Tuesday, January 31, 2017

WAZIRI WA BIASHARA ATOA WITO KWA SERIKALI KUWEKEZA KATIKA HISTORIA YA NCHI

Na Stella Kalinga
Waziri wa Viwanda,Biashara na Masoko wa Zanzibar,Mhe Amina Salum Ali ametoa wito kwa Serikali kuwekeza katika historia ya nchi na kurahisisha utaratibu wa kutembelea makumbusho ili wananchi wapate taarifa za kina na kujua historia ya nchi.

 Mhe.Waziri ameyasema hayo leo walayani Butiama alipotembelea makazi ya Hayati Baba wa Taifa Mwl.Julius Kambarage Nyerere na kuona kaburi lake katika eneo la Mwitongo wilayani humo.

Mhe.Waziri amesema ipo haja kwa Watanzania kufahamu historia ya nchi ili wailinde na kuienzi.

Aidha, ametoa wito kwa Watanzania kumuenzi Baba wa Taifa Mwl.Nyerere kwa kudumisha Armani,umoja na mshikamano ikiwa ni njia ya kuendeleza muungano aliouasisi kwa ushirikiano na Rais wa Kwanza wa Zanzibar,Hayati Sheikh  Abeid Aman Karume.

Mhe.Balozi Amina Salum Ali amepata fursa ya kutembelea maeneo mbalimbali ikiwa ni pamoja na nyumba alizoishi Hayati Mwl.Nyerere kabla na baada ya kuwa madarakani,makumbusho ya Mwl.Nyerere,makaburi ya wazazi wa Mwl.Nyerere, msitu wa Mwl.Nyerere,nyumba ya chifu wa Wazanaki,vihenge vya kuhifadhia mazao na maeneo mengine ambapo alipewa taarifa juu ya maeneo hayo

Naye Mkuu wa Mkoa wa Simiyu,Mhe Anthony Mtaka ametoa rai kwa viongozi hapa nchini kumuenzi kwa vitendo Hayati Baba Taifa,Mwl.Nyerere kwa kuendeleza mema aliyoyaanzisha kwa maslahi ya wananchi naTaifa kwa ujumla.

"Viongozi na hasa sisi vijana tunao wajibu wa kutekeleza kwa vitendo siyo Maneno mambo mema ya Mwl.Nyerere, mwalimu alikuwa mzalendo, hakupenda rushwa na ufisadi, alipenda haki, na sisi tunapaswa kumuenzi Mwl.Nyerere" amesema Mtaka.

Mhe.Waziri Balozi Amina Salum Ali amefanya ziara kwenye makazi ya Mwl.Nyerere wilayani Butiama akitokea mkoani Simiyu ambako alikuwa na ziara ya siku tatu yenye lengo la kutembelea na kuona maeneo mbalimbali yanayohusu sekta ya viwanda na biashara.

Akiwa Mkoani Simiyu Mhe Waziri ametembelea viwanda vidogo na vya kati vikiwemo kiwanda cha chaki (Maswa) na cha kusindika Maziwa(Meatu) pamoja na maeneo ya wawekezaji katika mazao ya biashara(Pamba)na chakula(mchele).

Mhe.Waziri amehitimisha ziara yake mkoani Simiyu kwa kuihakikishia Serikali ya Mkoa huo kuwa Zanzibar iko tayari kufanya biashara na mkoa huo hususani katika mazao ambayo yanaweza kutumika kama malighafi ya viwanda vya Zanzibar na mazao ya chakula kwa manufaa ya wananchi na Taifa kwa ujumla;jambo lililoungwa mkono na viongozi wa mkoa huyo.

 
Waziri wa Biashara,Viwanda na Masoko  wa Serikali za mapinduzi ya Zanzibar , Mhe. Balozi Amina Salum Ali (kulia), Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe.Anthony Mtaka  (kushoto) wakiwa katika eneo alizaliwa Hayati Baba wa Taifa Mwl.Julius Nyerere wakati alipotembea makazi ya Mw.Nyerere Mwitongo Wilayani Butiama.
Waziri wa Biashara,Viwanda na Masoko  wa Serikali za mapinduzi ya Zanzibar , Mhe. Balozi Amina Salum Ali (wa pili kushoto)  akiwasha mshumaa katika kaburi la Hayati Baba wa Taifa Mwl.Julius Nyerere wakati alipotembelea makazi ya Mw.Nyerere Mwitogo Wilayani Butiama
Waziri wa Biashara,Viwanda na Masoko  wa Serikali za mapinduzi ya Zanzibar , Mhe. Balozi Amina Salum Ali na baadhi ya viongozi wa Mkoa wa Simiyu wakipewa maelezo kuhusu kaburi la Hayati Baba wa Taifa Mwl.Nyerere na Mkurugenzi wa Makumbusho ya Mwl.Nyerere lililopo Mwitongo wilayani Butiama.

