Thursday, May 31, 2018

SIMIYU YAJIPANGA KUIIMARISHA SHULE YA SEKONDARI BARIADI KAMA SHULE MAALUM YA MICHEZO

Serikali mkoani Simiyu imesema imekusudia kuiimarisha shule ya Sekondari ya Bariadi ambayo ilitengwa kuwa Shule ya Michezo, kwa kujenga mabweni ya wanafunzi wa kike na wa kiume na kuiwekea miundombinu yote muhimu,  ikiwemo viwanja vya michezo yote kwa lengo la kuibua na kukuza vipaji vya wanafunzi.

Hayo yamesemwa na Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka wakati alipokuwa akifunga mashindano ya UMISSETA na UMITASHUMTA kimkoa katika viwanja vya Shule ya sekondari ya Wasichana Maswa.

"Ningehitaji tuifanye Shule ya Sekondari Bariadi kuwa shule maalum ya kimichezo ya Kimkoa, yenye mabweni ya wavulana na wasichana na tuiwekee miundombinu yote ya michezo ili watoto wote wenye vipaji vya michezo waende pale na nitaomba kibali walimu wa michezo wahamie hapo,  tufike mahali ambapo Bariadi Sekondari itatoa wachezaji wa kutumainiwa kwenye Taifa" amesema Mtaka.

Aidha, amewataka wanafunzi wote kuwa na mtazamo tofauti katika michezo kwa kuondokana na nadharia ya kuwa michezo ni afya, burudani na kwenda kwenye dhana ya michezo kama taaluma, ajira na biashara, ambapo amehimiza kuwa mkoa huo unafanya uwekezaji na mapinduzi ya michezo kibiashara katika Shule hiyo.

Mkuu huyo wa mkoa pia amewataka wanafunzi hao kuuwakilisha vema mkoa na kuwatakia heri na ushindi katika mashindano ya UMISSETA na UMITASHUMTA ngazi ya Taifa yatakayofanyika jijini Mwanza, huku akiwataka kuwa na nidhamu kipindi chote watakachokuwa huko na akaahidi kutoa zawadi mbalimbali kwa washiriki wote watakaporudi na ushindi.

Katika hatua nyingine Mtaka akiwakabidhi walimu na wanafunzi jezi zilizotolewa kwa udhamini wa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa, kupitia mradi wake wa Kiwanda cha Chaki (MASWA CHALKS) amewataka Wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi mkoani humo kujipanga kwa ajili ya kudhamini mashindano ya UMISSETA na UMITASHUMTA mwaka 2019 kupitia miradi inayotekelezwa kwenye maeneo yao ili kuendelea kuutangaza mkoa huo.

Afisa Elimu Mkoa wa Simiyu, Mwl. Julius Nestory amesema changamoto kubwa zilizowakabili washiriki wa mashindano hayo ni pamoja na upungufu wa viwanja katika shule za msingi na sekondari na kukosa wafadhili kutoka nje ili kuwezesha wanafunzi kukaa kambini muda mrefu kujiandaa na mashindano.

Kwa upande wao wanafunzi/ washiriki wa UMISSETA na UMITASHUMTA mkoa wa Simiyu wamemhakikishia Mkuu mkoa na wananchi kwa ujumla kuwa watarudi na ushindi katika mashindano hayo Kitaifa.

"Mwaka 2018 tumejipanga na ushindi ni lazima kwa mwaka huu sisi tunaenda Mwanza kushinda na kuchukua makombe, tunamhakikishia Mkuu wa Mkoa  na wananchi wote wa Simiyu kuwa tunarudi na ushindi" Alisema Mwanaidi Khamis kutoka  Maswa.

Jumla ya washiriki 811 wa michezo mbalimbali kutoka katika Halmashauri zote Sita za Mkoa wa Simiyu wameshiriki mashindano ya UMISSETA na UMITASHUMTA ngazi ya Mkoa kwa mwaka 2018.

MWISHO 



Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka (wa pili kulia) akikabidhi kombe la msindi wa jumla michezo ya UMISSETA kimkoa mwaka 2018 kwa Afisa Elimu wa Halmashauri ya Wilaya ya Busega, Mwl. Yassin Kitentya wakati wa kufunga mashindano ya UMISSETA UMITASHUMTA katika viwanja vya Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa  


Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka akizungumza na wanafunzi wanamichezo katika hafla ya kufunga Mashindano ya UMISSETA na UMITASHUMTA  katika viwanja vya Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa.



Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka (wa nne kulia) na baadhi ya wana michezo wakionesha jezi zilizotolewa na Kiwanda cha MASWA CHALK kama udhamini katika michezo ya UMISSETA na UMITASHUMTA, wakati wa kufunga mashindano ya UMISSETA UMITASHUMTA katika viwanja vya Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa  

Mkuu wa Wilaya ya Maswa, Mhe. Dkt. Seif Shekalaghe (wa nne kushoto) akiteta jambo na Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka(kulia), wakati wa kufunga mashindano ya UMISSETA UMITASHUMTA katika viwanja vya Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa .

Mkuu wa Wilaya ya Maswa, Mhe. Dkt. Seif Shekalaghe (wa nne kushoto) akiteta jambo na Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka(kulia), wakati wa kufunga mashindano ya UMISSETA UMITASHUMTA katika viwanja vya Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtakaakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya washiriki wa michezo, mara baada ya kufunga  Mashindano  ya UMISSETA na UMITASHUMTA kimkoa katika viwanja vya Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa.
Wanamichezo kutoka Wilaya ya Busega wakionesha onesho lao la ngoma za asili mbele ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu na Viongozi wengine wakati wa hafla ya kufunga mashindano hayo  katika viwanja vya Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa.
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa, Dkt. Fredrick  Sagamiko akitoa taarifa ya vitu ambavyo kiwanda cha Maswa Chalks Kimedhamini katika Mashindano  ya UMISSETA na UMITASHUMTA kimkoa, wakati wa kufunga mashindano hayo  katika viwanja vya Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa.

