Saturday, September 29, 2018

SERIKALI MKOANI SIMIYU YAJIPANGA KUDHIBITI ONGEZEKO LA VIFO VYA AKINA MAMA WAJAWAZITO


Mkoa wa Simiyu utahakikisha vifo vya akina mama wajawazito na watoto wachanga vinapungua kwa kuwa Serikali kwa kushirikiana na wadau mbalimbali imewekeza na kutumia gharama kubwa katika kuandaa wataalam(wakunga) wenye jukumu la kuhakikisha wanatoa huduma zitakazotoa majibu sahihi ya utatuzi wa changamoto hiyo.

Hayo yamesemwa na Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe.Festo Kiswaga wakati akifunga mafunzo ya wakunga yanayohusu utoaji wa huduma za dharura kwa wakina mama na watoto wachanga chini ya mradi wa Mkunga Okoa Maisha, kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka yaliyohusisha wakunga kutoka katika Halmashauri zote sita mkoani humo.

Kiswaga amesema pamoja na kuwepo dalili za kupungua kwa vifo vya akina mama wajawazito na  watoto wachanga mkoani huo bado ipo haja ya kujitathmini ili kubaini ukubwa wa tatizo kama njia ya kulipatia ufumbuzi wa kudumu.

“ Ni kweli ukilinganisha takwimu za mwaka jana na mwaka huu zinaonyesha idadi ya vifo vinavyotokana na matatizo mbalimbali ya uzazi vimepungua, lakini naomba niwape angalizo,  tusizichukulie takwimu hizi kama kigezo cha ubora wa huduma zinazotolewa katika vituo vyetu, bali iwe chachu ya kufanya kazi kwa bidii  ili fikapo mwezi Desemba mwaka huu tuwe katika nafasi ya juu zaidi”.

Aidha Kiswaga amewaasa wahitimu wa mafunzo hayo kuhakikisha wanaitumia kikamilifu elimu waliyoipata ili iwawezeshe kukabiliana na dharula wakati wa kuwahudumia wakina mama wajawazito na watoto wachanga na kuongeza kuwa serikali haitamvumilia mkunga yeyete atakayetumia kisingizio cha aina yoyote kwa kusababisha kifo cha mama au mtoto.

Halikadhalika Kiswaga ameishukuru serikali ya Canada kupitia chama cha wakunga cha nchi hiyo CAM na kusema kuwa imefanya uamuzi sahihi wa kuisaidia Tanzania katika eneo hili nyeti la kuwajengea uwezo wataalamu hao watakaotumika kuboresha huduma za  afya ya mama na mtoto na kuahidi kuwa serikali iko tayari kupokea ushauri utakaosaidia kukabiliana na changamoto hiyo.

Kwa upande wake rais wa chama cha wakunga Tanzania TAMA  Feddy Mwanga amesema tafiti za hivi karibuni zinaonyesha kuwa mkunga mwenye mafunzo yuko katika nafasi nzuri zaidi ya kukabiliana na changamoto zinazowakabili akina mama wajawazito na watoto wachanga kwa 87%.

“ Hivyo kwa sisi wakunga tunaamini hatua hiyo ni nzuri na kwamba kinachofuata sasa ni kuwahimiza wakina mama wahudhurie kliniki mapema na kwa wakati na hapa ndipo tunaweza kupima mafanikio ya mpango huu kupitia kwa wahitimu hawa tunaowakabidhi vyeti hii leo” alisema Bi Mwanga.

Akizungumza kwa niaba ya wahitimu wa mafunzo hayo yaliyobebwa na kauli mbiu ya Mkunga Okoa Maisha -Jonas Julius ameiomba Serikali kuboresha mazingira yao ya kutolea huduma ikiwemo kuwapatia nyumba za kuishi jirani na vituo vya kazi sambamba na kuwaendeleza kitaaluma ili waweze kukabiliana na changamoto zinazojitokeza.