Katibu Tawala Mkoa wa Simiyu,Ndg.Jumanne Sagini  akiwa na baadhi ya wataalam wa Wizara ya Biashara,Viwanda na Masoko Zanzibar wakiwa katika moja ya maeneo ya kumbukumbu yaliyotembelewa na Waziri wa Biashara,Viwanda na Masoko  wa Serikali za mapinduzi ya Zanzibar , Mhe. Balozi Amina Salum Ali alipotembelea makazi ya Hayati Baba wa Taifa Mwl.Nyerere
Waziri wa Biashara,Viwanda na Masoko  wa Serikali za mapinduzi ya Zanzibar , Mhe. Balozi Amina Salum Ali (mwenye suti nyeusi), viongozi na baadhi ya Wataalam wa Mkoa wa Simiyu wakiingia katika eneo la Makazi ya Hayati Baba wa Taifa Mwl.Julius Nyerere Mwitongo Wilayani Butiama

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu,Mhe.Anthony Mtaka akiwasha mshumaa katika kaburi la Hayati Baba wa Taifa Mwl.Julius Nyerere wakati alipotembelea makazi ya Mw.Nyerere Mwitogo Wilayani Butiama.

Katibu Tawala Mkoa wa Simiyu,Ndg.Jumanne Sagini, Waziri wa Biashara,Viwanda na Masoko Zanzibar Mhe. Balozi Amina Salum Ali , wataalam wa wizara hiyo na Wataalam  wa Mkoa wa Simiyuwakienda kuona moja ya nyumba ya Mwalimu Nyerere.
Waziri wa Biashara,Viwanda na Masoko Zanzibar Mhe. Balozi Amina Salum Ali , wataalam wa wizara hiyo, Viongozi na Watalaam wa Mkoa wa Simiyu wakipewa maelezo juu ya zana za asili mara baada ya kutembelea Makumbusho ya Hayati Baba wa Taifa,Mwl.Nyerere.
Waziri wa Biashara,Viwanda na Masoko  wa Serikali za mapinduzi ya Zanzibar , Mhe. Balozi Amina Salum Ali na baadhi ya viongozi wa Mkoa wa Simiyu wakipewa maelezo kuhusu moja ya nyumba za Hayati Baba wa Taifa Mwl.Nyerere na Mkurugenzi wa Makumbusho ya Mwl.Nyerere iliyopo Mwitongo wilayani Butiama.
Waziri wa Biashara,Viwanda na Masoko  wa Serikali za mapinduzi ya Zanzibar , Mhe. Balozi Amina Salum Ali (kushoto), akiwa nafimbo aliyopewa na Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe.Anthony Mtaka  (kulia) kama zawadi walipotembea makazi ya Mwl.Nyerere eneo la Mwitongo Wilayani Butiama.
Waziri wa Biashara,Viwanda na Masoko  wa Serikali za mapinduzi ya Zanzibar , Mhe. Balozi Amina Salum Ali  akiwa na viongozi na wataalam wa Mkoa wa Simiyu wakiwa katika moja ya nyumba ya Hayati Baba wa Taifa, Mwl.Nyerere.
Sehemu ya moja ya nyumba ya Hayati Baba wa Taifa, Mwl.Nyerere aliyoishi baada ya kuondoka madarakani.
Baadhi ya vihenge vilivyotumika na Hayati Mwl.Julius Nyerere kwa ajili ya kuhifadhia mazao ya nafaka.
Nyumba lilimo kaburi la Hayati Baba wa Taifa, Mwl.J.K. Nyerere.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe.Anthony Mtaka(kushoto) akimkabidhi Mwenyekiti wa Klabu ya Waandishi wa Habari ya Mkoa huo, Ndg.Frank Kasamwa  zawadi ya fimbo aliyonunua Katika Makumbusho ya Mwl.J.K Nyerere.
Baadhi ya vitu vilivyopo katika Makumbusho ya Mwl.Julius Kambarage Nyerere Mwitongo Butiama.
Waziri wa Biashara,Viwanda na Masoko  wa Serikali za mapinduzi ya Zanzibar , Mhe. Balozi Amina Salum Ali, viongozi na wataalam wa Mkoa wa Simiyu wakiwa katika picha ya pamoja nje ya jengo la Makumbusho la Mwl.Julius Kambarage Nyerere.
Waziri wa Biashara,Viwanda na Masoko  wa Serikali za mapinduzi ya Zanzibar , Mhe. Balozi Amina Salum Ali (mwenye suti nyeusi), viongozi na wataalam wa Mkoa wa Simiyu wakiwa katika moja ya miradi ya ufugaji wa samaki wilayani Busega.
Mkuu wa Wilaya ya Busega,Mhe.Tano Mwera akizungumza wakati wa ziara ya Waziri wa Biashara,Viwanda na Masoko  wa Serikali za mapinduzi ya Zanzibar , Mhe. Balozi Amina Salum Ali (mwenye suti nyeusi) wilayani humo.
Waziri wa Biashara,Viwanda na Masoko  wa Serikali za mapinduzi ya Zanzibar , Mhe. Balozi Amina Salum Ali (wa nne kushoto),, viongozi na wataalam wa Mkoa wa Simiyu wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya Waziri huyo kuhitimisha ziara ya siku tatu mkoani Humo.
Waziri wa Biashara,Viwanda na Masoko  wa Serikali za mapinduzi ya Zanzibar , Mhe. Balozi Amina Salum Ali akizungumza na viongozi na wataalamu wa mkoa wa Simiyu (hawapo pichani) wakati wa kuhitimisha ziara yake ya siku tatu Mkoani humo..