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka(katikati) akiwa na baadhi ya viongozi na wawakilishi wa wanamichezo wakionesha jezi zilizotolewa na Kiwanda cha MASWA CHALK kama mdhamini katika michezo ya UMISSETA na UMITASHUMTA, wakati wa kufunga mashindano ya UMISSETA UMITASHUMTA katika viwanja vya Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka (katikati) akionesha moja ya jezi zilizotolewa na Kiwanda cha MASWA CHALK kama mdhamini katika michezo ya UMISSETA na UMITASHUMTA, wakati wa kufunga mashindano ya UMISSETA UMITASHUMTA katika viwanja vya Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa



Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka (katikati) katika picha ya pamoja na baadhi ya washiriki wa Mashindano ya UMISSETA na UMITASHUMTA kimkoa, mara baada ya kufunga mashindano hayo katika viwanja vya Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa.

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka (wa nne kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na viongozi na baadhi ya wanamichezo mara baada ya kufunga  Mashindano  ya UMISSETA na UMITASHUMTA kimkoa katika viwanja vya Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa.

MASWA WARIDHIA KAYA KUCHANGIA SHILINGI ELFU 50 KWA MWAKA KWA AJILI YA MAENDELEO

Viongozi wa wananchi, wenyeviti wa vitongoji na vijiji 120 vya wilaya ya Maswa mkoani Simiyu wameridhia mchango wa shilingi elfu hamsini kila kaya kwa ajili ya shughuli za maendeleo ambao utatolewa kwa mwaka, ambapo baada ya kaya kutoa mchango huo hazitachangia mchango mwingine wowote.

Hayo wameyasema katika mkutano uliofanyika katika Uwanja wa Nguzo nane Mjini  Maswa baina ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Anthony Mtaka na viongozi wa vitongoji ,vijiji na  wadau mbalimbali wa maendeleo  ,wakiwemo viongozi wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa, viongozi wa dini  na  wananchi, lengo likiwa ni kujadili azimio lililopitishwa na Baraza la madiwani wa Halmashauri ya Maswa la Uchangiaji shughuli za maendeleo hususani ujenzi wa miundombinu ya elimu na afya.

“Kwanza ni  vizuri ikafahamika kwamba viongozi wa wananchi wameridhia mchango, hii habari ya nani kasema hapana ni lazima tutoe uhuru wa kutoa maoni, sidhani kama ingekuwa sahihi  tuje hapa tuamue kuwa haya ni maelekezo; lakini pili hatujasema adhabu kuwa asiyetoa mchango huu atafanywa nini waandishi wa habari saidieni kuondoa uzushi huu kwenye mitandao” amesema Mtaka.

Mtaka amesema ni vema  ikafahamika wazi kuwa baada ya kaya kutoa  mchango huu wananchi hawatachangiswa mchango wowote, huku akisisitiza kuwa mchngo huu hautazihusu zilizo chini ya Mpango wa Kunusuru kaya Maskini TASAF III pamoja na kaya za wananchi walio katika misamaha mbalimbali ya Serikali.

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka wakati akihitimisha mkutano huo amesema uamuzi wa kuwa na mchango huo umetokana na kuona wananchi wamekuwa wakichangishwa michango mingi ya rejareja ambayo ilikuwa ikizidi kiasi cha shilingi elfu 50,  hivyo Halmashauri ikaona ipo haja ya kuwa na mchango mmoja ambao utakuwa na unafuu.

“Huu mchango ni sawa na michango mingine ambayo Wananchi wamekuwa wakichangia siku zote kwa ajili ya shughuli za maendeleo, lakini sasa hivi Halmashauri baada ya kuona wananchi wakichangia rejareja wanachangia fedha nyingi, iliona ni vema kukawa na mchango mmoja kwa mwaka wa shilingi elfu 50” alifafanua Mtaka.
Awali akitoa ufafanuzi kuhusu mchango huo Mkuu wa Wilaya ya Maswa, Mhe. Dkt. Seif Shekalaghe amesema wilaya hiyo ilifikia uamuzi wa kuwa na mchango mmoja kutokana na michango iliyokuwa ikitolewa rejareja kutokuwa na matokeo yaliyokusudiwa, ikiwa ni pamoja na miradi iliyokusudiwa kujengwa na fedha za michango hiyo hususani miundombinu yal elimu na Afya kutokamilika kwa wakati.
Kwa upande wake Erasto Mbigili Mwenyekiti wa Kijiji cha Mbalagane amesema  anaunga mkono wazo la kuwa na mchango mmoja kwa mwaka ambao utawarahisishia Wenyeviti wa Vijiji na vitongoji na kuwaondolea kero ya kwenda kila mara kuwasumbua wananchi kuomba michango.

Naye John Dalawida Mwenyekiti Kitongoji cha Matale amesema anaunga mkono wazo hilo ambalo limeanzia kwa madiwani ambao ni wawakilishi wao na anaamini litasaidia ukamilishaji wa maboma ya vyumba vya madarasa na zahanati waliyoanza kujenga ili kuboresha miundombinu ya sekta ya elimu na afya wilayani Maswa.

