Thursday, April 30, 2020

MADENI YA PAMBA KULIPWA KABLA YA MSIMU MPYA : KATIBU MKUU KILIMO


Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo, Bw. Gerald Kusaya amesema Serikali itahakikisha madeni yote ya Vyama vya ushirika vya Msingi(AMCOS), wakulima, ushuru wa Halmashauri na Vyama Vikuu vya Ushirika (UNIONS) kwa zao la pamba ambayo bado hayajalipwa yanalipwa kabla ya kuanza kwa msimu mpya wa mwaka 2020.

Kusaya ameyasema hayo Aprili 29, 2020 katika kikao alichofanya na baadhi ya viongozi wa mkoa wa Simiyu na wanunuzi wa pamba ambacho kimefanyika Mjini Bariadi wakati akiwa katika ziara ya siku moja mkoani Simiyu.

“Serikali inayatambua madeni yote kwenye zao la pamba AMCOS na Vyama Vikuu vya Ushirika vinadai, Halmashauri zetu nazo zinadai ushuru lakini pia hata kwenye mfuko wa pembejeo; ni lengo la serikali na jitihada zinazofanywa na wizara ya Kilimo na wizara nyingine kwa kuwa hili ni suala mtambuka, kuhakikisha madeni yote yanamalizika kabla hatujaanza msimu mpya ,” alisema Kusaya.

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka amesema Vyama vya msingi havijalipwa, wakulima 7000 hawajalipwa na Halmashauri, hazijalipwa ushuru wa pamba takribanishilingi bilioni 3.5,  ambapo amebainisha kuwa mapato ya ndani ya Halmashauri yanategemea ushuru wa pamba kwa asilimia 70 hivyo madeni hayo yameathiri shughuli za uendeshaji wa Halmashauri.

“ Wakulima wetu 7000 bado wanadai fadha za kilo milioni 2.6, AMCOS zinadai shilingi bilioni 3.5, Chama chetu Kikuu cha Ushirika kinadai milioni 729, Halmashauri zetu zinadai bilioni 3.5 ni vema jambo hili likafanyiwa kazi na  (maeneo hayo) viungo vyote hivi kwenye zao la pamba vikaunganishwa vizuri ili kuwe na ufanisi katika msimu ujao,” alisema Mtaka.

Kwa upande wake Katibu wa Chama cha Wanunuzi wa Pamba nchini, Bwana Boazi Ogolla akitoa taarifa kwa niaba ya wanunuzi amesema wanunuzi wanaiomba Serikali kutekeleza ahadi yake ya kulipa fidia ya hasara waliyopata wanunuzi mara baada ya kununua pamba kwa bei elekezi ya shilingi 1200 ambayo ilikuwa juu zaidi ya bei ya soko la dunia.

Ogolla amesema kushindwa kulipwa fidia hiyo kumesababisha wanunuzi kushindwa kulipa ushuru wa pamba kwa Halmashauri, vyama vya ushirika, madeni ya wakulima, malipo ya mchango wa mfuko wa pembejeo, madeni ya watoa huduma na benki(wakopeshaji).

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Simiyu, Mhe. Enock Yakobo ameitaka serikali kutimiza ahadi hiyo ya kuhakikisha madeni yote yanalipwa kabla ya msimu kuanza ili msimu mpya usiwe na vikwazo vyovyote.

Katika hatua nyingine Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo, Gerald Musabila Kusaya  amesema hajaridhishwa na kasi ya ujenzi wa jengo la Wizara ya Kilimo linalojengwa viwanja vya Nane nane Nyakabindi Bariadi, Simiyu na kumtaka mkandarasi  ambaye ni Suma JKT kuhakikisha ujenzi unakamilika kabla ya Mei 30, 2020.

Ujenzi wa jengo hilo ulianza mwaka jana 2019  na lilitakiwa kukamilika machi 30 na hadi sasa limefikia asilimia 70 ya ujenzi huku changamoto ikitajwa kuwa ni mabadiliko ya mchoro.
MWISHO

 Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo, Bw. Gerald Kusaya akiangalia mbegu ya pamba yenye manyoya ambayo inachakatwa katika Kiwanda cha kuchambua pamba cha NGS kilichopo Bariadi wakati wa ziara yake ya siku moja Aprili 29, 2020 mkoani Simiyu.
 Katibu wa Chama cha Wanunuzi wa Pamba nchini, Boaz Ogolla akitoa maelezo ya hatua za uchambuzi wa pamba kwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo, Bw. Gerald Kusaya wakati alipotembelea kiwanda cha kuchambua pamba cha Alliance Ginnery Limited kilichopo Kasoli wilayani Bariadi wakati wa ziara yake ya siku moja Aprili 29, 2020. 
 Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka akizungumza na wadau wa pamba walioshiriki katika kikao cha Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo, Bw.Gerald Kusaya wakati wa zaira yake ya siku moja mkoani Simiyu, Aprili 29, 2020.
 Mmoja wa wanunuzi wa zao la pamba mkoani Simiyu, Bw. Gungu Silanga akichangia hoja katika kikao cha Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo, Bw. Gerald Kusaya wakati wa zaira yake ya siku moja mkoani Simiyu, Aprili 29, 2020.
 Katibu wa Chama cha Wanunuzi wa Pamba nchini na Mkurugenzi wa Kiwanda cha Kuchambua Pamba cha Alliance Ginneries Limited kilicopo Bariadi, Bw.  Boaz Ogolla(wa pili kulia)akimuongoza Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo, Bw.Gerald Kusaya wakati wa zaira yake ya siku moja mkoani Simiyu, Aprili 29, 2020.
 Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo, Bw. Gerald Kusaya akiangalia mbao zinazotumika katika ujenzi wa Jengo la Wizara ya Kilimo linalojengwa katika Uwanja wa Nanenane Nyakabindi Mjini Bariadi wakatinwa ziara yake ya siku moja Aprili 29, 2020.
 Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo, Bw. Gerald Kusaya akiangalia mafuta yanayozalishwa kutokana na mbegu za pamba katika Kiwanda cha kuchambua pamba cha NGS kilichopo wilayani Bariadi wakati wa ziara yake ya siku moja Aprili 29, 2020.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo, Bw. Gerald Kusaya (mwenye suti ya bluu) na viongozi wengine wakiondoa mara baada ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa Jengo la Wizara ya Kilimo linalojengwa katika Uwanja wa Nanenane Nyakabindi Mjini Bariadi wakati wa ziara yake ya siku moja Aprili 29, 2020.
 Mmoja wa Wafanyakazi katika kiwanda cha Alliance Ginnery akitoa maelezo kwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo, Bw. Gerald Kusaya(katikati) kuhusu namna mbegu za pamba zinavyochakatwa katika kiwanda hicho kilichopo Bariadi, Aprili 29, 2020 wakati wa ziara yake ya siku moja mkoani Simiyu.
 Sehemu ya mbele ya jengo la Wizara ya Kilimo linalojengwa katika Uwanja wa Nanenane Nyakabindi Mjini Bariadi
 Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo, Bw. Gerald Kusaya (mwenye suti ya bluu) na viongozi wengine wakiondoa mara baada ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa Jengo la Wizara ya Kilimo linalojengwa katika Uwanja wa Nanenane Nyakabindi Mjini Bariadi wakati wa ziara yake ya siku moja Aprili 29, 2020.
 Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo, Bw. Gerald Kusaya akizungumza na baadhi ya  viongozi wa mkoa wa Simiyu na baadhi ya wanunuzi wa pamba mkoani hapa,  katika kikao kilichofanyika Mjini Bariadi wakati wa ziara yake ya siku moja Aprili 29, 2020 mkoani Simiyu.
 Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bw. Ekwabi Mujungu akiwasilisha taarifa ya Mkoa kwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo, Bw. Gerald Kusaya (mwenye suti ya bluu) katika kikao cha Katibu Mkuu huyo,viongozi wa mkoa wa Simiyu na wanunuzi wa pamba, kilichofanyika Mjini Bariadi wakati wa ziara yake ya siku moja Aprili 29, 2020 mkoani Simiyu.

Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Simiyu, Bw. Mayunga George akichangia hoja katika kikao cha Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo, Bw. Gerald Kusaya wakati wa zaira yake ya siku moja mkoani Simiyu, Aprili 29, 2020.


Saturday, April 25, 2020

UONGOZI MASWA WATAKIWA KUMSIMAMIA MKANDARASI UJENZI WA VIWANDA VIKAMILIKE KWA WAKATI

Katibu Mkuu Ofisi ya Rais TAMISEMI, Mhandisi Joseph Nyamhanga ameutaka uongozi wa Wilaya ya Maswa kumsimamia Mkandarasi SUMA JKT anayejenga kiwanda cha chaki  na kiwanda cha vifungashio wilayani humo ili akamilishe ujenzi wa viwanda hivyo kwa wakati ili vianze uzalishaji.


Nyamhanga ameyasema hayo wakati wa ziara yake alipotembelea kuona maendeleo ya ujenzi wa viwanda hivyo eneo la Ng’hami ambapo ameutaka uongozi wa Wilaya ya Maswa kufuatilia uagizaji wa mitambo ya kiwanda cha chaki huku akiahidi kuwa ofisi yake itafuatilia kibali cha kuagiza Mitambo kwa ajili ya kiwanda cha vifungashio. katika Ofisi ya HAZINA(Wizara ya Fedha)ili miradi yote iende sambamba.



