mumba akiwasilisha taarifa ya mradi  hoja katika kikao cha Kamati ya Lishe Mkoa na Kamati tendaji  ya Mkoa ya uendeshaji wa mradi wa lishe wa Right Start Initiative, kilichofanyika Aprili 25, 2019 Mjini Bariadi.

Sunday, April 21, 2019

WAZIRI KAIRUKI ATOA WITO KWA WAWEKEZAJI WAZAWA KUCHANGAMKIA FURSA ZA UWEKEZAJI ZILIZOPO NCHINI NA KUSAJILI MIRADI YA UWEKEZAJI



Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Uwekezaji, Mhe.  Angela Kairuki ametoa wito kwa chama cha wanataaluma na wajasiriamali wa Kanisa la Waadventista Wasabato  Tanzania (ATAPE) na wawekezaji wengine wazawa kuchangamkia fursa mbalimbali za uwekezaji zilizopo nchini na kusajili miradi  yao ya Uwekezaji katika Tume ya uwekezaji ya Taifa (TIC).

Kairuki ameyasema hayo wakati akifunga Mkutano wa 20 wa chama cha wanataaluma na wajasiriamali wa Kanisa la Waadventista Wasabato  Tanzania (ATAPE) Mjini Bariadi, ambapo amebainisha kuwa kwa mwaka huu 2019 wawekezaji wazawa zaidi ya asilimia 72 wamesajili miradi yao ya uwekezaji TIC.

“ Kwa mwaka huu peke yake tumepata wawekezaji wazawa waliosajili miradi yao ya uwekezaji TIC zaidi ya asilimia 72, hii inanipa faraja sana kama waziri wa nchi ninayesimamia uwekezaji ninapoona Watanzania wenzangu wanachangamkia fursa”

"Naomba mchangamkie fursa hizo kwa sababu wawekezaji wa nje tunapenda waje tu endapo watakuja kuungana nasi kwenye mtaji, kubadilishana nasi ujuzi na uzoefu " alisema Kairuki.

Ameongeza kuwa Serikali imeendelea kuboresha mazingira ya biashara, uwekezaji na kuweka vipaumbele kwa ajili ya kuvutia wawekezaji katika sekta ambazo zitakuwana athari na tija kubwa kiuchumi kwa wananchi, ili kuimarisha minyororo ya thamani katika kilimo,uvuvi, na mifugo ambayo ni maeneo yanayoajiri Watanzania wengi zaidi.

Aidha, Waziri Kairuki amezitaja sekta nyingine za kipaumbele kuwa ni  uzalishaji wa mafuta ya kula kwa kutumia mbegu zinazozalishwa nchini, uzalishaji wa sukari, uzalishaji wa dawa za binadamu, vifaa tiba na kemikali, ujenzi wa miundombinu ya uvuvi wa kisasa, viwanda vya kuchakata samaki, kusindika nyama, viwanda vya kubangua korosho, viwanda vitakavyotumia pamba na viwanda vya  pembejeo na mbolea.

Katika hatua nyingine Waziri Kairuki ameipongeza ATAPE kwa jinsi  inavyoshirikiana na Serikali katika kutoa huduma mbalimbali za kijamii ikiwemo sekta ya afya, elimu, maji pamoja na huduma nyingine.

Kairuki amesema serikali pekee  haiwezi kutatua changamoto zote hivyo  kwa kushirikiana na wadau ikiwemo taasisi za dini wanaweza kuwahudumia wananchi na kuleta mabadiliko chanya ikiwa ni pamoja na  kuhubiri amani, huku akisisitiza kuwa masomo ya ujasiriamali yanayotolewa kwa wana ATAPE wayatumie kwa manufaa ya kanisa na jamii kwa ujumla.


Awali akimkatibisha waziri Kairuki, mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka amesema mkutano huo umewasaidia  watu wa  Simiyu  kukutana na watu wa maeneo mengine hatua iliyopelekea kubadilishana uzoefu  sambamba na kuongeza na kupata masoko mapya .

‘’watu wetu wameongeza wigo wa masoko, mmebadilishana uzoefu ....huu ni mkoa wa kibiashara na ni mkoa wenye fursa nyingi;  tunajenga tawi la chuo cha usimamizi wa fedha (IFM) hivyo ninawaalika wafanyabiashara na Watanzania wote kuja kuwekeza ujenzi wa hosteli eneo lile linalojengwa tawi hilo"alisisitiza Mtaka.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa ATAPE Freddie Manento amesema kwa miaka mitatu ATAPE imewekeza miradi ya bilioni 1.2 katika miradi yenye manufaa kwa kanisa, wanajamii na wana ATAPE.

Alisema wamewekeza kwenye miradi ya maji kwenye maeneo yenye uhitaji mkubwa, miradi ya miti ya matund), korosho na miradi ya mashamba ya mihogo kwa kutengeneza ajira na faida katika vijiji walivyolima mashamba yao.

