Sunday, July 14, 2019

DC BARIADI: WADAU WA AFYA ENDELEENI KUCHANGIA VITENDEA KAZI NA MIUNDOMBINU KUBORESHA HUDUMA ZA AFYA SIMIYU

Mkuu wa wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga amewaomba wadau wa afya waliopo mkoani Simiyu  kuendelea kuunga mkono juhudi za Serikali katika kuboresha huduma za afya  kwa kutenga bajeti kwa ajili ya kuchangia ununuzi wa vitendea kazi na  kujenga miundombinu ya afya.


Kiswaga amevitaja vitendea kazi hivyo kuwa ni pamoja na magari ya kubebea wagonjwa (ambulance), vifaa vya kwenye vituo vya afya ,zahanati na hospitali ili huduma ziendelee kutolewa kwa ufanisi mkubwa.

Ameyasema hayo katika kikao cha wadau wa afya kilichofanyika Mjini Bariadi wakati akimwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka kwenye kikao cha wadau wa afya kilichofanyika Julai 11 na Julai 12, 2019  kwenye ukumbi wa kanisa Katoliki mjini Bariadi.

Aidha ameongeza kuwa kuna kila sababu ya mashirika hayo kuongeza majengo na magari ili huduma za afya zizidi kuimarika mkoani hapo.

Pamoja na hayo amesema kuwa kama mkoa watahakikisha wanatoa ushirikiano wa kutosha kwa wadau wa afya mkoani hapo ili waweze kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi zaidi.

"kila shirika lililopo mkoani hapa linafanya kazi nzuri endeleeni kuzidisha juhudi hizo  bado tuna upungufu wa vitendea kazi , tunaomba muendelee kutafuta fedha huko ili kuhakikisha kwamba vitendea kazi kama magari, magari ya kubebea wagonjwa lakini pia majengo bado ni changamoto pamoja na kazi kubwa nzuri ambazo mmezifanya tunaombeni muendelee kuweka bajeti hizo "alisema Kiswaga na kuongeza kuwa:

“kama mkoa  tutahakikisha mashirika haya yanatekeleza majukumu yake bila wasiwasi wowote , watendaji kuanzia ngazi za chini sitegemei kusikia shirika limeshindwa kutekeleza shughuli zake eti kisa mtendaji kakwamisha , watendaji kuanzia ngazi ya chini hakikisheni mnatoa ushirikiano wa kutosha ili mashirika haya yatekeleze majukumu yake”aliongeza Kiswaga

Kwa upande wake Mwenyekiti wa wadau wa afya mkoani hapa Dkt Amiri Batenga ambaye ni mwakilishi wa shirika la umoja wa kimataifa linaloshughulikia idadi ya watu duniani UNFPA mkoa wa Simiyu amesema kuwa wameendelea kuboresha vituo vya kutolea huduma za afya lengo likiwa kupunguza vifo vya kina mama wajawazito na watoto wachanga.

Aidha, Dkt. Batenga ameongeza kuwa wameshatumia kiasi cha bilioni tano na nusu kwa ajili ya ujenzi na ukarabati wa majengo ,vifaa pamoja na magari mkoani Simiyu huku akiomba Serikali kuendele kusimamia na kuhakikisha vituo na vifaa hivyo vinafanya kazi iliyokusudiwa na wananchi waone haja ya kutumia vituo hivyo maana vimejwngwa kwa ajili yao.

“kujenga vituo vya afya ,kuweka vifaa na kufundisha watumishi ni jambo jingine vituo hivi vinatakiwa vitumike kina mama wajawazito wasipotumia hivi vituo yale malengo hayawezi fikiwa  …pale tumejenga vituo 38 nasasa hivi tumeongeza vingine viwili ili kufikia malengo lazima mama aje pale tukiunganisha nguvu ya pamoja  kina mama wakafika kwenye vituo vya afya vifo vitaisha kabisa”  alisema Batenga

Mkoa wa Simiyu una zaidi ya mashirika 17 yanayofanya kazi bega kwa bega na mkoa yakiwa na lengo la kuunga mkono juhudi za serikali katika sekta mbalimbali ikiwemo afya na elimu.
MWISHO




Mkuu wa wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga akizungumza na wadau wa afya mkoani Simiyu wakati akifungua kikao cha wadau hao, kwa niaba ya Mkuu wa mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka kilichofanyika Mjini Bariadi JulaI 11 na 12, 2019.