Mkoa wa Simiyu una jumla ya wakunga 500 ambapo  kupitia mpango huo jumla ya wakunga 220 wamenufaika na mafunzo hayo yanayofadhiliwa na CUSO International, Chama cha wakunga Tanzania (TAMA) pamoja na Chama cha wakunga Canada (CAM) .
MWISHO
Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga akifunga mafunzo ya wakunga yanayohusu utoaji wa huduma za dharura kwa akina mama wajawazito na watoto wachanga chini ya Mradi wa Mkunga Okoa Maisha, kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka, Septemba 28, 2018.
 Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga akifunga mafunzo ya wakunga yanayohusu utoaji wa huduma za dharura kwa akina mama wajawazito  na watoto wachanga chini ya Mradi wa Mkunga Okoa Maisha, kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka, Septemba 28, 2018. 


Rais wa chama cha wakunga Tanzania TAMA  Feddy Mwanga akitoa taarifa ya mafunzo ya wakunga yanayohusu utoaji wa huduma za dharura kwa  akina mama wajawazito na watoto wachanga chini ya Mradiwa Mkunga Okoa Maisha, wakati wa hafla ya kufunga mafunzo hayo mkoani Simiyu, Septemba 28, 2018.
Mkunga Jonas Julius akisoma risala mbele ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga aliyefunga mafunzo ya wakunga yanayohusu utoaji wa huduma za dharura kwa akina mama wajawazito na watoto wachanga chini ya Mradi wa Mkunga Okoa Maisha, kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka, Septemba 28, 2018.
 Mratibu wa Mradi wa Mkunga Okoa Maisha Martha Rimoy akitoa taarifa ya mafunzo ya utoaji wa huduma za dharura kwa akina mama wajawazito na watoto wachanga, katika hafla ya kufunga mafunzo hayo iliyofanywa na Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka, Septemba 28, 2018.


Mwakilishi wa Chama cha Wakunga cha nchini Canada (CAM) Bi. Sylivia akitoa uzoefu wake wa namna wakunga wanavyofanya kazi nchin humo, wakati wa hafla ya kufunga mafunzo ya utoaji wa huduma za dharura kwa akina mama wajawazito na watoto wachanga, iliyofungwa na Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka, Septemba 28, 2018.
Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Dkt. Mugune Maeka akizungumza jambo katika hafla ya kufunga mafunzo ya utoaji wa huduma za dharura kwa akina mama wajawazito na watoto wachanga, iliyofungwa na Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka, Septemba 28, 2018.
Mkuu wa Wilaya ya Bariadi Mhe. Festo Kiswa(katikati walioketi) akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa Chama cha wakunga nchini (TAMA), Mwakilishi wa Chama cha Wakunga cha nchini Canada (CAM) Bi. Sylivia, baadhi ya viongozi wa mkoa wa Simiyu na baadhi ya wakunga wa mkoa wa Simiyu walioshiriki mafunzo ya yanayohusu utoaji wa huduma za dharura kwa akina mama wajawazito na watoto wachanga, baada ya kufunga mafunzo hayo Septemba 28, 2018.
Mwakilishi wa Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bi. Grace Mgombera akizungumza jambo katika hafla ya kufunga mafunzo ya yanayohusu utoaji wa huduma za dharura kwa akina mama wajawazito  na watoto wachanga, iliyofungwa na Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka, Septemba 28, 2018.
Baadhi ya wakunga wa mkoa wa Simiyu walioshiriki mafunzo ya utoaji wa huduma za dharura kwa akina mama wajawazito na watoto wachanga, wakimsikiliza Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga aliyefunga mafunzo hayo, kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka, Septemba 28, 2018.
 Mkunga wa Zahanati ya Badugu, Bw. Ramdhani akipokea cheti cha kuhitimu mafunzo ya utoaji wa huduma za dharura kwa akina mama wajawazito na watoto wachanga,  kutoka kwa Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga aliyefunga mafunzo hayo, kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka, Septemba 28, 2018. 


Mkuu wa Wilaya ya Bariadi Mhe. Festo Kiswa(wa pili kulia) pamoja na viongozi wa Chama cha wakunga nchini (TAMA), , baadhi ya viongozi wa mkoa wa Simiyu na baadhi ya wakunga wa mkoa wa Simiyu wakiimba wimbo pamoja na wakunga(hawapo pichani) walioshiriki mafunzo ya ya utoaji wa huduma za dharura kwa akina mama wajawazito na watoto wachanga, kabla ya kufunga mafunzo hayo Septemba 28, 2018.