Monday, January 30, 2017

WAKULIMA NCHINI WASHAURIWA KULIMA KILIMO HAI KUONGEZA THAMANI YA MAZAO

Na Stella Kalinga

Wakulima  nchini wametakiwa kufanya maamuzi magumu yatakayoleta mapinduzi ya kiuchumi  kwa kulima kilimo HAI (kilimo kisichotumia kemikali za viwandani)  kinachozingatia kanuni bora kwa kuwa kimeonyesha tija katika kuongeza thamani ya mazao.

Wito huo umetolewa na Waziri wa Biashara,Viwanda na Masoko wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Mhe. Balozi Amina Salum Ali alipotembelea Kampuni ya Biore wilayani Meatu katika ziara yake ya kutembelea viwanda vidogo na vya kati  mkoani Simiyu.

Mhe. Balozi Amina Salum Ali amesema upo umuhimu sasa kwa viongozi wa serikali kuhakikisha wanafanya maamuzi magumu yatakayoboresha uchumi wa watanzania ikiwa ni pamoja na kutoa maelekezo sahihi ya kuzingatia kilimo  HAI (oganiki) kinachofuata kanuni bora za kilimo pasipo  kuchanganya na masuala ya kisiasa.

“Biashara ya sasa hivi inaelekea zaidi katika masuala mazima ya oganiki na ukiangalia kuna tofauti kubwa sana ya bei katika vitu vya oganiki na ambavyo siyo oganiki, kwa mfano Karafuu ya tunayoiuza ambayo siyo oganiki inauzwa shilingi 8100 na ambayo ni oganiki inauzwa 9900 kwa hiyo chochote ambacho ni oganiki unapata bei nzuri; watu wengi wanakimbia kulima kilimo hai kwa sababu ya hutumia nguvu zaidi katika usafi,  ulimaji ,ukaushaji wake ambao unazingatia viwango, lakini manufaa yake ni makubwa sana” amesema Balozi Amina Salum Ali.

Ameongeza Zanzibar imeingia katika hatua nyingine ambapo imedhamiria kuanzisha viwanda vitakavyotumia malighafi ambayo ni oganiki(hai) ambapo wanataka kulima maua, viungo na mazao mengine ambayo yatauzwa ndani na nje ya nchi, hivyo wako tayari kuwekeza mkoani Simiyu hususani katika ardhi ya kuzalisha mazao hayo.