Jeremia Shigala Diwani wa kata ya Zanzui amesema Baraza la madiwani lilizimia kuja na mchango huo baada ya wataalam wa Halmashauri kuonesha mchanganuo kuwa wananchi wilayani humo wamekuwa wakichangia wastani wa shilingi elfu 70 kwa mwaka,  hivyo alilipokea na kuahidi kwenda kuwaelimisha wananchi  juu ya umuhimu wa mchango huo wa mara moja.

Katika Mkutano huo viongozi wa Chama na Serikali walitoa michango yao ya fedha taslimu, ahadi na vifaa vya ujenzi ili kuuunga mkono wazo la ujenzi wa miundombinu ya elimu na afya katika wilaya ya Maswa, ambapo Mkuu wa Mkoa wa Simiyu aliahidi kutoa shilingi 1,000,000/=, Mkuu wa wilaya hiyo aliahidi kutoa shilingi 500,000/= Mkurugenzi wa Halmashauri aliahidi kutoa shilingi 500,000/= na Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM (NEC) akaahidi kutoa jumla ya mabati 500 kama mchango wake.
MWISHO
Mkuu wa Wilaya ya Maswa, Mhe.Dkt. Seif Shekalaghe akizungumza na Viongozi wa Vitongoji, Vijiji, Kata, Wilaya na Mkoani Simiyu katika Mkutano uliofanyika katika Uwanja wa Nguzo Nane Mjini Maswa.
Baadhi ya Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa wakifuatilia mkutano baina ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka   na viongozi wa vitongoji ,vijiji na  wadau mbalimbali wa maendeleo  ,wakiwemo viongozi wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa na   wananchi, lengo likiwa ni kujadili azimio lililopitishwa na Baraza la madiwani wa Halmashauri ya Maswa la Uchangiaji shughuli za maendeleo. 


Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa, Dkt. Fredrick Sagamiko (kulia) akifafanua jambo katika kikao cha Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka   na viongozi wa vitongoji ,vijiji na  wadau mbalimbali wa maendeleo  ,wakiwemo viongozi wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa na   wananchi, lengo likiwa ni kujadili azimio lililopitishwa na Baraza la madiwani wa Halmashauri ya Maswa la Uchangiaji shughuli za maendeleo. 
Diwani wa kata ya Zanzui Mhe. Jeremia Shigala akichangia hoja katika kikao cha Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka na viongozi wa vitongoji ,vijiji na  wadau mbalimbali wa maendeleo  ,wakiwemo viongozi wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa na wananchi, lengo likiwa ni kujadili azimio lililopitishwa na Baraza la madiwani wa Halmashauri ya Maswa la Uchangiaji shughuli za maendeleo. 

Baadhi ya Viongozi wa Mkoa wa Simiyu wakifurahia jambo katika Mkutano wa viongozi wa vitongoji ,vijiji na  wadau mbalimbali wa maendeleo  ,wakiwemo viongozi wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa na   wananchi, lengo likiwa ni kujadili azimio lililopitishwa na Baraza la madiwani wa Halmashauri ya Maswa la Uchangiaji shughuli za maendeleo.

Baadhi ya Wenyeviti wa Vitongoji na Vijiji vya Wilaya ya Maswa, wakifuatilia mkutano baina yao na Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka   na  wadau mbalimbali wa maendeleo  ,wakiwemo viongozi wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa na   wananchi, lengo likiwa ni kujadili azimio lililopitishwa na Baraza la madiwani wa Halmashauri ya Maswa la Uchangiaji shughuli za maendeleo. 

Mkuu wa Wilaya ya Maswa , Mhe. Dkt. Shekalaghe akipokea mchango kwa Katibu wa CCM Mkoa, Bw. Donald Magesa mara baada ya kikao cha Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka   na viongozi wa vitongoji ,vijiji na  wadau mbalimbali wa maendeleo  ,wakiwemo viongozi wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa na wananchi, lengo likiwa ni kujadili azimio lililopitishwa na Baraza la madiwani wa Halmashauri ya Maswa la Uchangiaji shughuli za maendeleo.
Mwenyekiti wa CCM Mkoa, Mhe. Enock Yakobo akifafanua jambo katika kikao cha Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka na viongozi wa vitongoji ,vijiji na  wadau mbalimbali wa maendeleo  ,wakiwemo viongozi wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa na   wananchi, lengo likiwa ni kujadili azimio lililopitishwa na Baraza la madiwani wa Halmashauri ya Maswa la Uchangiaji shughuli za maendeleo. 
Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Maswa, Mhandisi. Paul Jidayi akifafanua jambo katika kikao cha Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka na viongozi wa vitongoji ,vijiji na  wadau mbalimbali wa maendeleo  ,wakiwemo viongozi wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa na   wananchi, lengo likiwa ni kujadili azimio lililopitishwa na Baraza la madiwani wa Halmashauri ya Maswa la Uchangiaji shughuli za maendeleo.
Diwani wa Viti Maalum CCM , Mhe. Leticia Lolela akichangia hoja katika kikao cha Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka na viongozi wa vitongoji ,vijiji na  wadau mbalimbali wa maendeleo  ,wakiwemo viongozi wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa na wananchi, lengo likiwa ni kujadili azimio lililopitishwa na Baraza la madiwani wa Halmashauri ya Maswa la Uchangiaji shughuli za maendeleo.
Kutoka kulia mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Simiyu, Mhe. Enock Yakobo, Mkuu wa Mkoa huo, Mhe.Anthony Mtaka, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa, Dkt. Fredrick Sagamiko na Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM (NEC)  Mhe. Gungu Silanga  wakiteta jambo wakati wa kikao maalum cha kujadili azimio lililopitishwa na Baraza la madiwani wa Halmashauri ya Maswa la Uchangiaji shughuli za maendeleo katika Uwanja wa Nguzo Nane Mjini Maswa.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka akizungumza na na viongozi wa vitongoji ,vijiji na  wadau mbalimbali wa maendeleo  ,wakiwemo viongozi wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa na   wananchi, lengo likiwa ni kujadili azimio lililopitishwa na Baraza la madiwani wa Halmashauri ya Maswa la Uchangiaji shughuli za maendeleo.

Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Simiyu, Mhe. Enock Yakobo na Katibu Mkuu wa CCM mkoa, Bw. Donald Magesa wakiteta jambo wakati wa kikao maalum cha kujadili azimio lililopitishwa na Baraza la madiwani wa Halmashauri ya Maswa la Uchangiaji shughuli za maendeleo katika Uwanja wa Nguzo Nane Mjini Maswa.
Kutoka kulia Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Simiyu, Mhe. Enock Yakobo, Mkuu wa Mkoa, Mhe.Anthony Mtaka na Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM (NEC)  Mhe. Gungu Silanga  wakiteta jambo wakati wa kikao maalum cha kujadili azimio lililopitishwa na Baraza la madiwani wa Halmashauri ya Maswa la Uchangiaji shughuli za maendeleo katika Uwanja wa Nguzo Nane Mjini Maswa.

Saturday, May 26, 2018

KAMATI NA BODI ZA SHULE ZATAKIWA KUJIUZULU SHULE ZINAPOFANYA VIBAYA KWENYE MITIHANI


Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe. Anthony Mtaka amesema wakati umefika kwa kamati na bodi za Shule mkoani humo kujitathmini ikiwa zinafaa kuendelea na majukumu yao au kujiuzulu pale Shule zao zinapofanya vibaya katika mitihani  hususani ya Taifa.

Mtaka ameyasema hayo alipokuwa akizungumza na Wenyeviti wa Kamati na Bodi  za Shule za Halmashauri ya Mji Bariadi na Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi katika Ukumbi wa Shule ya Sekondari Bariadi,  katika kikao maalum kilicholenga  kujadiliana na kupanga maandalizi ya Kambi za kitaaluma kwa Kidato cha Nne na Darasa la Saba Wilayani humo.

Amesema mara nyingi wanafunzi wanapofanya vibaya kwenye mitihani wazazi wengi wamekuwa wakiwalaumu na kuwanyoshea vidole walimu badala ya kutathmini mchango wao katika ufaulu wa watoto wao.

“ Watoto wakifeli mnaanza kuwanyoshea walimu vidole, huu mwaka watoto wakifeli kamati za shule zijiuzulu, mnapowanyoshea walimu vidole hivi kamati za shule zenyewe huwa zinachukua wajibu gani, jiuzuluni ili waje wazazi wengine wenye mawazo mapya yatakayozivusha shule kwenda kwenye ufaulu mzuri” alisisitiza Mtaka.

Mtaka amewataka wazazi washikamane na Serikali pamoja na walimu katika kuhakikisha wanafanya mapinduzi ya Elimu kwa kuwa ufaulu wa wanafunzi unategemea ushirikiano wa wazazi, walimu na wanafunzi wenyewe, hivyo akasisitiza kuwa Wenyeviti wa Kamati na Bodi za Shule wakafanye vikao na wazazi kuweka mipango mizuri ya kufanikisha kambi za kitaaluma kwa wanafunzi wa kidato cha nne na darasa la saba pamoja na maendeleo ya elimu kwa ujumla.

 Aidha, kama Mwenyekiti wa Kamati ya ulinzi na Usalama ya Mkoa Mtaka amewahakikishia wazazi kuwa wanafunzi wote watakaokuwa katika kambi watatunzwa na kulindwa huku akiwatahadharisha watu wenye nia mbaya kutowafuatilia wanafunzi wa kike kwa lengo la kuwarubuni kwa namna yoyote kwa kuwa Serikali itawachukulia hatua wote watakaobainika.

Mtaka amesisitiza wazazi wote kuchangia mahitaji mbalimbali kwa wanafunzi watakaokuwa kambini ili kuwezesha kambi hizo kufanyika hususani chakula, huku akiwaeleza wazazi kuwa kupitia kambi hizo watarajie kuona mabadiliko ya kitaaluma kwa watoto wao.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga amezitaka Kamati na Bodi za Shule wilayani humo kufanya vikao na Wazazi kwa ajili ya kuwaeleza wajibu wao katika kufanikisha Kambi hizo za Kitaalamu na kuwasilisha taarifa ya utekelezaji wa agizo hilo Mei 30, 2018 ofisini kwake.

