Tuesday, August 25, 2020

DARASA LA SABA, KIDATO CHA NNE SIMIYU WAAHIDI KUFUATA NYAYO ZA KIDATO CHA SITA KUBAKI TATU BORA KITAIFA

Wanafunzi wa Darasa la Saba na Kidato cha nne Mkoani Simiyu wameahidi kufuata nyayo za kidato cha Sita kuendelea kufanya vizuri katika mitihani yao ya Kitaifa na kubaki katika nafasi tatu bora Kitaifa kama walivyofanya Kidato cha Sita mwaka 2020 ambapo mkoa umekuwa wa tatu kati ya mikoa 29.

Hayo yamesemwa na baadhi ya wanafunzi wa darasa la saba shule ya msingi Somanda (B ) na kidato cha nne kutoka Shule ya sekondari Simiyu (Bariadi) waliowawakilisha wenzao katika hafla ya kuwapongeza walimu na wanafunzi waliofanya vizuri katika mtihani wa kidato cha sita iliyofanyika24 Agosti 2020 Mjini Bariadi

“Tunawapongeza dada na kaka zetu  kidato cha sita kwa kufanya vizuri kwenye mtihani wao wa taifa tunaahidi kufanya vizuri kama wao;Shule yetu ya msingi Somanda B ina mkakati wa kuingia katika shule kumi bora kitaifa na kutoa wanafunzi wanne katika wanafunzi kumi bora Kitaifa,tunaahidi hatutawaangusha,”alisema Ezra Paulo mwanafunzi wa darasa la saba Somanda.

“ Matokeo ya Kidato cha Sita yametuhamasisha kujipanga zaidi kwa mwaka 2020, kupitia fursa mbalimbali ambazo tunapewa na viongozi wetu zikiwemo kambi za kitaaluma tunapata fursa ya kujisomea zaidi kuliko tukikaa majumbani, tunaahidi kufanya vizuri zaidi ya dada na kaka zetu walivyofanya ikizingatiwa kuwa shule yetu inabeba jina la mkoa,” Sarah Ndamo kutoka Simiyu Sekondari.

Kwa upande wake mwanafunzi Benard S. Benard kutoka shule ya sekondari Binza wilayani Maswa ambaye amepata daraja la kwanza pointi nne, amewaasa wanafunzi wenzake kuongeza bidii katika masomo kushirikiana na kuutumia vizuri muda wanaokuwa shuleni ili waweze kufikia malengo yao.

Naye Mkuu wa Shule ya Sekondari Bariadi, Mwl. Ally Simba amesema siri kubwa ya wanafunzi wa shule hiyo kufanya vizuri zaidi na kuifanya kuwa ya kwanza kimkoa na ya 24 Kitaifa ni kufanya mitihani ya mara kwa mara huku akibainisha kuwa wamejipanga kuwa katika shule kumi bora Kitaifa na kuibadilisha shule hiyo ili iwe miongoni mwa shule maalum nchini.

Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mkuu wa Wilaya ya Bariadi Mhe. Festo Kiswaga amesema siri kubwa ya kufanya vizuri ni mikakati iliyowekwa na mkoa pamoja na utekelezaji wake ikiwa ni pamoja na kuwajengea wanafunzi uwezo wa kujiamini huku akisisitiza kila mdau atimize wajibu wake ili mkoa uendelee kufanya vizuri.

Afisa Elimu wa Mkoa wa Simiyu, Mwl. Ernest Hinju amesema mkoa umetimiza azma yake ya kutoka nafasi ya 10 mwaka 2019 na kuingia nafasi ya  tatu Kitaifa mwaka 2020 na kuongeza ufaulu kutoka GPA ya 3.0443 kufikia  2.894; huku akishauri kuwa ili Simiyu iendelee kufanya vizuri zaidi ni vema  ufundishaji makini uimarishwe zaidi..

Jumla ya wanafunzi 955 walisajiliwa kufanya mtihani wa Taifa wa Kidato cha Sita mwaka 2020 mkoani Simiyu, kati yao wanafunzi watano hawakufanya mtihani na katika wanafunzi 950 waliofanya mtihani, wanafunzi 208 wamepata daraja la kwanza,  507 wamepata daraja la pili, 228  daraja la tatu,  wanafunzi 06 wamepata daraja la nne  na mmoja amepata daraja sifuri.

Pamoja na kutoa shilingi laki moja kwa kila alama A iliyopatikana kwenye somo lake mwalimu aliyefanya vizuri,wanafunzi wawili waliopata daraja la kwanza pointi nne wamepewa shilingi laki mbili kila mmoja;  Mkoa pia umetambua mchango wa aliyekuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bw. Jumanne Sagini  katika kukuza sekta ya elimu kwa kumtunuku cheti.