‘’Wana ATAPE wamejitoa kwelikweli na wameitikia dhana yetu ya kutumia vipaji na rasilimali zetu kwa ajili ya kazi ya MUNGU, hii iko katika mathayo 28;19, 20…hii ndio dhana yao’’ alisema Manento.

Mkutano wa Wanataaluma na Wajasiriamali (ATAPE) kutoka kanisa la Waadventista Wasabato umefanyika mkoani Simiyu kwa muda wa siku sita ambapo umehudhuriwa na wananchama zaidi ya 1500.

.....MWISHO....


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Uwekezaji Mhe. Angela Kairuki akizungumza na Wanachama wa Chama cha Wanataaluma na Wajasiriamali wa Kanisa la Waadventista Wasabato Tanzania(ATAPE), wakati wa kufunga mkutano mkuu wa 20 wa Chama hicho Mjini Bariadi,  Aprili 20, 2019.

Baadhi ya Wanachama wa Chama cha Wanataaluma na Wajasiriamali wa Kanisa la Waadventista Wasabato Tanzania(ATAPE), wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Uwekezaji, Mhe. Angela Kairuki wakati wa kufunga mkutano mkuu wa 20 wa Chama hicho Mjini Bariadi, Aprili 20, 2019.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu,Mhe. Anthony Mtaka akizungumza na Wanachama wa Chama cha Wanataaluma na Wajasiriamali wa Kanisa la Waadventista Wasabato Tanzania(ATAPE), wakati wa kufunga mkutano mkuu wa 20 wa Chama hicho Mjini Bariadi, Aprili 20, 2019.
Mwenyekiti wa Chama cha Wanataaluma na Wajasiriamali wa Kanisa la Waadventista Wasabato Tanzania(ATAPE), Bw. Freddie Manento akimtambulisha rasmi  Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Uwekezaji, Mhe. Angela Kairuki (mwenye skafu) kama mwanachama mpya mbele ya wanachama, wakati wa kufunga mkutano mkuu wa 20 wa chama hicho Mjini Bariadi, 2019. 
Kutoka kushoto Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Uwekezaji, Mhe. Angela Kairuki, Msaidizi wa Askofu Mkuu wa Kanisa la Waadventista Wasabato, Ukanda wa Afrika Mashariki na Kati(nchi 11) , Mchungaji Emanuel Pelote, Mkuu wa Mkoa wa Simiyu,Mhe. Anthony Mtaka na Mchungaji Joshua Njuguna kutoka nchini Kenya, wakifurahia jambo wakati wa kufunga mkutano mkuu wa 20 wa Chama cha Wanataaluma na Wajasiriamali wa Kanisa la Waadventista Wasabato Tanzania(ATAPE),  hicho Mjini Bariadi, Aprili 20, 2019.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu,Mhe. Anthony Mtaka(mwenye shati la Kitengekushoto) akiimba pamoja na wanakwaya ya Bulka kutoka Jijini Arusha, wakati wa kufunga mkutano mkuu wa 20 wa Chama cha Wanataaluma na Wajasiriamali wa Kanisa la Waadventista Wasabato Tanzania(ATAPE),  hicho Mjini Bariadi, Aprili 20, 2019.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu,Mhe. Anthony Mtaka akionesha ngao/tuzo alichopewa na Chama cha Wanataaluma na Wajasiriamali wa Kanisa la Waadventista Wasabato Tanzania(ATAPE),   kama shukrani ya kuwezesha mkutano mkuu wa 20 wa chama hicho kufanyika Mjini Bariadi mkoani Simiyu, wakati wa kufunga mkutano mkuu wa 20 wa chama hicho Mjini Bariadi, 2019.
Askofu wa Kanisa la Waadventista Wasabato Jimbo Kuu la Kaskazini , Dkt. Godwin Lekondayo akizungumza na Wanachama wa Chama cha Wanataaluma na Wajasiriamali wa Kanisa la Waadventista Wasabato Tanzania(ATAPE), wakati wa kufunga mkutano mkuu wa 20 wa Chama hicho Mjini Bariadi, Aprili 20, 2019.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Uwekezaji Mhe. Angela Kairuki akiteta jambo na Mkuu wa Mkoa wa Simiyu,Mhe. Anthony Mtaka, wakati wa kufunga mkutano mkuu wa 20 wa Chama cha Wanataaluma na Wajasiriamali wa Kanisa la Waadventista Wasabato Tanzania(ATAPE),Mjini Bariadi, Aprili 20, 2019 (wa pili kulia)  Askofu wa Kanisa la Waadventista Wasabato Jimbo Kuu la Kusini, Mch. Mark Malekana na kulia ni Katibu wa ATAPE James Laban.
Vijana watenegenza njia wa Kanisa la Waadventista Wasabato Tanzania wakitoa heshima kwa viongozi kablaya kufunga mkutano mkuu wa 20 wa Chama cha Wanataaluma na Wajasiriamali wa Kanisa la Waadventista Wasabato Tanzania(ATAPE),Mjini Bariadi, Aprili 20, 2019.
