Friday, June 26, 2020

AGPAHI, RUWASA WATOA MSAADA WA VIFAA KWA AJILI YA TAHADHARI YA MAAMBUKIZI YA CORONA SIMIYU


Shirika lisilo la Kiserikali la AGPAHI limetoa msaada wa jumla ya vifaa 50 vya kupima joto mwili vyenye thamani ya shilingi 12,500,000/= kwa mkoa wa Simiyu kwa ajili ya kuendelea kuchukua tahadhari dhidi ya maambukizi ya Virusi vya Corona.

Awali akizungumza kabla ya kukabidhi vifaa hivyo Mratibu wa AGPAHI Mkoa wa Simiyu, Dkt. Julius Sipemba amesema Shirika hilo limefuata maelekezo ya Serikali katika utoaji wa misaada ambapo amebainisha kuwa vifaa hivyo vimepitia wizara ya afya na kupata kibali cha kuvigawa katika mikoa ili vipelekwe katika vituo vya kutolea huduma.

Akipokea msaada huo kwa niaba ya serikali Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bw. Jumanne Sagini ameishukuru AGPAHI kwa kutoa vifaa vya kupima joto mwili na kusema kuwa awali Mkoa huo ulikuwa na uhaba wa vifaa hivyo; huku akibainisha kuwa vifaa hivyo vitasaidia hususani kwenye maeneo ambayo yalikuwa hayana ili kuwapima watu joto mwili kabla ya kuingia kwenye maeneo hayo.
Wakati huo huo Sagini ameushukuru Wakala wa Usambazaji Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) Mkoa wa Simiyu kwa msaada wa vifaa vya kunawia mikono kuunga mkono juhudi za serikali, katika kuchukua tahadhari ya maambukizi ya Virusi vya Corona na kusisitiza kuwa vifaa hivyo vitapelekwa katika maeneo yenye mkusanyiko wa watu wengi.

“RUWASA ni taasisi mpya lakini pamoja na upya wake wamejinyima na kutoa shilingi 1,750,000/= kununua vifaa hivi ili kuokoa maisha ya watu; pamoja na kuhakikisha tunapata maji safi na salama wameona waunge mkono juhudi za serikali kuhakikisha watu wananawa na sabuni na maji tiririka kujikinga na Corona, mkoa tunatambua mchango wenu,” alisema Sagini.

Akizungumza kwa niaba ya Meneja wa RUWASA Mkoa wa Simiyu, Mhandisi Mahobe Mahuyemba amesema RUWASA kama wakala mpya umetoa msaada huo ikiwa ni sehemu ya kuonesha uhusiano wake na jamii katika kile kinachofanyika katika utekelezaji wa miradi m ya maji na uhalisia wa maisha ya watu  huku akisisitiza kuwa vifaa hivyo kupelekwa katika maeneo yenye mikusanyiko ya watu ikiwemo shule na hospitali.

Kwa upande wake Mganga Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Dkt. Festo Dugange amewashukuru AGPAHI na RUWASA kwa msaada huo kwa jamii ya watu wa Simiyu huku akibainisha namna mkoa wa Simiyu ulivyonufaika na uwepo wa AGPAHI kama wadau muhimu wa afya.

“Kama mkoa tumekuwa tukishirikiana na AGPAHI kuboresha  huduma za afya katika nyanja mbalimbali ikiwemo kuboresha huduma za afya kwa watu wanaoishi na Virusi vya UKIMWI kwa kutoa huduma za matibabu, kujenga uwezo kwa watoa huduma wanaowahudumia, kutoa magari kwa ajili ya usimamizi shirikishi na kujenga miundombinu yakiwemo majengo,” amesema Dkt. Dugange.
MWISHO

 Mratibu wa Shirika lisilo la kiserikali la AGPAHI Mkoa wa Simiyu, Dkt. Julius Sipemba (kushoto) akimuonesha Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bw. Jumanne Sagini moja ya kifaa cha kupima joto mwili ambavyo vimetolewa msaada Juni 25, 2020  na Shirika hilo kwa mkoa wa Simiyu ili kuunga mkono juhui za Serikali katika tahadhari ya maambukizi ya virusi vya Corona.


 Mratibu wa Shirika lisilo la kiserikali la AGPAHI Mkoa wa Simiyu, Dkt. Julius Sipemba (kushoto) akimuonesha Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bw. Jumanne Sagini moja ya kifaa cha kupima joto mwili ambavyo vimetolewa msaada Juni 25, 2020  na Shirika hilo kwa mkoa wa Simiyu ili kuunga mkono juhui za Serikali katika tahadhari ya maambukizi ya virusi vya Corona.


 Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bw. Jumanne Sagini (wan ne kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya viongozi na watumishi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, AGPAHI na Wakala wa Usambazaji Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) mkoa wa Simiyu mara baada ya kupokea msaada wa vifaa vya kupima joto mwili kutoka AGPAHI na vifaa vya kunawia mikono Juni 25, 2020 kutoka RUWASA kwa ajili ya tahadhari ya maambukizi ya CORONA.


 Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bw. Jumanne Sagini akinawa mikono kwa sabuni na maji tiririka katika moja ya vifaa vilivyotolewa msaada na Wakala wa Usambazaji Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) mkoa wa Simiyu kwa ajili ya kuendelea kuchukua tahadhari dhidi ya CORONA, Kulia ni Mhandisi kutoka  RUWASA Simiyu Mahobe Mahuyemba.


 Sehemu ya msaada wa vifaa vya kunawia mikono vilivyotolewa kama msaada kwa mkoa wa Simiyu Juni 25, 2020  na Wakala wa Usambazaji Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) mkoa wa Simiyu kwa ajili ya kuendelea kuchukua tahadhari dhidi ya CORONA.


 Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bw. Jumanne Sagini akivikagua  vifaa vilivyotolewa msaada kwa mkoa huo na Wakala wa Usambazaji Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) mkoa wa Simiyu  kwa ajili ya kuendelea kuchukua tahadhari dhidi ya CORONA, kulia ni Mhandisi kutoka  RUWASA Simiyu Mahobe Mahuyemba.


 Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bw. Jumanne Sagini (wa tano kulia) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya viongozi na watumishi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, AGPAHI na Wakala wa Usambazaji Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) mkoa wa Simiyu mara baada ya kupokea msaada wa vifaa vya kupima joto mwili kutoka AGPAHI na vifaa vya kunawia mikono Juni 25, 2020 kutoka RUWASA kwa ajili ya tahadhari ya maambukizi ya CORONA.


 Mganga Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Dkt. Festo Dugange akimpima joto  Mhandisi kutoka  RUWASA Simiyu Mahobe Mahuyemba kwa kutumia kifaa cha kupimia joto mwili ambacho ni miongoni mwa vifaa hivyo 50 vilivyotolewa msaada na AGPAHI Juni 25, 2020 kwa ajili kuendelea kuchukua tahadhari dhidi ya maambukizi ya CORONA.


 Mratibu wa Shirika lisilo la kiserikali la AGPAHI Mkoa wa Simiyu, Dkt. Julius Sipemba (kushoto) akimuonesha Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bw. Jumanne Sagini moja ya kifaa cha kupimia joto mwili ambavyo vimetolewa msaada Juni 25, 2020  na Shirika hilo kwa mkoa wa Simiyu ili kuunga mkono juhui za Serikali katika tahadhari ya maambukizi ya virusi vya Corona.
Mratibu wa Shirika lisilo la kiserikali la AGPAHI Mkoa wa Simiyu, Dkt. Julius Sipemba (kushoto) akimuonesha Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bw. Jumanne Sagini moja ya kifaa cha kupimia joto mwili ambavyo vimetolewa msaada Juni 25, 2020  na Shirika hilo kwa mkoa wa Simiyu ili kuunga mkono juhui za Serikali katika tahadhari ya maambukizi ya virusi vya Corona.

Wednesday, June 24, 2020

MSD YAJIPANGA KUJENGA KIWANDA CHA KUTENGENEZA GOZI NA BANDEJI

Bohari ya Dawa (MSD) inatarajia kujenga kiwanda cha kutengeneza bidhaa za afya zitokanazo na pamba hususani gozi na bandeji katika Mkoa wa Simiyu.

Hayo yamebainishwa na Mkurugenzi Mkuu wa MSD , Brigedia Jenerali  Dkt. Gabriel Mhidze  wakati wa ziara yake aliyoifanya Juni 24, 2020 mkoani Simiyu kwa lengo  kukutana na viongozi wa mkoa, kuangalia eneo la ujenzi wa kiwanda hicho na kutembelea moja ya viwanda vya kuchambua pamba wilayani Bariadi.

“Kama MSD tutatengeneza gozi, bandeji zile ndogo za vidonda na hata zile pamba za masikioni lakini tutaanza kwa awamu kwanza, lakini naamini bidhaa nyingine za pamba pia tutazitengeneza,” alisema Dkt. Mhidze.

Aidha, Dkt. Mhidze amesema kwa sasa bidhaa hizo zinaagizwa kutoka nje ya nchi hivyo ikiwa zitaanza kuzalishwa hapa nchini kutakuwa na soko la uhakika la bidhaa hizo (vifaa tiba).

Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga amesema viongozi wote watatoa ushirikiano wote unaotakiwa na MSD huku akimhakikishia Mkurugenzi Mkuu wa MSD upatikanaji wa nguvu kazi kwa kiwanda hicho.