Mkuu wa Wilaya ya Bariadi Mhe. Festo Kiswa(wa pili kulia) pamoja na viongozi wa Chama cha wakunga nchini (TAMA), baadhi ya viongozi wa mkoa wa Simiyu na baadhi ya wakunga wa mkoa wa Simiyu wakiimba wimbo pamoja na wakunga(hawapo pichani) walioshiriki mafunzo ya ya utoaji wa huduma za dharura kwa akina mama wajawazito na watoto wachanga, kabla ya kufunga mafunzo hayo Septemba 28, 2018.
Baadhi ya wakunga wa mkoa wa Simiyu walioshiriki mafunzo ya utoaji wa huduma za dharura kwa akina mama wajawazito na watoto wachanga, wakimsikiliza Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga aliyefunga mafunzo hayo, kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka, Septemba 28, 2018. 
Baadhi ya wakunga wa mkoa wa Simiyu walioshiriki mafunzo ya utoaji wa huduma za dharura kwa akina mama wajawazito na watoto wachanga, wakimsikiliza Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga aliyefunga mafunzo hayo, kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka, Septemba 28, 2018.


SIMIYU YADHAMIRIA KUWAKOMBOA WAFUGAJI KWA KUWASAIDIA WAFUGE KISASA

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.  Anthony Mtaka amewataka wataalamu wa mifugo na kilimo kuachana na utamaduni wa kufanya kazi kwa mazoea huku akiwataka kuongeza ubunifu sambamba na kupanua wigo wa kutoa elimu kwa wafugaji ili kuongeza ufanisi katika sekta hiyo ambayo ni ya pili katika kuchangia pato la mkoa.


Mtaka ametoa kauli hiyo wakati akifungua warsha ya kujadili maendeleo ya sekta ya mifugo na mnyororo wake wa thamani iliyofanyika mjini Bariadi na kusema kuwa baada ya warsha hiyo anategemea kuwaona maafisa ugani na wataalamu wa mifugo wakiwaelimisha zaidi wafugaji mbinu bora za ufugaji wa kisasa ambazo zitabadili sura ya mkoa huo.

“ Hivi kwa nini tunakuwa watu wa kusifia nchi nyingine badala ya kujipanga ili na sisi hatimaye tuweze kuwa kama wao, utasikia mtu anasema ukitaka kujifunza mbinu bora za ufugaji nenda Ethiopia au Botswana, hivi sisi tunashindwa nini kuwa kama wao”, alihoji Mtaka.

Akisisitiza umuhimu wa kuwekeza katika elimu kwa wafugaji Mtaka  amewasisitiza wataalamu wa mifugo katika halmashauri  zote za wilaya mkoani Simiyu kuhakikisha wanatumia ubunifu wao kadiri iwezekanavyo kuwajengea uwezo wafugaji ili waweze kunufaika na sekta hiyo halikadhalika waweze kuchangia katika ukuaji wa sekta ya viwanda vitakavyohitaji malighafi zinazotokana na mifugo.

Kwa upande wake mwakilishi wa balozi wa Ireland ambaye ni mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Ubalozi huo Dkt. Niall Moris amesema nchi yake itaendelea kushirikiana na Tanzania katika suala zima la kuwajengea uwezo wataalamu wa mifugo mkoani Simiyu ili na wao wawe chachu ya kuisambaza elimu na ujuzi huo kwa wafugaji.

Dkt. Niall ameongeza kuwa serikali ya Ireland imevutiwa kushirikiana na mkoa wa Simiyu kutokana na mipango yake mizuri na sera zenye mwelekeo unaotia matumaini ya kumkomboa mfugaji na kuongeza kuwa hiyo ndio njia pekee itakayosaidia kuleta mapinduzi katika sekta ya mifugo.

Naye Mkurugenzi Mkuu wa tume ya Sayansi na teknolojia Dkt. George Mulamula amesema mabadiliko katika sekta ya mifugo yatasaidia kuleta msukumo katika sekta ya viwanda mkoani Simiyu na kusisitiza kuwa ongezeko la malighafi zitokanazo na mifugo zitaongeza msukumo kwa serikali na wadau wa maendeleo kufungua viwanda vingi zaidi.
 MWISHO
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka (kushoto) akizungumza na Watalaam kutoka kwa Ireland wakati walipofika ofisini kwake kabla ya kufanya warsha ya kujadili maendeleo ya sekta ya mifugo na mnyororo wake wa thamani iliyofanyika mjini Bariadi.