Kutoka kushoto ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Uwekezaji, Mhe. Angela Kairuki ,Mkuu wa Mkoa wa Simiyu,Mhe. Anthony Mtaka, Askofu wa Kanisa la Waadventista Wasabato Jimbo Kuu la Kusini, Mch. Mark Malekana na Katibu wa Chama cha Wanataaluma na Wajasiriamali wa Kanisa la Waadventista Wasabato Tanzania(ATAPE), James Laban wakifuatailia jambo kwa makini wakati wa kufunga mkutano mkuu wa 20 wa ATAPE  Mjini Bariadi, Aprili 20, 2019.
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi, Mhe. Robert Lweyo akimsalimia Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Uwekezaji, Mhe. Angela Kairuki mara baada ya kuwasili Mjini Bariadi kwa ajili ya kufunga mkutano mkuu wa 20 wa Chama cha Wanataaluma na Wajasiriamali wa Kanisa la Waadventista Wasabato Tanzania(ATAPE), Aprili 20, 2019. 
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Uwekezaji, Mhe. Angela Kairuki (mwenye skafu) akimkabidhi Askofu wa Kanisa la Waadventista Wasabato Jimbo Kuu la Kusini, Mch. Mark Malekana ngao/tuzo iliyotolewa na Chama cha Wanataaluma na Wajasiriamali wa Kanisa la Waadventista Wasabato Tanzania(ATAPE) kutambua mchango wake, wakati wa kufunga mkutano mkuu wa ATAPE Mjini Bariadi, Aprili 20, 2019.
Kwaya ya Kanisa la Waadventista Wasabato kutoka Suguti wilayani Musoma Mkoani Mara wakiimba wakati wa kufunga mkutano wa 20 wa Chama cha Wanataaluma na Wajasiriamali wa Kanisa la Waadventista Wasabato Tanzania(ATAPE) ,  Mjini Bariadi, Aprili 20, 2019.
Kwaya ya Kanisa la Waadventista Wasabato kutoka Nyarugusu Mkoani Geita wakiimba wakati wa kufunga mkutano wa 20 wa Chama cha Wanataaluma na Wajasiriamali wa Kanisa la Waadventista Wasabato Tanzania(ATAPE) ,  Mjini Bariadi, Aprili 20, 2019.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu,Mhe. Anthony Mtaka akifurahia jambo na Mchungaji Dkt. Joshua Njuguna kutoka nchini Kenya wakati wa kufunga mkutano wa 20 wa Chama cha Wanataaluma na Wajasiriamali wa Kanisa la Waadventista Wasabato Tanzania(ATAPE) ,  Mjini Bariadi, Aprili 20, 2019.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Uwekezaji Mhe. Angela Kairuki akizungumza na Wanachama wa Chama cha Wanataaluma na Wajasiriamali wa Kanisa la Waadventista Wasabato Tanzania(ATAPE), wakati wa kufunga mkutano mkuu wa 20 wa Chama hicho Mjini Bariadi,  Aprili 20, 2019.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu,Mhe. Anthony Mtaka(kulia) akiteta jambo na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Uwezeshaji, Mhe. Angela Kairuki, wakati wa kufunga mkutano wa 20 wa Chama cha Wanataaluma na Wajasiriamali wa Kanisa la Waadventista Wasabato Tanzania(ATAPE) ,  Mjini Bariadi, Aprili 20, 2019.
Baadhi ya wadau(waliosimama) waliotoa Ng’ombe 12 kwa ajili ya chakula cha wanachama wakati wa mkutano wa 20 wa Chama cha Wanataaluma na Wajasiriamali wa Kanisa la Waadventista Wasabato Tanzania(ATAPE) ,  kaam walivyotambulishwa na Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe. Anthony Mtaka wakati wa kufunga mkutano huo Mjini Bariadi, Aprili 20, 2019.
PICHA T:-Baadhi ya viongozi wa Serikali na Wanachama wa Chama cha Wanataaluma na Wajasiriamali wa Kanisa la Waadventista Wasabato Tanzania(ATAPE), wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Uwekezaji, Mhe. Angela Kairuki wakati wa kufunga mkutano mkuu wa 20 wa Chama hicho Mjini Bariadi, Aprili 20, 2019.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Uwekezaji, Mhe. Angela Kairuki akizungumza na Wanachama wa Chama cha Wanataaluma na Wajasiriamali wa Kanisa la Waadventista Wasabato Tanzania(ATAPE), wakati wa kufunga mkutano mkuu wa 20 wa Chama hicho Mjini Bariadi,  Aprili 20, 2019

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!