SERIKALI YATENGA BILIONI MOJA KUJENGA WODI HOSPITALI ZA WILAYA, UNUNUZI VIFAA TIBA


Katibu Mkuu wa Ofisi ya Rais TAMISEMI, Mhandisi. Joseph Nyamuhanga amesema Serikali katika Bajeti ya mwaka 2020/2021 Serikali imetenga kiasi cha shilingi bilioni moja kwa ajili ya ununuzi wa vifaa tiba na ujenzi wa wodi tatu katika kila Hospitali ya Wilaya kwenye Hospitali 67 za Wilaya zilizojengwa hapa nchini.
Mhandisi Nyamhanga ameyasema hayo wakati alipotembelea na kukagua maendeleo ya ujenzi wa Hospitali ya Halmashauri ya Wilaya Bariadi iliyopo kata ya Dutwa ambapo ameoneshwa kuridhishwa na kazi ya ujenzi inayoendelea.
Aidha, Nyamhanga ameziagiza Halmashauri 30 nchini zilizohamia katika maeneo mapya kiutawala pamoja na mikoa mipya kuanza maandalizi ya mchakato wa manunuzi kwa ajili ya ujenzi wa Majengo ya Utawala ili kufikia Desemba 31, 2020 Halmashauri hizo na mikoa mipya ziwe zimekamilisha ujenzi wa Majengo ya utawala.

Katibu Mkuu Ofisi ya Rais TAMISEMI, Mhandisi Joseph Nyamhanga(kushoto) akikagua maendeleo ya ujenzi wa hospitali ya Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi iliyopo kata ya Dutwa wakati wa ziara yake Aprili 23, 2020 mkoani Simiyu.

 Katibu Mkuu Ofisi ya Rais TAMISEMI, Mhandisi Joseph Nyamhanga akizungumza na viongozi wa Wilaya ya Bariadi na Mkoa wa Simiyu(hawapo pichani mara baada ya kutembelea hospitali ya Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi iliyopo kata ya Dutwa wakati wa ziara yake Mkoani Simiyu Aprili 23, 2020.

 Katibu Mkuu Ofisi ya Rais TAMISEMI, Mhandisi Joseph Nyamhanga(kushoto) akikagua maendeleo ya ujenzi wa hospitali ya Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi iliyopo kata ya Dutwa wakati wa ziara yake Aprili 23, 2020 mkoani Simiyu.

Katibu Mkuu Ofisi ya Rais TAMISEMI, Mhandisi Joseph Nyamhanga(mwenye suti nyeusi kulia) akiteta jambo na Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka (kushoto) wakati akikagua hospitali ya Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi iliyopo kata ya Dutwa wakati wa ziara yake Mkoani Simiyu Aprili 23, 2020.

 Baadhi ya majengo katika Hospitali ya Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi 

Katibu Mkuu Ofisi ya Rais TAMISEMI, Mhandisi Joseph Nyamhanga akiwa na  viongozi wa Wilaya ya Bariadi na Mkoa wa Simiyu alipotembelea  hospitali ya Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi iliyopo kata ya Dutwa wakati wa ziara yake Mkoani Simiyu Aprili 23, 2020. 

Meneja wa TARURA Halmashauri  ya Mji wa Bariadi, Mhandisi. Mathias Mugolozi akitoa taarifa ya Ujenzi wa Kituo cha Mabasi cha Kisasa cha Mjini Bariadi kwa Katibu Mkuu Ofisi ya Rais TAMISEMI, Mhandisi Joseph Nyamhanga(kulia), alipotembelea kituo hicho wakati wa ziara yake Mkoani Simiyu Aprili 23, 2020. 

Katibu Mkuu Ofisi ya Rais TAMISEMI, Mhandisi Joseph Nyamhanga  (kulia)  akipokea taarifa ya maendeleo ya ujenzi wa Jengo la Utawala la Halmashauri ya Mji wa Bariadi katika eneo la Nyaumata  wakati wa ziara yake Mkoani Simiyu Aprili 23, 2020. 

Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bw. Jumanne Sagini akitoa maelezo ya ujenzi wa Jengo la Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu kwa Katibu Mkuu Ofisi ya Rais TAMISEMI, Mhandisi Joseph Nyamhanga  katika eneo la Nyaumata  wakati wa ziara yake Mkoani Simiyu Aprili 23, 2020. 

Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bw. Jumanne Sagini akitoa maelezo ya ujenzi wa Kituo cha Mabasi cha Kisasa cha Mjini Bariadi kwa Katibu Mkuu Ofisi ya Rais TAMISEMI, Mhandisi Joseph Nyamhanga  wakati wa ziara yake Mkoani Simiyu Aprili 23, 2020. 
 Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi, Bw. Melkizedeck Humbe  akitoa taarifa ya mtanadao wa barabara za lami za mjini Bariadi kwa Katibu Mkuu Ofisi ya Rais TAMISEMI, Mhandisi Joseph Nyamhanga  wakati wa ziara yake Mkoani Simiyu Aprili 23, 2020.

 Sehemu ya mtandao wa bara bara za lami katika Mji wa Bariadi.

 Katibu Mkuu Ofisi ya Rais TAMISEMI, Mhandisi Joseph Nyamhanga  (kulia)  akiwa na  viongozi wa Wilaya ya Bariadi na Mkoa wa Simiyu alipotembelea  hospitali ya Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi iliyopo kata ya Dutwa wakati wa ziara yake Mkoani Simiyu Aprili 23, 2020. 


Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bw. Jumanne Sagini akitoa maelezo ya ujenzi wa Kituo cha Mabasi cha Kisasa cha Mjini Bariadi kwa Katibu Mkuu Ofisi ya Rais TAMISEMI, Mhandisi Joseph Nyamhanga  wakati wa ziara yake Mkoani Simiyu Aprili 23, 2020.
 Katibu Mkuu Ofisi ya Rais TAMISEMI, Mhandisi Joseph Nyamhanga  (wa  pili kulia) akikagua ujenzi wa kituoa cha mabasi Bariadi  akiwa na  viongozi wengine wa Wilaya ya Bariadi na Mkoa wa Simiyu wakati wa ziara yake Mkoani Simiyu Aprili 23, 2020.

 Katibu Mkuu Ofisi ya Rais TAMISEMI, Mhandisi Joseph Nyamhanga  (wa tatu kushoto)  na viongozi wa wengine wa Mkoa wa Simiyu wakiondoka eneo la Nyaumata baada ya kupokea taarifa ya maendeleo ya ujenzi wa Jengo la Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu katika eneo la Nyaumata  wakati wa ziara yake Mkoani Simiyu Aprili 23, 2020.


Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony  Mtaka akizungumza jambo mara tu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais TAMISEMI, Mhandisi Joseph Nyamhanga  (wa tatu kushoto)  alipowasili ofisi kwake mjini Bariadi kwa ajili ya ziara ya kikazi ya siku moja Aprili 23, 2020. 

Katibu Mkuu Ofisi ya Rais TAMISEMI, Mhandisi Joseph Nyamhanga akiwa na  viongozi wa Wilaya ya Bariadi na Mkoa wa Simiyu alipotembelea  hospitali ya Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi iliyopo kata ya Dutwa wakati wa ziara yake Mkoani Simiyu Aprili 23, 2020. 

Mratibu wa TARURA Mkoa, Dkt. Eng. Philimon Msomba (kushoto) akitoa taarifa juu ya ujenzi wa Megesho ya malori ya mji wa Bariadi kwa Katibu Mkuu Ofisi ya Rais TAMISEMI, Mhandisi Joseph Nyamhanga akiwa na  viongozi wa Wilaya ya Bariadi na Mkoa wa Simiyu alipotembelea  hospitali ya Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi iliyopo kata ya Dutwa wakati wa ziara yake Mkoani Simiyu Aprili 23, 2020. 


Katibu Mkuu Ofisi ya Rais TAMISEMI, Mhandisi Joseph Nyamhanga(mwenye suti nyeusi kushoto) akikagua maendeleo ya ujenzi wa hospitali ya Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi iliyopo kata ya Dutwa wakati wa ziara yake Aprili 23, 2020 mkoani Simiyu.

Wednesday, April 22, 2020

JBS FUEL COMPANY YATOA MSAADA KWA WATOTO WENYE UALBINO BUSEGA KUKABILI CORONA

Mkurugenzi wa Kampuni ya JBS Fuel Company Limited ya Mjini Bariadi, Bi. Lucy Sabu ametoa msaada chakula na vifaa mbalimbali vya kujikinga na maambukizi ya virusi vya Corona, katika kituo cha kulelea watoto wenye mahitaji maalumu cha Bikira Maria kilichopo Lamadi wilayani Busega.

