Thursday, December 27, 2018

JENERALI MABEYO ATOA WITO KWA VIONGOZI WA DINI KUHUBIRI AMANI

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi hapa nchini Jenerali Venance Mabeyo ametoa wito kwa Viongozi wa Dini nchini kuendelea kuhubiri amani ili kujenga jamii iliyo bora yenye kudumisha upendo na mshikamano.

Jenerali Mabeyo ametoa wito huo wakati wa ibada ya kubariki na kutabaruku Kanisa la Mtakatifu Petro, Kigango cha Kiloleli Parokia ya Ilumya wilayani Busega ambayo ilihudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Kitaifa akiwepo Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Simon Sirro, Naibu Gavana wa Benki Kuu, Dkt. Benard Kibese na viongozi wengine wa Chama na Serikali, ambapo alisisitiza kuwa amani ni msingi wa maendeleo kwa Taifa lolote duniani.

"Suala la amani na utulivu ni la msingi sana katika nchi yetu, kwa vile kila mwananchi ana dini yake tunaamini kuwa viongozi wa dini zote kwa kuwa wanasikilizwa sana  na waumini  wakiweka msisitizo katika suala la amani, amani itatawala na kutakuwa na utulivu"

“Utulivu huu tunauhitaji sana ili tupate maendeleo,  kama  viongozi wetu wa kisiasa wanavyosisitiza kuwa tudumishe amani na utulivu  tupate maendeleo, bila utulivu watu wakiwa wanahaingaika hakuna maendeleo kwa sababu hakuna shughuli mtu anaweza kufanya kama hana amani na utulivu, hivyo hataweza pia kuleta maendeleo yake, familia, jamii na Taifa kwa ujumla" alisema Jenerali Mabeyo

Kwa upande wake Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini Inspekta Jenerali Simon Sirro amesema vitendo vingi vya uvunjifu wa amani na uhalifu ikiwemo ukataji wa mapanga na mauaji ya vikongwe na yanachangiwa na watu kukosa hofu ya Mungu; hivyo nyumba za ibada(makanisa na misikiti) zinapojengwa kwa wingi zitakuwa msaada mkubwa sana kwa watu kuwa na hofu ya Mungu.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka amesema jamii inayoamini uwepo wa Mungu haiwezi kuwa na vitendo vya kisasi, kukatana mapanga na mauaji ya vikongwe huku akiwaasa Watanzania kukaa kwa amani na upendo bila kufanya mambo yanayoweza kuhatarisha amani.

Akibariki na kutabaruku Kanisa la Mtakatifu Petro, Kigango cha Kiloleli Parokia ya Ilumya wilayani Busega, Askofu wa Jimbo Katoliki Shinyanga, Muhashamu Liberatus Sangu amewataka Watanzania kupendana na kuacha roho ya ubinafsi na visasi.

Aidha, Askofu Sangu ametoa wito kwa viongozi na waumini kufanya nyumba za ibada zibaki nyumba za sala kama yanenavyo maandiko matakatifu na kamwe zisitumike kama majukwaa la wanasiasa.

" Palipo na msamaha pana umoja, uelewano na usawa lakini palipo na  kisasi hapana maendeleo; nyumba ya ibada isitumike kama jukwaa la Wanasiasa alisisitiza Muhashamu Askofu Sangu.

MWISHO

 Askofu wa Jimbo Katoliki Shinyanga, Muhashamu Liberatus Sangu(kushoto), Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka(katikati), Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Venance Mabeyo(kulia) wakifurahia jambo mara baada ya kumalizika kwa ibada ya kubariki na kutabaruku Kanisa la Mtakatifu Petro Kigango cha Kiloleli Parokia ya Ilumya wilayan Busega mkoani Simiyu, iliyofanyika Desemba 26, 2018.



Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi nchini Jeneral Venance Mabeyo akipokea mkono wa Heri ya Krismasi kutoka kwa Askofu wa Jimbo Katoliki Shinyanga, Muhashamu Liberatus Sangu, katika ibada ya kubariki na kutabaruku Kanisa la Mtakatifu Petro Kigango cha Kiloleli Parokia ya Ilumya wilayani Busega mkoani Simiyu, iliyofanyika Desemba 26, 2018.