Kwa upande wake Meneja wa Kiwanda cha kuchambua pamba cha Alliance Ginneries Limited kilichopo kata ya Kasoli wilayani Bariadi, Bw. Boaz Ogolla amemhakikishia Mkurugenzi Mkuu wa MSD upatikanaji wa malighafi ambayo ni pamba hai kutoka kwa wachambuzi wa pamba (ginners ) wa ndani ya nchi na hususani Mkoa wa Simiyu.
MWISHO




 Meneja wa Kiwanda cha kuchambua pamba cha Alliance Ginneries Limited kilichopo kata ya Kasoli wilayani Bariadi, Bw. Boaz Ogolla(kulia) akimuonesha Mkurugenzi Mkuu wa MSD , Brigedia Jenerali  Dkt. Gabriel Mhidze  aina ya pamba inayoweza kutumika kutengeneza vifaa tiba/bidhaa za afya zitokanazo na pamba wakati wa ziara yake kiwandani hapo Juni 23,2020
 Meneja wa Kiwanda cha kuchambua pamba cha Alliance Ginneries Limited kilichopo kata ya Kasoli wilayani Bariadi, Bw. Boaz Ogolla(kulia) akitoa maelezo kwa Mkurugenzi Mkuu wa MSD , Brigedia Jenerali  Dkt. Gabriel Mhidze (wa pili kulia mbele) wakati alipotembelea kiwanda hicho Juni 23, 2020.
 Meneja wa Kiwanda cha kuchambua pamba cha Alliance Ginneries Limited kilichopo kata ya Kasoli wilayani Bariadi, Bw. Boaz Ogolla (kushoto) akimuongoza Mkurugenzi Mkuu wa MSD, Brigedia Jenerali  Dkt. Gabriel Mhidze (wa pili kulia) na viongozi wengine wakati alipotembelea kiwanda hicho Juni 23, 2020.
 Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga akitoa taarifa kwa Mkurugenzi Mkuu wa MSD , Brigedia Jenerali  Dkt. Gabriel ajili Mhidze (wa pili kushoto ) na viongozi wengine mara baada ya kuwasili Mjini Bariadi Juni 23, 2020 kwa ya kuangalia mazingira ya ujenzi wa kiwanda cha kutemgeneza bidhaa za afya zitokanazo na pamba.
 Mkurugenzi Mkuu wa MSD , Brigedia Jenerali  Dkt. Gabriel ajili Mhidze (kulia) akizungumza na Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga mara baada ya kuwasili Mjini Bariadi Juni 23, 2020 kwa ya kuangalia mazingira ya ujenzi wa kiwanda cha kutemgeneza bidhaa za afya zitokanazo na pamba.
 Mkurugenzi Mkuu wa Bohari ya Dawa (MSD) , Brigedia Jenerali Dkt. Gabriel ajili Mhidze (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na viongozi na baaadhi ya watendaji wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, mara baada ya kuhitimisha mazungumzo na viongozi hao wakati wa ziara yake Mkoani Simiyu Juni 23, 2020.
 Meneja wa Kiwanda cha kuchambua pamba cha Alliance Ginneries Limited kilichopo kata ya Kasoli wilayani Bariadi, Bw. Boaz Ogolla akimuongoza Mkurugenzi Mkuu wa MSD, Brigedia Jenerali Dkt. Gabriel Mhidze na viongozi wengine wakati alipotembelea kiwanda hicho Juni 23, 2020.
 Mkurugenzi Mkuu wa Bohari ya Dawa (MSD), Brigedia Jenerali  Dkt. Gabriel Mhidze (wa pili kulia) akimweleza jambo Meneja wa Kiwanda cha kuchambua pamba cha Alliance Ginneries Limited kilichopo kata ya Kasoli wilayani Bariadi, Bw. Boaz Ogolla wakati alipotembelea kiwanda hicho Juni 23, 2020 kuona hali ya upatikanaji wa malighafi kwa ajili ya kiwanda cha bidhaa za afya zitokanazo na pamba.
 Meneja wa Kiwanda cha kuchambua pamba cha Alliance Ginneries Limited kilichopo kata ya Kasoli wilayani Bariadi, Bw. Boaz Ogolla (katikati) akimuongoza Mkurugenzi Mkuu wa MSD, Brigedia Jenerali  Dkt. Gabriel Mhidze (wa tatu kushoto) na viongozi wengine wakati alipotembelea kiwanda hicho Juni 23, 2020.
 Meneja wa Kiwanda cha kuchambua pamba cha Alliance Ginneries Limited kilichopo kata ya Kasoli wilayani Bariadi, Bw. Boaz Ogolla(kulia) akitoa maelezo kwa Mkurugenzi Mkuu wa Bohari ya Dawa (MSD) , Brigedia Jenerali  Dkt. Gabriel Mhidze (wa pili kulia mbele) wakati alipotembelea kiwanda hicho Juni 23, 2020.
 Meneja wa Kiwanda cha kuchambua pamba cha Alliance Ginneries Limited kilichopo kata ya Kasoli wilayani Bariadi, Bw. Boaz Ogolla (katikati) akitoa maelezo kwa Mkurugenzi Mkuu wa MSD , Brigedia Jenerali  Dkt. Gabriel Mhidze (wa pili kulia) wakati alipotembelea kiwanda hicho Juni 23, 2020.
 Meneja wa Kiwanda cha kuchambua pamba cha Alliance Ginneries Limited kilichopo kata ya Kasoli wilayani Bariadi, Bw. Boaz Ogolla (kulia) akitoa maelezo kwa Mkurugenzi Mkuu wa MSD , Brigedia Jenerali  Dkt. Gabriel Mhidze (wa tatu kulia) wakati alipotembelea kiwanda hicho Juni 23, 2020.
 Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga(wa tatu kulia) akimueleza jambo Mkurugenzi Mkuu wa Bohari ya Dawa (MSD) , Brigedia Jenerali  Dkt. Gabriel Mhidze (wa pili kulia mbele) wakati alipotembelea kiwanda cha kuchambua pamba cha Alliance Ginneries Limited kilichopo kata ya Kasoli wilayani Bariadi, Juni 23, 2020.

