Thursday, August 27, 2020

SUA YAAHIDI KUSAIDIA KUANZISHA KITUO CHA KUPIMA KIFUA KIKUU KWA KUTUMIA PANYA SIMIYU

Chuo Kikuu cha Kilimo Sokoine (SUA) kimeahidi kuwa kiko tayari  kuanzisha kituo cha kupima  makohozi  kwa kutumia panya waliofundishwa kubaini vijidudu vya Ugonjwa wa Kifua Kikuu ambao wanaweza kupima sampuli nyingi kwa wakati mmoja ikilinganishwa na vipimo vya maabara.

Hayo yamebainishwa jana na Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bi. Mmbaga kikao kazi cha tathmini ya utekelezaji wa mradi wa kudhibiti kifua kikuu ngazi ya jamii uliokuwa ukitekelezwa  na mkoa wa Simiyu kwa kushirikiana  na shirika lisilo la  Kiserikali la Management and Development for Health (MDH),  kwa miaka mitatu  kuanzia Januari 2018 na unatarajiwa kuhitimishwa Desemba 2020, ambacho kilifanyika jana Mjini Bariadi.

“Tumeona ni muhimu tukaangalia tunavyoweza kutumia teknolojia nyingine kufanya  upimaji wa Ugonjwa wa Kifua Kikuu, kwa mfano tumepata fursa ya kushirikiana na wenzetu wa SUA kipindi cha nanenane mwaka huu  wamesema wako tayari kutusaidia kuanzisha kituo cha upimaji wa makohozi kwa kutumia panya waliofundishwa,” alisema Mmbaga.

Aidha, Mmbaga amesema mkoa wa Simiyu umeonekana kufanya vizuri katika kuwafikia wagonjwa wa Kifua kikuu ikilinganishwa na mikoa mingine saba ambayo yote inatekeleza mradi wa kudhibiti kifua kikuu ngazi ya jamii chini ya shirika lisilo la  Kiserikali la Management and Development for Health (MDH) ambapo umevuka lengo na kuwafikia wananchi kwa asilimia 102.

Pamoja na mafanikio hayo Mmbaga ameelekeza wataalam wafanye tathmini ya malengo yao na waweke malengo mapya yatakayokusudia kuwafikia wananchi wengi wenye uhitaji, ili kupata jamii yenye afya itakayotekeleza kwa vitendo azma na dira ya mkoa ya kuwa mkoa wenye uchumi shindani kwa kutumia rasilimali na fursa zilizopo.

Kwa upande wake Mratibu wa Huduma za kudhibiti Kifua kikuu na Ukoma, Dkt. Emmanuel John amesema kwa mwaka 2019 Mkoa wa Simiyu ulikuwa na lengo la kuwafikia wagonjwa wa Kifua Kikuu 1631 ambapo mpaka kufikia mwezi Desemba 2019 wagonjwa takribani  1673 walikuwa wamefikiwa sawa na asilimia 102 ya lengo.

Dkt. John ameongeza kuwa katika wagonjwa waliokuwa wameanzishiwa matibabu kwa mwaka 2018/2019  asilimia 72 waliweza kupona kabisa, huku akibainisha kuwa katika asilimia 28  baadhi yao walifariki, baadhi walipotea katika mifumo ya matibabu (watoro); huku akiweka bayana kuwa kwa mwaka 2020,  lengo la Mkoa ni kuwafikia wagonjwa 1779.

Naye Kaimu Mganga Mkuu wa Simiyu, Dkt. Khamis Kulemba amesema kuwa wataalam wa afya ngazi ya mkoa na halmashauri watahakikisha wanafanya marejeo ya malengo yao yaweze kuakisi hali halisi ya mahitaji ya jamii ili wananchi wengi waweze kufikiwa na huduma za upimaji na matibabu ya Kifua Kikuu.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Shirika lisilo la Kiserikali la Management and Development for Health (MDH), Bw. Eliamin Busara amesema katika awamu ijayo shirika hilo linatarajia kujikita zaidi katika mpango wa Kifua Kikuu na uboreshaji wa huduma za mama na mtoto hususani katika kuzuia maambukizi ya Virusi vya UKIMWI.

