Wednesday, January 11, 2017

RAIS MAGUFULI AAGIZA ZABUNI YA UJENZI WA BARABARA YA BARIADI-MASWA KWA KIWANGO CHA LAMI ITANGAZWE

Na Stella Kalinga
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt John Pombe Joseph Magufuli amemuagiza Waziri wa Ujenzi,Uchukuzi na Mawasiliano, Mhe.Prof.Makame Mbarawa kuhakikisha zabuni ya ujenzi wa kipande cha barabara ya Bariadi hadi Maswa yenye urefu kilomita 49.2 kutangazwa ndani ya wiki moja kuanzia leo(11 Januari,2017).

Rais Magufuli ametoa agizo hilo leo wakati alipokuwa akiwahutubia wananchi wa Bariadi mkoani Simiyu katika uwanja wa Shule ya Msingi Somanda,  mara baada ya kufungua barabara ya kutoka Lamadi hadi Bariadi yanye urefu wa kilomita 71.8 akiwa katika ziara ya siku mbili mkoani Simiyu.

Mhe.Magufuli amesema Barabara ya Lamadi-Bariadi imekamilika kwa kutumia fedha za Serikali na kwa upande wa Barabara ya Maswa –Mwigumbi mkandarasi anaendela na kazi hivyo zabuni ya kipande kilichobakia cha Braidi Maswa itangazwe ili barabara ya lami kutoa Lamadi hadi Mwigumbi (Shinyanga) ikamilike kwa lengo la kurahisisha uchukuzi.

Aidha, Mhe.Rais Magufuli amesema endapo kutakuwa na barabara ya lami kutoka Lamadi(Busega) hadi Mwigumbi(Shinyanga) kutapunguza umbali wa kilomita zaidi ya 100 kwa watu watakakuwa wakisafiri kutoka Nairobi kwa kupitia Lamadi-Bariadi-Maswa-Mwigumbi ambao kwa sasa wanazunguka kupitia Mkoa wa Mwanza.

Mhe.Rais Magufuli ameongeza kuwa kukamilika kwa barabara hiyo kutaongeza wigo wa biashara kwa mkoa wa Simiyu   hivyo akawataka wananchi wa Simiyu kutunza barabara hiyo iliyokamilika(kipande chaLamadi-Bariadi) kwa kuacha kung’oa alama za barabarani.

Serikali imetimiza wajibu wake kwa kuwajengea barabara kwa fedha zake ili ninyi watu wa Simiyu mpata barabara, wajibu wenu ni kuitunza na muitunze kweli kweli”

Kwa upande wake Waziri wa Ujenzi,Uchukuzi na Mawasiliano ametoa wito kwa madereva kuacha kumwaga mafuta barabarani ili kuifanya barabara hiyo idumu na kuwa na uhai mrefu.

Hta hivyo Rais Magufuli ameupongeza uongozi wa Wakala wa Barabara (TANROADS) kwa kusimamia na kuhakikisha barabara ya Lamadi-Bariadi inakamilika ambapo amesema TANROADS imekuwa ikitekeleza majukumu yake vizuri hai iliyoifanya kushika nafasi ya tatu katika Bara la Afrika ikiongozwa na Wakala wa Barabara wa Afika Kusini na Namibia kwa kufanya kazi zenye ubora.

Wakati huo huo Rais Magufuli amempongeza Mkuu wa mkoa wa Simiyu kwa kuanza kutekelza sera ya Tanzania kwa vitendo kwa kuanziisha kiwanda cha kutengeneza chaki (Maswa), Kiwanda cha kusindika maziwa ( Meatu) jambo ambalo linasaidia katika kutoa ajira kwa watanzania; akawataka wakuu wa mikoa wengine kuiga mfano huo.

Rais Magufuli yupo katika ziara ya siku mbili mkoani Simiyu ambapo leo amepata fursa ya kuzungumza na wananchi wa wilaya ya Busega na Bariadi pamoja na kuweka Jiwe la Msingi katika Hospitali ya Mkoa wa Simiyu na kufungua barabara ya Lamadi-Bariadi yenye urefu wa Kilomita 71.8.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt John Pombe Joseph Magufuli akifungua barabara ya Lamadi-Bariadi Mjini Bariadi yenye urefu wa kilomita 71.8 iliyojengwa kwa kiwango cha lami, wakati wa ziara yake ya siku mbili mkoani Simiyu
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt John Pombe Joseph Magufuli akikata utepe kama ishara ya kufungua barabara ya Lamadi-Bariadi Mjini Bariadi yenye urefu wa kilomita 71.8 iliyojengwa kwa kiwango cha lami, wakati wa ziara yake ya siku mbili mkoani Simiyu.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt John Pombe Joseph Magufuli akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi wa Mkoa wa Simiyu, Wizara ya Ujenzi,Uchukuzi na Mawasiliano na Wakala wa Barabara (TANROADS) baada ya kufungua barabara ya Lamadi-Bariadi Mjini Bariadi yenye urefu wa kilomita 71.8 iliyojengwa kwa kiwango cha lami, wakati wa ziara yake ya siku mbili mkoani Simiyu


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt John Pombe Joseph Magufuli akiwa katika picha ya pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Simiyu(kulia) na Vingozi wa Madhehebu ya Dini baada ya kufungua barabara ya Lamadi-Bariadi Mjini Bariadi yenye urefu wa kilomita 71.8 iliyojengwa kwa kiwango cha lami, wakati wa ziara yake ya siku mbili mkoani humo
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt John Pombe Joseph Magufuli akiwa katika picha ya pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Waziri wa Ujenzi,Uchukuzi na Mawasiliano na baadhi ya watendaji wa Wakala wa Barabara (TANROADS) baada ya kufungua barabara ya Lamadi-Bariadi Mjini Bariadi yenye urefu wa kilomita 71.8 iliyojengwa kwa kiwango cha lami, wakati wa ziara yake ya siku mbili mkoani Simiyu.

Jiwe la Ufunguzi lililowekwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt John Pombe Joseph Magufuli katika barabara ya Lamadi-Bariadi Mjini Bariadi yenye urefu wa kilomita 71.8 iliyojengwa kwa kiwango cha lami, wakati wa ziara yake ya siku mbili mkoani humo.



0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!