Saturday, September 22, 2018

RC MTAKA, ASKOFU KANISA LA SDA WATOA SALAMU ZA POLE KUFUATIA AJALI YA MV NYERERE


Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka na Askofu wa Kanisa la Waadventista Wasabato Jimbo la Kusini mwa Tanzania, Mark Malekana,wametoa salamu za pole kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. John Mongela, wananchi wa Mwanza pamoja na familia na ndugu wa waliopoteza maisha katika ajali ya kuzama kwa Kivuko cha MV Nyerere iliyotokea Septemba 20, 2018 huko Ukerewe Mwanza.

Wakitoa salamu hizo kwa nyakati tofauti Septemba 22, 2018  wakati wa kufunga makambi ya Waadiventista Wasabato katika Uwanja wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi Mkoani Simiyu, Mhe. Mtaka na Askofu Malekana wamewaombea majeruhi wote wapone haraka na kurejea katika majukumu yao.

Kwa upande wake mkuu wa Mkoa wa Simiyu amasema msiba huo mkubwa umewagusa watu wengi ikiwepo mkoa waSimiyu ambapo mwalimu mmoja kutoka katika Kata ya Kalemela wilayani Busega amepoteza maisha katika ajali hiyo.

“Mkoa wa Simiyu katika wilaya ya Busega mwalimu wetu mmoja wa Shule ya msingi katika kata ya Kalemela, Mwalimu Mtaki  amefariki kwenye ajali hii alikuwa naenda kusalimia wazazi wake, huu ni msiba ambao umegusa maeneo mengi”

“ Kwa niaba ya wananchi wote wa mkoa wa Simiyu tunatoa salamu za pole kwanza kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. John Mongela, wananchi wa Mwanza lakini zaidi pole kwa familia ambazo zimeguswa na jambo hili tunawaombea kwa Mwenyezi Mungu marehemu wote na wale ambao wamenusurika Mungu aendelee kuwaimarisha wapone haraka” alisema Mtaka

Ameongeza kuwa Viongozi wa Mkoa wa Simiyu siku ya Jumapili tarehe 23 Septemba, 2018 wataungana na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa,  viongozi wa Mkoa wa Mwanza, viongozi wengine wa Serikali katika tukio la kuwahifadhi waliopoteza maisha katika ajali hiyo.

Naye Askofu wa Kanisa la Waadventista Wasabato Jimbo la Kusini mwa Tanzania, Mark Malekana amesema “Kwa niaba ya Kanisa la Waadventista Wasabato na washiriki wote napenda kutoa salamu za pole kwanza kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. John Mongela, wananchi wa Mwanza kwa msiba huu mzito ulioleta majonzi kwetu Watanzania”

“Kanisa pia linatoa pole kwa familia zilizoguswa na ajali hii na ni ombi la kanisa kwamba wale ambao walijeruhiwa Mungu awapatie uponyaji wa haraka na wale ambao wamelala ambao waliweka maisha yao kwa Yesu ahadi ni kwamba Yesu atakapokuja mara ya pili atawaita kutoka makaburini" alisema Askofu Malekana

Ameongeza kuwa Kanisa linaungana na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli, viongozi wengine na wananchi kuomba utulivu na mshikamano wakati huu wa majonzi.
MWISHO.




Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka akitoa salamu za pole kwa niaba ya wananchi wa mkoa huo, kufuatia vifo vilivyotokana na ajali ya kuzama kwa Kivuko cha MV Nyerere huko Ukerewe mkoani Mwanza, Septemba 20, 2018, salamu hizo zimetolewa wakati wa kufunga makambi ya Waadiventista Wasabato Septemba 22, 2018 katika Uwanja wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi Mkoani Simiyu. 