Wakati huo huo Busara ametoa wito kwa Serikali kupitia halmashauri kuwa na mipango ya namna ya kuendeleza huduma zilizokuwa zikitolewa kwa wananchi kupitia mradi huo ili huduma za afya zisitetereke hususani katika upimaji na matibabu ya Kifua Kikuu.

MWISHO

 Katibu Tawala wa mkoa wa Simiyu, Bi. Miriam Mmbaga akifungua kikao kazi cha tathmini ya utekelezaji wa mradi wa kudhibiti kifua kikuu ngazi ya jamii uliokuwa ukitekelezwa  na mkoa wa Simiyu kwa kushirikiana  na shirika lisilo la  Kiserikali la Management and Development for Health (MDH)  kwa miaka mitatu  kuanzia Januari 2018 na unatarajiwa kuhitimishwa Desemba 2020, ambacho kilifanyika jana Mjini Bariadi. 
Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika liliso la Kiserikali la Management and Development for Health (MDH), Emilian Busara  akitoa taarifa katika kikao kazi cha tathmini ya utekelezaji wa mradi wa kudhibiti kifua kikuu ngazi ya jamii uliokuwa ukitekelezwa  na mkoa wa Simiyu kwa kushirikiana  na shirika hilo kwa miaka mitatu  kuanzia Januari 2018 na unatarajiwa kuhitimishwa Desemba 2020, ambacho kilifanyika jana Mjini Bariadi. 

Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Dkt.  Khamis Kulemba akichangia hoja katika kikao kazi cha tathmini ya utekelezaji wa mradi wa kudhibiti kifua kikuu ngazi ya jamii uliokuwa ukitekelezwa  na mkoa wa Simiyu kwa kushirikiana  na shirika lisilo la  Kiserikali la Management and Development for Health (MDH)  kwa miaka mitatu  kuanzia Januari 2018 na unatarajiwa kuhitimishwa Desemba 2020, ambacho kilifanyika jana Mjini Bariadi. 

Katibu Tawala wa mkoa wa Simiyu, Bi. Miriam Mmbaga (kushoto) akiteta jambo na Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika liliso la Kiserikali la Management and Development for Health (MDH), Emilian Busara  katika kikao kazi cha tathmini ya utekelezaji wa mradi wa kudhibiti kifua kikuu ngazi ya jamii uliokuwa ukitekelezwa  na mkoa wa Simiyu kwa kushirikiana  na shirika hilo  kwa miaka mitatu  kuanzia Januari 2018 na unatarajiwa kuhitimishwa Desemba 2020, ambacho kilifanyika jana Mjini Bariadi. 
:- Katibu Tawala wa mkoa wa Simiyu, Bi. Miriam Mmbaga (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na washiriki wa  kikao kazi cha tathmini ya utekelezaji wa mradi wa kudhibiti kifua kikuu ngazi ya jamii uliokuwa ukitekelezwa  na mkoa wa Simiyu kwa kushirikiana  na shirika lisilo la  Kiserikali la Management and Development for Health (MDH)  kwa miaka mitatu  kuanzia Januari 2018 na unatarajiwa kuhitimishwa Desemba 2020,  mara baaada ya kufungua kikao hicho ambacho kilifanyika jana Mjini Bariadi. 

Baadhi ya washiriki wa kikao kazi cha tathmini ya utekelezaji wa mradi wa kudhibiti kifua kikuu ngazi ya jamii uliokuwa ukitekelezwa  na mkoa wa Simiyu kwa kushirikiana  na shirika lisilo la  Kiserikali la Management and Development for Health (MDH)  kwa miaka mitatu  kuanzia Januari 2018 na unatarajiwa kuhitimishwa Desemba 2020,  wakifuatilia mada zilikuwa zikiwasilishwa katika kikao hicho ambacho kilifanyika jana Mjini Bariadi. 