Meneja wa Kiwanda cha kuchambua pamba cha Alliance Ginneries Limited kilichopo kata ya Kasoli wilayani Bariadi, Bw. Boaz Ogolla(kulia) akimuonesha Mkurugenzi Mkuu wa MSD , Brigedia Jenerali  Dkt. Gabriel Mhidze  aina ya pamba inayoweza kutumika kutengeneza vifaa tiba/bidhaa za afya zitokanazo na pamba wakati wa ziara yake kiwandani hapo Juni 23,2020

Tuesday, June 23, 2020

WANANCHI SIMIYU WAIPONGEZA SERIKALI KUWAJENGEA MAHAKAMA


Wananchi wa Wilaya ya Bariadi Mkoani Simiyu wameipongeza Serikali kwa kuwajengea mahakama ya Wilaya ya Bariadi na Mahakama ya Hakimu Mkazi Simiyu jambo ambalo limeapunguzia adha ya kutumia gharama na muda mrefu kwenda kufuata huduma za mahakama katika mkoa wa Shinyanga kama ilivyokuwa awali.

Akizungumza katika hafla ya uzinduzi wa jengo la mahakama ya Hakimu Mkazi Simiyu na Mahakama ya Wilaya ya Bariadi ambayo ilifanyika Juni 22, 2020 Mjini Bariadi, Bw. Zengila Nyoni mkazi wa Bariadi ameomba watumishi wa mahakama kutoa huduma kwa kuzingatia misingi ya haki ili umuhimu wa uwepo wa mahakama uonekane kwa wananchi.

“Tunaishukuru Serikali kutujenge jengo zuri la mahakama, sasa hivi hatutasafiri kwenda Shinyanga kufuata huduma za mahakama ya hakimu mkazi ni hapa hapa tu; niwaombe mahakimu na majaji kutoa haki kwa wananchi ili tufurahie uwepo wa jengo hili zuri, maana haitakuwa na faida kama tumejengewa jengo zuri halafu huduma zisiwe nzuri,”alisema Nyoni.

Awali akizungumza katika uzinduzi huo Jaji kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Dkt. Eliezer Feleshi amewashauri Wakuu wa Wilaya na Mikoa nchini  kutumia kamati za maadili za wilaya ambazo wao ni wenyeviti wa kamati hizo kuwajadili mahakimu ambao wanaenda kinyume na maadili ya utumishi wa Umma.

 “ Ni aibu kwa Mkuu wa Wilaya au Mkuu wa Mkoa kusema kuwa hamtaki hakimu fulani kwenye eneo lake wakati  yeye ndiyo mwenyekiti wa kamati ya maadili ya wilaya au mkoa, mahakimu wasio waadilifu wafikisheni kwenye kamati za maadili, zile kamati zinajuimisha watu wengi wazuri; niendelee kuwasihi watumishi wa Mahakama kujiepusha na vitendo vilivyo kinyume na maadili,” alisea Jaji Feleshi.


