Tuesday, June 23, 2020

WANANCHI SIMIYU WAIPONGEZA SERIKALI KUWAJENGEA MAHAKAMA


Wananchi wa Wilaya ya Bariadi Mkoani Simiyu wameipongeza Serikali kwa kuwajengea mahakama ya Wilaya ya Bariadi na Mahakama ya Hakimu Mkazi Simiyu jambo ambalo limeapunguzia adha ya kutumia gharama na muda mrefu kwenda kufuata huduma za mahakama katika mkoa wa Shinyanga kama ilivyokuwa awali.

Akizungumza katika hafla ya uzinduzi wa jengo la mahakama ya Hakimu Mkazi Simiyu na Mahakama ya Wilaya ya Bariadi ambayo ilifanyika Juni 22, 2020 Mjini Bariadi, Bw. Zengila Nyoni mkazi wa Bariadi ameomba watumishi wa mahakama kutoa huduma kwa kuzingatia misingi ya haki ili umuhimu wa uwepo wa mahakama uonekane kwa wananchi.

“Tunaishukuru Serikali kutujenge jengo zuri la mahakama, sasa hivi hatutasafiri kwenda Shinyanga kufuata huduma za mahakama ya hakimu mkazi ni hapa hapa tu; niwaombe mahakimu na majaji kutoa haki kwa wananchi ili tufurahie uwepo wa jengo hili zuri, maana haitakuwa na faida kama tumejengewa jengo zuri halafu huduma zisiwe nzuri,”alisema Nyoni.

Awali akizungumza katika uzinduzi huo Jaji kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Dkt. Eliezer Feleshi amewashauri Wakuu wa Wilaya na Mikoa nchini  kutumia kamati za maadili za wilaya ambazo wao ni wenyeviti wa kamati hizo kuwajadili mahakimu ambao wanaenda kinyume na maadili ya utumishi wa Umma.

 “ Ni aibu kwa Mkuu wa Wilaya au Mkuu wa Mkoa kusema kuwa hamtaki hakimu fulani kwenye eneo lake wakati  yeye ndiyo mwenyekiti wa kamati ya maadili ya wilaya au mkoa, mahakimu wasio waadilifu wafikisheni kwenye kamati za maadili, zile kamati zinajuimisha watu wengi wazuri; niendelee kuwasihi watumishi wa Mahakama kujiepusha na vitendo vilivyo kinyume na maadili,” alisea Jaji Feleshi.


Jaji kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Dkt. Eliezer Feleshi(katikati) akikata utepe kuashiria uzinduzi wa jengo la mahakama ya wilaya ya Bariadi na mahakama Hakimu mkazi Simiyu, uzinduzi uliofanyika Mjini Bariadi Juni 22, 2020.
 Jaji kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Dkt. Eliezer Feleshi(katikati) akifungua kitambaa kuashiria uzinduzi wa jengo la mahakama ya wilaya ya Bariadi na mahakama Hakimu mkazi Simiyu, uzinduzi  uliofanyika Mjini Bariadi Juni 22, 2020.
 Jaji kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Dkt. Eliezer Feleshi akizungumza na viongozi mbalimbali, watumishi wa mahakama na wananchi katika hafla ya uzinduzi wa jengo la mahakama ya wilaya ya Bariadi na mahakama Hakimu mkazi Simiyu, uzinduzi uliofanyika Mjini Bariadi Juni 22, 2020.
 Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga akitoa salamu za Mkoa wa Simiyu kwa niaba ya mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka katika hafla ya uzinduzi wa jengo la mahakama ya wilaya ya Bariadi na mahakama Hakimu mkazi Simiyu, uzinduzi uliofanyika Mjini Bariadi Juni 22, 2020.
 Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Shinyanga, Mhe. Gerson Mdemu akizungumza na viongozi mbalimbali, watumishi wa mahakama na wananchi katika hafla ya uzinduzi wa jengo la mahakama ya wilaya ya Bariadi na mahakama Hakimu mkazi Simiyu, uzinduzi uliofanyika Mjini Bariadi Juni 22, 2020.
 Baadhi ya mahakimu na watumishi wengine wa mahakama mkoani Simiyu wakifurahia jambo katika hafla ya uzinduzi wa jengo la mahakama ya wilaya ya Bariadi na mahakama Hakimu mkazi Simiyu, uzinduzi uliofanyika Mjini Bariadi Juni 22, 2020.
 Baadhi ya Viongozi wakifuatilia kwa makini matukio mbalimbali katika hafla ya uzinduzi wa jengo la mahakama ya wilaya ya Bariadi na mahakama Hakimu mkazi Simiyu, uzinduzi uliofanyika Mjini Bariadi Juni 22, 2020.