Askofu wa Jimbo Katoliki Shinyanga, Muhashamu Liberatus Sangu akimshuhudia Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi nchini Jenerali Venance Mabeyo wakati akitia saini kama shahidi katika Hati ya kubariki na kutabaruku Kanisa la Mtakatifu Mtakatifu Petro Kigango cha Kiloleli Parokia ya Ilumya, katika ibada ya kubariki na kutabaruku  kanisa hilo, iliyofanyika Desemba 26, 2018.
Kutoka kushoto Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga, Naibu Gavana wa Benki Kuu, Dkt. Benard Kibese, Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka,Mkuu wa Jeshi la Polisi IGP Simon Sirro na Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Venance Mabeyo wakiwa katika ibada ya kubariki na kutabaruku Kanisa la Mtakatifu Petro Kigango cha Kiloleli Parokia ya Ilumya wilayan Busega mkoani Simiyu, iliyofanyika Desemba 26, 2018.
Wanakwaya ya Mtakatifu Maxmillian kutoka Parokia ya Segerea jijini Dar es salaam wakiimba katika katika ibada ya kubariki na kutabaruku Kanisa la Mtakatifu Petro Kigango cha Kiloleli Parokia ya Ilumya wilayan Busega mkoani Simiyu, iliyofanyika Desemba 26, 2018.
Askofu wa Jimbo Katoliki Shinyanga, Muhashamu Liberatus Sangu, Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka, Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Venance Mabeyo na viongozi wengine wakiwa na katika picha ya pamoja na watoto wenye ualbino wanaoishi katika kituo cha kulelea watoto wenye mahitaji maalum Lamadi, mara baada ya kumalizika kwa ibada ya kubariki na kutabaruku Kanisa la Mtakatifu Petro Kigango cha Kiloleli Parokia ya Ilumya wilayan Busega mkoani Simiyu, iliyofanyika Desemba 26, 2018.
Askofu wa Jimbo Katoliki Shinyanga, Muhashamu Liberatus Sangu( wa pili kushoto mbele) akiwaongoza waumini katika sala ya kuombea Kanisa la Mtakatifu Petro Kigango cha Kiloleli Parokia ya Ilumya wilayani Busega mkoani Simiyu katika ibada ya kubariki na kutabaruku  kanisa hilo, iliyofanyika Desemba 26, 2018.
Baadhi ya viongozi wa Mkoa wa Simiyu na wa Kitaifa wakiimba wimbo wa mimina Neema wa Kwaya ya Mwenyeheri Anuarite Makuburi jijini Dar es salaam, wakati wa ibada ya kubariki na kutabaruku Kanisa la Mtakatifu Petro Kigango cha Kiloleli Parokia ya Ilumya wilayan Busega mkoani Simiyu, iliyofanyika Desemba 26, 2018.
Mkuu wa mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka akipokea sakramenti ya mwili na damu ya Yesu Kristo wakati wa ibada ya kubariki na kutabaruku Kanisa la Mtakatifu Petro Kigango cha Kiloleli Parokia ya Ilumya wilayan Busega mkoani Simiyu, iliyofanyika Desemba 26, 2018.
Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini Inspekta wa  Polisi Simon Sirro akipokea sakramenti ya mwili na damu ya Yesu Kristo wakati wa ibada ya kubariki na kutabaruku Kanisa la Mtakatifu Petro Kigango cha Kiloleli Parokia ya Ilumya wilayan Busega mkoani Simiyu, iliyofanyika Desemba 26, 2018.
Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi nchini Jenerali Venance Mabeyo akipokea sakramenti ya mwili na damu ya Yesu Kristo wakati wa ibada ya kubariki na kutabaruku Kanisa la Mtakatifu Petro Kigango cha Kiloleli Parokia ya Ilumya wilayan Busega mkoani Simiyu, iliyofanyika Desemba 26, 2018.