Baadhi ya washiriki wa kikao kazi cha tathmini ya utekelezaji wa mradi wa kudhibiti kifua kikuu ngazi ya jamii uliokuwa ukitekelezwa  na mkoa wa Simiyu kwa kushirikiana  na shirika lisilo la  Kiserikali la Management and Development for Health (MDH)  kwa miaka mitatu  kuanzia Januari 2018 na unatarajiwa kuhitimishwa Desemba 2020,  wakifuatilia mada zilikuwa zikiwasilishwa katika kikao hicho ambacho kilifanyika jana Mjini Bariadi. 

Kutoka Kulia Katibu Tawala wa mkoa wa Simiyu, Bi. Miriam Mmbaga, Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Dkt.  Khamis Kulemba na washiriki wengine wa kikao kazi cha tathmini ya utekelezaji wa mradi wa kudhibiti kifua kikuu ngazi ya jamii uliokuwa ukitekelezwa  na mkoa wa Simiyu kwa kushirikiana  na shirika lisilo la  Kiserikali la Management and Development for Health (MDH)  kwa miaka mitatu  kuanzia Januari 2018 na unatarajiwa kuhitimishwa Desemba 2020, wakifurahia jambo katika kikao hicho kilichofanyika jana Mjini Bariadi. 

Baadhi ya washiriki wa kikao kazi cha tathmini ya utekelezaji wa mradi wa kudhibiti kifua kikuu ngazi ya jamii uliokuwa ukitekelezwa  na mkoa wa Simiyu kwa kushirikiana  na shirika lisilo la  Kiserikali la Management and Development for Health (MDH)  kwa miaka mitatu  kuanzia Januari 2018 na unatarajiwa kuhitimishwa Desemba 2020,  wakifuatilia mada zilikuwa zikiwasilishwa katika kikao hicho ambacho kilifanyika jana Mjini Bariadi. 

Baadhi ya washiriki wa kikao kazi cha tathmini ya utekelezaji wa mradi wa kudhibiti kifua kikuu ngazi ya jamii uliokuwa ukitekelezwa  na mkoa wa Simiyu kwa kushirikiana  na shirika lisilo la  Kiserikali la Management and Development for Health (MDH)  kwa miaka mitatu  kuanzia Januari 2018 na unatarajiwa kuhitimishwa Desemba 2020,  wakifuatilia mada zilikuwa zikiwasilishwa katika kikao hicho ambacho kilifanyika jana Mjini Bariadi. 

Mmoja wa wawasilishaji akiwasilisha taarifa katika kikao kazi cha tathmini ya utekelezaji wa mradi wa kudhibiti kifua kikuu ngazi ya jamii uliokuwa ukitekelezwa  na mkoa wa Simiyu kwa kushirikiana  na shirika lisilo la  Kiserikali la Management and Development for Health (MDH)  kwa miaka mitatu  kuanzia Januari 2018 na unatarajiwa kuhitimishwa Desemba 2020, ambacho kilifanyika jana Mjini Bariadi. 

Kutoka Kulia Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika liliso la Kiserikali la Management and Development for Health (MDH), Emilian Busara, Katibu Tawala wa mkoa wa Simiyu, Bi. Miriam Mmbaga, Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Dkt.  Khamis Kulemba wakifurahia jambo katika kikao kazi cha tathmini ya utekelezaji wa mradi wa kudhibiti kifua kikuu ngazi ya jamii uliokuwa ukitekelezwa  na mkoa wa Simiyu kwa kushirikiana  na shirika lisilo la  Kiserikali la Management and Development for Health (MDH)  kwa miaka mitatu  kuanzia Januari 2018 na unatarajiwa kuhitimishwa Desemba 2020, ambacho kilifanyika jana Mjini Bariadi. 

 

Moja ya panya wa Chuo Kikuu cha Kilimo Sokoine (SUA) wanaotumika kupima makohozi kubaini vijidudu vya Kifua Kikuu ambao tayari wamepewa mafunzo

0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!