Saturday, August 29, 2020

WASTAAFU WAWAASA WATUMISHI WA UMMA KUMTANGULIZA MUNGU, KUWA WAADILIFU NA KUJITUMA

Wastaafu kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu wamewaasa watumishi wa umma kumtanguliza Mungu, kuwa waadilifu na kujituma ili waweze kutimiza wajibu wao sawa sawa kwa maslahi yao binafsi na Taifa kwa ujumla. 

Hayo yamebainishwa na Bw. Elias Kasuka ambaye kwa sasa amestaafu utumishi wa umma akiwa kama Afisa Kilimo Mkuu baada ya kutumika kwa miaka 35 na Bw. Godfrey Machumu ambaye kwa sasa  amestaafu utumishi wa umma akiwa kama Mhasibu  Mkuu baada ya kutumika kwa miaka 37 katika Hafla fupi ya kuwapongeza wastaafu  hao wa mwaka 2019/2020 iliyofanyika Agosti 28, 2020 Mjini Bariadi. 

“Katika Utumishi wa Umma hampashwi kukata tamaa, binafsi nimeanzia mbali nikajiendeleza sikujali umri wangu, kikubwa ni kumtanguliza Mwenyezi Mungu katika kazi zenu mtafanikiwa tu,” alisema Bw. Godfrey Machumu. 

“Siri kubwa ya kufikia mpaka kustaafu kwangu ni kufanya kazi kwa bidii na uadilifu, nilifanya kazi bila kusukumwa mfano mzuri ni kwa namna nilivyoshiriki kuandaa Maonesho ya nanenane mwaka 2018 na 2019 ; pia nawashauri mheshimu wakubwa kwa wadogo,” alisema Bw. Elias Kasuka. 

Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bi.Miriam Mmbaga amewapongeza wastaafu hao kwa utumishi uliotukuka mpaka kufikia kustaafu huku akitoa wito kwa watumishi wengine kuiga mema waliyojifunza kupitia utumishi wa wastaafu hao ikiwa ni pamoja na kuona umuhimu wa kujiendeleza kielimu wakiwa kazini na kujiendeleza kimaisha. 

Katika hatua nyingine Bi. Mmbaga amewaasa watumishi kuishi na watu wote vizuri huku akisisitiza umuhimu wa kuacha alama katika kazi zao wanazofanya  ili hata watakapo staafu wakumbukwe kwa alama walizoacha kwenye maeneo waliyofanyia kazi.

MWISHO

Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bi. Miriam Mmbaga akimkabidhi cheti cha Utumishi uliotukuka Bw. Elias Kasuka ambaye kwa sasa amestaafu utumishi wa umma akiwa kama Afisa Kilimo Mkuu baada ya kutumika kwa miaka 35, katika Hafla fupi ya kuwapongeza wastaafu kwa mwaka 2019/2020 iliyofanyika Agosti 28, 2020 Mjini Bariadi, kushoto ni Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya utawala na Rasilimaliwatu Bw. Ekwabi Mujungu.

Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bi. Miriam Mmbaga akimkabidhi cheti cha Utumishi uliotukuka Bw. Godfrey Machumu ambaye kwa sasa amestaafu utumishi wa umma akiwa kama Mhasibu  Mkuu baada ya kutumika kwa miaka 37, katika Hafla fupi ya kuwapongeza wastaafu kwa mwaka 2019/2020 iliyofanyika Agosti 28, 2020 Mjini Bariadi.
Bw. Godfrey Machumu(wa pili kulia) ambaye kwa sasa  amestaafu utumishi wa umma akiwa kama Mhasibu  Mkuu baada ya kutumika kwa miaka 37,akionesha cheti cha utumishi uliotukuka alichokabidhiwa na Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu(wa pili kushoto) katika Hafla fupi ya kuwapongeza wastaafu kwa mwaka 2019/2020 iliyofanyika Agosti 28, 2020 Mjini Bariadi.

Bw. Elias Kasuka  ambaye kwa sasa  amestaafu utumishi wa umma akiwa kama Afisa Kilimo Mkuu  baada ya kutumika kwa miaka 35,akionesha cheti cha utumishi uliotukuka alichokabidhiwa na Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu(wa pili kushoto) katika Hafla fupi ya kuwapongeza wastaafu kwa mwaka 2019/2020 iliyofanyika Agosti 28, 2020 Mjini Bariadi.
Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya utawala na Rasilimaliwatu Bw. Ekwabi Mujungu akitoa maelezo mafupi kuhusu wastaafu wawili Bw. Elias Kasuka  ambaye kwa sasa  amestaafu utumishi wa umma akiwa kama Afisa Kilimo Mkuu  baada ya kutumika kwa miaka 35 na Bw. Godfrey Machumu ambaye kwa sasa amestaafu utumishi wa umma akiwa kama Mhasibu  Mkuu baada ya kutumika kwa miaka 37, katika Hafla fupi ya kuwapongeza wastaafu hao wa mwaka 2019/2020 iliyofanyika Agosti 28, 2020 Mjini Bariadi.

Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bi. Miriam Mmbaga akizungumza na watumishi wa Ofisi ya mkuu wa Mkoa wa Simiyu katika kikao chake na watumishi hao ambacho kilitumika kama sehemu ya kuwapongeza wastaafu wawili Bw. Elias Kasuka  ambaye kwa sasa  amestaafu utumishi wa umma akiwa kama Afisa Kilimo Mkuu  baada ya kutumika kwa miaka 35 na Bw. Godfrey Machumu ambaye kwa sasa amestaafu utumishi wa umma akiwa kama Mhasibu  Mkuu baada ya kutumika kwa miaka 37, kilichofanyika Agosti 28, 2020 Mjini Bariadi.
Kutoka kushoto Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya utawala na Rasilimaliwatu Bw. Ekwabi Mujungu, :- Bw. Elias Kasuka  ambaye kwa sasa  amestaafu utumishi wa umma akiwa kama Afisa Kilimo Mkuu  baada ya kutumika kwa miaka 35, Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bi. Miriam Mmbaga na Bw. Godfrey Machumu ambaye kwa sasa amestaafu utumishi wa umma akiwa kama Mhasibu  Mkuu baada ya kutumika kwa miaka 37, wakiagana baada ya Hafla fupi ya kuwapongeza wastaafu hao wa mwaka 2019/2020 iliyofanyika Agosti 28, 2020 Mjini Bariadi.

Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bi. Miriam Mmbaga (katikati kwa walioketi) akiwa katika picha ya pamoja na Bw. Elias Kasuka  (wa pili kushoto walioketi) ambaye kwa sasa  amestaafu utumishi wa umma akiwa kama Afisa Kilimo Mkuu  baada ya kutumika kwa miaka 35, Bw. Godfrey Machumu (wa pili kulia) ambaye kwa sasa amestaafu utumishi wa umma akiwa kama Mhasibu  Mkuu baada ya kutumika kwa miaka 37 na mkewe pamoja na watumishi wengine wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, baada ya Hafla fupi ya kuwapongeza wastaafu hao wa mwaka 2019/2020 iliyofanyika Agosti 28, 2020 Mjini Bariadi.

Kutoka kushoto Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya utawala na Rasilimaliwatu Bw. Ekwabi Mujungu,  Bw. Elias Kasuka  ambaye kwa sasa  amestaafu utumishi wa umma akiwa kama Afisa Kilimo Mkuu  baada ya kutumika kwa miaka 35, Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bi. Miriam Mmbaga na Bw. Godfrey Machumu ambaye kwa sasa amestaafu utumishi wa umma akiwa kama Mhasibu  Mkuu baada ya kutumika kwa miaka 37, katika picha ya pamoja baada ya Hafla fupi ya kuwapongeza wastaafu hao wa mwaka 2019/2020 iliyofanyika Agosti 28, 2020 Mjini Bariadi.

Kutoka kushoto Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Uchumi na Uzalishaji, Dkt. Gamitwe Mahaza,  Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya utawala na Rasilimaliwatu Bw. Ekwabi Mujungu,  Bw. Elias Kasuka  ambaye kwa sasa  amestaafu utumishi wa umma akiwa kama Afisa Kilimo Mkuu  baada ya kutumika kwa miaka 35, Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bi. Miriam Mmbaga na Bw. Godfrey Machumu ambaye kwa sasa amestaafu utumishi wa umma akiwa kama Mhasibu  Mkuu baada ya kutumika kwa miaka 37 na Mhasibu Mkuu wa Mkoa, Bw. Francis Makombe  katika picha ya pamoja baada ya Hafla fupi ya kuwapongeza wastaafu hao wa mwaka 2019/2020 iliyofanyika Agosti 28, 2020 Mjini Bariadi.

Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya utawala na Rasilimaliwatu Bw. Ekwabi Mujungu(kulia) akiteta jambo na Bw. Godfrey Machumu ambaye kwa sasa amestaafu utumishi wa umma akiwa kama Mhasibu  Mkuu baada ya kutumika kwa miaka 37 baada ya Hafla fupi ya kuwapongeza wastaafu  wa mwaka 2019/2020 iliyofanyika Agosti 28, 2020 Mjini Bariadi.

Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya utawala na Rasilimaliwatu Bw. Ekwabi Mujungu akitoa maelezo mafupi kuhusu wastaafu wawili Bw. Elias Kasuka  ambaye kwa sasa  amestaafu utumishi wa umma akiwa kama Afisa Kilimo Mkuu  baada ya kutumika kwa miaka 35 na Bw. Godfrey Machumu ambaye kwa sasa amestaafu utumishi wa umma akiwa kama Mhasibu  Mkuu baada ya kutumika kwa miaka 37, katika Hafla fupi ya kuwapongeza wastaafu hao wa mwaka 2019/2020 iliyofanyika Agosti 28, 2020 Mjini Bariadi.
Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bi. Miriam Mmbaga akimkabidhi zawadi ya shilingi 1,000,000/= kwa  Utumishi uliotukuka Bw. Godfrey Machumu ambaye kwa sasa amestaafu utumishi wa umma akiwa kama Mhasibu  Mkuu baada ya kutumika kwa miaka 37, katika Hafla fupi ya kuwapongeza wastaafu kwa mwaka 2019/2020 iliyofanyika Agosti 28, 2020 Mjini Bariadi.

Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bi. Miriam Mmbaga akimkabidhi zawadi ya shilingi 1,000,000/= kwa  Utumishi uliotukuka Bw. Elias Kasuka ambaye kwa sasa amestaafu utumishi wa umma akiwa kama Mhasibu  Mkuu baada ya kutumika kwa miaka 37, katika Hafla fupi ya kuwapongeza wastaafu kwa mwaka 2019/2020 iliyofanyika Agosti 28, 2020 Mjini Bariadi.

Bw. Elias Kasuka  ambaye kwa sasa  amestaafu utumishi wa umma akiwa kama Afisa Kilimo Mkuu  baada ya kutumika kwa miaka 35,akionesha cheti cha utumishi uliotukuka alichokabidhiwa na Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu(katikati) katika Hafla fupi ya kuwapongeza wastaafu kwa mwaka 2019/2020 iliyofanyika Agosti 28, 2020 Mjini Bariadi.

Bw. Elias Kasuka  ambaye kwa sasa  amestaafu utumishi wa umma akiwa kama Afisa Kilimo Mkuu  baada ya kutumika kwa miaka 35, akizungumza na watumishi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu mara baada ya kupokea zawadi ya  cheti cha utumishi uliotukuka na fedha taslimu shilingi 1,000,000/=kutoka kwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu(wa pili kushoto) katika Hafla fupi ya kuwapongeza wastaafu kwa mwaka 2019/2020 iliyofanyika Agosti 28, 2020 Mjini Bariadi.

Bw. Godfrey Machumu  ambaye kwa sasa  amestaafu utumishi wa umma akiwa kama Mhasibu Mkuu  baada ya kutumika kwa miaka 37, akizungumza na watumishi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu mara baada ya kupokea zawadi ya  cheti cha utumishi uliotukuka na fedha taslimu shilingi 1,000,000/=kutoka kwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu(wa pili kushoto) katika Hafla fupi ya kuwapongeza wastaafu kwa mwaka 2019/2020 iliyofanyika Agosti 28, 2020 Mjini Bariadi.
Baadhi ya watumishi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu wakifuatilia maelezo mafupi ya wastaafu Bw. Godfrey Machumu  ambaye kwa sasa  amestaafu utumishi wa umma akiwa kama Mhasibu Mkuu  baada ya kutumika kwa miaka 37 na Bw. Elias Kasuka  ambaye kwa sasa  amestaafu utumishi wa umma akiwa kama Afisa Kilimo Mkuu  baada ya kutumika kwa miaka 35, katika Hafla fupi ya kuwapongeza wastaafu hao wa mwaka 2019/2020 iliyofanyika Agosti 28, 2020 Mjini Bariadi.
Baadhi ya watumishi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu wakifuatilia maelezo mafupi ya wastaafu Bw. Godfrey Machumu  ambaye kwa sasa  amestaafu utumishi wa umma akiwa kama Mhasibu Mkuu  baada ya kutumika kwa miaka 37 na Bw. Elias Kasuka  ambaye kwa sasa  amestaafu utumishi wa umma akiwa kama Afisa Kilimo Mkuu  baada ya kutumika kwa miaka 35, katika Hafla fupi ya kuwapongeza wastaafu hao wa mwaka 2019/2020 iliyofanyika Agosti 28, 2020 Mjini Bariadi.

Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bi. Miriam Mmbaga (katikati kwa walioketi) akiwa katika picha ya pamoja na Bw. Elias Kasuka  (wa pili kushoto walioketi) ambaye kwa sasa  amestaafu utumishi wa umma akiwa kama Afisa Kilimo Mkuu  baada ya kutumika kwa miaka 35, Bw. Godfrey Machumu (wa pili kulia) ambaye kwa sasa amestaafu utumishi wa umma akiwa kama Mhasibu  Mkuu baada ya kutumika kwa miaka 37 na mkewe pamoja na watumishi wengine wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, baada ya Hafla fupi ya kuwapongeza wastaafu hao wa mwaka 2019/2020 iliyofanyika Agosti 28, 2020 Mjini Bariadi.

Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bi. Miriam Mmbaga (katikati kwa walioketi) akiwa katika picha ya pamoja na Bw. Elias Kasuka  (wa pili kushoto walioketi) ambaye kwa sasa  amestaafu utumishi wa umma akiwa kama Afisa Kilimo Mkuu  baada ya kutumika kwa miaka 35, Bw. Godfrey Machumu (wa pili kulia) ambaye kwa sasa amestaafu utumishi wa umma akiwa kama Mhasibu  Mkuu baada ya kutumika kwa miaka 37 na mkewe pamoja na watumishi wengine wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, baada ya Hafla fupi ya kuwapongeza wastaafu hao wa mwaka 2019/2020 iliyofanyika Agosti 28, 2020 Mjini Bariadi.

SIMIYU YAAHIDI KUSHIRIKI KIKAMILIFU MAULIDI YA KITAIFA MWAKA 2020 MKOANI KAGERA

Mkoa wa Simiyu umeahidi kushiriki kikamilifu katika maandalizi ya Maulidi ya Kitaifa inayotarajia kufanyika Oktoba mkoani Kagera. 

Kauli hiyo imetolewa na Katibu Tawala wa mkoa wa Simiyu, Bi. Miriam Mmbaga Agosti 28, 2020 wakati akizungumza na baadhi ya viongozi wa BAKWATA wa Mikoa ya Simiyu na Kagera waliomtembelea ofisini kwake kwa lengo la kuomba ushirikiano na mkoa wa Simiyu kushiriki katika kufanikisha Maulidi hiyo.

“Tumelipokea jambo hili kwa mikono miwili na tunaahidi kulifanyia kazi kwa wepesi kwa kushirikiana na viongozi, ninaomba kupitia Katibu wa BAKWATA  wa Mkoa wetu tutakaa pamoja tuone namna tutakavyolitekeleza na baadaye tutalifanyia maamuzi ndani ya muda mfupi tu ili maandalizi yaendelee,” alisema Bi. Mmbaga.

Kwa upande wake Sheikh wa Mkoa wa Kagera, Haruna Kichwabuta amesema ili sherehe ya Maulidi Kitaifa iweze kufanikiwa inahitaji ushirikiano wa Viongozi wa mikoa jirani jambo ambalo limekuwa likifanyika wakati wote huku akisisitiza kuwa anashukuru mkoa wa Simiyu kuonesha utayari wa kushiriki kufanikisha siku hiyo.

“Tumetoka Kagera tukiwa na Baraka zote za Mhe. Mkuu wa Mkoa wetu na alituhakikishia kuwa ameshawasiliana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Simiyu hivyo tunategemea kupata ushirikiano kutoka Simiyu kwa kuwa sisi ni mikoa jirani, kama mlivyoshiriki mwaka jana  kupitia kwa Mhe. Mkuu wa Mkoa Mhe. Mtaka Mkoani Mwanza naamini hata mwaka huu tutakuwa pamoja ,” alisema Sheikh Kichwabuta.

MWISHO

Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bi. Miriam Mmbaga (kulia) akizungumza na baadhi ya viongozi wa BAKWATA mkoa wa Simiyu na Kagera ambao wamemtembelea ofisini kwake kwa lengo la kuomba ushirikiano na mkoa wa Simiyu katika kufanikisha  maandalizi ya Maulidi ya Kitaifa inayotarajiwa kufanyika mwezi Oktoba 2020 mkoani Kagera.

Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bi. Miriam Mmbaga ( wa pili kulia) akifurahia jambo na Sheikh wa Mkoa wa Simiyu, Mahamoud Kalokola mara baada ya mazungumzo kati yake na viongozi wa BAKWATA  wa Mikoa ya Simiyu na Kagera yaliyolenga kuomba ushirikiano na mkoa wa Simiyu katika kufanikisha  maandalizi ya Maulidi ya Kitaifa inayotarajiwa kufanyika mwezi Oktoba 2020 mkoani Kagera.

Sheikh wa Mkoa wa Simiyu, Mahamoud Kalokola akitoa taarifa ya utangulizi kwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bi. Miriam Mmbaga (kushoto)  juu ya ujumbe wa viongozi wa BAKWATA  wa Mikoa ya Simiyu na Kagera uliofika ofisini kwake kuomba ushirikiano na mkoa wa Simiyu katika kufanikisha  maandalizi ya Maulidi ya Kitaifa inayotarajiwa kufanyika mwezi Oktoba 2020 mkoani Kagera.

Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bi. Miriam Mmbaga(katikati) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya viongozi wa BAKWATA mkoa wa Simiyu na Kagera mara baada ya mazungumzo kati yake na viongozi hao na baadhi ya watumishi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu yaliyolenga kuomba ushirikiano na mkoa wa Simiyu katika kufanikisha  maandalizi ya Maulidi ya Kitaifa inayotarajiwa kufanyika mwezi Oktoba 2020 mkoani Kagera.

Sheikh wa mkoa wa Kagera, Haruna Kichwabuta akisalimiana na Afisa Elimu wa Mkoa wa Simiyu, Mwl. Ernest Hinju mara baada ya mazungumzo kati ya Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bi. Miriam Mmbaga na viongozi wa BAKWATA  wa Mikoa ya Simiyu na Kagera yaliyolenga kuomba ushirikiano na mkoa wa Simiyu katika kufanikisha  maandalizi ya Maulidi ya Kitaifa inayotarajiwa kufanyika mwezi Oktoba 2020 mkoani Kagera.

Baadhi ya viongozi wa BAKWATA  wa Mikoa ya Simiyu na Kagera wakiwa ofisini kwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu kwa ajili ya mazungumzo yaiyolenga kuomba ushirikiano na mkoa wa Simiyu katika kufanikisha  maandalizi ya Maulidi ya Kitaifa inayotarajiwa kufanyika mwezi Oktoba 2020 mkoani Kagera.
Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bi. Miriam Mmbaga (kulia) akizungumza na baadhi ya viongozi wa BAKWATA mkoa wa Simiyu na Kagera ambao wamemtembelea ofisini kwake kwa lengo la kuomba ushirikiano na mkoa wa Simiyu katika kufanikisha  maandalizi ya Maulidi ya Kitaifa inayotarajiwa kufanyika mwezi Oktoba 2020 mkoani Kagera.

Thursday, August 27, 2020

SUA YAAHIDI KUSAIDIA KUANZISHA KITUO CHA KUPIMA KIFUA KIKUU KWA KUTUMIA PANYA SIMIYU

Chuo Kikuu cha Kilimo Sokoine (SUA) kimeahidi kuwa kiko tayari  kuanzisha kituo cha kupima  makohozi  kwa kutumia panya waliofundishwa kubaini vijidudu vya Ugonjwa wa Kifua Kikuu ambao wanaweza kupima sampuli nyingi kwa wakati mmoja ikilinganishwa na vipimo vya maabara.

Hayo yamebainishwa jana na Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bi. Mmbaga kikao kazi cha tathmini ya utekelezaji wa mradi wa kudhibiti kifua kikuu ngazi ya jamii uliokuwa ukitekelezwa  na mkoa wa Simiyu kwa kushirikiana  na shirika lisilo la  Kiserikali la Management and Development for Health (MDH),  kwa miaka mitatu  kuanzia Januari 2018 na unatarajiwa kuhitimishwa Desemba 2020, ambacho kilifanyika jana Mjini Bariadi.

“Tumeona ni muhimu tukaangalia tunavyoweza kutumia teknolojia nyingine kufanya  upimaji wa Ugonjwa wa Kifua Kikuu, kwa mfano tumepata fursa ya kushirikiana na wenzetu wa SUA kipindi cha nanenane mwaka huu  wamesema wako tayari kutusaidia kuanzisha kituo cha upimaji wa makohozi kwa kutumia panya waliofundishwa,” alisema Mmbaga.