Jaji kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Dkt. Eliezer Feleshi(katikati) akikata utepe kuashiria uzinduzi wa jengo la mahakama ya wilaya ya Bariadi na mahakama Hakimu mkazi Simiyu, uzinduzi uliofanyika Mjini Bariadi Juni 22, 2020.
 Jaji kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Dkt. Eliezer Feleshi(katikati) akifungua kitambaa kuashiria uzinduzi wa jengo la mahakama ya wilaya ya Bariadi na mahakama Hakimu mkazi Simiyu, uzinduzi  uliofanyika Mjini Bariadi Juni 22, 2020.
 Jaji kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Dkt. Eliezer Feleshi akizungumza na viongozi mbalimbali, watumishi wa mahakama na wananchi katika hafla ya uzinduzi wa jengo la mahakama ya wilaya ya Bariadi na mahakama Hakimu mkazi Simiyu, uzinduzi uliofanyika Mjini Bariadi Juni 22, 2020.
 Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga akitoa salamu za Mkoa wa Simiyu kwa niaba ya mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka katika hafla ya uzinduzi wa jengo la mahakama ya wilaya ya Bariadi na mahakama Hakimu mkazi Simiyu, uzinduzi uliofanyika Mjini Bariadi Juni 22, 2020.
 Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Shinyanga, Mhe. Gerson Mdemu akizungumza na viongozi mbalimbali, watumishi wa mahakama na wananchi katika hafla ya uzinduzi wa jengo la mahakama ya wilaya ya Bariadi na mahakama Hakimu mkazi Simiyu, uzinduzi uliofanyika Mjini Bariadi Juni 22, 2020.
 Baadhi ya mahakimu na watumishi wengine wa mahakama mkoani Simiyu wakifurahia jambo katika hafla ya uzinduzi wa jengo la mahakama ya wilaya ya Bariadi na mahakama Hakimu mkazi Simiyu, uzinduzi uliofanyika Mjini Bariadi Juni 22, 2020.
 Baadhi ya Viongozi wakifuatilia kwa makini matukio mbalimbali katika hafla ya uzinduzi wa jengo la mahakama ya wilaya ya Bariadi na mahakama Hakimu mkazi Simiyu, uzinduzi uliofanyika Mjini Bariadi Juni 22, 2020.

Jaji kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Dkt. Eliezer Feleshi(katikati walioketi) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya viongozi katika mhimili wa mahakama na mahakimu wa Mahakama mbalimbali mkoani Simiyu(waliosimama) baada ya uzinduzi wa jengo la mahakama ya wilaya ya Bariadi na mahakama Hakimu mkazi Simiyu, uzinduzi uliofanyika Mjini Bariadi Juni 22, 2020.
 Katibu wa Itikani na Uenezi wa CCM Mkoa wa Simiyu, Bw. Mayunga George akitoa salamu za Chama katika hafla ya uzinduzi wa jengo la mahakama ya wilaya ya Bariadi na mahakama Hakimu mkazi Simiyu, uzinduzi uliofanyika Mjini Bariadi Juni 22, 2020.
 Baadhi ya Viongozi wakifuatilia kwa makini matukio mbalimbali katika hafla ya uzinduzi wa jengo la mahakama ya wilaya ya Bariadi na mahakama Hakimu mkazi Simiyu, uzinduzi uliofanyika Mjini Bariadi Juni 22, 2020.
 Baadhi ya Viongozi wakifuatilia kwa makini matukio mbalimbali katika hafla ya uzinduzi wa jengo la mahakama ya wilaya ya Bariadi na mahakama Hakimu mkazi Simiyu, uzinduzi uliofanyika Mjini Bariadi Juni 22, 2020.
 Jaji kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Dkt. Eliezer Feleshi akiwaeleza jambo baadhi ya watumishi wa mahakama wakati alipopita kukagua jengo la jengo la mahakama ya wilaya ya Bariadi na mahakama Hakimu mkazi Simiyu,  katika hafla ya uzinduzi wa  wa jengo hilo uliofanyika Mjini Bariadi Juni 22, 2020. 
 Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Shinyanga, Mhe. Gerson Mdemu(kushoto akimuongoza Jaji kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Dkt. Eliezer Feleshi kuelekea katika eneo maalum lililoandaliwa kwa ajili ya kuzindua jengo la mahakama ya wilaya ya Bariadi na mahakama Hakimu mkazi Simiyu, uzinduzi uliofanyika Mjini Bariadi Juni 22, 2020.
 Baadhi ya viongozi wa taasisi, watumishi wa mahakama na wananchi wakifuatilia kwa makini matukio mbalimbali katika hafla ya uzinduzi wa jengo la mahakama ya wilaya ya Bariadi na mahakama Hakimu mkazi Simiyu, uzinduzi uliofanyika Mjini Bariadi Juni 22, 2020.
 Baadhi ya viongozi wakiwa katika hafla ya uzinduzi wa jengo la mahakama ya wilaya ya Bariadi na mahakama Hakimu mkazi Simiyu, uzinduzi uliofanyika Mjini Bariadi Juni 22, 2020.
 Jaji kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Dkt. Eliezer Feleshi(katikati walioketi) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya viongozi katika mhimili wa mahakama na (waliosimama) baada ya uzinduzi wa jengo la mahakama ya wilaya ya Bariadi na mahakama Hakimu mkazi Simiyu, uzinduzi uliofanyika Mjini Bariadi Juni 22, 2020.
 Sehemu ya mbele ya jengo la mahakama ya wilaya ya Bariadi na mahakama Hakimu mkazi Simiyu, lililozinduliwa na Jaji kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Dkt. Eliezer Feleshi Mjini Bariadi Juni 22, 2020.
Jaji kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Dkt. Eliezer Feleshi (wa pili kushoto) akipokea maelezo kutoka kwa mmoja wa watumishi kuhusu jengo la mahakama ya wilaya ya Bariadi na mahakama Hakimu mkazi Simiyu, baada ya uzinduzi wa jengo hilo uliofanyika Mjini Bariadi Juni 22, 2020.

