Thursday, January 19, 2017

BENKI YA TIB KUSAIDIA UJENZI WA KIWANDA CHA BIDHAA ZA HOSPITALI SIMIYU

Na Stella Kalinga
Benki ya maendeleo ya TIB imesema iko tayari kutoa mkopo kwa ajili ya ujenzi wa kiwanda cha kutengeneza bidhaa za hospitali  zitokanazo na zao la pamba mkoani Simiyu.

Hayo yamesemwa na Mkurugenzi Mkuu wa TIB Bw.Charles Singili katika kikao maalum kilichofanyika jijini Dar es Salaam, kati ya uongozi wa Benki hiyo na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Simiyu ikiongozwa na Mkuu wa Mkoa huo Mhe.Anthony Mtaka.

Singili amesema hakuna haja kwa Bohari ya Dawa hapa nchini (MSD) kutumia fedha nyingi kuagiza bidhaa za hospitali kama bandeji, mashuka, pamba za kusafishia na kufungia vidonda kutoka nje ya nchi wakati Mkoa wa Simiyu unaongoza kwa uzalishaji wa pamba hapa nchini.

Aidha, Singili amesema benki hiyo iko tayari kutoa mkopo kwa Halmashauri ya Wilaya Maswa kwa ajili ya kujenga kiwanda kikubwa cha chaki ili kukiwezesha kiwanda kuongeza uzalishaji utakaokidhi mahitaji.

“Benki iko tayari kusaidia wasilisheni andiko la mradi tulipitie na kuona namna ya kuwawezesha kupata mkopo wa kujenga kiwanda; mtakapojenga kiwanda kikubwa mtaisaidia serikali kupunguza gharama za usafirishaji wa chaki kutoka nje” alisema Singili.

Sambamba na hilo Singili amesema Benki ya TIB kwa kushirikiana na wadau wengine kama NHIF, NEMC, TBS,TIRDO,TFDA pamoja na kusaidia ujenzi wa kwanda cha kutengeneza bidhaa za Hospitali zitokanazo na Pamba, pia watasaidia ujenzi wa kiwanda cha kutengeneza maji ya kuwawekea wagonjwa( drip) mkoani Simiyu.

Kwa upande wao Mkuu wa Mkoa wa Simiyu,Mhe.Anthony Mtaka na Katibu Tawala Mkoa wa Mkoa huo wameushukuru uongozi wa Benki ya TIB kwa kuunga mkono juhudi za Viongozi wa Mkoa huo hususani katika utekelezaji wa Sera ya Tanzania ya Viwanda.
 
Mkurugenzi Mkuu wa TIB Ndg.Charles Singili akizungumza na Viongozi wa Mkoa wa Simiyu katika kikao kilichofanyika ukumbi wa Mkutano wa Benki hiyo jijini makao makuu Dar es Salaam.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Anthony Mtaka (wa pili kushoto) akizungumza na viongozi wa Mkoa huo na viongozi wa Benki ya TIB katika kikao maalum kilichofanyika ukumbi wa Mkutano wa Benki hiyo Makao makuu jijini Dar es Salaam.
Katibu Tawala Mkoa wa Simiyu,Ndg.Jumanne Sagini (kushoto) akizungumza na viongozi wa Mkoa huo na viongozi wa Benki ya TIB katika kikao maalum kilichofanyika ukumbi wa Mkutano wa Benki hiyo Makao makuu jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya viongozi wa mkoa wa Simiyu na viongozi wa Benki ya TIB wakiwa katika kikao maalum kilichofanyika ukumbi wa Mkutano wa Benki hiyo Makao makuu jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya Viongozi wa Mkoa wa Simiyu Simiyu wakimsikiliza Mkurugenzi Mkuu wa TIB Ndg.Charles Singili(hayupo pichani) katika kikao kilichofanyika ukumbi wa Mkutano wa Benki hiyo jijini makao makuu Dar es Salaam kati ya viongozi wa Benki  hiyo na Viongozi wa Mkoa wa Simiyu.








0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!