Wednesday, July 31, 2019

RAIS MAGUFULI KUZINDUA KAZI DATA YA WAKULIMA NANENANE KITAIFA SIMIYU: WAZIRI HASUNGA

Waziri wa Kilimo, Mhe.  Japhet Hasunga amesema Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt John Pombe Magufuli Agosti 8, 2019 ,anatarajiwa kuzindua kanzi data ya usajili wa wakulima kupitia mazao nane ya kimkakati, itakayosaidia kujua idadi ya wakulima sambamba na wakulima  kujua takwimu za mazao na upatikanaji wa masoko kwa urahisi kupitia njia ya mtandao .


Mhe. Hasunga ameyasema hayo Julai 30, 2019 wkati akikagua maendeleo ya maandalizi ya maonesho ya Nanenane Kitaifa Mkoani Simiyu, ambapo amesema pamoja na kuzindua kanzi data ya wakulima Mhe. Rais Magufuli anatarajiwa pia kuzindua mfumo wa kielectroniki utakaosaidia kujua idadi ya wakulima, mahali walipo,mazao wanayolima na ukubwa wa maeneo wanayolima.

“Tunataka kili Mtanzania popote alipo akitaka takwimu sahihi awe anaweza kuingia kwenye mfumo na akaziona,  ukitaka wakulima wa pamba wa pamba waonekane, tukakitaka wakulima wa mkonge waonekane, tunataka tuwe na uwezo wa kuwaona wakulima wakubwa, wa kati na wadogo na mahali walipo” alisema Mhe. Hasunga.

Pamoja na hayo ameongeza kuwa tarehe hiyo pia  Rais Dkt Magufuli atafungua soko la bidhaa ambalo litawawezesha  wakulima kuuza mazao yao nje ya nchi ambayo itasaidia kupata uhakika wa bei na  kuepuka madalali na kuleta uwazi ili kila mkulima /mdau yoyote  aweze kuona na kujua  bei  sambamba na kufahamiana .

Waziri Hasunga amesema  kwa upande wa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.Samia Suluhu Hassan , wakati  akizindua  maonesho ya nane nane Agosti  Mosi, 2019, anatarajiwa kuzungumzia masuala ya mazinigira  ambapo atazindua mkakati wa kuthibiti upotevu wa mazao utakao wezesha kujua hasara anazozipata mkulima hatua itakayopelekea kukabiliana nazo kwa wakati.

Aidha waziri Hasunga ameongeza kuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa atazindua bima ya mazao ambayo itasaidia kukabiliana na vihatarishi vya mazao mfano ukame na mafuriko sambamba na kuona maendeleo ya ushirika nchini na nafasi ya ushirika na namna ambavyo unawaunganisha wakulima ,wafugaji na wavuvi.

Katika hatua nyingine Waziri Hasunga amemtembelea mmoja wa wajasiriamali kutoka wilaya ya Meatu  Deke Ndabuli Maige anayetengeneza mashine za kupukuchua mahindi ambapo mjasiriamali hiyo amesema kuwa alianza kutengeneza mashine hizo tangu mwaka 2014 na  hadi sasa ameshatengeneza mashine 10 na tayari ameshauza mashine 7.

Pamoja na hayo ameongeza kuwa mashine hizo zinauwezo wa kupukuchua magunia 150 kwa siku huku akitumia lita saba za mafuta ya kuendeshea mashine hiyo kwa siku.

MWISHO


Waziri wa Kilimo, Mhe.  Japhet Hasunga (wa pili kushoto) akipokea maelezo juu ya teknolojia rahisi ya upandaji wa mazao ya mbogamboga katika Vipando vya Halmashauri ya Manispaa ya Musoma, wakati wa ziara yake ya kujionea maendeleo ya maandalizi ya Maonesho ya Nanenane Kitaifa yatakayofanyika Kanda ya Ziwa Mashariki katika Viwanja vya Nyakabindi mkoani Simiyu.