Akizungumza wakati wa kukabidhi msaada huo Bi. Sabu  amevitaja vifaa hivyo kuwa ni pamoja na Vitakasa mikono, sabuni za maji, ndoo kwa ajili ya maji ya kunawia mikono, mahindi na sukari vyote vikiwa na thamani ya shilingi milioni mbili (2,000,000/=).
Amesema wito uliotolewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli wa maombi ya siku ya tatu umemsukuma kutoa msaada huo kwani ameona ipo haja ya kuwasaidia wahitaji katika kipindi hiki cha Janga la Corona na kutoa wito kwa Watanzania kuendelea kuchukua tahadhari na kufuata maelekezo ya wataalam wa afya.
"Namshukuru sana Mhe. Rais kwa maono yake kwa Watanzania kufanya maombi ya siku tatu kumuomba Mungu atuepushe na Janga la Corona, maombi haya yamenikumbusha kuwakirimu wahitaji na ndiyo maana nimeguswa kufika katika kituo hiki; nitoe wito kwa Watanzania wote kuwakumbuka wahitaji katika kipindi hiki cha Janga la Corona," alisema Bi Lucy Sabu.
Akipokea msaada huo kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka, Mkuu wa Wilaya ya Busega Mhe. Tano Mwera amemshukuru Bi. Lucy Sabu kwa namna alivyoguswa kusaidia kituo hicho huku akiendelea kusisitiza wananchi kuchukua tahadhari na kumwelekeza Mkurugenzi wa kituo kuwa makini kudhibiti watu wanaoingia kituoni hapo ili kuwalinda watoto.
Naye Mratibu wa mapambano dhidi ya maambukizi ya Virusi vya Corona Mkoani Simiyu, Dkt. Khamis Kulemba ameutaka Uongozi wa kituo hicho kuongeza maeneo ya watoto kunawa mikono pamoja na kuwasisitiza kunawa mara kwa mara.
Mkurugenzi wa kituo cha Bikira Maria, Sister Helena Ntambulwa amemshukuru Bi. Lucy Sabu kwa msaada aliotoa na kuwashukuru viongozi wa Wilaya ya Busega na Mkoa wa Simiyu kwa namna wanavyokisaidia kituo hicho chenye jumla ya watoto 71 ambao wanatoka maeneo  mbalimbali ya Tanzania wakiwemo waliopoteza wazazi na waliotelekezwa.
Kwa upande wake Mjumbe wa Bodi ya wadhamini ya Kituo hicho, Bw. Belensi China amesema kituo hicho kinakabiliwa na changamoto mbalimbali, ikiwa ni pamoja na upungufu wa fedha za kulipa matibabu ya watoto na mishahara ya wafanyakazi; hivyo amewaomba Watanzania wenye mapenzi mema kuendelea kuwasaidia watoto hao wenye mahitaji maalum.

MWISHO
 :- Mkuu wa Wilaya ya Busega, Mhe. Tano Mwera (kushoto) akipokea  msaada wa chakula na vifaa vya kujikinga na maambukizi ya Virusi vya Corona uliotolewa na Mkurugenzi wa JBS Fuel Company Limited, Bi. Lucy Sabu (wa pili kulia) kwa kituo cha kulelea watoto wenye ualbino na watoto wenye mahitaji maalumu kilichopo Kata ya Lamadi wilayani Busega, Aprili 22, 2020 wakishuhudiwa na baaadhi ya watoto hao na Mlezi wao Sister Helena Ntambulwa.


 Mkuu wa Wilaya ya Busega, Mhe. Tano Mwera (kushoto) akipokea  msaada vifaa wa chakula na vifaa vya kujikinga na maambukizi ya Virusi vya Corona uliotolewa na Mkurugenzi wa JBS Fuel Company Limited, Bi. Lucy Sabu (wa pili kulia) kwa kituo cha kulelea watoto wenye ualbino na watoto wenye mahitaji maalumu kilichopo Kata ya Lamadi wilayani Busega, Aprili 22, 2020.


 Mkurugenzi wa Kituo cha Bikira Maria kinacholea watoto wenye ulbino na watoto wenye mahitaji maalum kilichopo Lamadi Busega, Sister Helena Ntabulwa (kushoto) akipokea msaada wa vifaa vya kujikinga na maambukizi ya Virusi vya Corona uliotolewa na Mkurugenzi wa JBS Fuel Company Limited, Bi. Lucy Sabu (wa pili kulia) kwa kituo hicho Aprili 22, 2020.


 Mkurugenzi wa JBS Fuel Company Limited, Bi. Lucy Sabu (katikati) akikabidhi msaada wa chakula na vifaa vya kujikinga na Maambukizi ya Virusi vya Corona Mkurugenzi wa kituo cha kulelea watoto wenye ualbino na watoto wenye mahitaji maalum kilichopo Kata ya Lamadi wilayani Busega, Sister Helena Ntabulwa(wa pili kushoto)  Aprili 22, 2020 wakishuhudiwa na baaadhi ya watoto hao.