Sehemu ya Kanisa la Mtakatifu Petro Kigango cha Kiloleli Parokia ya Ilumya Busega, lililobarikiwa na kutabarukiwa na Askofu wa Jimbo Katoliki Shinyanga, Muhashamu Liberatus Sangu Desemba 26, 2018.
Baadhi ya viongozi wa Serikali , vyombo vya ulinzi na usalama na waumini wakifuatilia ibada ya kubariki na kutabaruku Kanisa la Mtakatifu Petro Kigango cha Kiloleli Parokia ya Ilumya wilayani Busega mkoani Simiyu, iliyofanyika Desemba 26, 2018.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka (wa pili kulia) akiwa katika picha ya pamoja na Askofu wa Jimbo Katoliki Shinyanga, Muhashamu Liberatus Sangu( wa pili kushoto) na baadhi ya viongozi wa Serikali , vyombo vya ulinzi na usalama na waumini,  baada  ya ibada ya kubariki na kutabaruku Kanisa la Mtakatifu Petro Kigango cha Kiloleli Parokia ya Ilumya wilayan Busega mkoani Simiyu, iliyofanyika Desemba 26, 2018.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka(kulia) akiteta jambo na Askofu wa Jimbo Katoliki Shinyanga, Muhashamu Liberatus Sangu, baada  ya ibada ya kubariki na kutabaruku Kanisa la Mtakatifu Petro Kigango cha Kiloleli Parokia ya Ilumya wilayani Busega mkoani Simiyu, iliyofanyika Desemba 26, 2018.
Askofu wa Jimbo Katoliki Shinyanga, Muhashamu Liberatus Sangu( katikati) akiwa katika picha ya pamoja na mapadri walioshiriki katika ibada ya kubariki na kutabaruku Kanisa la Mtakatifu Petro Kigango cha Kiloleli Parokia ya Ilumya wilayani Busega mkoani Simiyu, iliyofanyika Desemba 26, 2018.
Askofu wa Jimbo Katoliki Shinyanga, Muhashamu Liberatus Sangu akitoa mahubiri katika ibada ya kubariki na kutabaruku Kanisa la Mtakatifu Petro Kigango cha Kiloleli Parokia ya Ilumya wilayani Busega mkoani Simiyu, iliyofanyika Desemba 26, 2018.
Askofu wa Jimbo Katoliki Shinyanga, Muhashamu Liberatus Sangu(kushoto) akizungumza jambo na Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka( wa pili kulia) na baadhi ya wanakwaya ya Mwenyeheri Anuarite Makuburi jijini Dar es salaam,  baada  ya ibada ya kubariki na kutabaruku Kanisa la Mtakatifu Petro Kigango cha Kiloleli Parokia ya Ilumya wilayani Busega mkoani Simiyu, iliyofanyika Desemba 26, 2018.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka(kulia)akiteta jambo na Askofu wa Jimbo Katoliki Shinyanga, Muhashamu Liberatus Sangu(kushoto) na baadhi ya wanakwaya ya Mwenyeheri Anuarite Makuburi jijini Dar es salaam,  baada  ya ibada ya kubariki na kutabaruku Kanisa la Mtakatifu Petro Kigango cha Kiloleli Parokia ya Ilumya wilayani Busega mkoani Simiyu, iliyofanyika Desemba 26, 2018.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka akifurahia jambo na Askofu wa Jimbo Katoliki Shinyanga, Muhashamu Liberatus Sangu(kushoto) na Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi nchini Jenrali Venance Mabeyo(kulia) baada  ya ibada ya kubariki na kutabaruku Kanisa la Mtakatifu Petro Kigango cha Kiloleli Parokia ya Ilumya wilayani Busega mkoani Simiyu, iliyofanyika Desemba 26, 2018.
kutoka kushoto Naibu Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, Dkt. Benard Kibese, Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka, Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini Inspekta wa  Polisi Simon Sirro wakifurahia jambo na kulia na Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi nchini Jenrali Venance Mabeyo akikabidhiwa mshumaa, katika ibada ya kubariki na kutabaruku Kanisa la Mtakatifu Petro Kigango cha Kiloleli Parokia ya Ilumya wilayani Busega mkoani Simiyu, iliyofanyika Desemba 26, 2018.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka akipokea mkono wa Heri ya Krismasi kutoka kwa Askofu wa Jimbo Katoliki Shinyanga, Muhashamu Liberatus Sangu, katika ibada ya kubariki na kutabaruku Kanisa la Mtakatifu Petro Kigango cha Kiloleli Parokia ya Ilumya wilayani Busega mkoani Simiyu, iliyofanyika Desemba 26, 2018.
Mwimbaji wa Nyimbo za Injili, Christina Shusho akiimba pamoja na wanakwaya ya Mtakatifu Maxmillian Parokia ya Segerea jijini Dar es salaam, baada ya ibada ya kubariki na kutabaruku Kanisa la Mtakatifu Petro Kigango cha Kiloleli Parokia ya Ilumya wilayani Busega mkoani Simiyu, iliyofanyika Desemba 26, 2018.
Paroko wa Parokia ya Ilumya, Michael Kumalija akitia saini Hati ya kubariki na kutabaruku Kanisa la Mtakatifu Petro Kigango cha Kiloleli Parokia ya Ilumya, katika ibada ya kubariki na kutabaruku  kanisa hilo, iliyofanyika Desemba 26, 2018.

