Sunday, January 8, 2017

WAFANYABIASHARA WA LAMADI KUANDALIWA MPANGO WA KUFANYA BIASHARA SAA 24

Na Stella Kalinga
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu amesema Serikali itaandaa mpango na utaratibu wa kuwawezesha wafanyabiashara wa kata ya Lamadi kufanya biashara zao kwa saa ishirini na nne.

Mtaka ameyasema hayo katika mkutano wa hadhara uliofanyika kata ya Lamadi wilayani Busega kwa lengo la kuhamasisha mpango wa Kilimo cha Umwagiliaji pamoja na kisikiliza kero za Wananchi na kuwapatia ufumbuzi wakati wa ziara yake wilayani humo.

Mtaka amesema Lamadi ni Kituo(centre) kikubwa cha biashara mkoani Simiyu ambacho watu kutoka mikoa na nchi mbalimbali wamekuwa wakipita hapo, hivyo ipo haja ya kukifanya kituo kikubwa zaidi kwa kukiwezesha kufanya kazi muda wote ili kuongeza kasi ya ukusanyaji wa kodi na ushuru na kuinua uchumi wa wananchi,Halmashauri ya Busega na Mkoa kwa ujumla.

“Watu wanatoka Kenya na mikoa mingine hapa nchini wakipita hapa saa tatu usiku baa, maduka na biashara nyingine zote zimefungwa; tunataka mapato ni lazima watu wafanye biashara ili tuyapate, naona ipo haja ya kuibadilisha Lamadi,  tutakaa na wenzetu wa Ulinzi na Usalama tuone namna nzuri itakayofaa kuwafanya wafanyabiashara wa makundi yote kufanya kazi muda wote wakiwa na uhakika wa usalama wao na biashara zao.” Alisema Mtaka.

Hata hivyo Mkuu huyo wa Mkoa amemtaka Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Busega kuweka viongozi sahihi na waadilifu katika Vijiji vya Kata ya Lamadi kwa kuwa ndiyo kata inayochangia kwa kiasi kikubwa mapato ya Halmashauri yake.

Sanjali na hilo Mhe.Mkuu wa Mkoa amewataka viongozi wa vijiji na Kata wa wilaya zote mkoani kwake kuhakikisha wanasoma taarifa ya  mapato na matumizi kwa wananchi kwa mujibu wa sheria na taratibu.

Wakati huo huo Mtaka amewahamasisha mpango wa kilimo cha umwagiliaji wilayani Busega ambao ameutambulisha kama kipaumbele cha mwaka 2017 kwa kuwashauri wajiorodheshe kwa viongozi wao wa vijiji na kujiunga katika vikundi ili watambuliwe na kuwezeshwa kwa pembejeo na miundombinu ya umwagiliaji.

Mtaka amesema Serikali iko tayari kuwasaidia wananchi hivyo watekeleze wajibu wao wa kulima na Serikali iko tayari kupeleka maji ili kuwaondoa wananchi wa Busega kwenye aibu ya kufa njaa wakati wana maji ya kudumu ya Ziwa Victoria.


Naye Chele Nkulima makaziwa Lamadi amempongeza Mkuu wa Mkoa kwa kuanzisha mpango huo wa kilimo cha umwagiliaji ambapo alimuomba Mkuu huyo wa Mkoa kuwasaidia wananchi wa Busega ili mradi huo uwafikie watu wote.


Mkuu wa Mkoa wa Simiyu yuko katika ziara ya siku 6 wilayani Busega ambapo anazungumza na wananchi kuelimisha na kuhamasisha wananchi kuhusu mpango wa kilimo cha umwagiliaji na kujibu kero mbalimbali za wananchiwa wilaya hiyo.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka (kulia) akizungumza na wananchi wa Kata ya Lamadi wilayani Busega katika Mkutano wa hadhara uliofanyika kwa lengo la kuwahamasisha kuhusu mpango wa kilimo cha umwagiliaji na kusikiliza kero zao na kuzipatia ufumbuzi.
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Busega,Ndg.Anderson Njiginya akizungumza na wananchi wa Kata ya Lamadi wilayani humo katika Mkutano wa hadhara ulioitishwa na Mkuu wa Mkoa wa Simiyu,Mhe. Anthony Mtaka kwa lengo la kuwahamasisha kuhusu mpango wa kilimo cha umwagiliaji na kusikiliza kero zao na kuzipatia ufumbuzi.
Mwenyekti wa CCM Mkoa wa Simiyu Mhe.Titus Kamani akizungumza na wananchi wa Kata ya Lamadi wilayani Busega  katika Mkutano wa hadhara ulioitishwa na Mkuu wa Mkoa wa Simiyu,Mhe. Anthony Mtaka kwa lengo la kuwahamasisha kuhusu mpango wa kilimo cha umwagiliaji na kusikiliza kero zao na kuzipatia ufumbuzi
Baadhi ya wananchi wa Kata ya Lamadi wilayani Busega wakimsikilizaMkuu wa Mkoa wa Simiyu,Mhe.Anthony Mtaka (hayupo pichani) katika Mkutano wa hadhara uliofanyika kwa lengo la kuwahamasisha kuhusu mpango wa kilimo cha umwagiliaji na kusikiliza kero zao na kuzipatia ufumbuzi.
Baadhi ya Viongozi na Maafisa waandamizi wa Mkoa wa Simiyu wakimsikilizaMkuu wa Mkoa huo ,Mhe.Anthony Mtaka (hayupo pichani) katika Mkutano wa hadhara uliofanyika kwa lengo la kuwahamasisha kuhusu mpango wa kilimo cha umwagiliaji na kusikiliza kero zao na kuzipatia ufumbuzi.
Baadhi ya wananchi wa Kata ya Lamadi wilayani Busega wakiwa wamejipanga kwa ajili ya kuwasilisha kero zao kwa  Mkuu wa Mkoa wa Simiyu,Mhe.Anthony Mtaka Busega katika Mkutano wa hadhara uliofanyika kwa lengo la kuwahamasisha kuhusu mpango wa kilimo cha umwagiliaji na kusikiliza kero zao na kuzipatia ufumbuzi.
Baadhi ya Wachungaji wa Makanisa ya Kipentekostiwa Kata ya Lamadi Wilayani Busega wakisali kabla ya kukabidhi mifuko ya saruji 10 waliyoitoa kwa ajili ya kuunga mkono juhudi za Serikali na wananchi katika ujenzi wa shule ya msingi Lamadi wilayani Busega.

0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!