Waziri wa Kilimo, Mhe.  Japhet Hasunga (wa pili kushoto) akipokea maelezo juu matumizi ya zana za kisasa za kilimo katika Banda la Jeshi la kujenga Taifa(JKT), wakati wa ziara yake ya kujionea maendeleo ya maandalizi ya Maonesho ya Nanenane Kitaifa yatakayofanyika Kanda ya Ziwa Mashariki katika Viwanja vya Nyakabindi mkoani Simiyu.
Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bw. Jumanne Sagini akitoa maelezo kwa Waziri wa Kilimo, Mhe.  Japhet Hasunga(kushoto), kuhusu jengo la Maonesho la Mkoa wa Simiyu, wakati wa ziara yake ya kujionea maendeleo ya maandalizi ya Maonesho ya Nanenane Kitaifa yatakayofanyika Kanda ya Ziwa Mashariki katika Viwanja vya Nyakabindi mkoani Simiyu.
Waziri wa Kilimo, Mhe.Japhet Hasunga (aliyeyoosha mkono)akiangalia mbegu ya ulezi, wakati wa ziara yake ya kujionea maendeleo ya maandalizi ya Maonesho ya Nanenane Kitaifa yatakayofanyika Kanda ya Ziwa Mashariki katika Viwanja vya Nyakabindi mkoani Simiyu.
Waziri wa Kilimo, Mhe.Japhet Hasunga (mbele)akiangalia vipando vya nyanya vya Jeshi la kujenga Taifa(JKT), wakati wa ziara yake ya kujionea maendeleo ya maandalizi ya Maonesho ya Nanenane Kitaifa yatakayofanyika Kanda ya Ziwa Mashariki katika Viwanja vya Nyakabindi mkoani Simiyu.
Mkuu wa Wilaya ya Meatu, Dkt. Joseph Chilongani(kulia) akitoa maelezo kwa Waziri wa Kilimo, Mhe. Japhet Hasunga(mwenye suti) juu ya mashine iliyotengnezwa na mjasiriamali  Deke Ndabuli Maige kutoka Meatu(wa pili kushoto)yenye uwezo wa kupukuchua gunia 150 kwa siku.
Mkuu wa Wilaya ya Kahama, Mhe. Anamringi Macha akimuonesha jambo Waziri wa Kilimo, Mhe.Japhet Hasunga (wa pili kushoto) wakati wa ziara yake ya kujionea maendeleo ya maandalizi ya Maonesho ya Nanenane Kitaifa yatakayofanyika Kanda ya Ziwa Mashariki katika Viwanja vya Nyakabindi mkoani Simiyu.
Baadhi ya wananchi wakipewa elimu juu ya namna ya kutambua noti bandia katika banda la Benki Kuu ya Tanzania (BOT), ikiwa ni maandalizi ya  Maonesho ya Nanenane Kitaifa yatakayofanyika Kanda ya Ziwa Mashariki katika Viwanja vya Nyakabindi mkoani Simiyu.
Moja ya zana za kisasa zinazopaswa kutumiwa na wakulima ili kuongeza tija ya uzalishaji zilizopo katika Banda la Jeshi la kujenga Taifa(JKT), litakalooneshwa katika Maonesho ya Nanenane Kitaifa yatakayofanyika Kanda ya Ziwa Mashariki katika Viwanja vya Nyakabindi mkoani Simiyu..
Viatu vya ngozi vilivyotenegenezwa na Shirika la Uzalishaji Mali la SUMA JKT, ambavyo vitapatikana Maonesho ya Nanenane Kitaifa yatakayofanyika Kanda ya Ziwa Mashariki katika Viwanja vya Nyakabindi mkoani Simiyu

Baadhi ya kuku walio katika Banda la JKT katika Maonesho ya Nanenane Kitaifa yatakayofanyika Kanda ya Ziwa Mashariki katika Viwanja vya Nyakabindi mkoani Simiyu

Mtaalam wa JKT (kulia) akitoa maelezo juu ya namna ya kufuga asmaki kwenye matanki kwa Waziri wa Kilimo, Mhe.Japhet Hasunga (wa nne kulia) katika Viwanja vya Maonesho ya Nanenane Kitaifa yatakayofanyika Kanda ya Ziwa Mashariki katika Viwanja vya Nyakabindi mkoani Simiyu

Waziri wa Kilimo, Mhe.Japhet Hasunga akiangalia  asali inayotoka mkoani Mra, mara baada ya kutembelea mabanda ya mkoa wa Mara, wakati wa ziara yake ya kujionea maendeleo ya maandalizi ya Maonesho ya Nanenane Kitaifa yatakayofanyika Kanda ya Ziwa Mashariki katika Viwanja vya Nyakabindi mkoani Simiyu.