Friday, June 19, 2020

CUAMM YAJENGA JENGO LA HUDUMA KWA WATU WENYE VVU SIMIYU


Shirika lisilo la kiserikali la CUAMM Doctors With Africa kupitia Mradi wa Test and Treat limejenga jengo jipya la huduma za tiba na matunzo kwa watu wenye maambukizi ya Virusi vya Ukimwi, kukarabati baadhi ya majengo na kuchimba kisima cha maji  katika zahanati ya Old Maswa iliyopo Halmashauri ya Mji wa Bariadi mkoani Simiyu.

Akizungumza katika hafla ya uzinduzi wa jengo hilo (katika zahanati ya Old Maswa  inayomilikiwa na  Jimbo Katoliki Shinyanga)   Juni 18, 2020  kwa niaba ya Askofu wa Jimbo Katoliki Shinyanga, Liberatus Sangu,  Makamu wa Askofu huyo Padri Kizito Nyanga,  ameishukuru CUAMM Doctors with Africa kwa msaada huo na kuahidi kuendelea kushirikiana na Serikali na wadau wote walio tayari kuhudumia watu.

“Tunawashukuru sana CUAMM kwa msaada wa jengo hili, vifaa na ukarabati wa majengo mengine katika zahanati ya Old Maswa; Kanisa lina kiu ya kuwafikia watu kwa huduma siyo maneno na liko tayari kushirikiana na wote wanaotaka kuwahudumia watu,” alisema Padri Nyanga.

Aidha, Padri Kizito ameishukuru serikali kwa kuliamini kanisa hususani jimbo Katoliki Shinyanga, kuliamini kanisa katika kutoa huduma kwa wananchi, kulidhamni katika kuendeleza huduma na kutoa ushauri wa mara kwa mara katika uendeshaji wa taasisi za kanisa.

Akizungumza kwa niaba ya Serikali katika uzinduzi wa jengo hilo Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Dkt.Khamis Kulemba amesema CUAMM ni miongoni mwa wadau ambao wanafanya kazi kulingana na malengo ya serikali ya mkoa ya kuboresha miundombinu katika sekta ya afya.

Wakati huo huo Kulemba amewataka wataalam afya katika Halmashauri ya Mji wa Bariadi kwa kushirikiana na watumishi wa Zahanati ya Old Maswa kuhakikisha huduma zinazotolewa katika jengo hilo la CTC na zahanati hiyo kwa ujumla zinakuwa ni za ubora unaotakiwa  na ziendane na thamani ya mradi huo.

Katika hatua nyingine Dkt. Kulemba ametoa wito kwa viongozi wa Dini mkoani Simiyu kuendelea kushirikiana na wataalam wa afya katika kulinda afya ya watu wanaoishi na Virusi vya Ukimwi(VVU),  wanaotumia dawa za kufubaza makali ya VVU katika kuwahimiza watumie dawa hizo kwa usahihi badala ya kuwataka kuacha kutumia dawa hizo baada ya kuwaombea.

“Nawaomba viongozi wa dini washirikiane na wataalam kulinda afya za watu wenye VVU, baadhi yao wamekuwa wakiwaombea watu wenye VVU na kuwaambia waache kutumia dawa; watu hao wakiacha kutumia dawa wanakuwa na hali mbaya; kuacha kutumia dawa na kuzirudia tena kunawaletea shida na kutengeneza usugu, nawaomba viongozi wa dini watusaidie kwenye hili,” alisema Kulemba.

Naye Mganga mfawidhi wa zahanati ya Old Maswa Ndaro Lawi amesema huduma za tiba na matunzo kwa watu wenye Virusi vya Ukimwi (VVU) katika zahanati hiyo zilianza mwaka 2016, ambapo hadi sasa  jumla ya watu 219 wameandikishwa katika kituo hicho na  wanapata huduma mbalimbali bila malipo.

Kwa upande wake Mratibu wa mradi wa Test and Treat kutoka CUAMM  Doctors With Africa  mikoa ya Shinyanga na Simiyu, Ndg. Ndg. Franscesco Bonanome amewashukuru watumishi wa CUAMM, viongozi wa Serikali na Jimbo Katoliki Shinyanga kwa namna walivyofanya kazi kwa ushirikiano na kuahidi kuwa shirika hilo litaendelea kufanya mambo makubwa siku za zijazo.