Aidha, Mmbaga amesema mkoa wa Simiyu umeonekana kufanya vizuri katika kuwafikia wagonjwa wa Kifua kikuu ikilinganishwa na mikoa mingine saba ambayo yote inatekeleza mradi wa kudhibiti kifua kikuu ngazi ya jamii chini ya shirika lisilo la  Kiserikali la Management and Development for Health (MDH) ambapo umevuka lengo na kuwafikia wananchi kwa asilimia 102.

Pamoja na mafanikio hayo Mmbaga ameelekeza wataalam wafanye tathmini ya malengo yao na waweke malengo mapya yatakayokusudia kuwafikia wananchi wengi wenye uhitaji, ili kupata jamii yenye afya itakayotekeleza kwa vitendo azma na dira ya mkoa ya kuwa mkoa wenye uchumi shindani kwa kutumia rasilimali na fursa zilizopo.

Kwa upande wake Mratibu wa Huduma za kudhibiti Kifua kikuu na Ukoma, Dkt. Emmanuel John amesema kwa mwaka 2019 Mkoa wa Simiyu ulikuwa na lengo la kuwafikia wagonjwa wa Kifua Kikuu 1631 ambapo mpaka kufikia mwezi Desemba 2019 wagonjwa takribani  1673 walikuwa wamefikiwa sawa na asilimia 102 ya lengo.

Dkt. John ameongeza kuwa katika wagonjwa waliokuwa wameanzishiwa matibabu kwa mwaka 2018/2019  asilimia 72 waliweza kupona kabisa, huku akibainisha kuwa katika asilimia 28  baadhi yao walifariki, baadhi walipotea katika mifumo ya matibabu (watoro); huku akiweka bayana kuwa kwa mwaka 2020,  lengo la Mkoa ni kuwafikia wagonjwa 1779.

Naye Kaimu Mganga Mkuu wa Simiyu, Dkt. Khamis Kulemba amesema kuwa wataalam wa afya ngazi ya mkoa na halmashauri watahakikisha wanafanya marejeo ya malengo yao yaweze kuakisi hali halisi ya mahitaji ya jamii ili wananchi wengi waweze kufikiwa na huduma za upimaji na matibabu ya Kifua Kikuu.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Shirika lisilo la Kiserikali la Management and Development for Health (MDH), Bw. Eliamin Busara amesema katika awamu ijayo shirika hilo linatarajia kujikita zaidi katika mpango wa Kifua Kikuu na uboreshaji wa huduma za mama na mtoto hususani katika kuzuia maambukizi ya Virusi vya UKIMWI.

Wakati huo huo Busara ametoa wito kwa Serikali kupitia halmashauri kuwa na mipango ya namna ya kuendeleza huduma zilizokuwa zikitolewa kwa wananchi kupitia mradi huo ili huduma za afya zisitetereke hususani katika upimaji na matibabu ya Kifua Kikuu.

MWISHO

 Katibu Tawala wa mkoa wa Simiyu, Bi. Miriam Mmbaga akifungua kikao kazi cha tathmini ya utekelezaji wa mradi wa kudhibiti kifua kikuu ngazi ya jamii uliokuwa ukitekelezwa  na mkoa wa Simiyu kwa kushirikiana  na shirika lisilo la  Kiserikali la Management and Development for Health (MDH)  kwa miaka mitatu  kuanzia Januari 2018 na unatarajiwa kuhitimishwa Desemba 2020, ambacho kilifanyika jana Mjini Bariadi. 
Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika liliso la Kiserikali la Management and Development for Health (MDH), Emilian Busara  akitoa taarifa katika kikao kazi cha tathmini ya utekelezaji wa mradi wa kudhibiti kifua kikuu ngazi ya jamii uliokuwa ukitekelezwa  na mkoa wa Simiyu kwa kushirikiana  na shirika hilo kwa miaka mitatu  kuanzia Januari 2018 na unatarajiwa kuhitimishwa Desemba 2020, ambacho kilifanyika jana Mjini Bariadi. 

Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Dkt.  Khamis Kulemba akichangia hoja katika kikao kazi cha tathmini ya utekelezaji wa mradi wa kudhibiti kifua kikuu ngazi ya jamii uliokuwa ukitekelezwa  na mkoa wa Simiyu kwa kushirikiana  na shirika lisilo la  Kiserikali la Management and Development for Health (MDH)  kwa miaka mitatu  kuanzia Januari 2018 na unatarajiwa kuhitimishwa Desemba 2020, ambacho kilifanyika jana Mjini Bariadi. 