Askofu wa Jimbo Katoliki Shinyanga, Muhashamu Liberatus Sangu, Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka, Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Venance Mabeyo na viongozi wengine wakiwa na katika picha ya pamoja na watoto wenye ualbino wanaoishi katika kituo cha kulelea watoto wenye mahitaji maalum Lamadi, mara baada ya kumalizika kwa ibada ya kubariki na kutabaruku Kanisa la Mtakatifu Petro Kigango cha Kiloleli Parokia ya Ilumya wilayan Busega mkoani Simiyu, iliyofanyika Desemba 26, 2018.

Sunday, December 23, 2018

WADAU WA ELIMU WACHANGIA ZAIDI YA SHILINGI MILIONI 250 UJENZI WA MADARASA BUSEGA


Wadau mbalimbali wa elimu wamechangia ujenzi wa vyumba vya madarasa katika Halmashauri ya Wilaya ya Busega mkoani Simiyu katika Harambee iliyofanyika Mjini Nyashimo, ambapo zimepatikana jumla ya shilingi 254, 969,000/= fedha taslimu zikiwa ni shilingi 15,360,000/= ahadi shilingi 241,809,000/= na mifuko ya saruji 127.

Akiongea na wadau hao Mwakilishi wa Mkuu wa Majeshi Jenerali Venance Mabeyo ambaye alialikwa kama Mgeni rasmi wa Harambee hiyo, Luteni Kanali Josephat Mshashi, Mkuu wa Kikosi cha 27 Makoko Musoma amesema upo umuhimu wa kuhakikisha watoto wanapata elimu kwa kuwa elimu ni urithi hivyo kila mmoja awe na uchungu wa kuona watoto wanasoma.

“Hakuna urithi tunaoweza kuwapa watoto wetu zaidi ya elimu tusipowapa elimu rasilimali zote ambazo tunazipigania leo hii, tunavyopambana kulikomboa Taifa letu kiuchumi itakuwa kazi bure kwa sababu tutabaki na Taifa la watu ambao ni watumwa wa watu wenye elimu” alisema Mshashi

Awali akitoa taarifa ya hali ya vyumba vya madarasa  Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Busega, Bw. Anderson Njinginya amesema halmashauri hiyo ina upungufu wa vyumba vya madarasa 107.

Mmoja wa Wadau wa elimu katika Wilaya ya Busega, Bw. Deo Kumalija ambaye alichangia katika harambee hiyo ametoa wito wadau wa maendeleo na wananchi kuchangia shughuli za maendeleo katika maeneo waliyopo, ikiwemo ujenzi wa shule kwa kuwa maendeleo yao yataletwa na wao wenyewe.

 Naye Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe. Anthony Mtaka ameupongeza uongozi wa wilaya ya Busega kuandaa harambee hiyo huku akiwataka kusimamia fedha zilizopatikana, ili zifanye kazi iliyokusudiwa, na kuwasisitiza wazazi, walezi na jamii yote kwa ujumla kuhakikisha wanafunzi wote waliochaguliwa kwenda kidato cha kwanza wanaenda shule.

“Nawapongeza sana viongozi wa wilaya ya Busega wakiongozwa na Mhe. DC kwa kuandaa harambee hii, fedha hizi mhakikishe zinasimamiwa vizuri na zifanye kazi iliyokusudiwa, lakini pia mhakikishe watoto wote waliochaguliwa wanaenda shule, haiwezekani juhudi kubwa namna hii ifanyike kuchangia halafu watoto wasiende shule” alisema Mtaka.

Mkuu wa Wilaya ya Busega Mhe. Tano Mwera amemhakikishia Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe. Anthony Mtaka kuwa Viongozi watasimamia fedha yote iliyopatikana na kuhakikisha inafanya kazi itakayokuwa na thamani halisi ya fedha hiyo(value for money).

Akitoa shukrani kwa viongozi na wadau mbalimbali wa elimu waliochangia katika harambee hiyo Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya Busega, Mhe. Vumi Magoti ametoa wito kwa madiwani kuwahamasisha wananchi kuchangia ujenzi wa vyumba vya madarasa katika kata zao, ili fedha zilizopatikana ziweze kuwasaidia katika ukamilishaji.