Baadhi ya mabanda ya maonesho yakiwa yamekamilika ikiwa ni hatua za mwisho za maandalizi ya Maonesho ya Nanenane Kitaifa yatakayofanyika Kanda ya Ziwa Mashariki katika Viwanja vya Nyakabindi mkoani Simiyu.
Kitalu nyumba cha Halmashauri ya Manispaa ya Musoma

Baadhi ya bidhaa za JKT zinazouzwa kwenye banda lao katika Maonesho ya Nanenane Kitaifa yatakayofanyika Kanda ya Ziwa Mashariki katika Viwanja vya Nyakabindi mkoani Simiyu.
Waziri wa Kilimo, Mhe.Japhet Hasunga akipewa maelezo kuhusu mbegu za zao la mtama, wakati wa ziara yake ya kujionea maendeleo ya maandalizi ya Maonesho ya Nanenane Kitaifa yatakayofanyika Kanda ya Ziwa Mashariki katika Viwanja vya Nyakabindi mkoani Simiyu.
Waziri wa Kilimo, Mhe.Japhet Hasunga akiangalia zao la mbogamboga aina ya kabichi katika vipando cya jeshi la Magereza, wakati wa ziara yake ya kujionea maendeleo ya maandalizi ya Maonesho ya Nanenane Kitaifa yatakayofanyika Kanda ya Ziwa Mashariki katika Viwanja vya Nyakabindi mkoani Simiyu.

Thursday, July 25, 2019

MAKAMU WA RAIS KUFUNGUA MAONESHO YA NANENANE KITAIFA 2019 MKOANI SIMIYU


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan anatarajia kuwa mgeni rasmi katika ufunguzi wa Maonesho ya Nanenane Kitaifa mwaka 2019, yatakayofanyika Kanda ya Ziwa Mashariki katika Viwanja vya Nyakabindi Mjini Bariadi kuanzia tarehe 29/07/2019 hadi 08/08/2019.

Hayo yamesemwa na Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka wakati akizungumza na waandishi wa habari  katika mkutano maalum wa kutoa taarifa kwa Umma uliofanyika  Mjini Bariadi, Julai 24, 2019.

Mtaka amesema Mhe Makamu wa Rais atafungua rasmi maonesho hayo Agosti Mosi, 2019 na waoneshaji mbalimbali zikiwemo Taasisi, Mashirika mbalimbali na wajasiriamali wataanza kuonesha teknolojia, huduma na bidhaa zao Julai 29, 2019 ikiwa ni maandalizi ya ufunguzi rasmi utakaofanywa na Mhe. Makamu wa Rais.

“Shughuli ya ufunguzi itafanywa tarehe 01/08/2019 na Mhe. Makamu wa Rai, haya ni maonesho ambayo yatakaribisha viongozi wa Kitaifa, Agosti 03, 2019 tutakuwa na Mhe. Waziri Mkuu, Agosti 06, 2019 tutakuwa na Waziri Mkuu Mstaafu, Mizengo Pinda na Kilele tunatarajia kuwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli” alisema.

Naibu Waziri wa Kilimo, Mhe. Omary Mgumba amesema ameridhishwa na maandalizi ya Maonesho ya nanenane yanayoendelea mkoani Simiyu na kutoa wito kwa wakulima na wananchi wote kwa ujumla kujitokeza kwa wingi kushiriki katika maonesho haya ili kuja kujionea teknolojia mbalimbali zitakazojibu changamoto za wakulima, wafugaji na wavuvi.