 Mkuu wa Wilaya ya Busega, Mhe. Tano Mwera akizungumza kabla ya kupokea msaada wa chakula na vifaa vya kujikinga na maambukizi ya Virusi vya Corona uliotolewa na Mkurugenzi wa JBS Fuel Company Limited, Bi. Lucy Sabu (hayupo pichani) kwa kituo cha kulelea watoto wenye ualbino na watoto wenye mahitaji maalum kilichopo Kata ya Lamadi wilayani Busega, Aprili 22, 2020.


 Mkurugenzi wa JBS Fuel Company Limited, Bi. Lucy Sabu (wa pili kulia) akiangalia mabweni ya watoto katika kituo cha kulelea watoto wenye ualbino na watoto wenye mahitaji maalum kilichopo Kata ya Lamadi wilayani Busega, kabla ya kukabidhi msaada wa chakula na vifaa vya kujikinga  na Maambukizi ya Virusi vya Corona Aprili 22, 2020.


 Mkurugenzi wa JBS Fuel Company Limited, Bi. Lucy Sabu (kulia) akionesha baadhi ya vitu alivyotoa msaada katika kituo cha kulelea watoto wenye ualbino na watoto wenye mahitaji maalum kilichopo Kata ya Lamadi wilayani Busega, kabla ya kukabidhi msaada huo wa chakula na vifaa vya kujikinga  na Maambukizi ya Virusi vya Corona Aprili 22, 2020.


 Mkurugenzi wa JBS Fuel Company Limited, Bi. Lucy Sabu (kulia) akionesha baadhi ya vitu alivyotoa msaada katika kituo cha kulelea watoto wenye ualbino na watoto wenye mahitaji maalum kilichopo Kata ya Lamadi wilayani Busega, kabla ya kukabidhi msaada huo wa chakula na vifaa vya kujikinga  na Maambukizi ya Virusi vya Corona Aprili 22, 2020.


 Mkurugenzi wa JBS Fuel Company Limited, Bi. Lucy Sabu (kulia) akionesha baadhi ya vitu alivyotoa msaada katika kituo cha kulelea watoto wenye ualbino na watoto wenye mahitaji maalum kilichopo Kata ya Lamadi wilayani Busega, kabla ya kukabidhi msaada huo wa chakula na vifaa vya kujikinga  na Maambukizi ya Virusi vya Corona Aprili 22, 2020.


Mkurugenzi wa JBS Fuel Company Limited, Bi. Lucy Sabu (wa tatu kulia) akiangalia mazingira katika katika kituo cha kulelea watoto wenye ualbino na watoto wenye mahitaji maalum kilichopo Kata ya Lamadi wilayani Busega, kabla ya kukabidhi msaada wa chakula na vifaa vya kujikinga  na Maambukizi ya Virusi vya Corona Aprili 22, 2020.

Saturday, April 18, 2020

WATU 34 WARUHUSIWA KUTOKA KARANTINI MKOANI SIMIYU

Mkuu  wa Mkoa wa Simiyu Anthony Mtaka amesema kuwa jumla ya watu 34 kati ya watu 120 waliokuwa kwenye uangalizi maalum (Karantini) mkoani Simiyu wameruhusiwa mara baada ya kupimwa na kukutwa hawana maambukizi ya Virusi vya Corona vinavyosababisha homa kali ya mapafu (COVID-19). 

Mtaka ameyasema hayo Aprili 18, 2020 wakati akizungumza na waumini wa Kanisa la Waadventista Wasabato (SDA) Bariadi Mjini, ambao wameitikia wito wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli kwa Watanzania kuingia katika maombi ya siku tatu (Aprili 17-19, 2020) kuliombea Taifa ili Mungu aliponye na janga la Corona.

“Tulikuwa na watu 120 waliokuwa chini ya uangalizi ambao pia wamekuwa wakipata elimu kuhusu maambukizi ya virusi vya Corona ili wakitoka wakawe msaada kwa familia zao; mpaka sasa watu 34 wameruhusiwa baada ya kupimwa na kuthibitika kwamba hawana maambukizi ya Corona, sisi kama mkoa tunaendelea kuchukua tahadhari zote,”alisema Mtaka.

Ameongeza kuwa waliowekwa karantini ni pamoja na wanaofanya biashara nchi jirani ambao waliomba wenyewe ili wajitenge na familia zao; pia wapo baadhi ambao familia ziliomba Serikali iwaweke kutokana na kujua kuwa wametoka nchi zenye maambukizi kwa hofu ya kupeleka maambukizi kwa familia zao ikiwa itatokea wameambukizwa virusi vya Corona.

