Thursday, April 11, 2019

WAJUMBE WA NEC WASHAURI UBUNIFU WA KAMBI ZA KITAALUMA SIMIYU UIGWE


Wajumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa (NEC) kutoka Mikoa ya Arusha na Geita wamewapongeza viongozi Mkoani Simiyu kwa ubunifu waliofanya kuanzisha kambi za kitaaluma kwa ajili ya kuongeza ufaulu na kutoa wito kwa viongozi wengine kuiga ubunifu huu ili waweze kuwasaidia wanafunzi kufanya vizuri katika mitihani yao.

Hayo yamesemwa na Ndg. Anna Agatha Msuya Mjumbe wa NEC (Arusha) na Ndg. Idd Kassim Idd Mjumbe wa NEC(Geita) mara baada ya kutembelea wanafunzi wa Kidato cha Sita mwaka 2019 walio katika kambi ya kitaaluma inayoendelea katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa, mara baada ya viongozi hao kuungana na Mjumbe wa NEC kutoka Mkoa wa Simiyu, Ndg. Emmanuel Gungu Silanga kukabidhi msaada wa chakula kwa wanafunzi hao Aprili 11, 2019.

Akizungumza mara baada ya msaada wa chakula kukabidhiwa Ndg. Anna Agatha Msuya amesema laiti kambi hizi zingekuwa zinafanyika katika maeneo mengi matokeo ya Mitihani hususani ya Taifa yangekuwa mazuri zaidi ya sasa kwani zimeonekana kuusaidia mkoa wa Simiyu kupanda kielimu.

“Nimevutiwa na ubunifu wa Simiyu kuwa na kambi za kitaaluma, tungekuwa na matokeo mazuri kama tungekuwa na viongozi wa Serikali wabunifu kama hapa Simiyu, naomba tulichokiona Simiyu kifanyike na mikoa mingine; mwaka juzi walikuwa wa 26 Kitaifa, mwaka jana wakawa wa 10 na naamini kwa kambi hii hatutaikosa Simiyu katika mikoa mitano bora” alisema Anna Agata Msuya.

Naye Ndg. Idd Kassim Idd Mjumbe wa NEC(Geita) pamoja na kupongeza juhudi za mkoa wa Simiyu katika elimu, ameahidi kuwa amejifunza kupitia kambi hiyo ya kitaaluma na kulichukua wazo hilo kwa jili ya kushauri viongozi wa mkoa wa Geita kuona namna ya kulifanyia kazi ili kuwa na ufaulu mzuri.

Aidha, Mwl. Ezekiel Mollel mwekezaji katika Sekta ya Elimu amesema suala la kambi za kitaaluma ni la kipekee kwa mkoa wa Simiyu, hivyo akatoa wito kwa mikoa mingine kuiga huku akiwaomba wadau mbalimbali wa elimu kuendelea kuchangia mahitaji mbalimbali ya wanafunzi walio katika kambi ili waweze kujifunza kwa amani wakiwa na mahitaji ya msingi.

Kwa upande wake Mjumbe wa NEC kutoka Mkoa wa Simiyu, Ndg. Emmanuel Gungu Silanga amesema ametimiza ahadi yake ya kutoa kilo 1000 za mchele na kilo 400 za maharage kwa wanafunzi wa kidato cha Sita na kueleza matarajiao ya wana Simiyu kwa wanafunzi hao kuwa, ni kuwaona wanasoma kwa bidii na hatimaye waifanye Simiyu kuwa ya kwanza Kitaifa mwaka 2019.