Aidha, Mhe. Mgumba ametoa wito kwa waoneshaji kuwa wabunifu katika teknolojia, huduma na bidhaa watakazoonesha ili maonesho haya yawe  chachu ya kuwasaidia wakulima, wavuvi na wafugaji  kuongeza tija katika uzalishaji

Naye Mkuu wa Mkoa wa Mara, Mhe. Adam Malima amesema matarajio ya mikoa ya Simiyu, Mara na Shinyanga inayounda Kanda ya Ziwa Mashariki ni kuwa na maonesho ya tofauti na mwaka jana, lengo likiwa ni kuifanya kanda hiyo kuwa ni mahali pa kudumu pa wakulima, wafugaji na wavuvi kuwa na maonesho ya kilimo biashara.

Maonesho ya Nanenane Kitaifa yanafanyika kwa mara ya pili sasa mkoani Simiyu tangu Kanda ya Ziwa ilipogawanywa katika kanda mbili yaani, Kanda ya Ziwa Mashariki(Simiyu, Mara na Shinyanga) na Kanda ya Ziwa Magharibi(Mwanza, Geita na Kagera) ambapo mwaka huu yanaadhimishwa chini ya kauli Mbiu:-“KILIMO, MIFUGO NA UVUVI KATIKA UKUAJI WA UCHUMI WA NCHI”
MWISHO
Naibu Waziri wa Kilimo, Mhe. Omary Mgumba (kulia) akikagua moja ya kitalu nyumba wakati wa ziara ya kukagua maandalizi ya Maonesho ya  Nanenane Kitaifa mwaka 2019 yatakayofanyika kuanzia Julai 28, 2019 Viwanja vya Nyakabindi Bariadi.
Mtaalam kutoka JKT (kulia) akitoa maelezo kwa Naibu Waziri wa Kilimo, Mhe. Omary Mgumba (katikati) wakati akikagua moja ya tanki la ufugaji wa samaki wakati wa ziara ya kukagua maandalizi ya Maonesho ya  Nanenane Kitaifa mwaka 2019 yatakayofanyika kuanzia Julai 28, 2019 Viwanja vya Nyakabindi Bariadi.
Naibu Waziri wa Kilimo, Mhe. Omary Mgumba (kulia) akikagua baadhi ya vipando wakati wa ziara ya kukagua maandalizi ya Maonesho ya  Nanenane Kitaifa mwaka 2019 yatakayofanyika kuanzia Julai 28, 2019 Viwanja vya Nyakabindi Bariadi.
Naibu Waziri wa Kilimo, Mhe. Omary Mgumba (kulia) akipokea maelezo kutoka kwa Afisa wa JKT akikagua baadhi ya vipando wakati wa ziara ya kukagua maandalizi ya Maonesho ya  Nanenane Kitaifa mwaka 2019 yatakayofanyika kuanzia Julai 28, 2019  Viwanja vya Nyakabindi Bariadi.
Baadhi ya vipando vilivyo katika Viwanja vya Maonesho ya  Nanenane Kanda ya Ziwa Mashariki vilivyopandwa kwa ajili ya maandalizi ya  Maonesho ya Nanenane Kitaifa mwaka 2019 .
Mtaalam kutoka JKT (kulia) akitoa maelezo kwa Naibu Waziri wa Kilimo, Mhe. Omary Mgumba (katikati) wakati akikagua moja ya Bwawa la ufugaji wa samaki wakati wa ziara ya kukagua maandalizi ya Maonesho ya  Nanenane Kitaifa mwaka 2019 yatakayofanyika kuanzia Julai 28, 2019 Viwanja vya Nyakabindi Bariadi.
Mtaalam kutoka JKT (kulia) akitoa maelezo kwa Naibu Waziri wa Kilimo, Mhe. Omary Mgumba wakati akikagua moja ya tanki la ufugaji wa samaki wakati wa ziara ya kukagua maandalizi ya Maonesho ya  Nanenane Kitaifa mwaka 2019 yatakayofanyika kuanzia Julai 28, 2019 Viwanja vya Nyakabindi Bariadi.
Mkuu wa Mkoa wa Mara, Mhe. Adam Kighoma Malima(kulia) akizungumza katika kikao cha Kamati ya maandalizi ya Maonesho ya Nanenane Kitaifa 2019 Kanda ya Ziwa Mashariki, kilichofanyika Julai 23, 2019 katika Viwanja vya Nyakabindi Bariadi, (kushoto) ni Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka.
Moja ya vipando vya mazao ya kilimo  katika viwanja vya Nanenane Nyakabindi 
Naibu Waziri wa Kilimo, Mhe. Omary Mgumba (kushoto) akiwa ameambatana na viongozi wengine wa Mkoa wa Simiyu na Wizara ya Kilimo wakati akikagua ujenzi wa majego ya kudumu katika VIwanja wa Nananenane Nyakabindi Bariadi