Askofu wa Kanisa la Waadventista Wasabato Jimbo la Kusini mwa Tanzania, Mark Malekana akitoa salamu za pole kwa niaba ya Kanisa hilo, kufuatia vifo vilivyotokana na ajali ya kuzama kwa Kivuko cha MV Nyerere huko Ukerewe mkoani Mwanza, Septemba 20, 2018, salamu hizo zimetolewa wakati wa kufunga makambi ya Waadiventista Wasabato  Septemba 22, 2018 katika Uwanja wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi Mkoani Simiyu.



Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka na Askofu wa Kanisa la Waadventista Wasabato Jimbo la Kusini mwa Tanzania, Mark Malekana wakiteta jambo wakati wa kufunga makambi ya Waadiventista Wasabato Septemba 22, 2018  katika Uwanja wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi Mkoani Simiyu.
Askofu wa Kanisa la Waadventista Wasabato Jimbo la Kusini mwa Tanzania, Mark Malekana(kushoto) akimkaribisha Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka azungumze na Waumini  wa Kanisa la Waadiventista Wasabato wakati wa kufunga makambi ya Waadiventista Wasabato Septemba 22, 2018 katika Uwanja wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi Mkoani Simiyu.
Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga akizungumza na Waumini wa wa Kanisa la Waadiventista Wasabato wakati wa kufunga makambi ya Waadiventista Wasabato Septemba 22, 2018 katika Uwanja wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi Mkoani Simiyu.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka(kushoto)  akizungumza na Kiongozi wa ATAPE mkoa wa Simiyu, Mhandisi. Paul Jidayi mara baada ya kufunga makambi ya Waadiventista Wasabato Septemba 22, 2018 katika Uwanja wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi Mkoani Simiyu.

Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga(kushoto)  akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wachungaji wa Kanisa la Waadiventista Wasabato wakifuatilia Hotuba ya mkuu wa mkoa wa Simiyu , Mhe. Anthony Mtaka(hayupo pichani)  wakati wa kufunga makambi ya Waadiventista Wasabato Septemba 22, 2018 katika Uwanja wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi Mkoani Simiyu.
Askofu wa Kanisa la Waadventista Wasabato Jimbo la Kusini mwa Tanzania, Mark Malekana akifurahia jambo wakati Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka alipozungumza na  Waumini  wa Kanisa hilo katika  kufunga makambi yao Septemba 22, 2018 katika Uwanja wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi Mkoani Simiyu.

Waimbaji wa Kwaya ya Kanisa la Waadventista Wasabato Kurasini wakimtukuza Mungu kwa nyimbo wakati wa kufunga makambi ya kanisa hilo  Septemba 22, 2018 katika Uwanja wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi Mkoani Simiyu.
Baadhi ya Waumini wa wa Kanisa la Waadiventista Wasabato wakifuatilia hotuba ya Mkuu wa  Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka  wakati wa kufunga makambi ya Waadiventista Wasabato Septemba 22, 2018 katika Uwanja wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi Mkoani Simiyu.
Watoto wa Waumini wa Kanisa la Waadiventista Wasabato wakionesha mambo mbalimbali waliyojifunza katika makambi Mjini Bariadi yliyofungwa Septemba 22, 2018 Mjini Bariadi.


Waimbaji wa Kwaya ya AY Nyarugusu Kanisa la Waadventista Wasabato Geita wakimtukuza Mungu kwa nyimbo wakati wa kufunga makambi ya kanisa hilo  Septemba 22, 2018 katika Uwanja wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi Mkoani Simiyu.


Baadhi ya Waumini wa wa Kanisa la Waadiventista Wasabato wakifuatilia hotuba ya Mkuu wa  Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka  wakati wa kufunga makambi ya Waadiventista Wasabato Septemba 22, 2018 katika Uwanja wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi Mkoani Simiyu.

Baadhi ya Waumini wa wa Kanisa la Waadiventista Wasabato wakifuatilia hotuba ya Mkuu wa  Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka  wakati wa kufunga makambi ya Waadiventista Wasabato Septemba 22, 2018 katika Uwanja wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi Mkoani Simiyu.

0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!