Pamoja na kutafuta wadua wa elimu waliochangia zaidi ya shilingi milioni 70 katika harambee hiyo Mbunge wa Jimbo la Busega, Mhe. Dkt. Raphael Chegeni amesema kwa kushirikiana na wadau ameshatoa vifaa vya ujenzi ikiwemo mabati 1700 na mifuko ya saruji 640 ambavyo vimeshasambazwa na kusaidia katika ujenzi wa vyumba vya madarasa wilayani humo.

MWISHO.


Wadau wa elimu na viongozi mbalimbali wa mkoa wa Simiyu wakichangia katika harambee ya kuchangia ujenzi wa vyumba vya madarasa wilayani Busega, iliyofanyika Mjini Nyashimo lengo likiwa ni kukabiliana na changamoto ya vyumba vya madarasa wilayani humo.
Mkuu wa Wilayaya Busega Mhe. Tano Mwera (kushoto) na Mbunge wa Busega,Mhe. Dkt. Raphael Chegeni wakiteta jambo katika harambee ya kuchangia ujenzi wa vyumba vya madarasa wilayani Busega, iliyofanyika Mjini Nyashimo lengo likiwa ni kukabiliana na changamoto ya vyumba vya madarasa wilayani humo.
Mwakilishi wa Mkuu wa Majeshi Jenerali Venance Mabeyo ambaye alialikwa kama Mgeni rasmi wa Harambee hiyo, Luteni Kanali Josephat Mshashi, Mkuu wa Kikosi cha 27 Makoko Musoma akizungumza na wadau wa elimu, katika harambee ya kuchangia ujenzi wa vyumba vya madarasa wilayani Busega, iliyofanyika Mjini Nyashimo lengo likiwa ni kukabiliana na changamoto ya vyumba vya madarasa wilayani humo.
Wadau wa elimu na viongozi mbalimbali wa mkoa wa Simiyu wakichangia katika harambee ya kuchangia ujenzi wa vyumba vya madarasa wilayani Busega, iliyofanyika Mjini Nyashimo lengo likiwa ni kukabiliana na changamoto ya vyumba vya madarasa wilayani humo.
Mdau wa Maendeleo katika Wilaya ya Busega, Bw. Deo Kumalija akichangia katika harambee ya kuchangia ujenzi wa vyumba vya madarasa wilayani Busega, iliyofanyika Mjini Nyashimo lengo likiwa ni kukabiliana na changamoto ya vyumba vya madarasa wilayani humo.



Wadau wa elimu na viongozi mbalimbali mkoani Simiyu wakifurahia katika harambee ya kuchangia ujenzi wa vyumba vya madarasa wilayani Busega, iliyofanyika Mjini Nyashimo lengo likiwa ni kukabiliana na changamoto ya vyumba vya madarasa wilayani humo.
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya Busega, Mhe. Vumi Magoti(kushoto) na Mkuu wa Wilaya ya Maswa, mhe. Dkt. Seif Shekalaghe wakiteta jambo katika harambee ya kuchangia ujenzi wa vyumba vya madarasa wilayani Busega, iliyofanyika Mjini Nyashimo lengo likiwa ni kukabiliana na changamoto ya vyumba vya madarasa wilayani humo.


Wadau wa elimu na viongozi mbalimbali mkoani Simiyu wakifurahia katika harambee ya kuchangia ujenzi wa vyumba vya madarasa wilayani Busega, iliyofanyika Mjini Nyashimo lengo likiwa ni kukabiliana na changamoto ya vyumba vya madarasa wilayani humo.