Naibu Waziri wa Kilimo, Mhe. Omary Mgumba akikagua vipando vya mazao ya iilimo katika viwanja vya Nanenane Nyakabindi, Julai 25, 2019.
Naibu Waziri wa Kilimo, Mhe. Omary Mgumba akikagua vipando vya mazao ya iilimo katika viwanja vya Nanenane Nyakabindi, Julai 25, 2019.


MAONESHO YA NANENANE KITAIFA 2019 YATABORESHWA ZAIDI YA MWAKA 2018: RC MARA


Mkuu wa Mkoa wa Mara, Mhe. Adam Malima amesema Mikoa ya Simiyu, Mara na Shinyanga inayounda Kanda ya Nanenane ya Ziwa Mashariki imekusudia kuboresha zaidi maonesho ya Nanenane Kitaifa mwaka 2019  ambayo yanafanyika kwa mara ya pili sasa katika kanda hii kwenye Viwanja vya Nyakabindi Bariadi Mkoani Simiyu.

Malima ameyasema hayo jana katika kikao maalum cha maandalizi cha Kanda hiyo kilichofanyika kwa lengo la kutathmini hali ya maandalizi ya maonesho hayo ambayo yanatarajia kuanza tarehe 29 Julai, 2019 na kuhitimishwa rasmi Agosti 08, 2019.

Amesema kanda imekusudia kuboresha upatikanaji wa huduma za maji, umeme na miundombinu mingine muhimu ikiwa ni pamoja na kuongeza majengo ya kudumu ili katika siku za usoni kanda ya Ziwa Mashariki iwe sehemu ya kudumu ya maonesho ya Kilimo Biashara.

“Mwaka huu tumekusudia kuboresha maonesho ya Nanenane Kitaifa kuliko mwaka jana 2018, tumekubaliana kuboresha upatikanaji wa huduma katika maeneo ya viwanja vua maonesho na pia  tunakusudia kuongeza upatikanaji wa majengo ya kudumu kwa sababu kwa kadri tunavyokwenda  tunatarajia hapa iwe ni sehemu ya Maonesho ya Kilimo Biashara kwa kanda hii” alisema

Naye Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka amesema Maonesho ya Nanenane mwaka 2019 yatakuwa na waoneshaji wengi wa teknolojia za kilimo kuliko miaka  iliyopia, hivyo akawahakikishia wananchi wote kuona teknolojia mbalimbali ikiwa ni pamoja na za upukuchuaji, utengenezaji wa chakula cha mifugo, ukataji majani ya mifugo, uvunaji na teknolojia nyingine nyingi.

Naye Mkurugenzi wa Maendeleo ya Mazao  Wizara ya Kilimo, Bw. Nyasebwa Chinagu amesema moja ya jukumu la wizara hiyo katika Maonesho haya ni kuhakikisha kuwa teknolojia sahihi zilizopo zinaoneshwa katika Maonesho ya nanenane ili wakulima, wafugaji na wavuvi waweze kupata maarifa na teknolojia sahihi katika kuongeza tija katika uzalishaji.

Maonesho ya haya yanatarajiwa kufunguliwa rasmi na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan na viongozi wengine wa Kitaifa watakuwepo katika siku maalum, akiwepo Waziri Mkuu wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa, Waziri Mkuu Mstaafu, Mhe. Mizengo Pinda na mgeni rasmi katika kilele cha maonesho haya anatarajiwa kuwa Rais wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli.

