Thursday, November 17, 2016

WAKAZI WA MASWA KUPATA HATI MILIKI ZA VIWANJA NDANI YA SIKU 90


Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. Angelina Mabula akizungumza na wananchi wa Wilaya ya Maswa katika mkutano wa hadhara uliofanyika viwanja Modeco  wakati wa ziara yake Mkoani Simiyu
Baadhi ya wanachi Wilaya ya Maswa wakimsikiliza : Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. Angelina Mabula katika Mkutano wa Hadhara uliofanyika viwanja vya Modeco wilayani humo.
Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. Angelina Mabula (kushoto) akipokelewa na Kaimu Katibu Tawala Mkoa, Donatus Weginah mara baada ya kuwasili katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu.

Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. Angelina Mabula akisalimiana na Katibu Tawala Msaidizi Seksheni ya Miundombinu, Mhandisi Deusdedit Mshuga mara baada ya kuwasili katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu.

Mkuu wa Wiaya ya Maswa, Mhe. Dkt. Seif Shekalaghe akizungumza na wananchi wa Wilaya ya Maswa kabla ya kumkaribisha Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. Angelina Mabula katika mkutano wa hadhara uliofanyika viwanja Modeco  wakati wa ziara yake Mkoani Simiyu.
Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. Angelina Mabula(wa pili kushoto ) akizungumza na wataalam wa Ardhi wa Mkoa wa Simiyu(hawapo pichani) katika ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mjini Bariadi.
Baadhi ya Viongozi na Wataalam wa Ardhi wa Mkoa wa Simiyu wakimsikiliza Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. Angelina Mabula (hayupo pichani) katika kikao kilichofanyika katika ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mjini Bariadi
Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. Angelina Mabula(kushoto) akiangalia Taarifa za Mfumo ukusanyaji wa tozo za ardhi kwenye Ofisi ya Idara ya Ardhi ya Halmashauri ya mji wa Bariadi, (kulia) ni Fundi Sanifu wa Halmashauri hiyo.
Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. Angelina Mabula akisalimiana na Mbunge wa Maswa Magharibi Mhe.Mashimba Ndaki mara baada ya kuwasili katika Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa

Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. Angelina Mabula akisalimiana na Mbunge wa Maswa Mashariki Mhe.Stanslaus Nyongo  mara baada ya kuwasili katika Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa.
Mwenyekiti wa Baraza la Ardhi la Wilaya ya Maswa, Mhe. Mdimi Ilanga akitoa ufafanuzi wa masaula mbalimbali yanayohusu baraza hilo katika kikao kilichofanyika Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa

Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. Angelina Mabula akipokea moja ya boksi la chaki za Maswa(Maswa Chalks) kutoka kwa Mkuu wa Wilaya ya Maswa Mhe. Dkt. Seif Shekalaghe mara baada ya kutembelea kiwanda cha kutengeneza Chaki na kununua chaki katoni kadhaa wilayani humo wakati wa ziara yake.


Afisa Ardhi wa Wilaya ya Maswa, Musa Warioba akitoa ufafanuzi juu ya kero na malalamiko mbalimbali yaliyotolewa na wananchi kwa Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi wakati wa mkutano wa hadhara ulifanyika jana katika uwanja wa Modeco wilayani humo.
Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. Angelina Mabula akiwa katika picha ya Pamoja na Viongozi wa Wilaya ya Maswa na Vijana wa Maswa Family alipotembea kiwanda cha kutengeneza Chaki wakati wa ziara yake wilayani humo.
  


Na Stella Kalinga
Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. Angelina Mabula amemtaka Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa, Dkt. Fredrick Sagamiko kutoa hati miliki za viwanja kwa wakazi wa wilaya hiyo ndani ya siku 90 (hadi kufikia tarehe 15 Februari, 2017 )
 Mhe. Mabula aliyasema hayo jana alipozungumza  na wananchi wa Wilaya ya Maswa katika Mkutano wa Hadhara uliofanyika katika uwanja wa Modeco akiwa katika ziara yake wilayani humo akitokea wilayani Bariadi

 Mhe. Mabula amesema wananchi walio na Matoleo ya Viwanja (Letter of offer) waliyopewa awali wawasilishe katika Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji, ili wapatiwe hati miliki ambazo zitawasaidia kuwahakikishia usalama wa nyumba zao kwa kupunguza hatari ya kutokea kwa migogoro isiyo ya lazima.

Aidha, Mhe.Mabula amesema wananchi watakapopata hati miliki hizo zitawasaidia kujikwamua kiuchumi katika kupata mikopo ya Benki na Taasisi nyingine za kifedha kama dhamana yao.

Kwa upande wake Mbunge wa Maswa Magharibi Mhe.Mashimba Ndaki amesema pamoja na Halmashauri kutoa hati hizo baadhi ya wananchi wana hati za kimila ambazo zimekuwa zikikataliwa katika baadhi ya  Taasisi za kifedha hivyo aliomba Mhe. Naibu waziri awasaidie wananchi hao.

Akitoa ufafanuzi juu ya suala hilo Mhe.Mabula amesema Hati za Kimila ni halali na kuna taasisi takribani saba zinazopokea hati hizo ambapo aliahidi kuwa Wizara ya Ardhi inaendelea kufanya mazungumzo na Taasisi nyingine za kifedha ili ziweze kuzitambua.

Wakati huo huo Mhe. Mabula amesema Halmashauri ihakikishe inapima maeneo yote Taasisi za Serikali na kutoa hati miliki kwa taasisi hizo ili kuepuka uvamizi utakaopelekea migogoro katika Serikali na wananchi.

Naibu Waziri aliongeza kuwa baada ya kupima maeneo hayo ya Taasisi za Serikali Wenyeviti wa mitaa na vijiji wapewe ramani  za maeneo husika ili wayalinde dhidi ya uvamizi na ujenzi holela.

Sambamba na hilo Mhe. Mabula amesema Wizara yake kwa kushirikiana na Halmashauri itaandaa utaratibu wa kuyajengea uwezo mabaraza ya Vijiji na Kata ili yashughulikie vema mashauri mbalimbali ya Ardhi kwa wakati na kuepuka kuliongezea mzigo Baraza la Ardhi la Wilaya.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Baraza la Ardhi la Maswa, Mhe. Mdimi Ilanga alisema amekuwa akipokeabaadhi ya  kesi ambazo zingeweza kufanyiwa kazi na Mabaraza ya kata hivyo endapo wajumbe wa mabaraza hayo watajengewa uwezo watasaidia kushughulikia kesi hizo.

Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Angelina Mabula amemaliza ziara yake ya siku mbili mkoani Simiyu ambapo alitembelea Wilaya ya Busega, Bariadi na Maswa na kuzungumza na Watalaam wa Ardhi wa mkoa huo, kutembelea maeneo ambayo Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) linatarajia kujenga nyuma na kuzungumza na wananchi kupitia mikutano ya hadhara.



0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!