Ujenzi wa Jengo la CTC na ukarabati wa majengo mengine katika Zahanati ya Old Maswa umegharimu shilingi 209, 885, 665/= huku uchimbaji wa kisima ukigharimu shilingi 39,533,540/=
MWISHO

Makamu wa Askofu wa Jimbo Katoliki Shinyanga, Padri Kizito Nyanga (katikati)  akikata utepe kuashiria uzinduzi wa jengo jipya la Huduma za tiba na matunzo kwa watuwanaoishi na Virusi vya Ukimwi (CTC) Juni 18, 2020  lililojengwa kwa msaada wa Shirika lisilo la Kiserikali la  Doctors With Africa- CUAMM kupitia mradi wa Test and Treat;  katika Zahanati ya Old Maswa inayomilikiwa na Kanisa Katoliki Jimbo la Shinyanga (Kulia) Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Dkt. Khamis Kulemba na (kushoto) Mratibu wa  Mradi wa Test and Treat Shinyanga na Simiyu , Ndg. Franscesco Bonanome. 
Mganga Mfawidhi wa Zahanati ya Old Maswa inayomilikiwa na Kanisa Katoliki Jimbo la Shinyanga (kushoto) akitoa maelezo ya utoaji wa huduma katika zahanati hiyo kwa viongozi mbalimbali walioshirikia katika hafla ya uzinduzi wa jengo jipya la Huduma za tiba na matunzo kwa watu wanaoishi na Virusi vya Ukimwi (CTC ) Juni 18, 2020  lililojengwa kwa msaada wa Shirika lisilo la Kiserikali la Doctors With Africa-CUAMM kupitia mradi wa Test and Treat (kulia) ni Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Dkt. Khamisi Kulemba wa  Mradi wa Test and Treat Shinyanga na Simiyu , Ndg. Franscesco Bonanome. 
Mhandisi wa ujezi aliyekuwa akisimamia ujezi wa  jengo jipya la Huduma za tiba na matunzo kwa watu wanaoishi naVirusi vya Ukimwi (CTC ) katika Zahanati ya Old Maswa lililojengwa kwa msaada wa Shirika lisilo la Kiserikali la Doctors With Africa- CUAMM kupitia mradi wa Test and Treat, akitoa maelezo ya namna ukarabati wa majengo mbalimbali katika zahanati ya Old Maswa ulivyofanyika kwa viongozi mbalimbali kabla ya uzinduzi wa jengo hilo Juni 18, 2020.
Makamu wa Askofu wa Jimbo Katoliki Shinyanga, Padri Kizito Nyanga akizungumza na viongozi na watendaji mbalimbali katika hafla ya uzinduzi wa jengo jipya la Huduma za tiba na matunzo kwa watu wanaoishi na Virusi vya Ukimwi (CTC ) Juni 18, 2020  lililojengwa kwa msaada wa Shirika lisilo la Kiserikali la  Doctors With Africa- CUAMM kupitia mradi wa;  katika Zahanati ya Old Maswa inayomilikiwa na Kanisa Katoliki.
Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa, Dkt. Khamis Kulemba akizungumza na viongozi na watendaji mbalimbali katika hafla ya uzinduzi wa jengo jipya la Huduma za tiba na matunzo kwa watuwanaoishi na Virusi vya Ukimwi (CTC ) Juni 18, 2020  lililojengwa kwa msaada wa Shirika lisilo la Kiserikali la  Doctors With Africa- CUAMM kupitia mradi wa Test and Treat;  katika Zahanati ya Old Maswa inayomilikiwa na kanisa Katoliki.
Mratibu wa  Mradi wa Test and Treat Shinyanga na Simiyu , Ndg. Franscesco Bonanome  akizungumza na viongozi na watendaji mbalimbali katika hafla ya uzinduzi wa jengo jipya la Huduma za tiba na matunzo kwa watu wanaoishi na Virusi vya Ukimwi (CTC )Juni 18, 2020  lililojengwa kwa msaada wa Shirika lisilo la Kiserikali la Doctors With Africa- CUAMM  kupitia mradi wa Test and Treat;  katika Zahanati ya Old Maswa inayomilikiwa na Kanisa Katoliki.
Makamu wa Askofu wa Jimbo Katoliki Shinyanga, Padri Kizito Nyanga (wa pili kulia walioketi) akiwa katika picha ya pamoja  na viongozi na watendaji mbalimbali katika hafla ya uzinduzi wa jengo jipya la Huduma za tiba na matunzo kwa watu wanaoishi na Virusi vya Ukimwi (CTC )Juni 18, 2020  lililojengwa kwa msaada wa Shirika lisilo la Kiserikali la Doctors With Africa- CUAMM  kupitia mradi wa Test and Treat;  katika Zahanati ya Old Maswa inayomilikiwa na Kanisa Kanisa Katoliki
Sehemu ya mbele ya jengo jipya la Huduma za tiba na matunzo kwa watu wenye Virusi vya Ukimwi (CTC) Juni 18, 2020  lililojengwa kwa msaada wa Shirika lisilo la Kiserikali la Doctors With Africa- CUAMM kupitia mradi wa Test and Treat;  katika Zahanati ya Old Maswa inayomilikiwa na Kanisa Katoliki.
