Sunday, January 8, 2017

MBUNGE AKABIDHI VYOMBO VYA KUPIKIA CHAKULA KWA SHULE ZA KUTWA SIMIYU

Na Stella Kalinga
Mbunge wa viti Maalum kupitia CCM Mkoa wa Simiyu,Mhe.Leah Komanya amekabidhi vyombo kwa ajili ya kupikia chakula cha Mchana katika shule za Msingi na Sekondari za Kutwa za Serikali Mkoani humo.

Makabidhiano hayo yameanyika jana katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu na kushuhudiwa na Wajumbe wa Kamati ya Ulinzi Mkoa, Maafisa Elimu, Waratibu wa Elimu Kata,Wakuu wa Shule na Walimu wakuu pamoja na Jumuiya ya Wanawake wa CCM (UWT) mkoa wa Simiyu.

Mhe.Komanya amekabidhi vyombo hivyo ili kutimiza ahadi yake aliyoitoa katika kikao cha Kamati ya Sherehe ya Mkoa mwishoni mwa mwezi Septemba, 2016 ya kuwasaidia wanafunzi kupata chakula shuleni kusoma na muda waliokuwa wanakwenda kutafuta chakula wautumie kwa ajili ya masomo.

Aidha, Mhe.Komanya amewaomba wadau wengine wa maendeleo kumuunga mkono katika kuchangia mahitaji mengine ya watoto yatakayowasaidia kupata chakula cha mchana.

Akizungumza kwa niaba ya Serikali ya Mkoa wa Simiyu, Mkuu wa Mkoa huo Mhe.Anthony Mtaka amemshukuru Mhe.Komanya kwa mchango wake huo ambao utakuwa msaada mkubwa katika maendeleo ya wanafunzi kitaaluma.

Aidha,Mhe.Mtaka amesema baada ya vikundi vya vijana kuanzisha miradi ya Usindikaji maziwa Meatu na utengenezaji wa Chaki Maswa wakishirikiana na Serikali anatamani kuwaona wanawake wa Jumuiya ya Wanawake wa CCM-UWT Mkoa wa Simiyu kutambua fursa zilizopo katika mkoa wao na kuanzisha miradi ya maendeleo.

Sambamba na hilo Mhe.Mtaka ameitaka Jumuiya hiyo kuanzisha miradi itakayojibu kero na matatizo ya jamii hususani wanawake ili wanawake na wasichana wenye matatizo wakimbilie kupata suluhu katika jumuiya badala ya kukaa na kusubiri shughuli za uchaguzi mkuu.

“Natamani kuiona UWT yenye maono na kubuni miradi itakayojibu kero za watu wanaowazunguka; natamani kuona mwanamke akipata tatizo aone msaada kutoka UWT na akimbilie UWT badala ya kutegemea taasisi za kijamii pekee” amesema Mtaka.

Wakati huo huo Mtaka amewataka wanawake wa jumuiya hiyo  na wanawake wengine kuwahamasisha watoto kwenda shue kwa kuwa watakapokula shuleni mchana watakuwa na uhakika wa kusoma vizuri na kufanya vizuri kitaaluma.

Mbunge Leah Komanya ametoa jumla ya sufuria 100 zenye ujazo wa lita 55 kwa kila moja ambazo zote zina thamani ya shilingi 5,000,000/=

Mbunge Viti Maalum Leah Komanya(kulia) akikabidhi sufuria alizozitoa kwa ajili yakupikia chakula cha mchana kwa shule za msingi na sekondari za kutwa Mkoani Simiyu,  kutoka kushoto Afisa Elimu Mkoa,Mwl.Julius Nestory, Mwenyekiti wa CCM Mkoa,Mhe.Titus Kamani,Mkuu wa Mkoa wa Simiyu,Mhe.Anthony Mtaka na wajumbe wengine wa UWT mkoa wa Simiyu.
Mkuu waMkoa wa Simiyu,Mhe.Anthony Mtaka(kushoto) akizungumza na viongozi wa mkoa huo na wajumbe wa Jumuiya ya Wanawake wa CCM katika makabidhiano ya vyombo vilivyotolewa na Mbunge Viti Maalum Mhe.Leah Komanya kwa ajili ya kupikia chakula cha mchana kwa shule za msingi na sekondari za kutwa mkoani humo .
Mbunge Viti Maalum Mkoa wa Simiyu Mhe.Leah Komanya (CCM) (kulia)akizungumza na viongozi wa mkoa huo na wajumbe wa Jumuiya ya Wanawake wa CCM katika makabidhiano ya vyombo alivyovitoa kwa ajili ya kupikia  chakula cha mchana kwa wanafunzi wa shule za msingi na sekondari za kutwa mkoani humo.
Baadhi ya viongozi na wanawake wanaounda Jumuiya ya Wanawake ya CCM (UWT) Mkoa wa Simiyu wakimsikiliza Mbunge Viti Maalum Mkoa wa Simiyu Mhe.Leah Komanya (CCM)(hayupo pichani) wakati wa makabidhiano ya vyombo alivyovitoa kwa ajili ya kupikia chakula cha mchana kwa wanafunzi wa shule za msingi na sekondari za kutwa mkoani humo.
Afisa Elimu Mkoa wa Simiyu,Mwl.Julius Nestory(wa pili kulia) akizungumza na viongozi wa mkoa huo na wajumbe wa Jumuiya ya Wanawake wa CCM katika makabidhiano ya vyombo vilivyotolewa na Mbunge Viti Maalum Mhe.Leah Komanya (CCM) kwa ajili ya kupikia chakula cha mchana kwa shule za msingi na sekondari za kutwa mkoani humo.
Mbunge Viti Maalum Mkoa wa Simiyu Mhe.Leah Komanya (CCM)(kushoto) akizungumza na baadhi ya wajumbe wa Kamti ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa mara baada ya makabidhiano ya vyombo alivyovitoa kwa ajili ya kupikia na chakula cha mchana kwa wanafunzi wa shule za msingi na sekondari za kutwa Mkoani humo.
Baadhi ya vyombo vya kupikia uji na chakula cha mchana kwa wananfunzi wa shule za msingina sekondari za kutwa mkoani Simiyu, vilivyotolewa na Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Simiyu,Mhe.Leah Komanya Mkoa wa Simiyu(CCM), vikishushwa kabla ya kukabidhiwa kwa uongozi wa mkoa huo

0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!