 Aidha, Mtaka amesema kuwa mpaka sasa mkoa wa Simiyu hauna mtu mwenye maambukizi ya Virusi vya Corona na kutoa wito kwa wananchi kuendelea kuchukua tahadhari huku wakimuomba Mungu bila kukoma ili aliponye Taifa na janga la kidunia la ugonjwa wa COVID 19.

Katika hatua nyingine Mtaka amewahimiza wazazi kuwasimamia watoto wao na kuhakikisha wanajisomea wakiwa nyumbani huku akiwaasa kutunza chakula na kuepuka kuuza mazao pasipo na ulazima wa kufanya hivyo.

Mchungaji wa Kanisa la SDA Bariadi Mjini, Marco Mlingwa amesema Kanisa hilo limepokea maelekezo ya Serikali na linaungana na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli kuliombea Taifa Mungu aliponye na janga la Corona.

Kwa upande wao waumini wa Kanisa la SDA Bariadi Mjini wamemshukuru Mhe. Rais kuruhusu ibada kufanyika kwa kuzingatia maelekezo ya watalaam wa afya na kubainisha kuwa wataendelea kumuomba Mungu aliepushe Taifa na Corona wakiamini kuwa Mungu atasikia wakiomba kwa imani na kwa bidii.

“Tunamshukuru Mhe. Rais kuruhusu ibada kuendelea kufanyika huku tukichukua tahadhari,  sisi Wakristo tunaamini watu tukiomba kwa bidii Mungu anasikia maombi, hivyo tukikutana na kuomba kwa bidii Mungu atasikia na kutuokoa na ugonjwa huu wa COVID 19,” alisema Paul Jidayi muumini SDA na Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Maswa.

“Sisi kama Wasabato tuna vipindi vyetu vya afya na kupitia vipindi hivyo tumeshajifunza na kuchukua tahadhari dhidi ya Corona kanisani na majumbani; pia tunaungana na Rais kuliombea Taifa tukiamini kuwa Mungu atatusikia maana hata zamani, nchi ya Ninawi walipelekewa taarifa kuwa wataangamizwa lakini walipomlilia Mungu aliwasikia na  hawakuangamia,” alisema Mariam Manyangu.

 MWISHO
Baadhi ya Wazee wa Kanisa wa Kanisa la SDA Bariadi mjini wakiwaongoza waumini wa kanisa hilo katika maombi maalum ya kuliombea Taifa, yaliyofanyika katika ibada Aprili 18, 2020 kuitikia wito wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli kwa Watanzania wote kuingia katika maombi ya siku tatu ( Aprili 17-19, 2020) kuliombea Taifa ili Mungu aliponye na janga la Corona.(mwenye Tai wa tatu kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka).
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka akizungumza na waumini wa Kanisa la Waadventista Wasabato Bariadi Mjini, Aprili 18, 2020 ambapo ameshiriki katika ibada ambayo waumini hao wameitikia wito wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.Dkt. John Pombe Magufuli kwa Watanzania wote kuingia katika maombi ya siku tatu ( Aprili 17-19, 2020) kuliombea Taifa ili Mungu aliponye na janga la Corona.
 Baadhi ya waumini wa Kanisa la Waadventista Wasabato Bariadi Mjini, Aprili 18, 2020 wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka ambapo ameshiriki ibada ambayo waumini hao wameitikia wito wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt.  John Pombe Magufuli kwa Watanzania wote kuingia katika maombi ya siku tatu ( Aprili 17-19, 2020) kuliombea Taifa ili Mungu aliponye na janga la Corona.


 Kwaya ya Kanisa la Waadventista Wasabato Bariadi Mjini wakiimba katika ibada ya Aprili 18, 2020 ambayo waumini wa kanisa hilo pia wameitikia wito wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli kwa Watanzania wote kuingia katika maombi ya siku tatu ( Aprili 17-19, 2020) kuliombea Taifa ili Mungu aliponye na janga la Corona.


 Mchungaji wa Kanisa la Waadventista Wasabato Bariadi Mjini, Marco Mlingwa akiwaongoza waumini wa kanisa hilo katika maombi maalum ya kuliombea Taifa, yaliyofanyika katika ibada Aprili 18, 2020 kuitikia wito wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli kwa Watanzania wote kuingia katika maombi ya siku tatu ( Aprili 17-19, 2020) kuliombea Taifa ili Mungu aliponye na janga la Corona.(wa pili kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka).


 Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka (mwenye tai katikati) akizungumza na baadhi ya viongozi wa Kanisa la waumini wameitikia wito wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli kwa Watanzania wote kuingia katika maombi ya siku tatu ( Aprili 17-19, 2020) kuliombea Taifa ili Mungu aliponye na janga la Corona.


 Baadhi ya waumini wa Kanisa la Waadventista Wasabato Bariadi Mjini, Aprili 18, 2020 wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka ambapo ameshiriki ibada ambayo waumini hao wameitikia wito wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli kwa Watanzania wote kuingia katika maombi ya siku tatu ( Aprili 17-19, 2020) kuliombea Taifa ili Mungu aliponye na janga la Corona.


 Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka (kushoto) na Mchungaji wa Kanisa la Waadventista Wasabato Bariadi Mjini, Marco Mlingwa wakiwa katika maombi kwenye ibada ambayo waumini wa Kanisa hilo wameitikia wito wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli kwa Watanzania wote kuingia katika maombi ya siku tatu ( Aprili 17-19, 2020) kuliombea Taifa ili Mungu aliponye na janga la Corona.


 Mchungaji wa Kanisa la Waadventista Wasabato Bariadi Mjini, Marco Mlingwa akihubiri katika ibada ya Aprili 18, 2020 ambayo waumini wa kanisa hilo pia wameitikia wito wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt.  John Pombe Magufuli kwa Watanzania wote kuingia katika maombi ya siku tatu ( Aprili 17-19, 2020) kuliombea Taifa ili Mungu aliponye na janga la Corona.


 Vijana wa Pathfinder katika Kanisa la Waadventista Wasabato Bariadi Mjini wakiimba katika ibada ya Aprili 18, 2020 ambayo waumini wa kanisa hilo pia wameitikia wito wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli kwa Watanzania wote kuingia katika maombi ya siku tatu ( Aprili 17-19, 2020) kuliombea Taifa ili Mungu aliponye na janga la Corona.
 Kwaya ya Kanisa la Waadventista Wasabato Bariadi Mjini wakiimba katika ibada ya Aprili 18, 2020 ambayo waumini wa kanisa hilo pia wameitikia wito wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli kwa Watanzania wote kuingia katika maombi ya siku tatu ( Aprili 17-19, 2020) kuliombea Taifa ili Mungu aliponye na janga la Corona.
 Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka (kushoto) na Mchungaji wa Kanisa la Waadventista Wasabato Mtaa wa Ntuzu Bariadi Mjini, Marco Mlingwa katika ibada ambayo waumini wa Kanisa hilo wameitikia wito wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt.John Pombe Magufuli kwa Watanzania wote kuingia katika maombi ya siku tatu ( Aprili 17-19, 2020) kuliombea Taifa ili Mungu aliponye na janga la Corona.
 Baadhi ya waumini wa Kanisa la Waadventista Wasabato Bariadi Mjini, Aprili 18, 2020 wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka ambapo ameshiriki ibada ambayo waumini hao wameitikia wito wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.Dkt.  John Pombe Magufuli kwa Watanzania wote kuingia katika maombi ya siku tatu ( Aprili 17-19, 2020) kuliombea Taifa ili Mungu aliponye na janga la Corona.
 Mchungaji wa Kanisa la Waadventista Wasabato Mtaa wa Ntuzu Bariadi Mjini, Marco Mlingwa akihubiri katika ibada ya Aprili 18, 2020 ambayo waumini wa kanisa hilo pia wameitikia wito wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli kwa Watanzania wote kuingia katika maombi ya siku tatu ( Aprili 17-19, 2020) kuliombea Taifa ili Mungu aliponye na janga la Corona.
 Baadhi ya Wazee wa Kanisa wa Kanisa la SDA Mtaa wa Ntuzu Bariadi mjini wakiwaongoza waumini wa kanisa hilo katika maombi maalum ya kuliombea Taifa, yaliyofanyika katika ibada Aprili 18, 2020 kuitikia wito wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.Dkt.  John Pombe Magufuli kwa Watanzania wote kuingia katika maombi ya siku tatu ( Aprili 17-19, 2020) kuliombea Taifa ili Mungu aliponye na janga la Corona.(mwenye Tai wa tatu kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka).
Baadhi ya waumini wa Kanisa la Waadventista Wasabato Bariadi Mjini, Aprili 18, 2020 wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka ambapo ameshiriki ibada ambayo waumini hao wameitikia wito wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt.  John Pombe Magufuli kwa Watanzania wote kuingia katika maombi ya siku tatu ( Aprili 17-19, 2020) kuliombea Taifa ili Mungu aliponye na janga la Corona.

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!