Thursday, May 14, 2020

SEKTA BINAFSI ILELEWE NA IPENDWE-RC MTAKA

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka ametoa wito kwa viongozi wa Serikali mkoani hapa kuilea na kuipenda sekta binafsi na kuona namna sahihi ya kutatua changamoto zinazoikabili badala ya kufikiria namna ya kukusanya mapato tu kutoka katika sekta hiyo.

Mtaka ameyasema hayo katika kikao maalum cha kujadili Hoja na mapendekezo ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kwa mwaka wa fedha 2018/2019 katika Halmashauri ya Mji wa Bariadi, ambapo Halmashauri ya Mji Bariadi na nyingine za Mkoa wa Simiyu pamoja na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa. Simiyu zimepata hati safi.

“Viongozi wa Serikali tujifunze kuilea sekta binafsi, sekta binafsi ni lazima ilelewe na ipendwe pia, tuone namna ya kutatua changamoto zinazoikabili na kuwafanya watu wapende kufanya biashara badala ya kufikiria kukusanya mapato tu,” alisema Mtaka.

Mtaka ametoa wito huo kutokana na mapendekezo yaliyotolewa katika ripoti ya CAG kuwa pamoja na Halmashauri ya Mji Bariadi kupata hati safi, iko haja kwa Halmashauri hiyo kuimarisha mifumo ya  ukusanyaji na  Usimamizi wa Mapato yatokanayo na vyanzo vya ndani, huku akisistiza kuweka utaratibu mzuri wa utoaji wa mikopo ya wanawake, vijana na wenye ulemavu kutoka katika asilimia 10 ya mapato hayo ya ndani.

Aidha, Mtaka amewataka Wakurugenzi wa Halmashauri zote mkoani Simiyu kuhakikisha wanawalipa madiwani stahili zao kabla ya muda wao kuisha (kabla ya mabaraza ya amadiwani kuvunjwa, “tusingehitaji tuvunje mabaraza madiwani wetu wakiwa wanadai stahili zao, Wakurugenzi wote hili liwe kipaumbele chenu.”

 Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka akizungumza na Madiwani na wataalam katika Kikao maalum cha Baraza la Madiwani wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi kilichofanyika Mei 12, 2020 kwa lengo la kujadili hoja na mapendekezo ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu  za Serikali (CAG) kwa mwaka wa fedha 2018/2019.
 Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi, Mhe. Robert Lweyo akifungua  Kikao maalum cha Baraza la Madiwani wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi kilichofanyika Mei 12, 2020 kwa lengo la kujadili hoja na mapendekezo ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu  za Serikali (CAG) kwa mwaka wa fedha 2018/2019.
 Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi, Bw. Melckizedeck  Humbe akitoa taarifa katika Kikao maalum cha Baraza la Madiwani wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi kilichofanyika Mei 12, 2020 kwa lengo la kujadili hoja na mapendekezo ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu  za Serikali (CAG) kwa mwaka wa fedha 2018/2019.
 Baadhi ya Madiwani na wataalam wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi wakiwa katika Kikao maalum cha Baraza la Madiwani wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi kilichofanyika Mei 12, 2020 kwa lengo la kujadili hoja na mapendekezo ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu  za Serikali (CAG) kwa mwaka wa fedha 2018/2019.
Baadhi ya Madiwani na wataalam wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi wakiwa katika Kikao maalum cha Baraza la Madiwani wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi kilichofanyika Mei 12, 2020 kwa lengo la kujadili hoja na mapendekezo ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu  za Serikali (CAG) kwa mwaka wa fedha 2018/2019.
Diwani wa Kata ya Nyangokolwa Mhe. Lukonge Nyakali akichangia katika Kikao maalum cha Baraza la Madiwani wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi kilichofanyika Mei 12, 2020 kwa lengo la kujadili hoja na mapendekezo ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu  za Serikali (CAG) kwa mwaka wa fedha 2018/2019.
Mkuu wa wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga akitoa salamu za Wilaya katika Kikao maalum cha Baraza la Madiwani wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi kilichofanyika Mei 12, 2020 kwa lengo la kujadili hoja na mapendekezo ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu  za Serikali (CAG) kwa mwaka wa fedha 2018/2019.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa Wa Simiyu, ACP. Henry Mwaibambe akizungumza katika Kikao maalum cha Baraza la Madiwani wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi kilichofanyika Mei 12, 2020 kwa lengo la kujadili hoja na mapendekezo ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu  za Serikali (CAG) kwa mwaka wa fedha 2018/2019.
Mkuu wa wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga akitoa salamu za Wilaya katika Kikao maalum cha Baraza la Madiwani wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi kilichofanyika Mei 12, 2020 kwa lengo la kujadili hoja na mapendekezo ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu  za Serikali (CAG) kwa mwaka wa fedha 2018/2019.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka akizungumza na Madiwani na wataalam katika Kikao maalum cha Baraza la Madiwani wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi kilichofanyika Mei 12, 2020 kwa lengo la kujadili hoja na mapendekezo ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu  za Serikali (CAG) kwa mwaka wa fedha 2018/2019.
Baadhi ya viongozi wakiwa katika Kikao maalum cha Baraza la Madiwani wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi kilichofanyika Mei 12, 2020 kwa lengo la kujadili hoja na mapendekezo ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu  za Serikali (CAG) kwa mwaka wa fedha 2018/2019.
  Wajumbe wa Kamati ya ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Simiyu wakifuatilia Kikao maalum cha Baraza la Madiwani wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi kilichofanyika Mei 12, 2020 kwa lengo la kujadili hoja na mapendekezo ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu  za Serikali (CAG) kwa mwaka wa fedha 2018/2019.

0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!