Friday, September 28, 2018

RC MTAKA APONGEZA GEITA KWA UBUNIFU KUFANYA MAONESHO YA KIPEKEE YA DHAHABU NCHINI


Mkuu wa Mkoa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka amewapongeza viongozi wa Mkoa wa Geita wakiongozwa na Mkuu wa Mkoa huo, Mhandisi. Robert  Gabriel kwa ubunifu waliofanya wa kufanya Maonesho ya Kipekee ya Teknolojia Bora ya  dhahabu hapa nchini.

Mtaka ameyasema hayo mara baada ya kuzungumza na viongozi wa Mkoa wa Geita na kutembelea mabanda ya maonesho katika Maonesho ya Dhahabu yanayofanyika  Uwanja wa CCM Kalangalala Mjini Geita kuanzia Septemba 24, 2018.

Amesema Watanzania wengi wamekuwa wakienda kushiriki maonesho ya dhahabu katika mataifa mbalimbali barani Afrika na nje ya bara la Afrika lakini kupitia maonesho haya Watanzania wameanza kujionea teknolojia mbalimbali za uchimbaji wa madini hapa nchini.

“ Ninawapongeza sana viongozi wa Geita kwa kuandaa maonesho haya ya kipekee hapa nchini, tumekuwa na shughuli nyingi sana za uchimbaji madini lakini sisi sote ni mashahidi shughuli hizi tumekuwa tukiziona wakati wa Mei Mosi kupitia kile chama kinachohusisha watu wanaofanya kazi za madini, hatujapata jambo linaloonesha shughuli za migodini na mazao yanayotokana na migodi kama dhahabu” alisema Mtaka.

Ameongeza kuwa ubunifu huo uliofanywa na Viongozi wa Mkoa wa Geita hasa wa kuyapa maonesho haya jina la Kiswahili ya “Maonesho ya Dhahabu” ambalo linasadifu shughuli zinazofanyika katika mkoa huo ambao ni mzalishaji mkubwa wa dhahabu, utachangia kuongeza watalii na wageni wengi watakaokuja hapa nchini kupitia maonesho hayo.

Mkuu wa Mkoa wa Geita, Mhandisi. Robert Gabriel ametoa wito kwa wananchi kujitokeza kushuhudia maonesho hayo ili kujionea teknolojia za uchimbaji madini, kupata huduma za kifedha katika taasisi za kifedha, kupata huduma na elimu juu ya utatuzi wa changamoto za kibiashara hususani upatikanaji wa mitaji na changamoto za uchimbaji katika kliniki ya biashara.

Aidha, Mhandisi. Gabriel amesema maendeleo katika mkoa wa Geita hayaepukiki kutokana na sekta ya madini kuwa na  mchango mkubwa katika uchumi ambapo amebainisha kuwa kupitia uchimbaji dhahabu mkoa unapata ushuru, fedha za msaada kwa jamii (Corporate  Social Responsibility) kutoka kwenye makampuni yanajihusisha na uchimbaji madini zilizosaidia utekelezaji wa miradi ya maendeleo.

Naye Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji wa Geita, Mhe. Leonald Bugomola amesema maonesho ya dhahabu mwaka 2019 yataanza mapema na Halmashauri yake kama mwenyeji wa maonyesho hayo imejipanga kutafuta eneo kubwa zaidi ekari 100 ,  kwa kuwa mpango wa mkoa ni kuwa na maonesho yenye hadhi ya Kimataifa yatakoshirikisha washiriki wengi ikilinganishwa na mwaka huu.

Nao baadhi ya wachimbaji wadogo wameshukuru uanzishwaji wa maonesho hayo ambayo yatasaidia kupata utaalamu juu teknolojia mbalimbali zinazotumika kuchimba madini na kupata elimu ya namna ya kukabiliana na changamoto mbalimbali katika sekta ya madini kutokana na wadau mbalimbali kukutanishwa pamoja na kujadiliana kuhusu maendeleo ya sekta ya madini.

Maonesho ya Teknolojia Bora  ya Dhahabu mkoani Geita yameanza Septemba 24, 2018 na yanatarajiwa kuhitimishwa Septemba 30, 2018 yakiwa na Kauli Mbiu: TEKNOLIJIA BORA YA UZALISHAJI WA DHAHABU KWA MAENDELEO YA KIJAMII NA UCHUMI WA VIWANDA”
MWISHO.


Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka (katikati) akiteta jambo na Mkuu wa Mkoa wa Geita, Mhandisi. Robert  Gabriel(kulia) wakati alipofika Mjini Geita kujionea Maonesho ya Dhahabu yanayofanyika katika Uwanja wa CCM Kalangalala Mjini Geita, kuanzia Septemba 24 hadi Septemba 30, 2018.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka(kushoto) na Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhandisi. Robert  Gabriel(kulia) wakifuatilia masuala mbalimbali yalikuwa yakiwasilishwa na wadau wa sekta ya madini katika kikao kilichofanyika Uwanja wa CCM Kalangalala Mjini Geita, kwenye Maonesho ya  Dhahabu kuanzia Septemba 24 hadi Septemba 30, 2018. 
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka akisaini kitabu cha wageni katika banda la Kampuni ya NGM Gold Mine inayomilikiwa na Bw. Gungu Silanga ambaye ni mkazi wa Simiyu wakati alipofika Mkoani  Geita Mjini Geita kujionea Maonesho ya Dhahabu yanayofanyika katika Uwanja wa CCM Kalangalala Mjini Geita, kuanzia Septemba 24 hadi Septemba 30, 2018. 
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka (kushoto) akisalimiana na Mbunge wa Geita Mjini Mhe. Constantine Kanyasu mara baada ya kuwasili Mkoani Geita, kujionea Maonesho ya Dhahabu yanayofanyika katika Uwanja wa CCM Kalangalala Mjini Geita, kuanzia Septemba 24 hadi Septemba 30, 2018.




 Baadhi ya Viongozi na wadau wa Madini wakifuatilia kikao kilichofanyika kwenye Uwanja wa CCM Kalangalala Mjini Geita, wakati wa  Maonesho ya  Dhahabu yanayofanyika kuanzia Septemba 24 hadi Septemba 30, 2018. 


Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony akiangalia bidhaa za Wajasiriamali katika Maonesho ya Dhahabu yanayofanyika katika Uwanja wa CCM Kalangalala Mjini Geita, kuanzia Septemba 24 hadi Septemba 30, 2018.
Baadhi ya wananchi wa Mji wa Geita wakiangalia teknolojia mbalimbali zinazotumika katika uchimbaji wa dhahabu, katika Maonesho ya Dhahabu yanayofanyika katika Uwanja wa CCM Kalangalala Mjini Geita, kuanzia Septemba 24 hadi Septemba 30, 2018.
 Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka na Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhandisi. Robert  Gabriel  wakitoka katika Banda la Maonesho la Mamlaka ya Mapato Tazania (TRA), katika Maonesho ya Dhahabu yanayofanyika katika Uwanja wa CCM Kalangalala Mjini Geita, kuanzia Septemba 24 hadi Septemba 30, 2018. 

Tuesday, September 25, 2018

VIFO VYA WATOTO WACHANGA VYAPUNGUA SIMIYU


Vifo vya Watoto Wachanga mkoani Simiyu vimepungua kutokana na Serikali kutoa elimu ya uzazi na wazazi kuanza kujifungulia katika vituo vya kutolea huduma ya afya.

Akizungumza na waandishi wa habari kwenye semina ya Mkunga Okoa Maisha iliyofanyika mwishoni mwa wiki jana mjini Bariadi, Katibu wa Wakunga mkoani humo Daud Marwa alisema vifo vimepungua kutokana na jamii kuanza kujenga tabia ya kujifungulia kwenye vituo vya kutolea huduma ya afya.

Alisema kwa mkoa wa Simiyu mwaka 2016 walizaliwa watoto 47,193 lakini waliokufa walikuwa 655, mwaka 2017 walizaliwa watoto 38,442 na walikufa watoto 617 huku mwaka huu wamezaliwa watoto 37,098 na hadi Septemba wamefariki watoto 290.

“Vifo vya Watoto Wachanga mkoani Simiyu vimepungua kutoka 617 mwaka 2017 na kufikia 290 hadi mwezi septemba mwaka huu kutokana serikali kutoa elimu ya uzazi na wazazi kuanza kujifungulia katika vituo vya kutolea huduma ya afya, hii ni jitihada kubwa sana kwani wakunga wamekuwa wakipatiwa mafunzo mara kwa mara, pia kuongezewa stadi za kumhudumia mama na mtoto mwenye uhitaji pindi anapozaliwa’’ alisema Marwa.

