Friday, January 20, 2017

KAMATI YA ULINZI NA USALAMA MKOA WA SIMIYU YATEMBELEA SUMA JKT DAR ES SALAAM

Na Stella Kalinga
Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Simiyu ikiongozwa na Mkuu wa Mkoa huo,Mhe.Anthony Mtaka  imetembelea SUMA JKT jijini  Dar es Salaam kuona pampu za umwagiliaji.

Lengo la ziara hiyo ni kujionea aina mbalimbali za pampu za umwagililiaji kwa kuwa Mkoa huo una mpango wa kuanza kutekeleza kilimo cha umwagiliaji wilayani Busega kama kipaumbele kwa mwaka 2017.


Pamoja na Wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa,viongozi wa wilaya ya Busega na Maswa pia walishiriki ziara hiyo.
Mkuu wa Mafunzo na Ufundi wa SUMA JKT (kulia) akitoa maelezo juu ya pampu ya umwagiliaji yenye uwezo kusukuma mapipa 13 ya maji kwa dakika kwa Mkuu wa Mkoa wa Simiyu,Mhe.Anthony Mtaka na wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wakati wa ziara yao jijini Dar es Salaam.
Mkuu wa Mafunzo na Ufundi wa SUMA JKT (kulia) akitoa maelezo juu ya pampu ya umwagiliaji yenye uwezo kusukuma mapipa 13 ya maji kwa dakika kwa Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka (kulia) na wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wakati wa ziara yao jijini Dar es Salaam.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu,Mhe.Anthony Mtaka akiwa na wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa, Viongozi na baadhi ya Watalaam wa Wilaya ya Busega na Maswa na Wataalam wa  Sekretarieti ya Mkoa wa Simiyu katika picha ya pamoja walipotembelea SUMA JKT jijini Dar es Salaam.

1 comment:

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!