Aidha Waziri huyo wa Zanzibar akizungumzia umuhimu wa biashara ya ndani ya nchi amesema takwimu zinaonyesha kuwa mataifa mengi ya Afrika yanafanya biashara ya ndani chini ya asilimia 27 na akasisitiza uboreshaji wa mifumo ya uendeshaji wa biashara na  mnyororo wa thamani ili Tanzania iweze kufikia uchumi wa kati.

Kwa upande wake mmoja wa wawekezaji anayetekeleza kilimo  HAI (kisichotumia madawa na kemikali za viwandani) kwa zao la pamba  Mkurugenzi wa Kampuni ya Biore Tanzania Niranjan Pattni  amekiri kuwepo kwa tija kubwa zaidi endapo wakulima wataingia katika mfumo wa kilimo HAI , ambapo Kampuni yake imekuwa ikitoa elimu ya kilimo na utunzaji wa mazao, mikopo ya gharama nafuu, pembejeo bora za kilimo  na kuwahakikishia soko la uhakika na nyongeza ya bei.

Naye Mkuu wa mkoa wa Simiyu,Mhe.Anthony Mtaka amesema ili kilimo kiweze kufikia kuwa eneo la kutegemewa kwenye malighafi katika Tanzania ya Viwanda,  ni lazima wananchi waende kwenye kilimo cha kisasa ambacho kinahitaji gharama ya mbegu bora, mbolea na pembejeo nyingine bora za kilimo.

“Sisi kama mkoa tunajipanga kuwa mkoa utakaozalisha bidhaa za afya zitokanazo na pamba na bidhaa hizi zinahitaji pamba iliyoandaliwa vizuri na mfano ni pamba ya Biore, kama ukitaka kupata eneo ambalo unaweza kujifunza pamba tutakayoihitaji kuzalisha kama malighafi ya bidhaa za kiwanda cha bidhaa za afya ni pamba ya Biore ambayo ni oganiki na ina gharama kubwa hata kwenye soko la Dunia” amesema Mtaka.

Mheshimiwa Balozi Amina Salum Ally amemaliza ziara yake wilayani Meatu na anatarajia kukamilisha ziara yake Mkoani Simiyu na kufanya majumuisho wilayani Busega, ambapo akiwa Wilayani Meatu ametembelea na kuona kiwanda cha kusindika maziwa, ng’ombe wa kisasa wa maziwa, mashamba ya malisho ya mifugo na kukutana na mwekezaji wa kampuni ya Biore Tanzania anayejishughulisha na kilimo cha pamba ya oganiki(pamba hai).


Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka (kulia) akimkabidhi Waziri wa Biashara,Viwanda na Masoko wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Mhe. Balozi Amina Salum Ali zawadi ya maziwa ambayo alipewa na Halmashauri ya Wilaya ya Meatu mara baada ya kutembelea kiwanda cha kusindika maziwa wakati wa ziara yake wilayani humo.
Waziri wa Biashara,Viwanda na Masoko wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Mhe. Balozi Amina Salum Ali(kulia) akipewa maelezo na mmoja wa vijana wa Meatu wanajishughulisha na usindikaji wa maziwa mara baada ya kutembelea kiwanda cha kusindika maziwa wakati wa ziara yake wilayani humo.
Waziri wa Biashara,Viwanda na Masoko wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Mhe. Balozi Amina Salum Ali(kushoto) akizungumza jambo na Mkuu wa Wilaya ya Meatu, Mhe.Joseph Chilongani wakati alipotembelea na kuona ng’ombe wa maziwa waliofugwa kwa ajili ya kuongeza hali ya upatikanaji wa maziwa kwa kiwanda cha maziwa wakati wa ziara yake wilayani humo.
Waziri wa Biashara,Viwanda na Masoko wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Mhe. Balozi Amina Salum Ali(kushoto) akizungumza na viongozi wa wilaya ya Meatu wakati akiwa katika ziara ya siku moja wilayani humo.
Mwenyekiti wa Halmsahauri ya Wilaya ya Meatu, Mhe.Pius Machungwa akimkabidhi Mkuu wa Mkoa wa Simiyu zawadi ya maziwa wakati wa ziara ya Waziri wa Biashara,Viwanda na Masoko wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Mhe. Balozi Amina Salum Ali wilayani humo
: Waziri wa Biashara,Viwanda na Masoko wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Mhe. Balozi Amina Salum Ali akiwa na viongozi wengine mara baada ya kutembelea kiwanda cha kusindika maziwa wilayani Meatu.
Mkuu wa Wilaya ya Meatu, Mhe.Joseph Chilongani  akitoa maelezo ya utangulizi kwa Waziri wa Biashara,Viwanda na Masoko wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Mhe. Balozi Amina Salum Ali mara baada ya kuwasili katika Ofisi ya Kampuni ya Biore Tanzania wakati wa ziara yake wilayani humo.
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Biore Tanzania inayojishughulisha na kilimo hai Ndg. Niranjan Pattni (kushoto) akisoma taarifa ya kampuni yake kwa Waziri wa Biashara,Viwanda na Masoko wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Mhe. Balozi Amina Salum Ali alipomtembelea wakati wa ziara yake wilayani humo.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka (wa pili kulia)  akizungumza na viongozi wa Mkoa, wilaya ya Meatu na Watumishi wa Biore Tanzania wakati wa ziara ya Waziri wa Biashara,Viwanda na Masoko wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Mhe. Balozi Amina Salum Ali wilayni Meatu.
Waziri wa Biashara,Viwanda na Masoko wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Mhe. Balozi Amina Salum Ali akipanda mti wa kumbukumbu katika eneo la kampuni ya Biore Tanzania mara baada ya kutembelea eneo hilo wakati wa ziara yake wilayani Meatu.
:-Mkuu wa Mkoa wa Simiyu,Mhe.Anthony Mtaka akipanda mti wa kumbukumbu katika eneo la kampuni ya Biore Tanzania wilayani Meatu wakati wa ziara ya Waziri wa Biashara,Viwanda na Masoko wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Mhe. Balozi Amina Salum Ali wilayani humo.
Waziri wa Biashara,Viwanda na Masoko wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Mhe. Balozi Amina Salum Ali(kushoto)akizunumza jambo na Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Meatu,Mhe.Juma Mwibuli akiwa wilayani humo wakati wa ziara yake Mkoani Simiyu.

