Friday, April 26, 2019

KATIBU MTENDAJI NECTA AWAASA KIDATO CHA SITA KUTOJIHUSHA NA UDANGANYIFU MTIHANI WA TAIFA


Katibu MTENDAJI wa Baraza la Taifa la Mitihani Tanzania (NECTA) amewataka wanafunzi wa kidato cha sita nchini, wanaotarajia kufanya mtihani wao wa mwisho mapema mwezi Mei, 2019 kuepuka aina yoyote ya udanganyifu kwenye mtihani huo.

Dkt. Msonde ameyasema hayo wakati akiongea na wanafunzi wa kidato cha sita mkoani Simiyu waliopo kwenye kambi ya kitaaluma katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa, ambayo inayohusisha wanafunzi 1166 kutoka shule 12 zikiwemo 10 za umma na mbili za binafsi zenye kidato cha sita.

"Niwatake msifanye asilani habari yoyote ya udanganyifu kwenye mtihani wenu, mkifanya hayo tu kwanza yatawafanya mshindwe lakini pili tutakaponusa tu harufu yoyote ya udanganyifu tutawafutia matokeo"alisema Dkt. Msonde.

Wakati huo huo Dot. msonde amewataka wanafunzi hao kuondokana na dhana kwamba mtihani wa Taifa ni mgumu hali inayopelekea kuwa na homa ya mtihani(hofu), badala yake wajiamini na wajiandae vema kwa kuzingatia waliyofundishwa na walimu wao.

Pamoja na hayo amewapongeza viongozi wa mkoa wa Simiyu kwa ubunifu wao wa kuanzisha kambi za kitaaluma hatua inayopelekea mkoa huo kupiga hatua ya katika ufaulu wa mitihani ya kidato cha sita na kidato cha nne.

Awali akimkaribisha Katibu Mtendaji wa NECTA,  Afisa Elimu mkoa wa Simiyu, Mwl. Ernest Hinju amesema kuwa awali mkoa ulikuwa na ufaulu mbaya lakini kupitia kambi ufaulu umepanda kuanzia matokeo ya kidato cha sita kutoka nafasi ya 26 mwaka 2017 hadi nafasi ya 10 mwaka 2018 na kidato cha nne kutoka nafasi ya 11 mwaka 2017 hadi nafasi ya 9 mwaka 2018.

Akiongea kwa niaba ya walimu mkuu wa shule ya sekondari ya wasichana Maswa Mwl. Kuyunga Jackson amesema kuwa vijana wa kidato cha sita Simiyu wamepikwa vizuri kitaaluma hivyo matarajio yao ni kuingia tatu bora kitaifa.

Katika hatua nyingine wanafunzi waliopo kambini hapo wamesema kuwa ujio wa katibu mtendaji NECTA umekuwa chachu ya ufaulu wao na kuahidi kuyafanyia kazi yale yote aliyoyaeleza ikiwemo kuepuka udanganyifu pamoja na kuondoa homa ya mtihani.

"Tunakushukuru Sana kwa ujio wako umetujenga na kutuondolea hofu ya mtihani, tutafanyia kazi uliyotueleza, tunakuhakikishia hatutajihusisha na udanganyifu wowote kwa sababu walimu wametuandaa vizuri na  tunajua udanganyifu unaweza kusababisha tusifikie ndoto zetu; tutazingatia yote tuliyofundishwa na walimu wetu" alisema Julieth John.
MWISHO

Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani la Taifa(NECTA), Dkt. Charles Msonde akizungumza na wanafunzi wa Kidato Cha Sita mkoani Simiyu walio katika kambi ya Kitaaluma katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa, wakati alipotembelea kambi hiyo Aprili 25,2019.
Baadhi ya Wanafunzi wa Kidato Cha Sita mkoani Simiyu wakimsikiliza Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani la Taifa(NECTA), Dkt. Charles Msonde (hayupo pichani) wakati alipowatembelea katika kambi ya Kitaaluma inayoendelea katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa, Aprili 25, 2019.
Afisa Elimu wa Mkoa wa Simiyu, Mwl. Ernest Hinju akizungumza kabla ya kumkaribisha Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani la Taifa(NECTA), Dkt. Charles Msonde azungumze na wanafunzi wa Kidato Cha Sita mkoani Simiyu, walio katika kambi ya Kitaaluma katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa  Aprili 25, 2019.
Mwanafunzi wa Kidato cha Sita Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa,  Julieth John akitoa shukrani kwa Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani la Taifa(NECTA), Dkt. Charles Msonde alipowatembelea Wanafunzi wa Kidato Cha Sita Mkoani Simiyu, Aprili 25, 2019  katika kambi ya Kitaaluma Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa
PICHA 4:-Mwanafunzi wa Kidato Cha Sita Shule ya Sekondari Simba wa Yuda,  Innocent Leonard  akitoa shukrani kwa Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani la Taiga(NECTA), Dkt. Charles Msonde alipowatembelea Wanafunzi wa Kidato Cha Sita Mkoani Simiyu, Aprili 25, 2019  katika kambi ya Kitaaluma Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa.
Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa, Mwl. Kuyunga Jackson akizungumza kwa niaba ya walimu wakati wa ziara ya Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani la Taifa(NECTA), Dkt. Charles Msonde katika kambi ya Kitaaluma kwa Wanafunzi wa KIDATO Cha Sita katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa, Aprili 25, 2019. 
Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani la Taifa(NECTA), Dkt. Charles Msonde(katikati kwa walioketi) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Maafisa wa Idara ya Elimu Mkoa wa Simiyu, walimu  wanafunzi wa Kidato Cha Sita mkoani Simiyu, Mara baada ya kuhitimisha ziara yake katika kambi ya Kitaaluma ya Wanafunzi wa Kidato cha Sita inayoendelea katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa.
Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani la Taifa(NECTA), Dkt. Charles Msonde (katikati kwa walioketi)akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Maafisa wa Idara ya Elimu Mkoa wa Simiyu, walimu  wanafunzi wa Kidato Cha Sita mkoani Simiyu, Mara baada ya kuhitimisha ziara yake katika kambi ya Kitaaluma ya Wanafunzi wa Kidato cha Sita inayoendelea katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa.
Picha 7:-Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani la Taifa(NECTA), Dkt. Charles Msonde(wa nne kulia) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Maafisa wa Idara ya Elimu Mkoa wa Simiyu, walimu mahiri wanaowafundisha wanafunzi wa Kidato Cha Sita katikankambibya Kitaaluma ya Wanafunzi wa Kidato Cha Sita mkoani Simiyu, Mara baada ya kutembelea kambi  hiyo Aprili 25, 2019 ambayo inayoendelea katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa.
Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani la Taifa(NECTA), Dkt. Charles Msonde(kushoto) akiteta jambo na Afisa Elimu wa Mkoa wa Simiyu, Mwl. Ernest Hinju wakati alipowatembeleawanafunzi wa kidato cha sita Simiyu katika kambi ya Kitaaluma inayoendelea katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa, Aprili 25, 2019.






0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!