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka(kushoto) akieta jambo na Katibu Tawala Mkoa wa Simiyu, Bw. Jumanne Sagini katika harambee ya kuchangia ujenzi wa vyumba vya madarasa wilayani Busega, iliyofanyika Mjini Nyashimo lengo likiwa ni kukabiliana na changamoto ya vyumba vya madarasa wilayani humo.
Katibu Tawala Mkoa wa Simiyu, Bw. Jumanne Sagini(wa pili kushoto)  akiteta jambo na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya Busega, Mhe. Vumi Magoti katika harambee ya kuchangia ujenzi wa vyumba vya madarasa wilayani Busega, iliyofanyika Mjini Nyashimo lengo likiwa ni kukabiliana na changamoto ya vyumba vya madarasa wilayani humo.
Kutoka kushoto Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka, Katibu Tawala Mkoa wa Simiyu, Bw. Jumanne Sagini, Mkuu wa Wilaya ya Maswa, mhe. Dkt. Seif Shekalaghe na Mbunge wa Jimbo la Busega, Mhe. Dkt. Raphael Chegeni  wakiteta jambo, katika harambee ya kuchangia ujenzi wa vyumba vya madarasa wilayani Busega, iliyofanyika Mjini Nyashimo lengo likiwa ni kukabiliana na changamoto ya vyumba vya madarasa wilayani humo.
Mkuu wa Wilaya ya Bariadi,Mhe. Festo Kiswaga akizungumza na wadau wa elimu katika harambee ya kuchangia ujenzi wa vyumba vya madarasa wilayani Busega, iliyofanyika Mjini Nyashimo lengo likiwa ni kukabiliana na changamoto ya vyumba vya madarasa wilayani humo.
Baadhi ya viongozi wa mkoa wa Simiyu na wadau waelimu wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya harambee ya kuchangia ujenzi wa vyumba vya madarasa wilayani Busega, iliyofanyika Mjini Nyashimo lengo likiwa ni kukabiliana na changamoto ya vyumba vya madarasa wilayani humo.
Mkuu wa Wilaya ya Maswa, Mhe. Dkt. Seif Shekalaghe akizungumza na wadau wa elimu katika harambee ya kuchangia ujenzi wa vyumba vya madarasa wilayani Busega, iliyofanyika Mjini Nyashimo lengo likiwa ni kukabiliana na changamoto ya vyumba vya madarasa wilayani humo.

Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bw. Jumanne Sagini akiwasilisha mchango wa Sekretarieti ya Mkoa, katika harambee ya kuchangia ujenzi wa vyumba vya madarasa wilayani Busega, iliyofanyika Mjini Nyashimo lengo likiwa ni kukabiliana na changamoto ya vyumba vya madarasa wilayani humo.

Mfanyabiashara na Mjumbe wa NEC , Bw. Gungu Silanga Shekalaghe akizungumza na wadau wa elimu katika harambee ya kuchangia ujenzi wa vyumba vya madarasa wilayani Busega, iliyofanyika Mjini Nyashimo lengo likiwa ni kukabiliana na changamoto ya vyumba vya madarasa wilayani humo.
Mkuu wa Wilaya ya Busega,  Mhe. Tano Mwera akizungumza na wadau wa elimu katika harambee ya kuchangia ujenzi wa vyumba vya madarasa wilayani Busega, iliyofanyika Mjini Nyashimo lengo likiwa ni kukabiliana na changamoto ya vyumba vya madarasa wilayani humo.
Mdau wa elimu katika Wilaya ya Busega, Bw. Deo Kumalija akizungumza na wadau wa elimu wenzake katika harambee ya kuchangia ujenzi wa vyumba vya madarasa wilayani Busega, iliyofanyika Mjini Nyashimo lengo likiwa ni kukabiliana na changamoto ya vyumba vya madarasa wilayani humo.
Mwenyekiti wa Kamati ya Huduma za Jamii, Mhe. Mickness Mahela(wa pili kushoto) akiwa na madiwani wenzake wakiwasilisha mchango wa madiwani katika harambee ya kuchangia ujenzi wa vyumba vya madarasa wilayani Busega, iliyofanyika Mjini Nyashimo lengo likiwa ni kukabiliana na changamoto ya vyumba vya madarasa wilayani humo.
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Busega, Bw. Anderson Njiginya( wa pili kushoto)  na baadhi ya wakuu wa idara wakiwasilisha mchango wao katika harambee ya kuchangia ujenzi wa vyumba vya madarasa wilayani Busega, iliyofanyika Mjini Nyashimo lengo likiwa ni kukabiliana na changamoto ya vyumba vya madarasa wilayani humo.
Baadhi ya wadau wa elimu wakifuatilia harambee ya kuchangia ujenzi wa vyumba vya madarasa wilayani Busega, iliyofanyika Mjini Nyashimo lengo likiwa ni kukabiliana na changamoto ya vyumba vya madarasa wilayani humo.



Baadhi ya wadau wa elimu wakifuatilia harambee ya kuchangia ujenzi wa vyumba vya madarasa wilayani Busega, iliyofanyika Mjini Nyashimo lengo likiwa ni kukabiliana na changamoto ya vyumba vya madarasa wilayani humo.
Baadhi ya wadau wa elimu wakifuatilia harambee ya kuchangia ujenzi wa vyumba vya madarasa wilayani Busega, iliyofanyika Mjini Nyashimo lengo likiwa ni kukabiliana na changamoto ya vyumba vya madarasa wilayani humo.

