Saturday, June 6, 2020

USIMAMIZI WA TAALUMA SIMIYU ULENGE KULETA MATOKEO: SAGINI


Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bw. Jumanne Sagini amewataka viongozi na watendaji waandamizi katika idara ya elimu mkoani hapa kuhakikisha kuwa kila mmoja katika eneo lake anasimamia taaluma kwa kuzingatia matokeo yanayotarajiwa na mkoa.

Sagini ameyasema hayo jana katika kikao kazi cha viongozi hao ambacho kimewahusisha maafisa Elimu na Maafisa Taaluma wa Wilaya, Maafisa Takwimu, wawakilishi wa Wakuu wa Shule,  walimu wakuu, waratibu elimu kata, wadhibiti ubora pamoja na maafisa wa Tume ya Utumishi wa Walimu kilichofanyika katika shule ya Msingi Lukungu wilayani Busega.

“Mnapojadili hapa kila mmoja akumbuke nafasi yake katika kuhakikisha kuwa usimamizi wa taaluma kwenye mkoa wetu unaendelea kutupa matokeo tunayoyatarajia, kila kada yenu mnapokutana mkumbuke ajenda ya mkoa wetu sisi elimu na ndiyo kipaumbele chetu,” alisema Sagini.

0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!