Thursday, February 28, 2019

SERIKALI KUZINDUA MFUKO WA WATU WENYE ULEMAVU


Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia watu wenye ulemavu, Mhe. Stella Ikupa amesema Serikali inatarajia kuzindua rasmi mfuko wa watu wenye ulemavu ambao utakuwa ukishughulikia masuala mbalimbali ya watu wenye ulemavu ikiwemo kutoa ruzuku kwa vyama vya watu wenye ulemavu.

Mhe. Ikupa ameyasema hayo wakati akizungumza na viongozi na watendaji wa Serikali na  watu wenye ulemavu wakati akiwa katika ziara ya kikazi wilayani humo, Februari 26,2019.

Amesema taratibu zote zimekamilika na sasa iko katika hatua za mwisho ili mfuko huo uweze kuzinduliwa huku akibainisha kuwa Baraza la Ushauri kwa watu wenye Ulemavu Taifa nalo litazinduliwa hivi karibuni kwa kuwa tayari Mwenyekiti wa Baraza hilo ameshateuliwa na Rais wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli.

“Tayari tumeshapata Mwenyekiti wa lile Baraza la Ushauri kwa watu wenye ulemavu ambaye ameteuliwa na Mhe. Rais na tunaamini muda si mrefu lile baraza litazinduliwa na litaendelea kufanya kazi kwa mujibu wa sheria” alisema Naibu Waziri Ikupa.

Katika hatua nyingine Mhe. Ikupa amepongeza viongozi wa Wilaya ya Meatu kwa namna wanavyoshughulikia masuala ya watu wenye ulemavu na wakati huo huo akawapongeza watu wenye ulemavu wilayani humo kutumia vema fedha za mikopo wanazopata kutokana asilimia mbili za mapato ya ndani ya Halmashauri kwa kuanzisha shughuli za ujasiriamali.

Aidha, ametoa wito kwa watu wenye ulemavu kujitokeza kwa wingi kuomba mikopo hiyo ambayo haina riba ili waweze kuanzisha shughuli za ujasiriamali zitakazowasaidia kujikwamua kiuchumi na kuondokana na utegemezi.

Mkuu wa Wilaya ya Meatu, Dkt. Joseph Chilongani amesema Halmashauri ya Wilaya hiyo imetenga takribani shilingi milioni Sabini kwa ajili ya kuwawezesha kiuchumi watu wenye ulemavu na akatoa wito kwao kujitokeza kuomba mikopo ili iwasaidie kuanzisha shughuli za kuwaingizia kipato.

Kwa upande wao watu wenye ulemavu wameiomba Serikali kwa kushirikiana na wadau mbalimbali kusaidia katika utatuzi wa changamoto mbalimbali zinazowakabili ikiwa ni pamoja na ukosefu vifaa saidizi kwa watu wenye ulemavu na kutengeneza mazingira wezeshi shuleni kwa wanafunzi wenye ulemavu.

“ Tunaomba Serikali yetu kwa kushirikiana na wadau itusaidie kupata nyenzo saidizi kama fimbo nyeupe kwa wasioona, viungo bandia na baiskeli za miguu mitatu kwa walemavu wa viungo” alisema Ndimila Luyoja Katibu wa SHIVYAWATA wilaya ya Meatu.

“ Tunaomba vifaa saidizi vya kukuza maandishi kwa wanafunzi  wenye ualbino na pia walimu wawape nafasi ya kukaa mbele madarasani ili waweze kuona vizuri kama wanafunzi wengine kwa sababu wasipopata nafasi hiyo watashindwa kuona vizuri ubaoni kutokana na wao kuwa na uoni hafifu”Mwenyekiti wa Chama cha Watu wenye ualbino Meatu.

Naye Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Festo Kiswaga amesema Serikali mkoani humo itaendelea kutoa kipaumbele kwa watu wenye uelemavu ambapo amesema wataendelea kujumuishwa katika agenda ya ujenzi wa uchumi wa viwanda kufikia uchumi wa kati mkoani humo.

Akiwa Wilayani Meatu, Mhe. Naibu Waziri amezungumza na viongozi, watu wenye ulemavu, kuona kazi mbalimbali za watu wenye ulemavu na kutembelea mradi wa Kitalu nyumba ili kujionea utekelezaji wake.
MWISHO



Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia watu wenye Ulemavu, Mhe. Stella Ikupa(katikati) akizungumza na viongozi na watendaji wa Wilaya ya Meatu pamoja na watu wenyeulemavu wakati akiwa katika ziara yake ya kikazi wilayani humo, Februari 26, 2019.
Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia watu wenye Ulemavu, Mhe. Stella Ikupa(wa tatu kulia) akiangalia baadhi ya kazi za wajasiriamali wenye ulemavu , wakati akiwa katika ziara yake ya kikazi wilayani humo, Februari 26, 2019.
Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia watu wenye Ulemavu, Mhe. Stella Ikupa(aliyeshika mkeka kushoto) akiangalia baadhi ya kazi za wajasiriamali wenye ulemavu , wakati akiwa katika ziara yake ya kikazi wilayani humo, Februari 26, 2019.