Katibu Tawala wa mkoa wa Simiyu, Bi. Miriam Mmbaga (kushoto) akiteta jambo na Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika liliso la Kiserikali la Management and Development for Health (MDH), Emilian Busara  katika kikao kazi cha tathmini ya utekelezaji wa mradi wa kudhibiti kifua kikuu ngazi ya jamii uliokuwa ukitekelezwa  na mkoa wa Simiyu kwa kushirikiana  na shirika hilo  kwa miaka mitatu  kuanzia Januari 2018 na unatarajiwa kuhitimishwa Desemba 2020, ambacho kilifanyika jana Mjini Bariadi. 
:- Katibu Tawala wa mkoa wa Simiyu, Bi. Miriam Mmbaga (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na washiriki wa  kikao kazi cha tathmini ya utekelezaji wa mradi wa kudhibiti kifua kikuu ngazi ya jamii uliokuwa ukitekelezwa  na mkoa wa Simiyu kwa kushirikiana  na shirika lisilo la  Kiserikali la Management and Development for Health (MDH)  kwa miaka mitatu  kuanzia Januari 2018 na unatarajiwa kuhitimishwa Desemba 2020,  mara baaada ya kufungua kikao hicho ambacho kilifanyika jana Mjini Bariadi. 

Baadhi ya washiriki wa kikao kazi cha tathmini ya utekelezaji wa mradi wa kudhibiti kifua kikuu ngazi ya jamii uliokuwa ukitekelezwa  na mkoa wa Simiyu kwa kushirikiana  na shirika lisilo la  Kiserikali la Management and Development for Health (MDH)  kwa miaka mitatu  kuanzia Januari 2018 na unatarajiwa kuhitimishwa Desemba 2020,  wakifuatilia mada zilikuwa zikiwasilishwa katika kikao hicho ambacho kilifanyika jana Mjini Bariadi. 

Baadhi ya washiriki wa kikao kazi cha tathmini ya utekelezaji wa mradi wa kudhibiti kifua kikuu ngazi ya jamii uliokuwa ukitekelezwa  na mkoa wa Simiyu kwa kushirikiana  na shirika lisilo la  Kiserikali la Management and Development for Health (MDH)  kwa miaka mitatu  kuanzia Januari 2018 na unatarajiwa kuhitimishwa Desemba 2020,  wakifuatilia mada zilikuwa zikiwasilishwa katika kikao hicho ambacho kilifanyika jana Mjini Bariadi. 

Kutoka Kulia Katibu Tawala wa mkoa wa Simiyu, Bi. Miriam Mmbaga, Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Dkt.  Khamis Kulemba na washiriki wengine wa kikao kazi cha tathmini ya utekelezaji wa mradi wa kudhibiti kifua kikuu ngazi ya jamii uliokuwa ukitekelezwa  na mkoa wa Simiyu kwa kushirikiana  na shirika lisilo la  Kiserikali la Management and Development for Health (MDH)  kwa miaka mitatu  kuanzia Januari 2018 na unatarajiwa kuhitimishwa Desemba 2020, wakifurahia jambo katika kikao hicho kilichofanyika jana Mjini Bariadi. 

Baadhi ya washiriki wa kikao kazi cha tathmini ya utekelezaji wa mradi wa kudhibiti kifua kikuu ngazi ya jamii uliokuwa ukitekelezwa  na mkoa wa Simiyu kwa kushirikiana  na shirika lisilo la  Kiserikali la Management and Development for Health (MDH)  kwa miaka mitatu  kuanzia Januari 2018 na unatarajiwa kuhitimishwa Desemba 2020,  wakifuatilia mada zilikuwa zikiwasilishwa katika kikao hicho ambacho kilifanyika jana Mjini Bariadi. 

Baadhi ya washiriki wa kikao kazi cha tathmini ya utekelezaji wa mradi wa kudhibiti kifua kikuu ngazi ya jamii uliokuwa ukitekelezwa  na mkoa wa Simiyu kwa kushirikiana  na shirika lisilo la  Kiserikali la Management and Development for Health (MDH)  kwa miaka mitatu  kuanzia Januari 2018 na unatarajiwa kuhitimishwa Desemba 2020,  wakifuatilia mada zilikuwa zikiwasilishwa katika kikao hicho ambacho kilifanyika jana Mjini Bariadi. 