Aliongeza kuwa timu ya watumishi wa afya inaendelea kufanya ufuatiliaji na usimamizi ili kuhakikisha kila mama mjamzito anajifungua salama na mtoto mchanga anaendelea kuishi akiwa salama.

Kwa upande wake Mratibu wa Mradi wa Mkunga Okoa Maisha Martha Rimoy alisema akinamama wajawazito wengi wao wanapoteza maisha kutokana na kutoka damu nyingi kabla ya kujifungua, wakati wa kujifungua na baada ya kujifungua.

Alisema wanawake 556 kati ya vizazi hai 100,000 hufariki dunia kila mwaka kutokana na kutokwa damu wakati wa kujifungua na kifafa cha mimba, uzazi pingamizi, na uambukizo.

Aliongeza kuwa kutokana na takwimu hizo, hali ya vifo vya wakinamama na watoto wachanga  bado ni mbaya sana hivyo serikali, wadau wa maendeleo na wananchi wanatakiwa kupiga vita vifo hivyo.

Aidha,  katibu huyo alisema baadhi ya wanawake mkoani Simiyu bado wanajifungulia majumbani kutokana na kuwepo kwa wakunga wa jadi na akabainisha kuwa wanaendelea kutoa elimu kwa wakina mama ili waache tabia hiyo badala yake wajifungulie katika vituo vya kutolea huduma za afya ili kuepuka vifo vinavyoweza kuzuilika.

‘’Tunaendelea kutoa elimu kwa wakunga wa jadi na wakinamama wajawazito ili wakipata matatizo ambayo yanazuilika waweze kuwahi vituo vya kutolea huduma za afya, kutoa mafunzo kwa watoa huduma na pia kuboresha sehemu za kutolea huduma’’ alisema Martha Rimoyi.

Naye Katibu Mkuu wa chama cha Wakunga nchini ambaye pia ni Mwalimu wa Wakunga chuo kikuu cha afya na sayansi shirikishi (MUHAS) Dkt. Sebalda Leshabari alisema kazi ya mkunga ni kumshauri mama mjamzito juu ya masuala ya uzazi hadi anapojifungua, lakini kazi ya muuguzi ni kuhudumia mgonjwa.

Alisema wakunga ni watu wenye taaluma ya ukunga na wenye stadi za kuhudumia mama mjamzito, wenye kugundua viashiria vya hatari kwa wajawazito na kutoa rufaa tofauti na wakunga wa jadi ambao hawana taaluma yoyote.

‘’Wakunga wa jadi hawana stadi na utaalamu pindi mama mjamzito anapokuwa na dalili za kushindwa kujifungua salama, hivyo tunawaomba wakinamama wajawazito wajenge tabia ya kujifungulia kwenye vituo vya kutolea huduma ya afya ili kuzuiwa vifo visivyokuwa vya lazima’’ alisema Dkt. Leshabari.

Semina hiyo ya siku moja kwa waandishi wa Habari mkoa wa Simiyu ililenga kuwajengea uelewa na kufahamu juu ya mkunga, muuguzi na mkunga wa jadi kupitia mradi wa Mkunga Okoa Maisha unaolenga kupunguza vifo vya akinamama wajawazito na watoto wachanga.
MWISHO.



Katibu wa Chama cha Wakunga Tanzania, Dkt. Sebalda Leshabari akizungumza na waandishi wa habari wa mkoa wa Simiyu katika semina ya Mkunga Okoa Maisha iliyofanyika mwishoni mwa wiki jana mjini Bariadi.
Mratibu wa Mradi wa Mkunga Okoa Maisha Martha Rimoy akizungumza na waandishi wa habari wa mkoa wa Simiyu katika semina ya Mkunga Okoa Maisha iliyofanyika mwishoni mwa wiki jana mjini Bariadi.
Katibu wa Wakunga mkoani Simiyu Daud Marwa(kulia) na baadhi ya waandishi wa habari wa mkoa wa Simiyu wakimsikiliza Katibu wa Chama cha Wakunga Tanzania, Dkt. Sebalda Leshabari katika semina ya Mkunga Okoa Maisha iliyofanyika mwishoni mwa wiki jana mjini Bariadi.
Baadhi ya waandishi wa habari wa mkoa wa Simiyu wakifuatlia mada mbalimbali zilizowasilishwa katika semina ya Mkunga Okoa Maisha iliyofanyika mwishoni mwa wiki jana mjini Bariadi.
Baadhi ya waandishi wa habari wa mkoa wa Simiyu wakifuatlia mada mbalimbali zilizowasilishwa katika semina ya Mkunga Okoa Maisha iliyofanyika mwishoni mwa wiki jana mjini Bariadi.

