Wednesday, February 20, 2019

IGP SIRRO: JESHI LA POLISI HALITAWAFUMBIA MACHO WATAKAOBAINIKA KUJIHUSISHA NA MAUAJI YA WATOTO LAMADI


Mkuu wa Jeshi la Polisi hapa nchini IGP Simon Sirro amesema Jeshi la Polisi halitawafumba macho wale wote watakaobainika kuhusika katika mauaji ya watoto katika Kata ya Lamadi wilayani Busega na badala yake litawashughulikia kwa mujibu wa sheria.

Inspekta wa Polisi Sirro ameyasema hayo wakati akizungumza na wananchi wa Kata ya Lamadi Wilaya ya Busega Mkoani Simiyu katika Mkutano wa hadhara uliofanyika katika Uwanja wa Kisesa Kijiji cha Lamadi, kufuatia matukio ya mauaji yaliyoripotiwa mwishoni mwa mwaka jana na hivi karibuni.

IGP Sirro amewatoa hofu wananchi wa Lamadi na kuwasihi kuendelea kuliamini jeshi la Polisi kuwa liko imara na kuwahakikishia kwamba Serikali yao ipo kazini kuhakikisha mauaji hayo yanakomeshwa.

Amesema mauaji hayo yamekuwa yakihusishwa na imani za kishirikina na ramli chonganishi hivyo akawataka waganga wa jadi wanaojihusisha na ramli chonganishi kuacha mara moja maana ni kinyume na sheria, huku akiwataka waganga ambao bado hawajasajiliwa kwa mujibu wa sheria wafanye hivyo haraka.

“Tutawashughulikia wote wanaotaka kuwafanya wana Lamadi wasiishi kwa amani, kwa sababu tunaamini waliofanya haya ni wanaopiga ramli chonganishi ambao ni wachache, nitumie nafasi hii kuwataka waganga ambao hawajasajiliwa kwenda kujisajili haraka, msipojisajili tutawachukulia hatua pia” alisema

Aidha, Sirro ametoa wito kwa jamii kuachana na imani za kishirikiana, mila na desturi potofu ambazo amesema zinarudisha nyuma maendeleo, badala yake akataka elimu iendelee kutolewa kwa jamii ili iweze kubadilika.

Katika hatua nyingine IGP Sirro aliwataka wananchi na viongozi Mkoa Simiyu kushirikiana na jeshi hilo, huku akisisitiza  kuwa ushirikiano watakaotoa kwa polisi ndiyo utasaidia wahusika wote kukamatwa.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka  amesema kufuatia mauaji hayo Serikali imeshawafikisha mahakamani watuhumiwa wa mauaji ya watoto.

Aidha, Mtaka amebainisha kuwa kabla ya watuhumiwa kufikishwa mahakamani Serikali kupitia vyombo vyake vya dola ilisimamia zoezi la upigaji kura za siri ambazo wananchi waliomba wapige ili kuwabaini wauaji hao ambalo lilifanyika 13 Februari, 2019.
MWISHO.
Mkuu wa Jeshi la Polisi hapa nchini IGP Simon Sirro

0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!