Jaji kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Dkt. Eliezer Feleshi(katikati walioketi) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya viongozi katika mhimili wa mahakama na mahakimu wa Mahakama mbalimbali mkoani Simiyu(waliosimama) baada ya uzinduzi wa jengo la mahakama ya wilaya ya Bariadi na mahakama Hakimu mkazi Simiyu, uzinduzi uliofanyika Mjini Bariadi Juni 22, 2020.
 Katibu wa Itikani na Uenezi wa CCM Mkoa wa Simiyu, Bw. Mayunga George akitoa salamu za Chama katika hafla ya uzinduzi wa jengo la mahakama ya wilaya ya Bariadi na mahakama Hakimu mkazi Simiyu, uzinduzi uliofanyika Mjini Bariadi Juni 22, 2020.
 Baadhi ya Viongozi wakifuatilia kwa makini matukio mbalimbali katika hafla ya uzinduzi wa jengo la mahakama ya wilaya ya Bariadi na mahakama Hakimu mkazi Simiyu, uzinduzi uliofanyika Mjini Bariadi Juni 22, 2020.
 Baadhi ya Viongozi wakifuatilia kwa makini matukio mbalimbali katika hafla ya uzinduzi wa jengo la mahakama ya wilaya ya Bariadi na mahakama Hakimu mkazi Simiyu, uzinduzi uliofanyika Mjini Bariadi Juni 22, 2020.
 Jaji kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Dkt. Eliezer Feleshi akiwaeleza jambo baadhi ya watumishi wa mahakama wakati alipopita kukagua jengo la jengo la mahakama ya wilaya ya Bariadi na mahakama Hakimu mkazi Simiyu,  katika hafla ya uzinduzi wa  wa jengo hilo uliofanyika Mjini Bariadi Juni 22, 2020. 
 Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Shinyanga, Mhe. Gerson Mdemu(kushoto akimuongoza Jaji kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Dkt. Eliezer Feleshi kuelekea katika eneo maalum lililoandaliwa kwa ajili ya kuzindua jengo la mahakama ya wilaya ya Bariadi na mahakama Hakimu mkazi Simiyu, uzinduzi uliofanyika Mjini Bariadi Juni 22, 2020.
 Baadhi ya viongozi wa taasisi, watumishi wa mahakama na wananchi wakifuatilia kwa makini matukio mbalimbali katika hafla ya uzinduzi wa jengo la mahakama ya wilaya ya Bariadi na mahakama Hakimu mkazi Simiyu, uzinduzi uliofanyika Mjini Bariadi Juni 22, 2020.
 Baadhi ya viongozi wakiwa katika hafla ya uzinduzi wa jengo la mahakama ya wilaya ya Bariadi na mahakama Hakimu mkazi Simiyu, uzinduzi uliofanyika Mjini Bariadi Juni 22, 2020.
 Jaji kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Dkt. Eliezer Feleshi(katikati walioketi) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya viongozi katika mhimili wa mahakama na (waliosimama) baada ya uzinduzi wa jengo la mahakama ya wilaya ya Bariadi na mahakama Hakimu mkazi Simiyu, uzinduzi uliofanyika Mjini Bariadi Juni 22, 2020.
 Sehemu ya mbele ya jengo la mahakama ya wilaya ya Bariadi na mahakama Hakimu mkazi Simiyu, lililozinduliwa na Jaji kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Dkt. Eliezer Feleshi Mjini Bariadi Juni 22, 2020.
Jaji kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Dkt. Eliezer Feleshi (wa pili kushoto) akipokea maelezo kutoka kwa mmoja wa watumishi kuhusu jengo la mahakama ya wilaya ya Bariadi na mahakama Hakimu mkazi Simiyu, baada ya uzinduzi wa jengo hilo uliofanyika Mjini Bariadi Juni 22, 2020.

0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!