Kiswaga amesema Kamati zote ambazo zitashindwa kutekeleza agizo hilo zitavunjwa na Wenyeviti na wajumbe wa Kamati hizo watawajibishwa
.
Wilaya ya Bariadi itazindua rasmi kambi za Kitaaluma kwa wanafunzi wa  Kidato cha Nne na Darasa la Saba Juni 06 mwaka huu.
MWISHO:
Baadhi ya Wenyeviti wa Bodi na Kamati za Shule wa Wilaya ya Bariadi, wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka (hayupo pichani) katika kikao maalum cha maandalizi ya Kambi za Kitaaluma kwa wanafunzi wa kidato cha nne na Darasa la saba zinazotarajiwa kufanyika mwezi Juni kwa siku 21,   kilichofanyika Shule ya Sekondari Bariadi.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka akizungumza na Wenyeviti wa Kamati na  Bodi za Shule za Wilaya ya Bariadi (hawapo pichani) , katika kikao maalum cha maandalizi ya Kambi za Kitaaluma kwa wanafunzi wa kidato cha nne na Darasa la Saba zinazotarajiwa kufanyika mwezi Juni kwa siku 21, kilichofanyika Shule ya Sekondari Bariadi
Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga akizungumza na Wenyeviti wa Kamati na  Bodi za Shule za Wilaya ya Bariadi (hawapo pichani) , katika kikao maalum cha maandalizi ya Kambi za Kitaaluma kwa wanafunzi wa kidato cha nne na Darasa la Saba zinazotarajiwa kufanyika mwezi Juni kwa siku 21, kilichofanyika Shule ya Sekondari Bariadi
Baadhi ya Wenyeviti wa Bodi na Kamati za Shule wa Wilaya ya Bariadi, wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka (hayupo pichani) katika kikao maalum cha maandalizi ya Kambi za Kitaaluma kwa wanafunzi wa kidato cha nne na Darasa la saba zinazotarajiwa kufanyika mwezi Juni kwa siku 21, kilichofanyika Shule ya Sekondari Bariadi.
Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga akifurahia jambo katika kikao maalum cha maandalizi ya Kambi za Kitaaluma kwa wanafunzi wa kidato cha nne na Darasa la Saba zinazotarajiwa kufanyika mwezi Juni kwa siku 21, kilichofanyika Shule ya Sekondari Bariadi, (kulia) Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi, Bw. Melkezedeck Humbe.
Baadhi ya Wenyeviti wa Bodi na Kamati za Shule wa Wilaya ya Bariadi, wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka (hayupo pichani) katika kikao maalum cha maandalizi ya Kambi za Kitaaluma kwa wanafunzi wa kidato cha nne na Darasa la saba zinazotarajiwa kufanyika mwezi Juni kwa siku 21, kilichofanyika Shule ya Sekondari Bariadi.

RC MTAKA:TUTAWALINDA NA KUWATUNZA WANAFUNZI KIDATO CHA NNE, DARASA LA SABA WATAKAOKAA KAMBI ZA KITAALUMA MWEZI JUNI

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, mhe.Anthony Mtaka amewahakikishia wazazi wote mkoani humo kuwa Serikali itawalinda na kuwatunza watoto wote kwa muda wa siku zote watakaokuwa katika Kambi za Kitaaluma kwa Kidato cha Nne na Darasa la Saba, ambazo zinazotarajiwa kuanza rasmi mapema mwezi Juni mwaka huu kwa mkoa mzima.


Mtaka ameyasema hayo alipokuwa akizungumza na Wenyeviti wa Kamati na Bodi za Shule katika Shule ya Msingi Mshikamano Wilayani Meatu katika kikao maalum kilicholenga  kujadiliana juu ya maandalizi ya Kambi hizo Wilayani humo.

Amesema Serikali imebeba dhamana ya  kuwaweka wanafunzi kambini kwa lengo la kuwaandaa vema ili waweze kufanya vizuri katika mitihani yao na kuongeza ufaulu, hivyo haitawafumbia macho wale wote watakaoonekana kwa njia moja ama nyingine kuharibu jitihada hizo.

“Nawaambia hapa wananchi wa Meatu, kambi za wanafunzi wetu za kitaaluma mziogope kama ukoma, sisi hatuwezi kubeba dhamana ya watoto wa watu kwenda kwenye makambi halafu aje mtu anajipitisha pitisha kwenye kambi kufuatilia na kutaka kuwarubuni watoto wetu wa kike, nawaeleza hapa mtakuwa halali ya polisi” alisema Mtaka.

Ameongeza kuwa wakati wote wanafunzi watakapokuwa kambini Serikali itawawezesha walimu kupata stahili zao kutekeleza majukumu yao na kwa kushirikiana na wadau wengine itatoa mahitaji maalum kwa wanafunzi wa kike, hivyo akawataka wazazi kujiandaa kuchangia chakula kwa ajili ya watoto wao ambacho ni sehemu ya kile ambacho kingetumika wakiwa nao nyumbani.

Aidha, Mtaka amewataka wazazi, walimu kushikamana na Serikali katika kufikia azma ya kufanya mapinduzi ya Elimu mkoani Simiyu kwa kila mmoja kutimiza wajibu wake badala ya kuwatupia lawama walimu pekee kila wanafunzi wanapofanya vibaya katika mitihani yao, kwa kuwa ufaulu wa mwanafunzi unategemea  ushirikiano katika ya walimu, wazazi na wanafunzi.

Kwa upande wao Wenyeviti wa Bodi na Kamati za Shule wamepongeza kuwepo kwa kambi hizo za Kitaaluma na wakakiri kuwa kambi hizo zinaweza kuwa suluhu ya kuondokana na daraja la nne na sifuri kwa kidato cha nne na kuongeza ufaulu kwa wanafunzi wa darasa la saba na wakatoa maoni yao.

“ Binafsi nampongeza Mkuu wa mkoa kwa kuja na wazo hili la kufanya makambi ya kitaaluma kwenye mkoa wetu, napendekeza kambi hizi zisiishie kwenye hizo siku 21 za mwezi wa sita tu,  wazazi tushikamane tuchange chakula watoto wetu wakae kambi hata mwezi wa tisa” alisema Mchungaji Fabian Kuzenza.