Mratibu wa Shughuli za Kudhiti na kupambana na UKIMWI, Dkt. Khamis Kulemba akiwasilisha mada katika kikao cha wadau wa afya, kilichofanyika kilichofanyika Mjini Bariadi JulaI 11 na 12, 2019.

Mwakilishi wa Shirika la DOCTOR WITH AFRICA akiwasilisha mada katika kikao cha wadau wa afya, kilichofanyika kilichofanyika Mjini Bariadi JulaI 11 na 12, 2019.
Baadhi ya viongozi na wadau wa afya mkoani Simiyu wakimsikiliza Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga, katika kikao cha wadau hao, kwa niaba ya Mkuu wa mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka kilichofanyika Mjini Bariadi JulaI 11 na 12, 2019.
Afisa Lishe wa Mkoa wa Simiyu, Dkt. Chacha Magige akiwasilisha mada kuhusu hali ya lishe katika mkoa, kwenye kikao cha wadau wa afya, kilichofanyika kilichofanyika Mjini Bariadi JulaI 11 na 12, 2019.
Baadhi ya viongozi na wadau wa afya mkoani Simiyu wakimsikiliza Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga, katika kikao cha wadau hao, kwa niaba ya Mkuu wa mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka kilichofanyika Mjini Bariadi JulaI 11 na 12, 2019.
Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bw. Donatus Weginah akizungumza kabla ya kumkaribisha Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga kufungua kikao cha wadau wa afya mkoa wa Simiyu kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa, Mhe. Anthony Mtaka kilichofanyika Mjini Bariadi JulaI 11 na 12, 2019.
Mwakilishi wa Shirika lisilo la kiserikali la AMREF zlinaloanya kazi zake mkoani SImiyu, akiwasilisha mada katika kikao cha wadau wa afya, kilichofanyika kilichofanyika Mjini Bariadi JulaI 11 na 12, 2019.
Mwakilishi wa Shirika lisilo la kiserikali la CUAMM zlinaloanya kazi zake mkoani SImiyu, akiwasilisha mada katika kikao cha wadau wa afya, kilichofanyika kilichofanyika Mjini Bariadi JulaI 11 na 12, 2019.
Mwakilishi wa Shirika lisilo la kiserikali la AMREF zlinaloanya kazi zake mkoani SImiyu, akiwasilisha mada katika kikao cha wadau wa afya, kilichofanyika kilichofanyika Mjini Bariadi JulaI 11 na 12, 2019.
Baadhi ya viongozi na wadau wa afya mkoani Simiyu wakimsikiliza Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga, katika kikao cha wadau hao, kwa niaba ya Mkuu wa mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka kilichofanyika Mjini Bariadi JulaI 11 na 12, 2019.
Baadhi ya viongozi na wadau wa afya mkoani Simiyu wakimsikiliza Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga, katika kikao cha wadau hao, kwa niaba ya Mkuu wa mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka kilichofanyika Mjini Bariadi JulaI 11 na 12, 2019.
Mwenyekiti wa wadau wa afya mkoani Simiyu, Dkt Amiri Batenga ambaye ni mwakilishi wa shirika la umoja wa kimataifa linaloshughulikia idadi ya watu duniani (UNFPA)mkoa wa Simiyu, akiwasilisha mada katika kikao cha wadau wa afya, kilichofanyika kilichofanyika Mjini Bariadi JulaI 11 na 12, 2019.
Mganga Mkuu wa Halmashauri ya mji wa Bariadi, Dkt. Mike Mabimbi akichangia hoja katika kikao cha wadau wa afya, kilichofanyika kilichofanyika Mjini Bariadi JulaI 11 na 12, 2019.
Baadhi ya viongozi na wadau wa afya mkoani Simiyu wakimsikiliza Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga, katika kikao cha wadau hao, kwa niaba ya Mkuu wa mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka kilichofanyika Mjini Bariadi JulaI 11 na 12, 2019.
Mkuu wa wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga akizungumza na wadau wa afya mkoani Simiyu wakati akifunga kikao cha wadau hao, kwa niaba ya Mkuu wa mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka kilichofanyika Mjini Bariadi JulaI 11 na 12, 2019.

0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!