Maonesho ya Nanenane Kitaifa yanafanyika kwa mara ya pili sasa mkoani Simiyu chini ya kauli Mbiu:-“KILIMO, MIFUGO NA UVUVI KATIKA UKUAJI WA UCHUMI WA NCHI” tangu Kanda ya Ziwa ilipogawanywa katika kanda mbili yaani, Kanda ya Ziwa Mashariki(Simiyu, Mara na Shinyanga) na Kanda ya Ziwa Magharibi(Mwanza, Geita na Kagera).
MWISHO




Mkuu wa Mkoa wa Mara, Mhe. Adam Kighoma Malima akizungumza katika kikao cha Kamati ya maandalizi ya Maonesho ya Nanenane Kitaifa 2019 Kanda ya Ziwa Mashariki, kilichofanyika Julai 23, 2019 katika Viwanja vya Nyakabindi Bariadi.

Kutoka kushoto Mkuu wa Mkoa, Mhe. Anthony Mtaka, Mkuu wa Mkoa wa Mara, Adam Kighoma Malima wakimsikiliza Mkuu wa Wilaya ya Kahama, Mhe. Anamringi Macha katika kikao cha Kamati ya maandalizi ya Maonesho ya NanenaneKitaifa 2019  Kanda ya Ziwa Mashariki, kilichofanyika Julai 23, 2019 katika Viwanja vya Nyakabindi Bariadi.
Kutoka kulia Mkuu wa Wilaya ya Kahama, Mhe. Anamringi Macha, Mkuu wa Mkoa wa Mara, Adam Kighoma Malima wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa, Mhe. Anthony Mtaka katika kikao cha Kamati ya maandalizi ya Maonesho ya Nanenane 2019 yanayofanyika Kanda ya Ziwa Mashariki, kilichofanyika Julai 23, 2019 katika Viwanja vya Nyakabindi Bariadi.
Baadhi ya wajumbe wa kikao cha Kamati ya maandalizi ya Maonesho ya Nanenane Kitaifa mwaka 2019 yanayofanyika Kanda ya Ziwa Mashariki, kilichofanyika Julai 23, 2019 katika Viwanja vya Nyakabindi Bariadi.
Baadhi ya wajumbe  wa kikao cha Kamati ya maandalizi ya Maonesho ya Nanenane Kitaifa mwaka 2019 yanayofanyika Kanda ya Ziwa Mashariki, klichofanyika Julai 23, 2019 katika Viwanja vya Nyakabindi Bariadi.
Mkuu wa Mkoa wa Mara, Mhe. Adam Kighoma Malima(kulia) akizungumza katika kikao cha Kamati ya maandalizi ya Maonesho ya Nanenane Kitaifa 2019 Kanda ya Ziwa Mashariki, kilichofanyika Julai 23, 2019 katika Viwanja vya Nyakabindi Bariadi, (kushoto) ni Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka.
Baadhi ya vipando vya mazao ya kilimo vilivyopo katika Viwanja vya Nyakabindi Bariadi Simiyu
Naibu Waziri wa Kilimo, Mhe. Omary Mgumba akipewa maelezo ya ufugaji wa samaki katika banda la maonesho la JKT katika Viwanja vya Nyakabindi Bariadi.

Sunday, July 21, 2019

NEC KUANZA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA JULAI 31, MKOANI SIMIYU

Tume ya Taifa ya Uchaguzi inatarajia kuanza rasmi zoezi la Uboreshaji wa Daftari la kudumu la wapiga kura mkoani Simiyu kuanzia  Julai 31, 2019 hadi Agosti 06, 2019 ambapo zoezi hilo kitaifa  lilizinduliwa rasmi Julai 18, 2019.


Akifungua mkutano wa wadau wa Uchaguzi mkoani Simiyu, Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe Jaji wa Mahakama ya Rufaa, Semistocles Kaijage amesema  Tume imekamilisha maandalizi ya uboreshaji daftari ambayo ni pamoja na kuhakiki vituo vya kujiandikisha, uandikishaji wa majaribio, maandalizi ya vifaa vya uboreshaji daftari, mkakati wa elimu kwa mpiga kura na uzinduzi wa uboreshaji wa daftari la kudumu  la wapiga kura.