Sunday, January 29, 2017

WAZIRI WA VIWANDA ,BIASHARA NA MASOKO WA ZANZIBAR AANZA ZIARA YA SIKU TATU MKOANI SIMIYU

Na Stella Kalinga

Waziri wa Viwanda,Biashara na Masoko wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Mhe.Balozi Amina Salum Ali ameanza ziara ya kikazi ya siku tatu mkoani Simiyu.

Mhe.Waziri akiwa mkoani Simiyu atatembelea maeneo mbalimbali yanayogusa wizara yake ikiwa ni pamoja kutembelea viwanda vidogo na vya kati vinavyochakata na kuzalisha bidhaa mbalimbali ambazo malighafi yake inapatikana hapa nchini.

Akizungumza na viongozi wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Balozi Amina Salum Ali amesema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar iko tayari kufanya biashara na wananchi/wafanyabiashara wa Mkoa huo kwa lengo la kuboresha biashara ya ndani ya nchi ikiwa ni njia mojawapo  ya kudumisha Muungano kati ya pande zote za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Mhe.Waziri amesema Serikali ya mapinduzi ya Zanzibar inataka kufanya biashara ya viungo(spices), mazao ya jamii ya mikunde na mchele, ambapo amewaeleza viongozi wa Mkoa wa Simiyu kuwa endapo Serikali ya Mkoa huo itaihakikishia Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar upatikanaji wa bidhaa hizo hakutakuwa na haja ya kuagiza kutoka nje ya nchi.

Ameongeza kuwa biashara ya wenyewe kwa wenyewe itawahakikishia wananchi kupata soko la uhakika hali itakayowawezesha kuinua uchumi wao.

“Biashara hii itafanikiwa ikiwa kila mmoja atatimiza wajibu wake na ni lazima kuwe na mkakati wa pamoja utakaoenda sambamba na utekelezaji wa Sera ya Tanzania ya Viwanda na itawezekana kufikia Uchumi wa Kati” alisema Mhe. Waziri Amina Salum Ali.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe.Anthony Mtaka amesema Mkoa huo uko tayari kushirikiana na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika masuala ya biashara hususani kwenye mazao ya mikunde na viungo ambapo amesema watawahamasisha wananchi kulima mazao hayo kwa kilimo chenye tija(kilimo biashara).