“Naunga mkono kuwepo makambi ya kitaaluma na namsukuru Mkuu wa Mkoa kuzungumza na sisi,  hii imetusaidia kuwa na uelewa wa pamoja naomba pia atusaidie wajumbe wetu wa kamati za shule wapewe mafunzo wawe na uelewa mpana wa masuala mbalimbali, ili wawe wanawaeleza wazazi mambo wanayoyafahamu” Elias Kamweji Mwenyekiti Kamati ya Shule ya Msingi Paji.

Mwezi Juni mwaka huu Wilaya zote mkoani Simiyu zitafungua Kambi za Kitaaluma kwa wanafunzi wa Kidato cha Nne na Darasa la Saba kwa muda wa siku 21 na katika siku hizo wanafunzi wote watafanya mtihani wa majaribio kwa ajili ya maandalizi ya Mitihani ya Kitaifa iliyo mbele yao
MWISHO

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka akizungumza na Wenyeviti wa Kamati na  Bodi za Shule za Wilaya ya Meatu (hawapo pichani) , katika kikao maalum cha maandalizi ya Kambi za Kitaaluma kwa wanafunzi wa kidato cha nne na Darasa la Saba zinazotarajiwa kufanyika mwezi Juni kwa siku 21, kilichofanyika Shule ya msingi Mshikamano
Baadhi ya Wenyeviti wa Bodi na Kamati za Shule wa Wilaya ya Meatu, wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka (hayupo pichani) katika kikao maalum cha maandalizi ya Kambi za Kitaaluma kwa wanafunzi wa kidato cha nne na Darasa la saba zinazotarajiwa kufanyika mwezi Juni kwa siku 21, kilichofanyika Shule ya msingi Mshikamano

Mkuu wa Wilaya ya Meatu, Mhe. Dkt. Joseph Chilongani ( wa kwanza mstari wa mbele)  na viongozi wengine wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka( hayupo pichani) alipokuwa akizungumza na Wenyeviti wa Kamati na  Bodi za Shule za Wilaya hiyo  (hawapo pichani) , katika kikao maalum cha maandalizi ya Kambi za Kitaaluma kwa wanafunzi wa kidato cha nne na Darasa la Saba, kilichofanyika Shule ya msingi Mshikamano.
Mchungaji Fabian Kuzenza akichangia hoja katika kikao cha Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka na Wenyeviti wa Kamati na  Bodi za Shule za Wilaya ya Meatu (hawapo pichani) , katika kikao maalum cha maandalizi ya Kambi za Kitaaluma kwa wanafunzi wa kidato cha nne na Darasa la Saba zinazotarajiwa kufanyika mwezi Juni kwa siku 21, kilichofanyika Shule ya msingi Mshikamano,
Bi. Minza Sibaba Mjumbe Bodi ya Shule Nyanza akichangia hoja katika kikao cha Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka na Wenyeviti wa Kamati na  Bodi za Shule za Wilaya ya Meatu (hawapo pichani) , katika kikao maalum cha maandalizi ya Kambi za Kitaaluma kwa wanafunzi wa kidato cha nne na Darasa la Saba zinazotarajiwa kufanyika mwezi Juni kwa siku 21, kilichofanyika Shule ya msingi Mshikamano.
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Meatu, Bw. Fabian Manoza akifafanua jambo katika kikao cha Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka na Wenyeviti wa Kamati na  Bodi za Shule za Wilaya hiyo, katika kikao maalum cha maandalizi ya Kambi za Kitaaluma kwa wanafunzi wa kidato cha nne na Darasa la Saba zinazotarajiwa kufanyika mwezi Juni kwa siku 21, kilichofanyika Shule ya msingi Mshikamano.
Baadhi ya Wenyeviti wa Bodi na Kamati za Shule wa Wilaya ya Meatu, wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka (hayupo pichani) katika kikao maalum cha maandalizi ya Kambi za Kitaaluma kwa wanafunzi wa kidato cha nne na Darasa la saba zinazotarajiwa kufanyika mwezi Juni kwa siku 21, kilichofanyika Shule ya msingi Mshikamano.

CHUO CHA MIPANGO WASHUKURU UONGOZI MKOA WA SIMIYU KWA KUWAPA ENEO LA KUJENGA TAWI LAO MJINI BARIADI

Baraza la Uongozi wa Chuo cha Mipango Dodoma limeushukuru , uongozi wa Mkoa wa Simiyu kwa kukubali kutoa eneo la ekari 50 bure kwa ajili ya ujenzi wa Tawi jipya la chuo hicho , katika Kata ya Nyakabindi Halmashauri ya Mji wa Bariadi.

Shukrani hizo zimetolewa na Kaimu Mwenyekiti wa  Baraza la Uongozi wa Chuo cha Mipango Bibi.Mugabe Mtani , katika mazungumzo maalum na viongozi wa Mkoa wa Simiyu muda mfupi kabla ya kikao cha Baraza hilo  kilichofanyika mkoani Simiyu.

Kaimu Mwenyekiti  wa Baraza la Uongozi wa Chuo cha Mipango Bibi. Mugabe Mtani  ameshukuru  kwa niaba ya Chuo hicho  kwa kupewa eneo hilo ambalo litawawezesha kujenga miundombinu ya kutosha ya chuo hicho katika Mkoa wa Simiyu.

 “Tunashukuru sana uongozi wa Mkoa wa Simiyu kwa kutupa hili eneo kubwa katika wakati huu ambao sisi tunaona ni wakati muafaka kwa sababu tulikuwa kwenye mkakati wa kutafuta eneo la kujenga, pale Mwanza tuna eneo ambalo kama tungelitumia lingetugharimu fedha nyingi kuliko hili la Simiyu kwa sababu liko kwenye mawe” alisema Mtani.