Amesema  uboreshaji huu hautawahusisha wapiga kura wote walioandikishwa kwenye daftari la kudumu la wapiga kura mwaka 2015 bali utawahusu wapiga kura wapya ambao wametimiza miaka 18, wale ambao watatimmiza.umri wa miaka 18 siku ya uchaguzi Mkuu mwaka 2020, ambao wamehama katika maeneo ya awali ya uchaguzi na wale ambao kadi zao zimeharibika

Katika hatua nyingine Jaji Kaijage ametoa rai kwa wananchi wote wenye sifa kujitokeza kwa wingi ili kuboresha taarifa zao, huku akitoa wito kwa viongozi wa vyama vya siasa,  kuzingatia sheria za uchaguzi na kanuni zake katika zoezi hili la uboreshaji na maelekezo kwa Vyama vya Siasa kuhusu uboreshaji.

Kwa upande wake Afisa TEHAMA Mwandamizi kutoka Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Bw. Frank Mhando amesema Tume imefanya uhakiki wa vituo vya uandikishaji ambavyo vimeongezeka kutoka 36,549 mwaka 2015 hadi 37,407 mwaka 2018 (Tanzania Bara), upande wa Tanzania Zanzibar vimeongezeka kutoka 380 mwaka 2015 hadi 407 mwaka 2018; huku akifafanua kuwa katika uandishaji huu kila Kijiji au Mtaa utakuwa na angalau Kituo kimoja cha kujiandikisha.

Naye Mratibu wa Zoezi la Uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura Mkoani Simiyu, Bw. Maganga Simon amesema mkoa umejiandaa vizuri ili kufanikisha zoezi ambapo wananchi wenye sifa zaidi ya 700,000 wanatarajia kuandikishwa katika daftari hilo huku akiwasisitiza viongozi wote mkoani hapo  kuwahamasisha wananchi wenye sifa kujitokeza kujiandikisha.

“Mkoa wetu ni mwenyeji wa Maonesho ya Nanenane Kitaifa mwaka2019, tutatumia fursa hiyo kuhamasisha, kutakuwa na bango kubwa litakaloonesha kuwa kuanza  Julai 31 hadi Agosti 6 2019 mkoa wetu utashiriki kikamilifu kwenye  zoezi la uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura na Simiyu tumejipanga kufanikisha zoezi hili ambalo linasimamiwa na Tume ya Taifa ya uchaguzi” alisema

Akizungumza kwa niaba ya watu wenye ulemavu,  Katibu wa Chama cha Viziwi (CHAVITA) Mkoa wa Simiyu, Alex Benson amewaomba viongozi wa vyama vya siasa kuwapa fursa watu wenye ulemavu kuwania nafasi mbalimbali, huku akisisitiza wasimamizi kupewa mafunzo ya lugha ya  alama ili kurahisisha mawasiliano  na watu wenye ulemavu pindi wanapoenda kujiandikisha na kupiga kura.

Naye Dora Stephano kutoka katika ASASI za kiraia amesema Tume ione uwezekano wa kuongeza ushirikishwaji wa asasi za kiraia nyingi zaidi, ili kuongeza wigo wa kutoa elimu kwa wapiga kura juu ya masuala mbalimbali ya uandikishaji na uchaguzi.