Wakizungumza kwa niaba ya wanafunzi wenzao wa kidato cha Sita mwaka 2019 walioko kambini Hidaya Simba(Maswa Girls) na Masanja Ng’hwenu (Meatu) wamewashukuru viongozi hao kwa msaada wa chakula walioutoa na kuahidi kuwa shukrani yao kubwa kwa walimu, viongozi, wazazi na wadau wa elimu wanaowasaidia ni kufanya vizuri na kuifanya Simiyu iwe nambari moja.
Pamoja na kilo 1000 za mchele na kilo 400 za maharage  zilizotolewa na  Mjumbe wa NEC (Simiyu), Ndg. Emmanuel Gungu Silanga, Ndg. Idd Kassim Idd Mjumbe wa NEC(Geita) ametoa kilo 200 za mchele, Mwenyekiti wa UWT Mkoa wa Simiyu ametoa kilo 100, Mdau wa Elimu Ezekiel Mollel kilo 50 na Ndg. Anna Agatha Msuya Mjumbe wa NEC (Arusha) ameahidi kutoa zawadi kwa wanafunzi watakaopata daraja la kwanza(divion one)
MWISHO
Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa(NEC) kutoka mkoa wa Simiyu, Ndg. Emmanuel Gungu Silanga (katikati mbele), Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa Mkoa wa Arusha, Ndg. Anna Agatha Msuya(wa sita kushoto mbele) wakiwa na baadhi ya viongozi  wa Serikali na wanafunzi wa kidato cha Sita mwaka 2019 Mkoani Simiyu, wakati  wa makabidhiano ya chakula (mchele na maharage),  kilichotolewa na Ndg. Emmanuel Gungu Silanga na Wajumbe wenzake wa NEC na baadhi ya viongozi CCM mkoa kwa wanafunzi hao walio katika kambi ya Kitaaluma inayoendelea katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa .

Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa kutoka Mkoa wa Arusha, Ndg. Anna Agatha Msuya akizungumza na wanafunzi wa Kidato cha Sita mwaka 2019 walio katika Kambi ya Kitaaluma inayoendelea katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa, alipotembelea shuleni hapo wakati Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa(NEC) mkoa wa Simiyu, Ndg. Emmanuel Gungu Silanga na viongozi wengine walipokabidhi msaada chakula kwa wanafunzi hao Aprili 11, 2019.
 Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa(NEC) kutoka mkoa wa Simiyu, Ndg. Emmanuel Gungu Silanga akizungumza na wanafunzi wa Kidato cha Sita mwaka 2019 walio katika Kambi ya Kitaaluma inayoendelea katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa, kabla ya kukabidhi msaada wa chakula  kwa ajili ya wanafunzi hao Aprili 11, 2019.
 Baadhi ya wanafunzi wa Kidato cha Sita walio katika Kambi ya Kitaaluma katika Shule ya Sekondari Maswa, wakifurahia masuala mbalimbali yaliyokuwa yakiwasilishwa na Viongozi mbalimbali wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa(NEC) na Mkoa wa Simiyu, waliofika shuleni hapo kwa ajili ya kukabidhi msaada wa chakula na kuzungumza na wanafunzi hao Aprili 11, 2019. 

Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa(NEC) kutoka Mkoa wa Geita, Ndg. Idd Kassim Idd akizungumza na wanafunzi wa Kidato cha Sita mwaka 2019 walio katika Kambi ya Kitaaluma inayoendelea katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa, alipotembelea shuleni hapo wakati Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa(NEC) mkoa wa Simiyu, Ndg. Emmanuel Gungu Silanga alipokabidhi msaada wa kilo 100 za mchele na kilo 400 za maharage kwa ajili ya chakula kwa wanafunzi hao Aprili 11, 2019.
Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa kutoka Mkoa wa Arusha, Ndg. Anna Agatha Msuya akimpongeza mmoja wa wanafunzi wa Kidato cha Sita mwaka 2019  Mkoa wa Simiyu, mara baada ya kutoa maneno ya shukrani kwa baadhi ya viongozi mbalimbali wa Halmashauri kuu ya CCM Taifa NEC na Mkoa wa Simiyu waliofika shuleni Aprili 11, 2019 hapo na kutoa msaada wa chakula.
Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa kutoka Mkoa wa Arusha, Ndg. Anna Agatha Msuya(katikati) akizungumza jambo na baadhi ya viongozi na wanafunzi wa Kidato cha Sita mwaka 2019 walio katika kambi ya Kitaaluma inayoendelea katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa, allipotembelea shuleni hapo Aprili 11, 2019.
 Mwenyekiti wa UWT Mkoa wa Simiyu, Mariam Manyangu akizungumza na wanafunzi wa Kidato cha Sita mwaka 2019 walio katika Kambi ya Kitaaluma inayoendelea katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa, wakati alipotembelea shuleni hapo wakati Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa(NEC) mkoa wa Simiyu, Ndg. Emmanuel Gungu Silanga alipokabidhi msaada wa kilo 1000 za mchele na kilo 400 za maharage kwa ajili ya chakula kwa wanafunzi hao Aprili 11, 2019. 