Mkuu wa Wilaya ya Meatu, Mhe. Dkt. Joseph Chilongani akimkaribisha Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia watu wenye Ulemavu, Mhe. Stella Ikupa mara baada ya kuwasili Mjini Mwanhuzi Meatu wakati akiwa katika ziara yake ya kikazi wilayani humo, Februari 26, 2019.
Mwenyekiti wa SHIVYAWATA  Wilaya ya Meatu ambaye pia ni mlemavu wa macho, Bw. Charles Hilu akiwasilisha changamoto za watu wenye ulemavu kwa  Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia watu wenye Ulemavu, Mhe. Stella Ikupa (wa pili kulia) wakati akiwa katika ziara yake ya kikazi wilayani humo, Februari 26, 2019.
Baadhi ya watoto wenye ulemavu wa kusikia wilayani Meatu wakifuatilia hotuba ya Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia watu wenye Ulemavu, Mhe. Stella Ikupa(hayupo pichani) kwa usaidizi wa Mkalimani wa lugha ya alama, wakati wa  ziara ya kikazi ya kiongozi huyo wilayani humo, Februari 26, 2019.
Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia watu wenye Ulemavu, Mhe. Stella Ikupa akitoka katika Kitalu Nyumba(Green House)  kilichopo Mwanhuzi Wilayani Meatu mara baada ya kukikagua, wakati akiwa katika ziara yake ya kikazi wilayani humo, Februari 26, 2019.
Afisa Kilimo wa Wilaya ya Meatu Bw. Thomas Shilabu akitoa maelezo juu ya mfumo wa umwagiliaji  uliowekwa katika Mradi wa Kitalu nyumba (green house) unaotekelezwa na Vijana ;  kwa Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia watu wenye Ulemavu, Mhe. Stella Ikupa wakati akiwa katika ziara yake ya kikazi wilayani humo, Februari 26, 2019.
Mbunge wa Viti maalum Mkoa wa Simiyu (CCM) Mhe. Leah Komanya akizungumza katika kikao cha Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia watu wenye Ulemavu, Mhe. Stella Ikupa na viongozi wa Wilaya ya Meatu, wakati wa ziara ya kikazi ya Naibu Waziri huyo  wilayani humo, Februari 26, 2019.
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Meatu, Mhe. Pius Machungwa akizungumza katika kikao cha Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia watu wenye Ulemavu, Mhe. Stella Ikupa na viongozi wa Wilaya ya Meatu na watu wenye ulemavu, wakati wa ziara ya kikazi ya Naibu Waziri huyo  wilayani humo, Februari 26, 2019.
Baadhi ya Viongozi na watu wenye ulemavu wilayani Meatu wakiwa katika kikao na Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia watu wenye Ulemavu, Mhe. Stella Ikupa , wakati wa ziara ya kikazi ya Naibu Waziri huyo  wilayani humo, Februari 26, 2019.
Mwakilishi wa  Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Anthony Mtaka, ambaye ni Mkuu wa Wilaya ya Bariadi , Mhe. Festo Kiswaga akizungumza na viongozi wa wilaya ya Meatu na baadhi ya watu wenye ulemavu katika kikao cha Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia watu wenye Ulemavu, Mhe. Stella Ikupa , wakati wa ziara ya kikazi ya Naibu Waziri huyo  wilayani humo, Februari 26, 2019.
Baadhi ya Viongozi na watu wenye ulemavu wilayani Meatu wakiwa katika kikao na Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia watu wenye Ulemavu, Mhe. Stella Ikupa , wakati wa ziara ya kikazi ya Naibu Waziri huyo  wilayani humo, Februari 26, 2019
Baadhi ya Viongozi na watu wenye ulemavu wilayani Meatu wakiwa katika Kitalu nyumba kilichopo Mwanhuzi wakati  Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia watu wenye Ulemavu, Mhe. Stella Ikupa  alipotembelea kujionea utekelezaji wa Mradi wa Kitalu Nyumba katika ziara ya kikazi wilayani humo, Februari 26, 2019.
Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia watu wenye Ulemavu, Mhe. Stella Ikupa (katikati) akizungumza naviongozi wa Wilaya ya Meatu, mara baada ya kuwasili wilayani humo kwa ziara ya kikazi, Februari 26, 2019. 

0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!