Baadhi ya waandishi wa habari wa mkoa wa Simiyu wakifuatlia mada mbalimbali zilizowasilishwa katika semina ya Mkunga Okoa Maisha iliyofanyika mwishoni mwa wiki jana mjini Bariadi.

Saturday, September 22, 2018

RC MTAKA, ASKOFU KANISA LA SDA WATOA SALAMU ZA POLE KUFUATIA AJALI YA MV NYERERE


Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka na Askofu wa Kanisa la Waadventista Wasabato Jimbo la Kusini mwa Tanzania, Mark Malekana,wametoa salamu za pole kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. John Mongela, wananchi wa Mwanza pamoja na familia na ndugu wa waliopoteza maisha katika ajali ya kuzama kwa Kivuko cha MV Nyerere iliyotokea Septemba 20, 2018 huko Ukerewe Mwanza.

Wakitoa salamu hizo kwa nyakati tofauti Septemba 22, 2018  wakati wa kufunga makambi ya Waadiventista Wasabato katika Uwanja wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi Mkoani Simiyu, Mhe. Mtaka na Askofu Malekana wamewaombea majeruhi wote wapone haraka na kurejea katika majukumu yao.

Kwa upande wake mkuu wa Mkoa wa Simiyu amasema msiba huo mkubwa umewagusa watu wengi ikiwepo mkoa waSimiyu ambapo mwalimu mmoja kutoka katika Kata ya Kalemela wilayani Busega amepoteza maisha katika ajali hiyo.

“Mkoa wa Simiyu katika wilaya ya Busega mwalimu wetu mmoja wa Shule ya msingi katika kata ya Kalemela, Mwalimu Mtaki  amefariki kwenye ajali hii alikuwa naenda kusalimia wazazi wake, huu ni msiba ambao umegusa maeneo mengi”

“ Kwa niaba ya wananchi wote wa mkoa wa Simiyu tunatoa salamu za pole kwanza kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. John Mongela, wananchi wa Mwanza lakini zaidi pole kwa familia ambazo zimeguswa na jambo hili tunawaombea kwa Mwenyezi Mungu marehemu wote na wale ambao wamenusurika Mungu aendelee kuwaimarisha wapone haraka” alisema Mtaka

Ameongeza kuwa Viongozi wa Mkoa wa Simiyu siku ya Jumapili tarehe 23 Septemba, 2018 wataungana na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa,  viongozi wa Mkoa wa Mwanza, viongozi wengine wa Serikali katika tukio la kuwahifadhi waliopoteza maisha katika ajali hiyo.

Naye Askofu wa Kanisa la Waadventista Wasabato Jimbo la Kusini mwa Tanzania, Mark Malekana amesema “Kwa niaba ya Kanisa la Waadventista Wasabato na washiriki wote napenda kutoa salamu za pole kwanza kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. John Mongela, wananchi wa Mwanza kwa msiba huu mzito ulioleta majonzi kwetu Watanzania”

“Kanisa pia linatoa pole kwa familia zilizoguswa na ajali hii na ni ombi la kanisa kwamba wale ambao walijeruhiwa Mungu awapatie uponyaji wa haraka na wale ambao wamelala ambao waliweka maisha yao kwa Yesu ahadi ni kwamba Yesu atakapokuja mara ya pili atawaita kutoka makaburini" alisema Askofu Malekana

Ameongeza kuwa Kanisa linaungana na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli, viongozi wengine na wananchi kuomba utulivu na mshikamano wakati huu wa majonzi.
MWISHO.




Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka akitoa salamu za pole kwa niaba ya wananchi wa mkoa huo, kufuatia vifo vilivyotokana na ajali ya kuzama kwa Kivuko cha MV Nyerere huko Ukerewe mkoani Mwanza, Septemba 20, 2018, salamu hizo zimetolewa wakati wa kufunga makambi ya Waadiventista Wasabato Septemba 22, 2018 katika Uwanja wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi Mkoani Simiyu. 



