Monday, March 28, 2016

MTAKA AHIMIZA UFUGAJI WA SAMAKI SIMIYU



Mkuu wa mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony John Mtaka amehimiza wataalam wa uvuvi kuanzisha  mradi wa ufugaji wa samaki katika  mabwawa ili kuwahakikishia  wananchi wa mkoa wa Simiyu upatikanaji wa kitoweo pamoja na kutoa fursa ya ajira kwa vijana.

Mkuu wa Mkoa ametoa kauli hiyo katika kikao alichofanya kati ya viongozi wa taasisi za serikali, binafsi, timu za menejimenti za Mamlaka za Serikali za Mitaa (CMT), viongozi wa dini, vyama vya siasa na wadau wengine wa maendeleo kilichofanyika mwanzoni wa wiki hii,  katika ukumbi wa K.K.K.T Bariadi.
Alisema Ofisi yake itatafuta wataalam wa ufugaji wa samaki kutoka chuo cha Ukiriguru cha jijini Mwanza ambao watafanya tathmini na kutoa ushauri wa kitaalamu ili kufanikisha lengo hilo.
“Hatuwezi kuendelea kutegemea samaki kutoka sehemu nyingine wakati tuna mabwawa katika mkoa wetu ambayo yanafaa kabisa kwa ufugaji wa samaki na kuwaongezea fursa ya ajira vijana wetu,” alisema Mtaka.
Baadhi ya viongozi walioshiriki kikao hicho walisema watamuunga mkono Mkuu huyo wa mkoa kwa kuwahamasisha vijana kushirikiana na Serikali katika kutekeleza mradi huo.

0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!