Wadau wa Nishati na Maji
mkoani Simiyu wameiomba Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji
(EWURA) kuangalia namna ya kuwasaidia wananchi wanaotumia chupa za
maji kusafirisha mafuta vijijini na badala yake watafute njia mbadala ili
kuepusha majanga ya moto na uchakachuaji wa nishati hiyo.
Wadau hao wametoa
ushauri huo katika mkutano baina ya watendaji wa Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma
za Nishati na Maji (EWURA) uliolenga kuelimisha wadau Mkoani Simiyu kuhusu majukumu
ya Mamlaka hiyo, uliofanyika Mjini Bariadi Februari 21, 2019.
Wakizungumza katika mkutano huo wamesema kutokuwepo
vyombo maalum vya ubebaji wa mafuta ya taa , petroli na diseli ni Moja ya
tatizo kubwa, hivyo ni vema (EWURA) ikaja na njia mbadala ya kuwawezesha
wananchi kusafirisha kwa usalama nishati hiyo.
“Tunaomba
EWURA isaidie kuja na namna bora, vifaa vidogo vitakavyouzwa kwa bei rahisi ili
wananchi waweze kusafirisha na kuhifadhi kwa urahisi kwa sababu yanawasaidia
sana” amesema Mkaguzi wa Jeshi la Zimamoto Wilaya ya Bariadi, Maulo Kigahe.
Katika
hatua nyingine wadau hao wamezungumzia suala la urasimu katika kuunganishwa kwa
umeme kwa wananchi katika baadhi ya ofisi za Mameneja wa TANESCO na kuomba EWURA ione namna ya kuwasaidia
wananchi wasaidiwe kupata huduma kwa wakati.
“
Kuna wananchi wakitaka kuunganishiwa
umeme majumbani kwao wanadaiwa pesa mara shilingi laki tano, mara milioni moja
hivi EWURA wanayajua matatizo haya? Tukizingatia kuwa umeme ni moja ya huduma
muhimu kwa mwananchi tubadilike maana hata kule vijijini tulikozaliwa tunahitaji
umeme” alisema Mkuu wa Gereza Wilaya ya
Bariadi, Kajungu Massami.
Naye
Saibogi Mwandu mwananchi kutoka Bariadi amesema ni vema wafanyabiashara wadogo
hususani wanaouza mafuta ya petroli kwenye chupa wakapewa elimu ya namna ya
kutunza mafuta hayo kwani wengi wao wamekuwa wakitunza bidhaa hiyo ndani.
Kwa upande wake
Afisa Mkuu wa Mawasiliano (EWURA) makao makuu Wilfred Mwakalosi amesema EWURA
katika kipindi cha miaka mitatu iliyopita imeshabuni mwongozo utakaosaidia
wawekezaji wa vijijini kuwekeza kwenye vituo vya gharama nafuu.
Akifunga mkutano
huo Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe Festo Kiswaga kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa
Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka amewataka wadau wote kuwa mabalozi wazuri wa EWURA
ili wasaidie kufikisha elimu waliyoipata katika maeneo yao.
Awali akifungua
mkutano huo, Kiswaga amesema Mkoa wa Simiyu umejipanga katika utekelezaji wa
Sera ya Viwanda kwa kujenga viwanda ikiwemo kiwanda cha vifaa tiba, kiwanda cha
chaki na vingine ambavyo vitahitaji huduma za nishati na maji , hivyo ameiomba
EWURA kushirikiana na Taasisi zinazohusika na utoaji wa huduma hizo katika
kuhakikisha zinatolewa katika viwango vinavyokidhi mahitaji ili Mkoa uweze
kufikia malengo yake katika uzalishaji katika viwanda.
MWISHO.
Baadhi ya viongozi na
wadau wakiwa katika Mkutano wa kuelimisha wadau Mkoani Simiyu kuhusu majukumu
ya Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA), uliofanyika Mjini
Bariadi Februari 21, 2019.
Mkuu
wa Wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga akifungua Mkutano wa kuelimisha wadau Mkoani
Simiyu kuhusu majukumu ya Mamlaka ya Udhibiti wa Nishati na Maji (EWURA) kwa niaba
ya Mkuu wa Mkoa huo, Mhe. Anthony Mtaka, uliofanyika Mjini Bariadi Februari 21,
2019
Kaimu Meneja wa Mamlaka
ya Udhibiti wa Nishati na Maji (EWURA) wa Kanda ya Ziwa Mhandisi. Loden
Kitumbika akiwasilisha mada katika Mkutano wa kuelimisha wadau Mkoani Simiyu kuhusu
majukumu ya Mamlaka hiyo, uliofanyika Mjini Bariadi Februari 21, 2019.
Afisa Mawasiliano Mkuu
kutoka Mamlaka ya Udhibiti wa Nishati na
Maji (EWURA), Bw. Wilfred Mwakalosi akiwasilisha mada katika Mkutano wa
kuelimisha wadau Mkoani Simiyu kuhusu majukumu ya Mamlaka hiyo, uliofanyika
Mjini Bariadi Februari 21, 2019.
Mkuu wa Wilaya ya
Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga(kulia) na Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu,
Bw. Ekwabi Mujungu wakifuatilia kwa makini mada zikiwasilishwa katika Mkutano
wa kuelimisha wadau kuhusu majukumu ya Mamlaka ya Udhibiti wa Nishati na Maji
(EWURA) Mkoani Simiyu, uliofanyika Mjini Bariadi Februari 21, 2019.
Kaimu Meneja wa Mamlaka
ya Udhibiti wa Nishati na Maji (EWURA) wa Kanda ya Ziwa Mhandisi. Loden
Kitumbika akitoa utangulizi wa lengo la Mkutano wa kuelimisha wadau kuhusu
majukumu ya Mamlaka hiyo Mkoani Simiyu, uliofanyika Mjini Bariadi Februari 21,
2019.
Baadhi ya viongozi wa
Mkoa wa Simiyu, wakiwa katika Mkutano wa kuelimisha wadau Mkoani Simiyu kuhusu
majukumu ya Mamlaka ya Udhibiti wa Nishati na Maji (EWURA), uliofanyika Mjini
Bariadi Februari 21, 2019.
Baadhi ya viongozi wa
Mkoa wa Simiyu na wadau, wakiwa katika Mkutano wa kuelimisha wadau Mkoani
Simiyu kuhusu majukumu ya Mamlaka ya Udhibiti wa Nishati na Maji (EWURA),
uliofanyika Mjini Bariadi Februari 21, 2019.
0 comments:
Post a Comment