Kwa upande wake Kaimu Mkuu wa Chuo cha Mipango, Hozen Mayaya amesema iwapo chuo hicho kitakamilika kujengwa  kitasaidia kutoa mafunzo ya maendeleo vijijini na hivyo kusaidia upatikanaji wa watalaam hapa nchini wakiwemo wa mipango pamoja na kusaidia katika ufanyaji wa tafiti mbalimbali.

Ameongeza kuwa upatikanaji wa eneo hilo utasaidia lengo la Chuo la kuwa vituo vingi kadri mahitaji yanavyoongezeka jambo ambalo litasaidia pia kusogeza huduma karibu na wananchi.

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi ambako eneo hilo lipo, Bw. Melkizedeck Humbe amesema Chuo cha Mipango kitapojengwa Mkoani Simiyu kitakuwa msaada mkubwa kwa Mkoa huo ambao unajipambanua kwa Uchumi wa viwanda.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka amesema kuwepo kwa chuo hicho kutaongeza hamasa ya elimu kwa vijana wanaomaliza  elimu ya sekondari na kidato cha sita kujiunga na vyuo vya elimu ya juu ,huku akitoa wito kwa  Taasisi zingine za umma na binafsi kuwekeza katika sekta ya elimu.

“ Sisi kama Mkoa tunatoa fursa kwa Wakuu wote wa Vyuo Vikuu hapa nchini wanaotaka kujenga matawi ya Vyuo vyao ili waondokane na kulipa fedha nyingi kwa ajili ya pango la majengo, mkoa wa Simiyu unawaakaribisha na tunawahakikishia upatikanaji wa Ardhi Bure” alisema Mtaka.

MWISHO:

Kaimu Mwenyekiti  wa Baraza la Uongozi wa Chuo cha Mipango Bibi. Mugabe Mtani akizungumza na viongozi wa Mkoa wa Simiyu mara baada ya kuwasili mjini Bariadi kwa ajili ya kikao cha Baraza hilo  na kuona eneo lililotolewa na Mkoa huo kwa ajili ya kujenga Tawi la Chuo hicho mkoani Simiyu.
Kaimu Mkuu wa Chuo cha Mipango Hozen Mayaya akizungumza na viongozi wa Mkoa wa Simiyu mara baada ya kuwasili mjini Bariadi kwa ajili ya kikao cha Baraza la Uongozi wa Chuo hicho  na kuona eneo lililotolewa na Mkoa huo kwa ajili ya kujenga Tawi la Chuo hicho mkoani Simiyu.
Katibu Tawala Mkoa wa Simiyu, Ndg Jumanne Sagini akizungumza na baadhi ya wajumbe wa Baraza la Uongozi wa Chuo cha Mipango waliofika Mkoani humo  kwa ajili ya kikao cha Baraza hilo na kuona eneo lililotolewa na Mkoa huo kwa ajili ya kujenga Tawi la Chuo hicho mkoani Simiyu.
Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe.Festo Kiswaga akiwakaribisha  wajumbe wa Baraza la Uongozi wa Chuo cha Mipango waliofika  Mjini Bariadi kwa ajili ya kikao cha Baraza hilo na kuona eneo lililotolewa na Mkoa wa Simiyu  kwa ajili ya kujenga Tawi la Chuo hicho mkoani Simiyu.
Kaimu  Mwenyekiti  wa Baraza la Uongozi wa Chuo cha Mipango Bibi. Mugabe Mtani akisaini kitabu cha wageni katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu mara baada ya kuwasili mjini Bariadi kwa ajili ya kikao cha Baraza hilo na kuona eneo lililotolewa na Mkoa huo kwa ajili ya kujenga Tawi la Chuo hicho mkoani Simiyu.
Katibu Tawala Mkoa wa Simiyu, Ndg Jumanne Sagini akifurahia jambo na mmoja wa wajumbe wa Baraza la Uongozi wa Chuo  cha Mipango waliofika Mkoani humo  kwa ajili ya kikao cha Baraza hilo na kuona eneo lililotolewa na Mkoa huo kwa ajili ya kujenga Tawi la Chuo hicho mkoani Simiyu,
Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga (kulia), Kaimu Mwenyekiti  wa Baraza la Uongozi wa Chuo cha Mipango Bibi. Mugabe Mtani (kushoto) wakifuatilia bbadhi ya hoja zilizokuwa zikiwasilishwa na wajumbe wa Baraza hilo waliofika Mjini Bariadi kwa ajili ya kikao cha Baraza hilo  na kuona eneo lililotolewa na Mkoa huo kwa ajili ya kujenga Tawi la Chuo hicho mkoani Simiyu.

Kaimu Mkuu wa Chuo cha Mipango Hozen Mayaya(kulia) na baadhi ya wajumbe wa Baraza la Uongozi wa Chuo hicho wakifuatilia mazungumzo kati ya viongozi wa mkoa wa Simiyu na Kaimu Mwenyekiti  wa Baraza la Uongozi wa Chuo hicho Bibi. Mugabe Mtani (hawapo pichani) walipofika Mjini Bariadi kwa ajili ya kikao cha Baraza hilo na kuona eneo lililotolewa na Mkoa huo kwa ajili ya kujenga Tawi la Chuo hicho mkoani Simiyu.