Saturday, December 15, 2018

SIMIYU YAIDHINISHIWA BILIONI 13 MATENGENEZO YA BARABARA, MIRADI YA MAENDELEO

Mkoa wa Simiyu umeidhinishiwa jumla ya shilingi bilioni 13.1 kwa ajili ya matengenezo ya barabara na  miradi ya maendeleo katika bajeti ya mwaka 2018/2019.

Hayo yamebainishwa na Meneja wa Wakala wa Barabara (TANROADS)'Mkoa wa Simiyu, Mhandisi. Albert Kent wakati akiwasilisha taarifa katika Kikao cha Bodi ya Barabara ya Mkoa, kilichofanyika Desemba 14, 2018 Mjini Bariadi.

Kent amesema kati ya fedha hizo shilingi bilioni 11.461 zimeidhinishwa kwa ajili ya matengenezo ya barabara kutoka katika mfuko wa barabara na shilingi bilioni 1.595 utekelezaji wa miradi 12  ya maendeleo  yenye urefu wa kilometa 78.2.

Aidha, Kent amezungumzia maendeleo ya ujenzi wa daraja la mto Sibiti na kubainisha kuwa ujenzi wake umefikia asilimia 85 na jitihada zinaendelea kufanyika, ili ifikapo mwezi Machi, 2019 liwe limekamilika kama ilivyoelekezwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. John Pombe Magufuli mwezi Septemba, 2018 wakati akiweka jiwe la msingi la ujenzi wa daraja hilo.

Naye Mratibu wa Wakala wa Barabara Mijini na Vijijini (TARURA), Mhandisi. Salvatory Yambi amesema katika bajeti ya mwaka 2018/2019 Mkoa wa Simiyu umeidhinishiwa jumla ya shilingi bilioni 5.4  na kubainisha kuwa hadi sasa TARURA inaendelea kutekeleza miradi 29 yenye thamani ya zaidi ya shilingi bilioni 3.6 ambayo ipo katika hatua mbalimbali za utekelezaji.

Awali akifungua kikao cha Bodi ya Barabara kwa niaba ya Mwenyekiti wa kikao hicho na Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka, Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga amepongeza TANROADS na TARURA kwa kazi kubwa wanayoifanya mkoani humo, hususani katika kusimamia ujenzi na matengenezo barabara hali iliyochangia kuufungua mkoa na kuchochea kukua kwa uchumi.

Akichangia hoja katika kikao hicho, Mbunge wa Bariadi, Mhe. Andrew Chenge ameshauri kuwepo na uhusiano wa karibu kati ya TARURA na Halmashauri hususani katika maandalizi ya Bajeti, ili vipaumbele vya TARURA vizingatie vipaumbele vya Halmashauri ambao ndio wanaokutana na  wananchi moja kwa moja na kujua mahitaji yao.

Naye Katibu Tawala wa Mkoa Simiyu, Jumanne Sagini ametoa wito kwa Wakurugenzi wa halamshauri kutenga fedha kwa ajili ya matengenezo ya barabara ambazo haziko chini ya TARURA hususani katika kipindi hiki cha maandalizi ya bajeti.

Katika kikao hiki pia wajumbe mbalimbali walipata nafasi ya kuchangia hoja ambazo zililenga kuboresha miundombinu ya barabara na madaraja, masuala yote ambayo Mhandisi Kent alieleza kuwa yatafanyiwa kazi na yanayohitaji hatua zaidi kutoka katika wizara yenye dhamana yatafikishwa.

"Nashauri wananchi washirikishwe katika zoezi la uwekaji wa alama za vivuko wakati barabara ya Maswa-Bariadi itakapokamilika ili viwekwe mahali penye uhitaji" Mkuu wa Wilaya ya Maswa, Mhe. Dkt. Seif Shekalaghe

"Ili daraja la Sibiti liweze kuleta tija zaidi tunaomba TANROADS iandae mpango wa dharura wa kujenga daraja la Mto Itembe ili kuwaondolea adha wananchi  waweze kuvuka kutoka eneo moja  kwenda kwingine pindi mvua zinaponyesha." Mhe. Leah Komanya, Mbunge wa Viti Maalum CCM.

