Monday, January 30, 2017

WAKULIMA NCHINI WASHAURIWA KULIMA KILIMO HAI KUONGEZA THAMANI YA MAZAO

Na Stella Kalinga

Wakulima  nchini wametakiwa kufanya maamuzi magumu yatakayoleta mapinduzi ya kiuchumi  kwa kulima kilimo HAI (kilimo kisichotumia kemikali za viwandani)  kinachozingatia kanuni bora kwa kuwa kimeonyesha tija katika kuongeza thamani ya mazao.

Wito huo umetolewa na Waziri wa Biashara,Viwanda na Masoko wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Mhe. Balozi Amina Salum Ali alipotembelea Kampuni ya Biore wilayani Meatu katika ziara yake ya kutembelea viwanda vidogo na vya kati  mkoani Simiyu.

Mhe. Balozi Amina Salum Ali amesema upo umuhimu sasa kwa viongozi wa serikali kuhakikisha wanafanya maamuzi magumu yatakayoboresha uchumi wa watanzania ikiwa ni pamoja na kutoa maelekezo sahihi ya kuzingatia kilimo  HAI (oganiki) kinachofuata kanuni bora za kilimo pasipo  kuchanganya na masuala ya kisiasa.

“Biashara ya sasa hivi inaelekea zaidi katika masuala mazima ya oganiki na ukiangalia kuna tofauti kubwa sana ya bei katika vitu vya oganiki na ambavyo siyo oganiki, kwa mfano Karafuu ya tunayoiuza ambayo siyo oganiki inauzwa shilingi 8100 na ambayo ni oganiki inauzwa 9900 kwa hiyo chochote ambacho ni oganiki unapata bei nzuri; watu wengi wanakimbia kulima kilimo hai kwa sababu ya hutumia nguvu zaidi katika usafi,  ulimaji ,ukaushaji wake ambao unazingatia viwango, lakini manufaa yake ni makubwa sana” amesema Balozi Amina Salum Ali.

Ameongeza Zanzibar imeingia katika hatua nyingine ambapo imedhamiria kuanzisha viwanda vitakavyotumia malighafi ambayo ni oganiki(hai) ambapo wanataka kulima maua, viungo na mazao mengine ambayo yatauzwa ndani na nje ya nchi, hivyo wako tayari kuwekeza mkoani Simiyu hususani katika ardhi ya kuzalisha mazao hayo.

Aidha Waziri huyo wa Zanzibar akizungumzia umuhimu wa biashara ya ndani ya nchi amesema takwimu zinaonyesha kuwa mataifa mengi ya Afrika yanafanya biashara ya ndani chini ya asilimia 27 na akasisitiza uboreshaji wa mifumo ya uendeshaji wa biashara na  mnyororo wa thamani ili Tanzania iweze kufikia uchumi wa kati.

Kwa upande wake mmoja wa wawekezaji anayetekeleza kilimo  HAI (kisichotumia madawa na kemikali za viwandani) kwa zao la pamba  Mkurugenzi wa Kampuni ya Biore Tanzania Niranjan Pattni  amekiri kuwepo kwa tija kubwa zaidi endapo wakulima wataingia katika mfumo wa kilimo HAI , ambapo Kampuni yake imekuwa ikitoa elimu ya kilimo na utunzaji wa mazao, mikopo ya gharama nafuu, pembejeo bora za kilimo  na kuwahakikishia soko la uhakika na nyongeza ya bei.

Naye Mkuu wa mkoa wa Simiyu,Mhe.Anthony Mtaka amesema ili kilimo kiweze kufikia kuwa eneo la kutegemewa kwenye malighafi katika Tanzania ya Viwanda,  ni lazima wananchi waende kwenye kilimo cha kisasa ambacho kinahitaji gharama ya mbegu bora, mbolea na pembejeo nyingine bora za kilimo.

“Sisi kama mkoa tunajipanga kuwa mkoa utakaozalisha bidhaa za afya zitokanazo na pamba na bidhaa hizi zinahitaji pamba iliyoandaliwa vizuri na mfano ni pamba ya Biore, kama ukitaka kupata eneo ambalo unaweza kujifunza pamba tutakayoihitaji kuzalisha kama malighafi ya bidhaa za kiwanda cha bidhaa za afya ni pamba ya Biore ambayo ni oganiki na ina gharama kubwa hata kwenye soko la Dunia” amesema Mtaka.

Mheshimiwa Balozi Amina Salum Ally amemaliza ziara yake wilayani Meatu na anatarajia kukamilisha ziara yake Mkoani Simiyu na kufanya majumuisho wilayani Busega, ambapo akiwa Wilayani Meatu ametembelea na kuona kiwanda cha kusindika maziwa, ng’ombe wa kisasa wa maziwa, mashamba ya malisho ya mifugo na kukutana na mwekezaji wa kampuni ya Biore Tanzania anayejishughulisha na kilimo cha pamba ya oganiki(pamba hai).


Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka (kulia) akimkabidhi Waziri wa Biashara,Viwanda na Masoko wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Mhe. Balozi Amina Salum Ali zawadi ya maziwa ambayo alipewa na Halmashauri ya Wilaya ya Meatu mara baada ya kutembelea kiwanda cha kusindika maziwa wakati wa ziara yake wilayani humo.
Waziri wa Biashara,Viwanda na Masoko wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Mhe. Balozi Amina Salum Ali(kulia) akipewa maelezo na mmoja wa vijana wa Meatu wanajishughulisha na usindikaji wa maziwa mara baada ya kutembelea kiwanda cha kusindika maziwa wakati wa ziara yake wilayani humo.
Waziri wa Biashara,Viwanda na Masoko wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Mhe. Balozi Amina Salum Ali(kushoto) akizungumza jambo na Mkuu wa Wilaya ya Meatu, Mhe.Joseph Chilongani wakati alipotembelea na kuona ng’ombe wa maziwa waliofugwa kwa ajili ya kuongeza hali ya upatikanaji wa maziwa kwa kiwanda cha maziwa wakati wa ziara yake wilayani humo.
Waziri wa Biashara,Viwanda na Masoko wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Mhe. Balozi Amina Salum Ali(kushoto) akizungumza na viongozi wa wilaya ya Meatu wakati akiwa katika ziara ya siku moja wilayani humo.
Mwenyekiti wa Halmsahauri ya Wilaya ya Meatu, Mhe.Pius Machungwa akimkabidhi Mkuu wa Mkoa wa Simiyu zawadi ya maziwa wakati wa ziara ya Waziri wa Biashara,Viwanda na Masoko wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Mhe. Balozi Amina Salum Ali wilayani humo
: Waziri wa Biashara,Viwanda na Masoko wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Mhe. Balozi Amina Salum Ali akiwa na viongozi wengine mara baada ya kutembelea kiwanda cha kusindika maziwa wilayani Meatu.
Mkuu wa Wilaya ya Meatu, Mhe.Joseph Chilongani  akitoa maelezo ya utangulizi kwa Waziri wa Biashara,Viwanda na Masoko wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Mhe. Balozi Amina Salum Ali mara baada ya kuwasili katika Ofisi ya Kampuni ya Biore Tanzania wakati wa ziara yake wilayani humo.
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Biore Tanzania inayojishughulisha na kilimo hai Ndg. Niranjan Pattni (kushoto) akisoma taarifa ya kampuni yake kwa Waziri wa Biashara,Viwanda na Masoko wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Mhe. Balozi Amina Salum Ali alipomtembelea wakati wa ziara yake wilayani humo.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka (wa pili kulia)  akizungumza na viongozi wa Mkoa, wilaya ya Meatu na Watumishi wa Biore Tanzania wakati wa ziara ya Waziri wa Biashara,Viwanda na Masoko wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Mhe. Balozi Amina Salum Ali wilayni Meatu.
Waziri wa Biashara,Viwanda na Masoko wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Mhe. Balozi Amina Salum Ali akipanda mti wa kumbukumbu katika eneo la kampuni ya Biore Tanzania mara baada ya kutembelea eneo hilo wakati wa ziara yake wilayani Meatu.
:-Mkuu wa Mkoa wa Simiyu,Mhe.Anthony Mtaka akipanda mti wa kumbukumbu katika eneo la kampuni ya Biore Tanzania wilayani Meatu wakati wa ziara ya Waziri wa Biashara,Viwanda na Masoko wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Mhe. Balozi Amina Salum Ali wilayani humo.
Waziri wa Biashara,Viwanda na Masoko wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Mhe. Balozi Amina Salum Ali(kushoto)akizunumza jambo na Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Meatu,Mhe.Juma Mwibuli akiwa wilayani humo wakati wa ziara yake Mkoani Simiyu.

1 comment:


  1. Hello.
    Mimi ni Mr Rahel binafsi wakopeshaji mkopo ambao hutoa maisha wakati nafasi ya mkopo kwa watu binafsi, makampuni ya biashara, bima, nk Je, katika shida yoyote ya kifedha au katika haja ya mkopo wa kuwekeza au unahitaji mkopo kulipa bili yako kutafuta hakuna zaidi kama sisi ni hapa kufanya matatizo yako yote ya kifedha kitu cha zamani. Sisi kutoa kila aina ya mkopo katika dhehebu lolote fedha kwa kiwango cha 2% bila fee.I upfront wanataka kutumia kati hii kubwa ya kukufahamisha kwamba tuko tayari kukusaidia kwa aina yoyote ya mkopo kutatua kwamba tatizo.Kama yako ya kifedha ndiyo basi kupata nyuma sasa kupitia barua pepe (rahelcohranloan@gmail.com) kwa maelezo zaidi, wewe ni sana makala.

    ReplyDelete

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!