Kuhusu uhakika wa upatikanaji wa mchele Mtaka amesema Mkoa wake ka kushirikiana na wadau wengine ikiwepo Benki ya NMB utaanza kutekeleza mradi wa kilimo cha umwagiliaji wilayani Busega ambao ni kipaumbele cha mkoa kwa mwaka 2017, ambapo wananchi watakuwa na uwezo wa kulima mpunga kwa kutumia maji ya uhakika ya Ziwa Victoria, hivyo kupitia mradi huo wananchi wataweza kuuza mchele Zanzibar.

“ Mhe..Waziri tumeamua kama mkoa kulima kilimo cha umwagiliaji Busega kwa kuwa tuna uhakika wa maji ili wananchi wa wetu walime mpunga, hatuwezi tukawa tunaletewa mchele kutoka nje na nchi ambazo zinatumia maji ya Ziwa victoria na sisi tulionalo hapa tunaliangalia tu, .......Nikuahidi kuwa hatutakuangusha” alisema Mtaka

Mhe.Balozi Amina Salum Ali amefanya ziara hii kutekeleza agizo la Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt.Ali Mohamed Shein  aliyoitoa wakati wa Maadhimisho Kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru, Wiki ya Vijana na Kumbukizi ya Kifo cha Baba wa Taifa Mwl.Julius Kambarage Nyerere Oktoba  2016,  yaliyofanyika Kitaifa Mkoani Simiyu; ambapo alielekza kuwa
baadhi ya mawaziri wake watakuja kwa ajili ya kujadili namna ya Kujenga urafiki na ushirika kati ya Zanzibar na Mkoa wa Simiyu katika masuala ya sekta mbalimbali ikiwemo elimu, kilimo na viwanda.
Waziri wa Viwanda,Biashara na Masoko wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Mhe.Balozi Amina Salum Ali(wa tatu kushoto) akiangalia chaki zilizotengenezwa na vijana wa Maswa Family mara baada ya kutembelea kiwanda cha Chaki wilayani Maswa wakati wa ziara yake Mkoani Simiyu.

Waziri wa Viwanda,Biashara na Masoko wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Mhe.Balozi Amina Salum Ali(mwenye ushungi ) akiangalia namna chaki zinavyotengenezwa na vijana wa Maswa Family mara baada ya kutembelea kiwanda cha Chaki wilayani Maswa wakati wa ziara yake Mkoani Simiyu.
Waziri wa Viwanda,Biashara na Masoko wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Mhe.Balozi Amina Salum Ali(mwenye ushungi) akipewa maelezo mafupi juu ya utengenezaji wa chaki na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa, Dkt.Fredrick Sagamiko (wa pili kushoto) mara baada ya kutembelea kiwanda cha Chaki wilayani Maswa wakati wa ziara yake Mkoani Simiyu.
Waziri wa Viwanda,Biashara na Masoko wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Mhe.Balozi Amina Salum Ali(mwenye ushungi rangi ya maziwa (kushoto)) akiangalia mchele ulikobolewa na kupangwa katika madaraja tofauti mara baada ya kutembelea kiwanda cha kukoboa mpunga na kupanga mchele katika madaraja cha N.G.S Company Liimited kilichopo Majahida Mjini Bariadi.
Mkurugenzi wa N.G.S Company Limited, Njalu Silanga ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama cha Wafanyabiashara Mkoa wa Simiyu(kulia) akimkabidhi Waziri wa Viwanda,Biashara na Masoko wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Mhe.Balozi Amina Salum Ali (kushoto) zawadi ya mchele baada ya kutembelea kiwanda chake kilichopo Majahida Mjini Bariadi wakati wa ziara yake mkoani Simiyu
Mkurugenzi wa N.G.S Company Limited, Njalu Silanga ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama cha Wafanyabiashara Mkoa wa Simiyu(kulia) akimuonesha Waziri wa Viwanda,Biashara na Masoko wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Mhe.Balozi Amina Salum Ali (wa pili kushoto) baadhi ya maghala ya kuhifadhia nafaka mara baada ya  kutembelea kiwanda kukoboa mpunga na kupanga mchele katika madaraja (ambacho ni mali ya N.G.S Company Limited ) kilichopo Majahida Mjini Bariadi wakati wa ziara yake mkoani Simiyu.
Waziri wa Viwanda,Biashara na Masoko wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Mhe.Balozi Amina Salum Ali (kushoto) akipokea maelezo kutoka kwa mtalaam wa kusindika mafuta ya alizeti katika moja ya kiwanda cha kusindika mafuta hayo wilayani Maswa wakati wa ziara yake mkoani Simiyu.
Mkurugenzi wa N.G.S Company Limited, Njalu Silanga ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama cha Wafanyabiashara Mkoa wa Simiyu(kushoto) akitoa maelezo kwa Waziri wa Viwanda,Biashara na Masoko wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Mhe.Balozi Amina Salum Ali (wa pili kushoto) kabla ya waziri huyo   kutembelea kiwanda kukoboa mpunga na kupanga mchele katika madaraja (ambacho ni mali ya N.G.S Company Limited ) wakati wa ziara yake mkoani Simiyu.
Mkulima wa Kijiji cha Senani , Bw. Lupande Nila wilayani Maswa akimwelezea Waziri wa Viwanda,Biashara na Masoko wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Mhe.Balozi Amina Salum Ali juu ya zana za kisasa za kilimo alizotengeneza kwa kushirikiana na wenzake mara baada ya Waziri huyo kutembelea shamba  lake na kuona zana anazozitumia wakati akiwa katika ziara yake Mkoani Simiyu
Waziri wa Viwanda,Biashara na Masoko wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Mhe.Balozi Amina Salum Ali akisaini kitabu cha Wageni katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, mara baada ya kuwasili Mjini Baridi kwa lengo la kuanza ziara ya siku tatu mkoani humo.
Mkurugenzi Mwendeshaji wa Shirika la Biashara la  Zanzibar, Dkt. Said Seif Mzee akichangia jambo mara baada ya kupata taarifa ya Mkoa wakati wa ziara ya :- Waziri wa Viwanda,Biashara na Masoko wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Mhe.Balozi Amina Salum Ali mkoani Simiyu.