MWISHO


Mkuu wa Wilaya ya Bariadi. Mhe. Festo Kiswaga akimkabidhi zawadi ya shilingi laki tano Mkuu wa Shule ya sekondari Bariadi, Mwl. Ally Simba iliyotolewa kama pongezi kwa shule hiyo kushika nafasi ya kwanza kati ya shule 10 mkoani Simiyu na ambayo imeshika nafasi ya 24 Kitaifa kati ya shule zaidi ya 500, katika hafla ya kuwapongeza walimu na wanafunzi waliofanya vizuri katika mtihani wa kidato cha sita ambapo mkoa wa Simiyu umeshika nafasi ya tatu Kitaifa.

Mkuu wa Wilaya ya Bariadi. Mhe. Festo Kiswaga akimkabidhi zawadi Mwanafunzi Benard S Benard .kutoka Shule ya Sekondari Binza wilayani Maswa aliyepata daraja la kwanza pointi nne, wakati wa hafla ya kuwapongeza walimu na wanafunzi waliofanya vizuri katika Mtihani wa Taifa wa kidato cha Sita mwaka 2020 ambapo mkoa wa Simiyu umeshika nafasi ya tatu Kitaifa, iliyofanyika Agosti 24, 2020 Mjini Bariadi.


Mkuu wa Wilaya ya Bariadi. Mhe. Festo Kiswaga akimkabidhi zawadi Mwanafunzi Mussa Abdallah kutoka Shule ya Sekondari Bariadi wilayani Bariadi aliyepata daraja la kwanza pointi nne, wakati wa hafla ya kuwapongeza walimu na wanafunzi waliofanya vizuri katika Mtihani wa Taifa wa kidato cha Sita mwaka 2020 ambapo mkoa wa Simiyu umeshika nafasi ya tatu Kitaifa, iliyofanyika Agosti 24, 2020 Mjini Bariadi.

Baadhi ya viongozi katika idara ya elimu, walimu, wanafunzi na wadau wa elimu wakifuatilia matukio mbalimbali katika hafla ya kuwapongeza walimu na wanafunzi waliofanya vizuri katika Mtihani wa Taifa wa kidato cha Sita mwaka 2020 ambapo mkoa wa Simiyu umeshika nafasi ya tatu Kitaifa, iliyofanyika Agosti 24, 2020 Mjini Bariadi.

Baadhi ya wanafunzi wa darasa la saba katika Shule ya Msingi Somanda B Mjini Bariadi wakieleza malengo yao katika kufikia nafasi ya kwanza kitaifa katika Mtihani wao wa Taifa, katika hafla ya kuwapongeza walimu na wanafunzi waliofanya vizuri katika Mtihani wa Taifa wa kidato cha Sita mwaka 2020 ambapo mkoa wa Simiyu umeshika nafasi ya tatu Kitaifa, iliyofanyika Agosti 24, 2020 Mjini Bariadi.
Kutoka kulia ni mwanafunzi Mussa Abdallah kutoka shule ya sekondari Bariadi, wilayani Bariadi na Benard Benard kutoka shule ya sekondari Binza wilayani Maswa waliofanya vizuri katika mtihani wa kidato cha sita kwa kupata “division one’ ya  pointi nne kila mmoja , wakiwa katika hafla ya kuwapongeza walimu na wanafunzi waliofanya vizuri katika Mtihani wa Taifa wa kidato cha Sita mwaka 2020 ambapo mkoa wa Simiyu umeshika nafasi ya tatu Kitaifa, iliyofanyika Agosti 24, 2020 Mjini Bariadi.

Mkuu wa Shule ya Sekondari ya wasichana Maswa, Mwl. Kuyunga Jackson akieleza jambo katika hafla ya kuwapongeza walimu na wanafunzi waliofanya vizuri katika Mtihani wa Taifa wa kidato cha Sita mwaka 2020 ambapo mkoa wa Simiyu umeshika nafasi ya tatu Kitaifa, iliyofanyika Agosti 24, 2020 Mjini Bariadi.

Shekhe wa mkoa wa Simiyu, Mahamoud Kalokola akieleza jambo katika hafla ya kuwapongeza walimu na wanafunzi waliofanya vizuri katika Mtihani wa Taifa wa kidato cha Sita mwaka 2020 ambapo mkoa wa Simiyu umeshika nafasi ya tatu Kitaifa, iliyofanyika Agosti 24, 2020 Mjini Bariadi.


Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bi. Miriam Mmbaga akieleza jambo katika hafla ya kuwapongeza walimu na wanafunzi waliofanya vizuri katika Mtihani wa Taifa wa kidato cha Sita mwaka 2020 ambapo mkoa wa Simiyu umeshika nafasi ya tatu Kitaifa, iliyofanyika Agosti 24, 2020 Mjini Bariadi.

Mchungaji wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Usharika wa Somanda Bw. Timotheo Alfred akieleza jambo katika hafla ya kuwapongeza walimu na wanafunzi waliofanya vizuri katika Mtihani wa Taifa wa kidato cha Sita mwaka 2020 ambapo mkoa wa Simiyu umeshika nafasi ya tatu Kitaifa, iliyofanyika Agosti 24, 2020 Mjini Bariadi.

Katibu wa CCM Mkoa wa Simiyu, Bi. Haula Kachwamba  akieleza jambo katika hafla ya kuwapongeza walimu na wanafunzi waliofanya vizuri katika Mtihani wa Taifa wa kidato cha Sita mwaka 2020 ambapo mkoa wa Simiyu umeshika nafasi ya tatu Kitaifa, iliyofanyika Agosti 24, 2020 Mjini Bariadi.

Baadhi ya viongozi kutoka katika Vyombo vya Ulinzi na Usalama mkoa wa Simiyu wakifuatilia matukio mbalimbali katika hafla ya kuwapongeza walimu na wanafunzi waliofanya vizuri katika Mtihani wa Taifa wa kidato cha Sita mwaka 2020 ambapo mkoa wa Simiyu umeshika nafasi ya tatu Kitaifa, iliyofanyika Agosti 24, 2020 Mjini Bariadi.

Mkuu wa Wilaya ya Maswa, mhe. Aswege Kaminyoge akieleza jambo katika hafla ya kuwapongeza walimu na wanafunzi waliofanya vizuri katika Mtihani wa Taifa wa kidato cha Sita mwaka 2020 ambapo mkoa wa Simiyu umeshika nafasi ya tatu Kitaifa, iliyofanyika Agosti 24, 2020 Mjini Bariadi.

Mkuu wa Wilaya ya Meatu, Dkt. Joseph Chilongani  akieleza jambo katika hafla ya kuwapongeza walimu na wanafunzi waliofanya vizuri katika Mtihani wa Taifa wa kidato cha Sita mwaka 2020 ambapo mkoa wa Simiyu umeshika nafasi ya tatu Kitaifa, iliyofanyika Agosti 24, 2020 Mjini Bariadi.


Baadhi  ya wanafunzi wa kidato cha nne shule ya sekondari ya Simyu Mjini Bariadi, wakieleza malengo yao katika kufikia nafasi ya kwanza kitaifa katika Mtihani wao wa Taifa, katika hafla ya kuwapongeza walimu na wanafunzi waliofanya vizuri katika Mtihani wa Taifa wa kidato cha Sita mwaka 2020 ambapo mkoa wa Simiyu umeshika nafasi ya tatu Kitaifa, iliyofanyika Agosti 24, 2020 Mjini Bariadi.

Mmoja wa walimu katika shule ya sekondari ya wasichana Maswa akipokea zawadi kutoka Mkuu wa Wilaya ya Bariadi. Mhe. Festo Kiswaga katika hafla ya kuwapongeza walimu na wanafunzi waliofanya vizuri katika Mtihani wa Taifa wa kidato cha Sita mwaka 2020 ambapo mkoa wa Simiyu umeshika nafasi ya tatu Kitaifa, iliyofanyika Agosti 24, 2020 Mjini Bariadi.

Baadhi ya walimu, wanafunzi na wadau wa elimu wakifuatilia matukio mbalimbali katika hafla ya kuwapongeza walimu na wanafunzi waliofanya vizuri katika Mtihani wa Taifa wa kidato cha Sita mwaka 2020 ambapo mkoa wa Simiyu umeshika nafasi ya tatu Kitaifa, iliyofanyika Agosti 24, 2020 Mjini Bariadi.

Mkuu wa Wilaya ya Bariadi. Mhe. Festo Kiswaga akimkabidhi zawadi Mwalimu wa Somo la Kiswahili katika shule ya sekondari Bariadi, Mwl. Makame S. Makame kutokana na yeye kufanya vizuri katika somo lake, katika hafla ya kuwapongeza walimu na wanafunzi waliofanya vizuri katika mtihani wa kidato cha sita ambapo mkoa wa Simiyu umeshika nafasi ya tatu Kitaifa, iliyofanyika Agosti 24, 2020 Mjini Bariadi.