Thursday, May 24, 2018

RC MTAKA ASHAURI TFDA KUFUNGUA OFISI KATIKA MIKOA


Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka ameishauri Mamlaka ya Chakula na Dawa hapa nchini (TFDA) kufungua Ofisi katika Mikoa ili kusogeza huduma karibu na wananchi na kuongeza ufanisi hususani katika kipindi hiki ambacho Serikali ya awamu ya Tano inahimiza utekelezaji wa ajenda ya Viwanda.

Mtaka ameyasema hayo Mei 23 wakati akifungua kikao kazi cha Wahariri na waandishi wa habari wa mikoa ya Simiyu na Mara kilicholenga kuhamasisha Sheria ya Chakula, dawa na vipodozi sura Na.219, ambacho kilifanyika Mjini Bariadi.

Amesema wakati huu ambao Sera ya Viwanda ni kipaumbele cha nchi ni vema Ofisi za TFDA zikawepo katika kila Makao Makuu ya  mkoa ili pale watu wanapotaka kujenga viwanda vitakavyozalishwa dawa, chakula na vipodozi waweze kupata huduma zinazotakiwa kwa wakati badala ya kufuata huduma katika ofisi za kanda.

“Mhe. Rais anapohimiza ajenda ya viwanda kwenye nchi TFDA inabidi ione umuhimu wa kuwa na Ofisi kwenye mikoa, ili mfano watu wa Simiyu wanapohitaji kufungua kiwanda cha bidhaa ambazo zinaihusu TFDA wasilazimike kwenda Mwanza kufauta huduma” alisema.

Aidha, Mtaka ameishauri Mamlaka ya Chakula na Dawa Nchini - TFDA  kutoa ufafanuzi wa mara kwa mara kuhusu dawa, chakula na vipodozi kupitia  vyombo vya habari,  ili jamii iweze kuwa na uelewa mpana wa madhara yatokanayo matumizi na bidhaa bandia na zenye madhara kwa binadamu.

Katika hatua nyingine Mkuu huyo wa mkoa ametoa wito kwa waandishi wa habari baada ya kupata mafunzo kutoka TFDA kuwa mabalozi  wazuri wa TFDA katika kufafanua masuala yote yenye sintofahamu na kuandika habari za kiuchunguzi zilizofanyiwa utafiti kuhusu dawa, chakula na vipodozi.

Naye Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TFDA, Bi Agnes Sitta Kijo amewataka Waandishi wa habari kutoa taarifa pale wanapobaini uwepo bidhaa ambazo si salama kwa matumizi ya binadamu huku akiwasisitiza kujikita katika uandishi wa Habari za kiuchunguzi.

Baadhi ya washiriki wa kikao kazi hicho kutoka Mikoa ya Simiyu na Mara wamesema mafuzo waliyapata yamewasaidia kupata uelewa wa Sheria ya ya Chakula, dawa na vipodozi sura Na.219 na masuala mbalimbali yahusuyo chakula, dawa na vipodozi hivyo watakuwa mabalozi wazuri watakaowasaidia wananchi kupata uelewa juu ya masuala hayo.

“ Elimu niliyoipata imenisaidia na kupitia elimu hii kuhusu masuala ya chakula, dawa na vipodozi mimi kama mwandishi nitakuwa balozi mzuri ili kuwasaidia wananchi kujua madhara ya bidhaa zisizo salama kwa afya ya binadamu” alisema Shushu Joel kutoka Simiyu.

“Mafunzo haya yatatusaidia waandishi habari kujikita katika kuandika habari za kiuchunguzi zitakazowasaidia wananchi kujua madhara ya bidhaa zisizo salama kwa afya ya binadamu ” alisema Frankius Cleopas Mwandishi kutoka mkoani Mara.
MWISHO


Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka akifungua kikao kazi cha Wahariri na waandishi wa habari wa mikoa ya Simiyu na Mara kilicholenga kuhamasisha wa sheria ya Chakula, dawa na vipodozi sura Na.219, ambacho kilifanyika Mjini Bariadi.




Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TFDA, Bi Agnes Sitta Kijo akizungumza na Wahariri na waandishi wa habari wa mikoa ya Simiyu na Mara katika kikao kazi kilicholenga kuhamasisha wa sheria ya Chakula, dawa na vipodozi sura Na.219, ambacho kilifanyika Mjini Bariadi
Baadhi ya Wahariri na waandishi wa habari wa mikoa ya Simiyu na Mara katika wakiwa katika kikao kazi kilicholenga kuhamasisha wa sheria ya Chakula, dawa na vipodozi sura Na.219, ambacho kilifanyika Mjini Bariadi.
Baadhi ya Wahariri na waandishi wa habari wa mikoa ya Simiyu na Mara katika wakiwa katika kikao kazi kilicholenga kuhamasisha wa sheria ya Chakula, dawa na vipodozi sura Na.219, ambacho kilifanyika Mjini Bariadi.
Kutoka kushoto Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TFDA, Bi Agnes Sitta Kijo, Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka na Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe.Festo Kiswaga wakifuatilia kikao kazi cha wahariri na waandishi wa habari wa mikoa ya Simiyu na Mara kilicholenga kuhamasisha wa sheria ya Chakula, dawa na vipodozi sura Na.219, ambacho kilifanyika Mjini Bariadi.
Baadhi ya Maafisa kutoka Mamlaka ya Chakula na Dawa(TFDA) wakiteta jambo katika kikao kazi cha wahariri na waandishi wa habari wa mikoa ya Simiyu na Mara kilicholenga kuhamasisha wa sheria ya Chakula, dawa na vipodozi sura Na.219, ambacho kilifanyika Mjini Bariadi.

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!