Baadhi ya wanafunzi wa kidato cha Sita na Mkuu wa Shule ya Sekondari Itilima, Mwl. Flora Shimbi  wakifurahi jambo na Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa kutoka Mkoa wa Arusha, Ndg. Anna Agatha Msuya, baada ya ziara yake katika kambi ya kitaaluma inayoendelea shule ya sekondari ya wasichana Maswa, wakati Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa(NEC) mkoa wa Simiyu, Ndg. Emmanuel Gungu Silanga alipokabidhi msaada wa kilo 1000 za mchele na kilo 400 za  maharage kwa ajili ya chakula na baadhi ya viongozi wengine wa CCM (NEC) na Viongozi wa CCM Mkoa wa Simiyu kwa wanafunzi hao Aprili 11, 2019. 

Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa(NEC) kutoka Mkoa wa Arusha, Ndg. Anna Agatha Msuya(katikati) akizungumza jambo na baadhi ya viongozi na wanafunzi wa Kidato cha Sita mwaka 2019 walio katika kambi ya Kitaaluma inayoendelea katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa, alipotembelea shuleni wakati Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa(NEC) mkoa wa Simiyu, Ndg. Emmanuel Gungu Silanga alipokabidhi msaada wa gunia 10 za mchele na gunia mbili za maharage kwa ajili ya chakula na baadhi ya viongozi wengine wa CCM (NEC) na Viongozi wa CCM Mkoa wa Simiyu pia walipokabidhi msaada wa chakula kwa wanafunzi hao Aprili 11, 2019.

Baadhi ya Viongozi wa CCM Halmashauri Kuu ya CCM Taifa(NEC) na CCM Mkoa wa Simiyu na baadhi ya walimu wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kutoa msaada wa chakula kwa wanafunzi wa Kidato cah Sita mwaka 2019 walio katika Kambi ya Kitaaluma katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa.
Mdau wa Elimu wa Mkoa wa Simiyu ambaye ni Katibu wa Mbunge wa Nyamagana, Bi. Flora Magabe akizungumza na wanafunzi wa Kidato cha Sita mwaka 2019 walio katika Kambi ya Kitaaluma inayoendelea katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa, alipotembelea shuleni hapo wakati Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa(NEC) kutoka mkoa wa Simiyu, Mhe. Emmanuel Gungu Silanga alipokabidhi msaada wa gunia 10 za mchele na gunia mbili za maharage na viongozi wengine walipokabidhi msaada wa chakula kwa ajili wanafunzi hao Aprili 11, 2019.
 Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa(NEC) kutoka Mkoa wa Arusha, Mhe. Anna Agatha Msuya akimpongeza mmoja wa wanafunzi wa Kidato cha Sita mwaka 2019  Mkoa wa Simiyu, mara baada ya kutoa maneno ya shukrani kwa baadhi ya viongozi mbalimbali wa Halmashauri kuu ya CCM Taifa NEC na Mkoa wa Simiyu waliofika shuleni hapo Aprili 11, 2019 na kutoa msaada wa chakula.
Kutoka kushoto ni Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa(NEC) kutoka mkoa wa Simiyu, Mhe. Emmanuel Gungu Silanga, Ndg. Idd Kassim Idd Mjumbe wa NEC(Geita), Katibu Tawala Wilaya ya Maswa, Bw. Godwin Chacha, Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa(NEC) kutoka Mkoa wa Arusha, Mhe. Anna Agatha Msuya na Mwl. Ezekiel Mollel mwekezaji katika Sekta ya Elimu wakiwa katika mazungumzo kabla ya zoezi la makabidhiano ya msaada wa chakula cha wanafunzi walio kambi ya kitaaluma wilayani Maswa.

0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!