Baadhi ya viongozi katika idara ya elimu, walimu, wanafunzi na wadau wa elimu wakifuatilia matukio mbalimbali katika hafla ya kuwapongeza walimu na wanafunzi waliofanya vizuri katika Mtihani wa Taifa wa kidato cha Sita mwaka 2020 ambapo mkoa wa Simiyu umeshika nafasi ya tatu Kitaifa, iliyofanyika Agosti 24, 2020 Mjini Bariadi.



Mkuu wa Wilaya ya Bariadi. Mhe. Festo Kiswaga akimkabidhi zawadi mmoja wa walimu kutoka shule ya sekondari Bariadi , katika hafla ya kuwapongeza walimu na wanafunzi waliofanya vizuri katika mtihani wa kidato cha sita ambapo mkoa wa Simiyu umeshika nafasi ya tatu Kitaifa, iliyofanyika Agosti 24, 2020 Mjini Bariadi.

Mwenyekiti wa Chama cha Walimu Tanzania mkoa wa Simiyu, Mwl. Kulwa Dwese akieleza jambo katika hafla ya kuwapongeza walimu na wanafunzi waliofanya vizuri katika Mtihani wa Taifa wa kidato cha Sita mwaka 2020 ambapo mkoa wa Simiyu umeshika nafasi ya tatu Kitaifa, iliyofanyika Agosti 24, 2020 Mjini Bariadi.

Mkuu wa Shule ya Sekondari Bariadi mkoani Simiyu, Mwl. Ally Simba akieleza jambo katika hafla ya kuwapongeza walimu na wanafunzi waliofanya vizuri katika Mtihani wa Taifa wa kidato cha Sita mwaka 2020 ambapo mkoa wa Simiyu umeshika nafasi ya tatu Kitaifa, iliyofanyika Agosti 24, 2020 Mjini Bariadi.

Kutoka kushoto Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka, Afisa Elimu wa Mkoa, Mwl. Ernest Hinju na Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga wakiteta jambo kabla ya kukabidhi zawadi kwa walimu na wanafunzi, katika hafla ya kuwapongeza walimu na wanafunzi waliofanya vizuri katika Mtihani wa Taifa wa kidato cha Sita mwaka 2020 ambapo mkoa wa Simiyu umeshika nafasi ya tatu Kitaifa, iliyofanyika Agosti 24, 2020 Mjini Bariadi.

Mkuu wa Wilaya ya Itilima, Mhe. Benson Kilangi  akieleza jambo katika hafla ya kuwapongeza walimu na wanafunzi waliofanya vizuri katika Mtihani wa Taifa wa kidato cha Sita mwaka 2020 ambapo mkoa wa Simiyu umeshika nafasi ya tatu Kitaifa, iliyofanyika Agosti 24, 2020 Mjini Bariadi.

Baadhi ya wanafunzi wa shule za sekondari wilayani Bariadi wakifuatilia matukio mbalimbali katika hafla ya kuwapongeza walimu na wanafunzi waliofanya vizuri katika Mtihani wa Taifa wa kidato cha Sita mwaka 2020 ambapo mkoa wa Simiyu umeshika nafasi ya tatu Kitaifa, iliyofanyika Agosti 24, 2020 Mjini Bariadi.

Baadhi ya Makatibu Tawala wa Wilaya mkoa wa Simiyu wakiteta jambo katika hafla ya kuwapongeza walimu na wanafunzi waliofanya vizuri katika Mtihani wa Taifa wa kidato cha Sita mwaka 2020 ambapo mkoa wa Simiyu umeshika nafasi ya tatu Kitaifa, iliyofanyika Agosti 24, 2020 Mjini Bariadi.

Baadhi ya wanafunzi wa shule za  msingi wilayani Bariadi wakifuatilia matukio mbalimbali katika hafla ya kuwapongeza walimu na wanafunzi waliofanya vizuri katika Mtihani wa Taifa wa kidato cha Sita mwaka 2020 ambapo mkoa wa Simiyu umeshika nafasi ya tatu Kitaifa, iliyofanyika Agosti 24, 2020 Mjini Bariadi.

Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bi. Miriam Mmbaga(kushoto) akipokea cheti cha shukrani kwa naiba ya aliyekuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bw. Jumanne Sagini kwa kutambua mchango wake katika kuinua kiwango cha elimu mkoa wa Simiyu wakati wa uongozi wake, katika hafla ya kuwapongeza walimu na wanafunzi waliofanya vizuri katika Mtihani wa Taifa wa kidato cha Sita mwaka 2020 ambapo mkoa wa Simiyu umeshika nafasi ya tatu Kitaifa, iliyofanyika Agosti 24, 2020 Mjini Bariadi


0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!