Friday, January 20, 2017

JINGU ASEMA SIMIYU IMEONYESHA MFANO


Na Stella Kalinga
Mwenyekiti wa Baraza la Uwezeshaji wananchi Kiuchumi  ,Ndg. John Jingu amesema Mkoa wa Simiyu umeonesha mfano wa namna viongozi wanavyoweza kutumia nafasi zao katika kuwaletea wananchi maendeleo.

Jingu ameyasema hayo leo katika kikao maalum kilichofanyika kati ya Uongozi wa Baraza hilo na Viongozi wa Mkoa wa Simiyu katika Ofisi za Baraza hilo jijini Dar es Salaam.

Jingu amempongeza Mkuu wa mkoa wa Simiyu,Mhe.Anthony Mtaka na viongozi wenzake kwa kutambua dhamira ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli  katika kuwaletea wananchi maendeleo na kuitekeleza kwa vitendo.

“Tunaona namna mnavyofanya kazi na mnatembea kwenye maneno yenu, mmefanikiwa kuanzisha viwanda sasa hivi mnajipanga na kilimo cha umwagiliaji; mimi niseme tu kwamba tumepata mahali pa kujifunza na tutawashauri watu wengine waje wajifunze Simiyu” alisema Jingu.

Akizungumza katika kikao hicho Mkuu wa mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka amesema Serikali mkoani humo imedhamiria kuzalisha  mazao yote ambayo malighafi yake inapatikana hapa nchini, ikiwa ni pamoja na kuyaongezea thamani mazao yote yatokanayo na kilimo na mifugo.

Mtaka amesema wao kama mkoa wameanzisha mfumo wa kuendesha miradi mbalimbali kwa Ubia kati ya Sekta Binafsi na Serikali (PPP) ambapo katika miradi ya Kiwanda cha Chaki na Kiwanda cha maziwa ambayo imeanza kutekelezwa mkoani humo,  Halmashauri ya Wilaya ya Maswa na Meatu wamekuwa wakiendesha miradi hiyo kwa ubia na vikundi vya vijana.

“Tunataka ‘kutransform’ mkoa wetu ambao utakuwa ‘model’ katika kutekeleza dhamira ya Mhe.Rais, dhamira yangu na wenzangu ni kufanya kitu cha tofauti na tutafanya kwa kuwa tumeamua” alisema Mtaka.

Aidha , Mtaka ametoa wito kwa viongozi wa Baraza la Uwezeshaji Wanachi Kiuchumi kuwasaidia wananchi katika kufikia azma ya kuwa na Tanzania yenye uchumi wa kati.

