Saturday, January 14, 2017

RC SIMIYU AWAONGOZA WATUMISHI WA UMMA KUFANYA MAZOEZI KUTEKELEZA AGIZO LA MHE.MAKAMU WA RAIS

Na Stella Kalinga
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu,Mhe.Anthony Mtaka amewaongoza Watumishi wa Umma mkoani humo kutekeleza agizo la Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Mhe.Samia Suluhu Hassan,  la kufanya mazoezi kwa lengo la kukabiliana na ongezeko la magonjwa yasiyoambukiza kama kisukari,shinikizo la damu, saratani na magonjwa ya moyo.

Mazoezi hayo  na michezo mbalimbali iliyowahusisha watumishi kutoka Serikali kuu, Mamlaka za Serikali za Mitaa na baadhi ya Taasisi nyingine za Serikali yamefanyika katika Uwanja wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi kuanzia saa kumi na mbili  hadi saa 3:45 asubuhi.

Akifungua mazoezi hayo Mkuu wa Mkoa wa Simiyu amewataka watumishi wa umma na wananchi kwa ujumla kutekeleza agizo la Mhe.Makamu wa Rais na  kujenga tabia ya kufanya mazoezi ili kuimarisha afya zao.

Mtaka amesema Serikali kwa kushirikiana na wadau mbalimbali ina mkakati wa kukarabati uwanja wa Halmshauri ya Mji wa Bariadi na kuhakikisha kuwa viwanja vya michezo yote ikiwepo mpira wa wavu, mpira wa kikapu, mpira wa pete, mpira wa miguu vinatengenezwa vizuri ili watu wapate mahali pa kufanya mazoezi na kucheza michezo hiyo.

Mtaka ameongeza kuwa uwanja wa Shule ya Msingi Somanda umeshatengenezwa na kuwekewa mahitaji yote muhimu kwa ajili ya mchezo wa riadha, hivyo watumishi na wananchi wanaopenda mchezo wa riadha watatumia uwanja huo.

Aidha, Mkuu huyo wa mkoa ammetoa wito kwa  Maafisa michezo na Maafisa utamaduni Mkoani humo kuwa na mipango kazi itakayowawezesha kuhamasisha na kusimamia uendeshaji wa shughuli za michezo ili uwe endelevu katika Mkoa.

“ Maafisa michezo na Maafisa utamaduni msiishie kuaandaa michezo ya UMISETA na UMITASHUMTA tu, andaeni mipango kazi itakayoendeleza michezo; Afisa Michezo na Utamaduni Mji wa Bariadi utumie uwanja huu kuandaa mabonanza ya michezo mbalimbali na burudani kutoka vikundi vya ngoma vinavyotambulisha utamaduni wa huku, nina uhakika wananchi watapenda kuona mambo hayo”  amesema Mtaka.

Naye Katibu Tawala Mkoa ametoa wito kwa watumishi wa Taasisi za Serikali ambazo hazikushiriki kufanya mazoezi ya wiki ya pili ya mwezi huu kuungana pamoja na watumishi wengine wiki ya pili ya mwezi Februari.

 Michezo iliyochezwa leo baada ya kumaliza mazoezi ni pamoja na mpira wa miguu(wanaume), kuvuta kamba(wanaume na wanawake), kufukuza kuku(wanaume na wanawake na mbio za mita 100 kwa wanaume na wanawake.

Katika mpira wa miguu timu ya watumishi wa Serikali kuu na Timu ya Watumishi wa Mamlaka za Serikali zimetoka sare ya bila kufungana, kuvuta kamba wanaume Timu ya Sekretarieti ya mkoa iliibuka kidedea dhidi ya Timu ya Halmashauri ya Wilaya na Mji Bariadi, wakati kwa wanawake Timu ya Halmashauri iliiburuza timu ya Sektarieti ya Mkoa.

Katika mchezo wa kufukuza kuku wanawake na wanaume,  watumishi wa Sekretarieti ya Mkoa waliwashinda watumishi wa Halmashauri ya mji Bariadi na Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka (wa nne kushoto) akishiriki mazoezi na watumishi wa Umma wa Mkoa huo yaliyofanyika katika Uwanja wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi kwa lengo la kutekelezwa kwa agizo la Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.Samia Suluhu Hassan, (kushoto) Mkuu wa Wilaya ya Bariadi,Mhe.Festo Kiswaga.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu,Mhe.Anthony Mtaka (wa tatu kushoto) pamoja na baadhi ya viongozi na watumishi Umma wa Mkoa huo wakiingia katika uwanja wa Halmashauri ya Mji kwa ajili ya kufanya mazoezi kutekeleza agizo la Mhe.Makamu wa Rais, baada ya kutembea umbali wa zaidi ya  kilomita 2 kutoka Somanda.
Katibu Tawala Mkoa wa Simiyu, Ndg.Jmanne Sagini(wa pili kushoto) akishiriki mazoezi ya viungo na watumishi wa Umma wa Mkoa huo yaliyofanyika katika Uwanja wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi kwa lengo la kutekelezwa kwa agizo la Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.Samia Suluhu Hassan.

Baadhi ya Watumishi wa Umma wakifanya mazoezi katika Uwanja wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi kwa lengo la kutekelezwa kwa agizo la Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.Samia Suluhu Hassan.



Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka (wa pili kulia) akizungumza na watumishi wa Umma wa Mkoa huo katika ufunguzi wa hamasa ya kufanya mazoezi uliyofanyika katika Uwanja wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi kwa lengo la kutekelezwa kwa agizo la Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.Samia Suluhu Hassan.
Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe.Festo Kiswaga (kulia) akizungumza na watumishi wa Umma wa Mkoa huo katika ufunguzi wa hamasa ya kufanya mazoezi uliyofanyika katika Uwanja wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi kwa lengo la kutekelezwa kwa agizo la Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.Samia Suluhu Hassan.
Timu ya wanaume ya Sekretarieti ya mkoa wa Simiyu wakivuta kamba dhidi ya wapinzani wao Timu ya Halmashauri ya Mji Bariadi na Halmashauri ya Wilaya Bariadi(hawapo pichani)
Timu ya wanawake ya Sekretarieti ya mkoa wa Simiyu wakivuta kamba dhidi ya wapinzani wao Timu ya Halmashauri ya Mji Bariadi na Halmashauri ya Wilaya Bariadi(hawapo pichani)
Nahodha wa Timu ya Mpira wa Miguu Sekretarieti ya Mkoa Simiyu, Bw.Mustapha Kimomwe(kulia) akimtambulisha Katibu Tawala wa Mkoa huo,Ndg Jumanne Sagini  (wa pili kulia) wachezaji wa timu yake kabla ya mpira kuanza,  katika uwanja  wa Halmashauri ya Mji Bariadi.
Nahodha wa Timu ya Mpira wa Miguu ya Hlmashauri ya Mji na Wilaya ya Bariadiakimtambulisha Katibu Tawala wa Mkoa huo,Ndg Jumanne Sagini  (kushoto) wachezaji wa timu yake kabla ya mpira kuanza,  katika uwanja  wa Halmashauri ya Mji Bariadi.
Baadhi ya Watumishi wa Umma wakikimbia mbio za Mita 100 katika ufunguzi wa hamasa ya kufanya mazoezi uliyofanyika katika Uwanja wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi kwa lengo la kutekelezwa kwa agizo la Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.Samia Suluhu Hassan.

0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!