Mkutano wa wadau wa uchaguzi mkoani Simiyu, umewahusisha  Mratibu wa Uandikishaji wa Mkoa, Viongozi wa Vyama vya siasa Viongozi wa dini, wawakilishi wa watu wenye ulemavu, wawakilishi wa vijana, wawakilishi wa wanawake, wawakilishi wa asasi za kiraia, watendaji wa Tume na waandishi wa habari.
MWISHO
Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe Jaji  wa Mahakama ya Rufaa, Semistocles Kaijage akifungua Mkutano wa wadau wa Uchaguzi Mkoani Simiyu, uliofanyika julai 20, 2019 Mjini Bariadi.
Afisa TEHAMA Mwandamizi kutoka Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Bw. Frank Mhando akiwasilisha mada katika mkutano wa wadau wa uchaguzi Mkoani Simiyu, uliofanyika julai 20, 2019 Mjini Bariadi.
Baadhi ya viongozi wa dini, , viongozi wa asasi zisizosa Kiserikali na wawakilishi wa vijna , wanawake na watu wenye ulemavu wakifuatilia hotuba ya Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe Jaji  wa Mahakama ya Rufaa, Semistocles Kaijage(hayupo pichani) wakati akifungua Mkutano wa wadau wa Uchaguzi Mkoani Simiyu, Julai 20, 2019 Mjini Bariadi.
Baadhi ya viongozi wa dini, , viongozi wa asasi zisizosa Kiserikali na wawakilishi wa vijna , wanawake na watu wenye ulemavu wakifuatilia hotuba ya Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe Jaji  wa Mahakama ya Rufaa, Semistocles Kaijage(hayupo pichani) wakati akifungua Mkutano wa wadau wa Uchaguzi Mkoani Simiyu, Julai 20, 2019 Mjini Bariadi.
Baadhi ya viongozi wa Vyama vya siasa wakifuatilia hotuba ya Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe Jaji  wa Mahakama ya Rufaa, Semistocles Kaijage(hayupo pichani) wakati akifungua Mkutano wa wadau wa Uchaguzi Mkoani Simiyu, Julai 20, 2019 Mjini Bariadi.
Afisa TEHAMA Mwandamizi kutoka Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Bw. Frank Mhando akiwasilisha mada katika mkutano wa wadau wa uchaguzi Mkoani Simiyu, uliofanyika julai 20, 2019 Mjini Bariadi.
Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe Jaji  wa Mahakama ya Rufaa, Semistocles Kaijage akifungua Mkutano wa wadau wa Uchaguzi Mkoani Simiyu, uliofanyika Julai 20, 2019 Mjini Bariadi,(kulia) Mratibu wa Zoezi la Uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura Mkoani Simiyu, Bw. Maganga Simon.
Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe Jaji  wa Mahakama ya Rufaa, Semistocles Kaijage(katikati walioketi) akiwa katika picha ya pamoja viongozi wa dini mkoani Simiyu mara baada ya kufungua Mkutano wa wadau wa Uchaguzi Mkoani humo, uliofanyika Julai 20, 2019 Mjini Bariadi.
Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe Jaji  wa Mahakama ya Rufaa, Semistocles Kaijage(katikati walioketi) akiwa katika picha ya pamoja viongozi asasi mbalimbali za kiraia mkoani Simiyu mara baada ya kufungua Mkutano wa wadau wa Uchaguzi Mkoani humo, uliofanyika Julai 20, 2019 Mjini Bariadi.
Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe Jaji  wa Mahakama ya Rufaa, Semistocles Kaijage(katikati walioketi) akiwa katika picha ya pamoja waandishi wa habari mkoani Simiyu mara baada ya kufungua Mkutano wa wadau wa Uchaguzi Mkoani humo, uliofanyika Julai 20, 2019 Mjini Bariadi.
Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe Jaji  wa Mahakama ya Rufaa, Semistocles Kaijage(katikati walioketi) akiwa katika picha ya pamoja Viongozi wa Vyama vya siasa mkoani Simiyu mara baada ya kufungua Mkutano wa wadau wa Uchaguzi Mkoani humo, uliofanyika Julai 20, 2019 Mjini Bariadi.
Baadhi ya viongozi wa Vyama vya siasana asasi za kiraia  wakifuatilia hotuba ya Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe Jaji  wa Mahakama ya Rufaa, Semistocles Kaijage(hayupo pichani) wakati akifungua Mkutano wa wadau wa Uchaguzi Mkoani Simiyu, Julai 20, 2019 Mjini Bariadi.
Katibu wa itikadi na Uenezi wa CCM Mkoa wa Simiyu, Ndg. Mayunga George akichangia hoja katika Mkutano wa wadau wa Uchaguzi Mkoani Simiyu, uliofanyika julai 20, 2019 Mjini Bariadi.
Bi, Dora Stephano kutoka katika Asasi za Kiraia akichangia hoja katika Mkutano wa wadau wa Uchaguzi Mkoani Simiyu, uliofanyika Julai 20, 2019 Mjini Bariadi.




Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!