Kwa upande wake Katibu Tawala Mkoa wa Simiyu,Ndg.Jumanne Sagini ameomba Baraza la Uwezeshaji la Taifa kushirikiana na Viongozi wa mkoa wa Simiyu kuwasaidia wananchi katika masuala mbalimbali ya kiuchumi ili kuleta matokeo chanya.

Wakati huo huo Afisa Kilimo wa Wilaya ya Busega Ndg.Juma Chacha ameomba Baraza la Uwezeshaji kupitia programu yake ya mfuko wa pembejeo za kilimo,  lishirikiane na Mkoa wa Simiyu kuwahakikishia wananchi uhakika wa pembejeo za kilimo ili kuwasaidia kuongeza uzalishaji.


Naye Katibu Mtendaji wa Baraza hilo, Bengi Issa amesema Baraza limekuwa likifanya kazi na makundi mbalimbali ya watu katika jamii kwa kuwashirikisha kujenga na kuendeleza uchumi,kuwepo kwa mazingira rafiki katika ufanyaji biashara,kupatikana kwa mitaji ya gharama nafuu, kuhimiza uwepo wa bidhaa bora na masoko,kuimarisha vyama vya ushirika na vikundi vya kiuchumi, kuhimiza matumizi bora ya ardhi na kuwahamasisha kushiriki katika masuala ya ubinafishaji ikiwa ni pamoja na ununuzi wa hisa za makampuni kupitia masoko ya hisa.
Mwenyekiti wa Baraza la uwezeshaji Wananchi Kiuchumi ,Ndg.John Jingu (wa pili kulia) akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi wa Mkoa wa Simiyu mara baada ya kumaliza kikao kati ya uongozi wa baraza na viongozi wa Simiyu Jijini Dar es Salaam, (kushoto) Katibu Mtendaji, Bengi Issa, (wa pili kushoto) Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka,( kulia) Katibu Tawala mkoa,Ndg.Jumanne Sagini.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu,Mhe.Anthony Mtaka  akizungumza katika kikao kilichofanyika kati ya viongozi wa mkoa huo na Viongozi wa Baraza la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi kilichofanyika jijini Dar es salaam
Katibu Mtendaji wa Baraza la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi akizungumza    katika kikao kilichofanyika kati ya viongozi wa mkoa wa Simiyu na Viongozi wa Baraza hilo kilichofanyika jijini Dar es salaam
Baadhi ya Viongozi wa Mkoa wa Simiyu wakimsikiliza Mwenyekiti wa Baraza la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi katika kikao kilichofanyika kati ya viongozi wa mkoa huo na Viongozi wa Baraza la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi kilichofanyika jijini Dar es salaam.

KAMATI YA ULINZI NA USALAMA MKOA WA SIMIYU YATEMBELEA SUMA JKT DAR ES SALAAM

Na Stella Kalinga
Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Simiyu ikiongozwa na Mkuu wa Mkoa huo,Mhe.Anthony Mtaka  imetembelea SUMA JKT jijini  Dar es Salaam kuona pampu za umwagiliaji.

Lengo la ziara hiyo ni kujionea aina mbalimbali za pampu za umwagililiaji kwa kuwa Mkoa huo una mpango wa kuanza kutekeleza kilimo cha umwagiliaji wilayani Busega kama kipaumbele kwa mwaka 2017.


Pamoja na Wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa,viongozi wa wilaya ya Busega na Maswa pia walishiriki ziara hiyo.
Mkuu wa Mafunzo na Ufundi wa SUMA JKT (kulia) akitoa maelezo juu ya pampu ya umwagiliaji yenye uwezo kusukuma mapipa 13 ya maji kwa dakika kwa Mkuu wa Mkoa wa Simiyu,Mhe.Anthony Mtaka na wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wakati wa ziara yao jijini Dar es Salaam.
Mkuu wa Mafunzo na Ufundi wa SUMA JKT (kulia) akitoa maelezo juu ya pampu ya umwagiliaji yenye uwezo kusukuma mapipa 13 ya maji kwa dakika kwa Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka (kulia) na wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wakati wa ziara yao jijini Dar es Salaam.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu,Mhe.Anthony Mtaka akiwa na wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa, Viongozi na baadhi ya Watalaam wa Wilaya ya Busega na Maswa na Wataalam wa  Sekretarieti ya Mkoa wa Simiyu katika picha ya pamoja walipotembelea SUMA JKT jijini Dar es Salaam.

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!