Askofu wa Kanisa la Waadventista Wasabato Jimbo la Kusini mwa Tanzania, Mark Malekana akitoa salamu za pole kwa niaba ya Kanisa hilo, kufuatia vifo vilivyotokana na ajali ya kuzama kwa Kivuko cha MV Nyerere huko Ukerewe mkoani Mwanza, Septemba 20, 2018, salamu hizo zimetolewa wakati wa kufunga makambi ya Waadiventista Wasabato  Septemba 22, 2018 katika Uwanja wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi Mkoani Simiyu.



Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka na Askofu wa Kanisa la Waadventista Wasabato Jimbo la Kusini mwa Tanzania, Mark Malekana wakiteta jambo wakati wa kufunga makambi ya Waadiventista Wasabato Septemba 22, 2018  katika Uwanja wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi Mkoani Simiyu.
Askofu wa Kanisa la Waadventista Wasabato Jimbo la Kusini mwa Tanzania, Mark Malekana(kushoto) akimkaribisha Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka azungumze na Waumini  wa Kanisa la Waadiventista Wasabato wakati wa kufunga makambi ya Waadiventista Wasabato Septemba 22, 2018 katika Uwanja wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi Mkoani Simiyu.
Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga akizungumza na Waumini wa wa Kanisa la Waadiventista Wasabato wakati wa kufunga makambi ya Waadiventista Wasabato Septemba 22, 2018 katika Uwanja wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi Mkoani Simiyu.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka(kushoto)  akizungumza na Kiongozi wa ATAPE mkoa wa Simiyu, Mhandisi. Paul Jidayi mara baada ya kufunga makambi ya Waadiventista Wasabato Septemba 22, 2018 katika Uwanja wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi Mkoani Simiyu.

Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga(kushoto)  akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wachungaji wa Kanisa la Waadiventista Wasabato wakifuatilia Hotuba ya mkuu wa mkoa wa Simiyu , Mhe. Anthony Mtaka(hayupo pichani)  wakati wa kufunga makambi ya Waadiventista Wasabato Septemba 22, 2018 katika Uwanja wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi Mkoani Simiyu.
Askofu wa Kanisa la Waadventista Wasabato Jimbo la Kusini mwa Tanzania, Mark Malekana akifurahia jambo wakati Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka alipozungumza na  Waumini  wa Kanisa hilo katika  kufunga makambi yao Septemba 22, 2018 katika Uwanja wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi Mkoani Simiyu.

Waimbaji wa Kwaya ya Kanisa la Waadventista Wasabato Kurasini wakimtukuza Mungu kwa nyimbo wakati wa kufunga makambi ya kanisa hilo  Septemba 22, 2018 katika Uwanja wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi Mkoani Simiyu.
Baadhi ya Waumini wa wa Kanisa la Waadiventista Wasabato wakifuatilia hotuba ya Mkuu wa  Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka  wakati wa kufunga makambi ya Waadiventista Wasabato Septemba 22, 2018 katika Uwanja wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi Mkoani Simiyu.
Watoto wa Waumini wa Kanisa la Waadiventista Wasabato wakionesha mambo mbalimbali waliyojifunza katika makambi Mjini Bariadi yliyofungwa Septemba 22, 2018 Mjini Bariadi.


Waimbaji wa Kwaya ya AY Nyarugusu Kanisa la Waadventista Wasabato Geita wakimtukuza Mungu kwa nyimbo wakati wa kufunga makambi ya kanisa hilo  Septemba 22, 2018 katika Uwanja wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi Mkoani Simiyu.


Baadhi ya Waumini wa wa Kanisa la Waadiventista Wasabato wakifuatilia hotuba ya Mkuu wa  Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka  wakati wa kufunga makambi ya Waadiventista Wasabato Septemba 22, 2018 katika Uwanja wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi Mkoani Simiyu.

Baadhi ya Waumini wa wa Kanisa la Waadiventista Wasabato wakifuatilia hotuba ya Mkuu wa  Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka  wakati wa kufunga makambi ya Waadiventista Wasabato Septemba 22, 2018 katika Uwanja wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi Mkoani Simiyu.

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!