Thursday, June 13, 2019

WAZIRI MKUU APONGEZA SIMIYU KUJENGA SHULE YA MICHEZO

Waziri Mkuu Jamhuri ya Muungan, Mhe. Kassim Majaliwa(Mb), ameupongeza Mkoa wa Simiyu kwa kuwa mmoja kati ya Mikoa ya mfano katika kutekeleza agizo lake la mwaka jana alilolitoa kupitia michezo hiyo la kuanzishwa kwa shule maalumu za michezo.


Waziri Mkuu ameyasema hayo Juni 10, 2019 wakati wa ufunguzi wa Mashindano ya UMISSETA Kitaifa katika Uwanja wa Nangwanda Sijaona Mjini Mtwara.

Mkoa wa Simiyu umejenga Shule ya Sekondari itakayokuwa kituo cha kukuza vipaji vya wanafunzi katika michezo. “Naagiza mwakani wanafunzi wote walioonesha vipaji katika michezo watakaofaulu Mtihani wa Elimu ya Msingi wapangwe katika shule hiyo ili wakakuze vipaji vyao.”

                             Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. , Kassim Majaliwa 
Wanamichezo kutoka Mkoa wa Simiyu wakiingia kwenye uwanja wa Nangwanda Sijaona kushiriki katika Ufunguzi wa Michezo ya UMISETA uliofanywa na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, Juni 10, 2019. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka ( wa tatu kulia) akiwa nabaadhi ya wataalam wakiangalia baadhi ya mawe yaliyotolewa katika eneo unapojengwa uwanja wa mpira wa miguu katika Shule ya Sekondari Simiyu.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka  na baadhi ya wananchi wa Kata ya Malambo  wakishuhudia zoezi la kutoa mawe katika eneo unapojengwa uwanja wa mpira wa miguu katika Shule ya Sekondari Simiyu.


0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!