Friday, January 20, 2017

JINGU ASEMA SIMIYU IMEONYESHA MFANO


Na Stella Kalinga
Mwenyekiti wa Baraza la Uwezeshaji wananchi Kiuchumi  ,Ndg. John Jingu amesema Mkoa wa Simiyu umeonesha mfano wa namna viongozi wanavyoweza kutumia nafasi zao katika kuwaletea wananchi maendeleo.

Jingu ameyasema hayo leo katika kikao maalum kilichofanyika kati ya Uongozi wa Baraza hilo na Viongozi wa Mkoa wa Simiyu katika Ofisi za Baraza hilo jijini Dar es Salaam.

Jingu amempongeza Mkuu wa mkoa wa Simiyu,Mhe.Anthony Mtaka na viongozi wenzake kwa kutambua dhamira ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli  katika kuwaletea wananchi maendeleo na kuitekeleza kwa vitendo.

“Tunaona namna mnavyofanya kazi na mnatembea kwenye maneno yenu, mmefanikiwa kuanzisha viwanda sasa hivi mnajipanga na kilimo cha umwagiliaji; mimi niseme tu kwamba tumepata mahali pa kujifunza na tutawashauri watu wengine waje wajifunze Simiyu” alisema Jingu.

Akizungumza katika kikao hicho Mkuu wa mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka amesema Serikali mkoani humo imedhamiria kuzalisha  mazao yote ambayo malighafi yake inapatikana hapa nchini, ikiwa ni pamoja na kuyaongezea thamani mazao yote yatokanayo na kilimo na mifugo.

Mtaka amesema wao kama mkoa wameanzisha mfumo wa kuendesha miradi mbalimbali kwa Ubia kati ya Sekta Binafsi na Serikali (PPP) ambapo katika miradi ya Kiwanda cha Chaki na Kiwanda cha maziwa ambayo imeanza kutekelezwa mkoani humo,  Halmashauri ya Wilaya ya Maswa na Meatu wamekuwa wakiendesha miradi hiyo kwa ubia na vikundi vya vijana.

“Tunataka ‘kutransform’ mkoa wetu ambao utakuwa ‘model’ katika kutekeleza dhamira ya Mhe.Rais, dhamira yangu na wenzangu ni kufanya kitu cha tofauti na tutafanya kwa kuwa tumeamua” alisema Mtaka.

Aidha , Mtaka ametoa wito kwa viongozi wa Baraza la Uwezeshaji Wanachi Kiuchumi kuwasaidia wananchi katika kufikia azma ya kuwa na Tanzania yenye uchumi wa kati.

Kwa upande wake Katibu Tawala Mkoa wa Simiyu,Ndg.Jumanne Sagini ameomba Baraza la Uwezeshaji la Taifa kushirikiana na Viongozi wa mkoa wa Simiyu kuwasaidia wananchi katika masuala mbalimbali ya kiuchumi ili kuleta matokeo chanya.

Wakati huo huo Afisa Kilimo wa Wilaya ya Busega Ndg.Juma Chacha ameomba Baraza la Uwezeshaji kupitia programu yake ya mfuko wa pembejeo za kilimo,  lishirikiane na Mkoa wa Simiyu kuwahakikishia wananchi uhakika wa pembejeo za kilimo ili kuwasaidia kuongeza uzalishaji.


Naye Katibu Mtendaji wa Baraza hilo, Bengi Issa amesema Baraza limekuwa likifanya kazi na makundi mbalimbali ya watu katika jamii kwa kuwashirikisha kujenga na kuendeleza uchumi,kuwepo kwa mazingira rafiki katika ufanyaji biashara,kupatikana kwa mitaji ya gharama nafuu, kuhimiza uwepo wa bidhaa bora na masoko,kuimarisha vyama vya ushirika na vikundi vya kiuchumi, kuhimiza matumizi bora ya ardhi na kuwahamasisha kushiriki katika masuala ya ubinafishaji ikiwa ni pamoja na ununuzi wa hisa za makampuni kupitia masoko ya hisa.
Mwenyekiti wa Baraza la uwezeshaji Wananchi Kiuchumi ,Ndg.John Jingu (wa pili kulia) akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi wa Mkoa wa Simiyu mara baada ya kumaliza kikao kati ya uongozi wa baraza na viongozi wa Simiyu Jijini Dar es Salaam, (kushoto) Katibu Mtendaji, Bengi Issa, (wa pili kushoto) Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka,( kulia) Katibu Tawala mkoa,Ndg.Jumanne Sagini.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu,Mhe.Anthony Mtaka  akizungumza katika kikao kilichofanyika kati ya viongozi wa mkoa huo na Viongozi wa Baraza la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi kilichofanyika jijini Dar es salaam
Katibu Mtendaji wa Baraza la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi akizungumza    katika kikao kilichofanyika kati ya viongozi wa mkoa wa Simiyu na Viongozi wa Baraza hilo kilichofanyika jijini Dar es salaam
Baadhi ya Viongozi wa Mkoa wa Simiyu wakimsikiliza Mwenyekiti wa Baraza la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi katika kikao kilichofanyika kati ya viongozi wa mkoa huo na Viongozi wa Baraza la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi kilichofanyika jijini Dar es salaam.

1 comment:


  1. Hello.
    Mimi ni Mr Rahel binafsi wakopeshaji mkopo ambao hutoa maisha wakati nafasi ya mkopo kwa watu binafsi, makampuni ya biashara, bima, nk Je, katika shida yoyote ya kifedha au katika haja ya mkopo wa kuwekeza au unahitaji mkopo kulipa bili yako kutafuta hakuna zaidi kama sisi ni hapa kufanya matatizo yako yote ya kifedha kitu cha zamani. Sisi kutoa kila aina ya mkopo katika dhehebu lolote fedha kwa kiwango cha 2% bila fee.I upfront wanataka kutumia kati hii kubwa ya kukufahamisha kwamba tuko tayari kukusaidia kwa aina yoyote ya mkopo kutatua kwamba tatizo.Kama yako ya kifedha ndiyo basi kupata nyuma sasa kupitia barua pepe (rahelcohranloan@gmail.com) kwa maelezo zaidi, wewe ni sana makala.

    ReplyDelete

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!