Mwenyekiti Halmashauri ya Mji wa Bariadi, Mhe. Robert Lweyo ameshauri  ijengwe  round about (mzunguko) Mjini Bariadi katika makutano ya barabara ya Ngulyati-Bariadi, Lamadi- Bariadi na Maswa-Bariadi, jambo ambalo Mhandisi Kent aliahidi kuliandikia barua na na kuliwasilisha katika wizara yenye dhamana na ujenzi.
MWISHO

Meneja wa Wakala wa Barabara(TANROADS) Mkoa wa Simiyu, Mhandisi. Albert Kent akiwasilisha taarifa yake ya Mkoa katika kikao cha Bodi ya barabara , kilichofanyika Desemba 14, 2018 Mjini Bariadi.
Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga akifungua kikao cha bodi ya barabara kwa niaba ya Mwenyekiti wa kikao hicho, Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka(hayupo pichani), kilichofanyika Desemba 14, 2018 Mjini Bariadi. 
Mratibu wa Wakala wa Barabara mijini na Vijijini(TARURA)Mkoa wa Simiyu, Mhandisi. Salvatory Yambi taarifa yake ya Mkoa katika kikao cha Bodi ya barabara , kilichofanyika Desemba 14, 2018 Mjini Bariadi.


Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bw. Jumanne Sagini akifafanua jambo katika kikao cha Bodi ya barabara , kilichofanyika Desemba 14, 2018 Mjini Bariadi.


Baadhi ya wajumbe wa Kikao cha Bodi ya Barabara Mkoa wa Simiyu wakifuatilia kwa makini masuala mbalimbali yaliyokuwa yakijadiliwa katika kikao hicho, Desemba 14, 2018 Mjini Bariadi.
Mbunge wa Jimbo la Bariadi, Mhe. Andrew Chenge akichangia hoja katika kikao cha Bodi ya barabara mkoa wa Simiyu , kilichofanyika Desemba 14, 2018 Mjini Bariadi.

Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Simiyu, Mhe. Leah Komanya akichangia hoja katika kikao cha Bodi ya barabara , kilichofanyika Desemba 14, 2018 Mjini Bariadi.
Baadhi ya wajumbe wa Kikao cha Bodi ya Barabara Mkoa wa Simiyu wakifuatilia kwa makini masuala mbalimbali yaliyokuwa yakijadiliwa katika kikao hicho, Desemba 14, 2018 Mjini Bariadi.


Mkuu wa Wilaya ya Busega, Mhe. Tano Mwera(kushoto) na Mkuu wa Wilaya ya Maswa, Mhe. Dkt.Seif Shekalaghe wakitelezana jambo, katika kikao cha Bodi ya barabara mkoa wa Simiyu , kilichofanyika Desemba 14, 2018 Mjini Bariadi.

Baadhi ya wajumbe wa Kikao cha Bodi ya Barabara Mkoa wa Simiyu wakifuatilia kwa makini masuala mbalimbali yaliyokuwa yakijadiliwa katika kikao hicho, Desemba 14, 2018 Mjini Bariadi.
Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Simiyu, Mhe. Enock Yakobo(kushoto) na Mbunge wa Jimbo la Bariadi, Mhe. Andrew Chenge wakiangalia kwa makini taarifa zilizopo katika makablasha , wakati wa kikao cha Bodi ya barabara mkoa wa Simiyu , kilichofanyika Desemba 14, 2018 Mjini Bariadi.
Mwenyekiti wa Halamshauri ya Mji wa Bariadi, Mhe. Robert Lweyo akichangia hoja katika kikao cha Bodi ya barabara mkoa wa Simiyu , kilichofanyika Desemba 14, 2018 Mjini Bariadi.
Baadhi ya wajumbe wa Kikao cha Bodi ya Barabara Mkoa wa Simiyu wakifuatilia kwa makini masuala mbalimbali yaliyokuwa yakijadiliwa katika kikao hicho, Desemba 14, 2018 Mjini Bariadi.
Mkuu wa Wilaya ya Maswa, Mhe. Dkt. Seif Shekalaghe akichangia hoja katika kikao cha Bodi ya barabara mkoa wa Simiyu , kilichofanyika Desemba 14, 2018 Mjini Bariadi.


Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Simiyu, Deusdedit Nsimeki akichangia hoja katika kikao cha Bodi ya barabara mkoa wa Simiyu , kilichofanyika Desemba 14, 2018 Mjini Bariadi.

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!