Mmoja wa wawasilishaji akiwasilisha taarifa katika kikao kazi cha tathmini ya utekelezaji wa mradi wa kudhibiti kifua kikuu ngazi ya jamii uliokuwa ukitekelezwa  na mkoa wa Simiyu kwa kushirikiana  na shirika lisilo la  Kiserikali la Management and Development for Health (MDH)  kwa miaka mitatu  kuanzia Januari 2018 na unatarajiwa kuhitimishwa Desemba 2020, ambacho kilifanyika jana Mjini Bariadi. 

Kutoka Kulia Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika liliso la Kiserikali la Management and Development for Health (MDH), Emilian Busara, Katibu Tawala wa mkoa wa Simiyu, Bi. Miriam Mmbaga, Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Dkt.  Khamis Kulemba wakifurahia jambo katika kikao kazi cha tathmini ya utekelezaji wa mradi wa kudhibiti kifua kikuu ngazi ya jamii uliokuwa ukitekelezwa  na mkoa wa Simiyu kwa kushirikiana  na shirika lisilo la  Kiserikali la Management and Development for Health (MDH)  kwa miaka mitatu  kuanzia Januari 2018 na unatarajiwa kuhitimishwa Desemba 2020, ambacho kilifanyika jana Mjini Bariadi. 

 

Moja ya panya wa Chuo Kikuu cha Kilimo Sokoine (SUA) wanaotumika kupima makohozi kubaini vijidudu vya Kifua Kikuu ambao tayari wamepewa mafunzo

KATAVI WAFANYA ZIARA SIMIYU KUJIFUNZA NAMNA YA KUFANYA MAONESHO YA NANENANE

Timu ya wataalam kutoka Mkoa wa Katavi imefanya ziara  Agosti 26, 2020 mkoani Simiyu kwa lengo la kujifunza namna kufanya Maonesho ya Kilimo na Sherehe za Wakulima (Nanenane) ambayo yamefanyika Kitaifa kwa miaka mitatu mfululizo (2018-2020) mkoani hapa.

Akizungumza na wataalam hao Katibu Tawala wa mkoa wa Simiyu, Bi. Miriam Mmbaga amesema ni vema maonesho hayo yakaakisi mahitaji ya wakulima, wafugaji na wavuvi ili kuwasaidia kupata elimu na kuona teknolojia mbalimbali zitakazowawezesha kufanya shughuli za kilimo, ufugaji na uvuvi kwa tija.

Aidha , Bi. Mmbaga ameongeza kuwa ushiriki wa taasisi mbalimbali za Umma na binafsi katika maonesho haya una manufaa kwa wakulima, wafugaji na wavuvi kwa kuwa huwa zinatoa huduma ambazo zinayagusa makundi hayo yote matatu.

 "Ili kuboresha Maonesho ya Nanenane suala la uendelevu wa viwanja ni la kulizingatia sana hususani katika dhana ya kutoa elimu kwa wakulima ili waweze kupata elimu ya kilimo bora, wakati wote wanapohitaji kupitia viwanja hivyo," alisema Bi. Mmbaga.

Pichani ni Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bi. Miriam Mmbaga akizungumza na wataalam hao na akiwa katika picha ya pamoja mara baada ya ziara hiyo.

MWISHO 




DCP KADASHARI AFANYA ZIARA SIMIYU KUKAGUA UTAYARI WA POLISI

 Kaimu Kamishina wa Fedha na Logistiki wa Jeshi la Polisi ambaye pia ni mlezi wa mikoa ya Kipolisi ya Simiyu, Geita, Kagera, Mara, Mwanza na Tarime, Dhahiri Kidavashari amefanya ziara  Agosti 26, 2020 mkoani Simiyu.

Katika ziara yake amekutana na viongozi na askari wa Jeshi la polisi Viongozi wa Mkoa ambapo ziara yake ililenga kuangalia utayari wa askari wa jeshi la Polisi kuelekea katika Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Oktoba 28 mwaka huu.

"Sisi kama Jeshi la Polisi tumejipanga katika kuhakikisha kwamba amani na utulivu unatawala katika kipindi cha kuanzia kampeni mpaka matokeo yanapotangazwa na nchi inakuwa salama; tunaangalia utayari wa askari wetu katika rasimali watu, vitendea kazi pamoja na elimu na utayari wa jumla kwa jamii," alisema Kidavasha.

Pichani ni kiongozi huyo alipokutana na Katibu Tawala wa mkoa wa Simiyu, Bi. Miriam Mmbaga akiwa ameambatana na viongozi wa Jeshi la Polisi wa Mkoa wa Simiyu akiwepo Kamanda wa Polisi wa mkoa wa Simiyu, Henry Mwaibambe.







Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!