Saturday, August 1, 2020

MAKAMU WA RAIS AZITAKA TAASISI ZA FEDHA KUONGEZA FURSA ZA MIKOPO KWA WAKULIMA

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan amezitaka taasisi za fedha hapa nchini kuongeza fursa za mikopo kwa wakulima, wafugaji na wavuvi ili kuongeza tijakatika uzalishaji.

 Makamu wa Rais ameyasema hayo Agosti Mosi, 2020 katika ufunguzi wa Maonesho ya Nanenane yaliyofanyika Kitaifa katika kanda ya ziwa Mashariki viwanja vya Nyakabindi Bariadi Mkoani Simiyu.

 “Benki za CRDB, NMB na NBC zimejiongeza sana katika kutoa mikopo kwa wakulima, wafugaji na wavuvi, katika mikopo iliyotolewa katika kipindi hiki ni asilimia 09 tu  ya mikopo ndiyo iliyokwenda kwenye sekta ya kilimo, ninaomba mikopo katika sekta hii iongezwe ili tuweze kuongeza tija katika kilimo, mifugo na uvuvi,” alisema Mhe. Makamu wa Rais.

Aidha, Makamu wa Rais ametoa rai kwa Watafiti wote nchini kutoa matokeo ya tafiti zao ili yaweze kuwasaidia maafisa ugani na wadau wengine ili wakulima waweze kunufaika na mtokeo hayo.

Katika hatua nyingine Mhe. Makamu wa Rais ameipongeza Wizara ya Kilimo kwa kujenga jengo la kudumu katika Viwanja vya Nyakabindi Bariadi na kwa kuwa limejengwa kwa gharama kubwa ameelekeza litumike kwa malengo yaliyokusudiwa.

Akizungumzia Kauli Mbiu ya Maonesho ya Nanenane mwaka 2020 inayosema “ KWA MAENDELEO YA KILIMO, MIFUGO NA UVUVI CHAGUA VIONGOZI BORA 2020,” Mhe. Makamu wa Rais ametoa wito kwa wananchi wote kuwa wakati utakapofika wachague viongozi wenye sifa, wazalendo na wenye kuweka maslahi ya Taifa mbele kuliko maslahi binafsi.

Kwa upande wake Waziri wa Kilimo, Mhe. Japhet Hasunga amesema serikali imeimarisha mfumo wa upatikanaji wa pembejeo za kilimo ambapo kwa sasa serikali imehakikisha pembejeo zinapatikana kwa wakati jambo lililopelekea nchi kuwa na utoshelevu wa chakula kwa zaidi ya asilimia 120.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka amesema ipo hoja na haja kwa  Wizara ya kilimo kufanya viwanja vya Nyakabindi kuwa endelevu na kufikiria katika kanda walizonazo, (eneo gani) kanda ipi kati ya hizo itakuwa kituo mahiri cha shughuli za wakulima, wafugaji na wavuvi kufanya maonesho yatakayolenga kuwa maonesho ya Kimataifa badala ya kufanya mzunguko katika kanda hizo.   


Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan akionesha nakala za mwongozo wa Taifa wa Uongezaji wa Virutubisho na Mafunzoya Lishe kwa wakulima mara baada ya kuuzindua Agosti Mosi, 2020 katika Maonesho ya Nanenane Kitaifa yanayoendelea katika Viwanja vya Nyakabindi Mkoani Simiyu, kushoto ni Waziri wa Kilimo, Mhe. Japhet Hasunga na Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka (kulia).

TAZAMA PICHA MBALIMBALI, MAKAMU WA RAIS AKITEMBELEA MABANDA YA MAONESHO, AKIZUNGUZA NA VIONGOZI NA WANANCHI NA VIONGOZI WENGINE PAMOJA NA WANANCHI KATIKA  UFUNGUZI WA MAONESHO YA NANENANE KITAIFA 2020 VIWANJA VYA NYAKABINDI.







  






























0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!