 Mganga Mfawidhi wa Zahanati ya Old Maswa inayomilikiwa na Kanisa Katoliki Jimbo la Shinyanga (kushoto) akitoa maelezo ya utoaji wa huduma katika zahanati hiyo kwa viongozi mbalimbali walioshirikia katika hafla ya uzinduzi wa jengo jipya la Huduma za tiba na matunzo kwa watu wanaoishi na Virusi vya Ukimwi (CTC ) Juni 18, 2020  lililojengwa kwa msaada wa Shirika lisilo la Kiserikali la Doctors With Africa-CUAMM kupitia mradi wa Test and Trea.t 
 :- Makamu wa Askofu wa Jimbo Katoliki Shinyanga, Padri Kizito Nyanga (wa pili kulia walioketi) akiwa katika picha ya pamoja  na viongozi na watendaji mbalimbali katika hafla ya uzinduzi wa jengo jipya la Huduma za tiba na matunzo kwa watu wanaoishi na Virusi vya Ukimwi (CTC )Juni 18, 2020  lililojengwa kwa msaada wa Shirika lisilo la Kiserikali la Doctors With Africa- CUAMM  kupitia mradi wa Test and Treat;  katika Zahanati ya Old Maswa inayomilikiwa na Kanisa Kanisa Katoliki.
 Mhandisi wa ujenzi aliyekuwa akisimamia ujezi wa  jengo jipya la Huduma za tiba na matunzo kwa watu wanaoishi naVirusi vya Ukimwi (CTC ) katika Zahanati ya Old Maswa lililojengwa kwa msaada wa Shirika lisilo la Kiserikali la Doctors With Africa- CUAMM kupitia mradi wa Test and Treat, akitoa maelezo ya namna ukarabati wa majengo mbalimbali katika zahanati ya Old Maswa ulivyofanyika kwa viongozi mbalimbali kabla ya uzinduzi wa jengo hilo Juni 18, 2020.
 Mwakilishi wa Mganga Mkuu wa Halashauri ya Mji wa Bariadi, akitoa taarifa katika hafla ya uzinduzi wa jengo jipya la Huduma za tiba na matunzo kwa watu wanaoishi na Virusi vya Ukimwi (CTC ) Juni 18, 2020  lililojengwa kwa msaada wa Shirika lisilo la Kiserikali la Doctors With Africa-CUAMM kupitia mradi wa Test and Treat 
 Baadhi ya viongozi wakikagua ujenzi wa nyumba ya pampu ya kisima cha maji kilichochimwa kwa msaada wa Shirika lisilo la Kiserikali la Doctor With Africa CUAMM katika zahanati ya Old Maswa kabla ya uzinduzi wa jengo jipya la Huduma za tiba na matunzo kwa watu wanaoishi na Virusi vya Ukimwi (CTC ) Juni 18, 2020  lililojengwa kwa msaada wa Shirika lisilo la Kiserikali la Doctors With Africa-CUAMM kupitia mradi wa Test and Treat 
 Makamu wa Askofu wa Jimbo Katoliki Shinyanga, Padri Kizito Nyanga (katikati), Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Dkt. Khamis Kulemba(kulia) na (kushoto) Mratibu wa  Mradi wa Test and Treat Shinyanga na Simiyu , Ndg. Franscesco Bonanome wakipiga makofi kufurahia  uzinduzi wa jengo jipya la Huduma za tiba na matunzo kwa watuwanaoishi na Virusi vya Ukimwi (CTC) Juni 18, 2020  lililojengwa kwa msaada wa Shirika lisilo la Kiserikali la  Doctors With Africa- CUAMM kupitia mradi wa Test and Treat;  katika Zahanati ya Old Maswa inayomilikiwa na Kanisa Katoliki Jimbo la Shinyanga.
 Mganga Mfawidhi wa Zahanati ya Old Maswa inayomilikiwa na Kanisa Katoliki Jimbo la Shinyanga (kushoto) akitoa maelezo ya utoaji wa huduma katika zahanati hiyo kwa viongozi mbalimbali walioshirikia katika hafla ya uzinduzi wa jengo jipya la Huduma za tiba na matunzo kwa watu wanaoishi na Virusi vya Ukimwi (CTC ) Juni 18, 2020  lililojengwa kwa msaada wa Shirika lisilo la Kiserikali la Doctors With Africa-CUAMM kupitia mradi wa Test and Treat.
Baadhi ya Viongozi wa kanisa Jimbo Katoliki Shinyanga, Serikali na Shirika lisilo la Kiserikali wakifuatilia  matukio mbalimbali katika hafla ya uzinduzi wa jengo jipya la Huduma za tiba na matunzo kwa watu wanaoishi na Virusi vya Ukimwi (CTC ) Juni 18, 2020  lililojengwa kwa msaada wa Shirika lisilo la Kiserikali la Doctors With Africa-CUAMM kupitia mradi wa Test and Treat.





Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!