Friday, July 27, 2018

WAZIRI MKUCHIKA AAGIZA HALMASHAURI KUTENGA MAENEO YA KUANZISHA VITUO VYA URASIMISHAJI NA UENDELEZAJI BIASHARA

Waziri wa Nchi  Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala bora Kapteni Mstaafu George Mkuchika ameziagiza  halmashauri zote nchini  kutenga maeneo ya uanzishwaji vituo vya urasimishaji biashara kwa wananchi ili waweze kuondokana na umasikini.


Agizo hilo limetolewa na kwa naiba yake na Mkuu wa Wilaya ya Bariadi Festo Kiswaga  katika uzinduzi wa kituo kimoja cha urasimishaji na uendelezaji biashara katika Halmashauri ya Mji wa Bariadi.

Amesema MKURABITA ndio nyenzo muhimu ya kuwawezesha, kuibua na kuendeleza uwezo wa wananchi kuwa wawekezaji wa ndani wanaowajibika kutengeneza mtaji, soko, ajira na kujenga uchumi wa viwanda ndani ya mfumo rasmi, hivyo ipo haja kwa halmashauri kutenga maeneo kwa ajili ya vituo vya urasimishaji biashara  ili kuwasaidia wananchi.

“ Ni matumaini yangu kuwa vituo vya kurasimisha biashara vitatumika pia kutambua na kuzitumia fursa za uwekezaji ambazo zinatengenezwa na kuimarishwa, nitumie fursa hii kuzitaka Halmashauri zote nchini kutenga maeneo kwa ajili ya uanzishwaji wa vituo hivi katika kuchochea ujenzi wa uchumi wa viwanda vinavyomilikiwa na wananchi” alisema Kiswaga akisoma hotuba ya Waziri Mkuchika 
.
Aidha, amewahamasisha wafanyabiashara na wananchi wote mkoani Simiyu kutumia huduma zipatikanazo katika vituo vya kusajili na kuendeleza biashara zao, huku akiwasisitiza wafanyabiashara wadogo kama mamalishe, wamachinga na waendesha bodaboda kutumia Kituo cha Bariadi, ili waweze kujiondoa katika mfumo usio rasmi na kuingia katika mfumo rasmi wa uchumi.

Mwenyekiti wa Kamati ya Uongozi ya MKURABITA Daniel Ole Njoolay ameiomba Serikali kutoa nyenzo za kutosha za kusukuma urasimishaji na uendelezaji wa biashara kukuza mitaji ya wafanyabiashara kwa kuwa hadi sasa utafiti unaonesha kuwa kuwa zaidi ya asilimia 90 ya biashara si rasmi.

Mwenyekiti Mstaafu wa mpango wa kurasimisha Rasilimali na Biashara za Wanyonge Tanzania (MKURABITA) John Chiligati ametoa wito kwa wakazi wa Mkoa wa Simiyu hususani Bariadi kutumia hati miliki za kimila kama dhamana ya kupata mikopo ya kuendeleza kilimo, kuanzisha viwanda na biashara.

Mtendaji mkuu wa MKURABITA Seraphia Mgembe amewashukuru wote waliopata mafunzo ya urasimishaji na uendelezaji wa biashara na kuahidi kuwafuatilia na kuhakikisha kuwa miaka ijayo waweze kufanikiwa kiuchumi.

Baadhi ya washiriki wa Mafunzo ya urasimishaji na uendelezaji wa biashara wameishukuru Serikali kwa mpango huo kuanzisha mradi wa kituo kimoja cha urasimishaji na uendelezaji biashara, kupitia MKURABITA na kuomba waendelee kupewa mafunzo ili wawze kunufaika na biashara zao.

“Tunaomba tuendelee kupigwa msasa zaidi na zaidi ili tuweze kutunza mahesabu ya biashara zetu vizuri, tuweze kulipa kodi na kuendeleza biashara zetu katika mfumo ulio rasmi” alisema Mashaka Than mfanyabiashara kutoka Bariadi.

Kwa mujibu wa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi, Bw. Melkizedeck Humbe Kituo Kimoja cha Urasimishaji na Uendelezaji wa Biashara kilichofunguliwa Julai 26, 2018 kitatoa huduma za leseni za biashara, usajili wa biashara, huduma za kibenki, TRA, Mifuko ya Hifadhi ya Jamii, wakala wa vipimo na huduma za kampuni binafsi ya GODTEC.




Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga akikata utepe kuashiria ufunguzi  wa Kituo Kimoja cha Urasimishaji  na Uendelezaji  Biashara katika Halmashauri ya Mji wa Bariadi, ambaye alifungua kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma  na Utawala Bora, Mhe. Kapt.George Mkuchika Julai 26, 2018.
Mwenyekiti wa Bodi ya MKURABITA Mhe. Daniel Ole Njoolay akizungumza viongozi mbalimbali na wafanyabiasha  katika hafla  ufunguzi wa wa Kituo Kimoja cha Urasimishaji  na Uendelezaji  Biashara katika Halmashauri ya Mji wa Bariadi, iliyofanyika  Julai 26, 2018.
Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga  akisoma hotuba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma  na Utawala Bora, Mhe. Kapt.George Mkuchika, katika hafla  ufunguzi wa wa Kituo Kimoja cha Urasimishaji  na Uendelezaji  Biashara katika Halmashauri ya Mji wa Bariadi, iliyofanyika  Julai 26, 2018. 
Mwakilishi wa kampuni sita ya Mjini Bariadi ambazo watu wake walipata mafunzo ya urasimishaji na uendelezaji biashara kutoka MKURABITA , Bw. Elimringi Lyimo  akisoma risala katika hafla  ufunguzi wa wa Kituo Kimoja cha Urasimishaji  na Uendelezaji  Biashara katika Halmashauri ya Mji wa Bariadi iliyofanyika Julai 26, 2018.
Katibu Tawala Mkoa wa Simiyu, Bw. Jumanne Sagini akiteta jambo na Mratibu wa MKURABITA Bi. Seraphia Mgembe katika hafla  ufunguzi wa wa Kituo Kimoja cha Urasimishaji  na Uendelezaji  Biashara katika Halmashauri ya Mji wa Bariadi iliyofanyika Julai 26, 2018.
Baadhi ya Maafisa Biashara wa Halmashauri 21 zinazounda Kanda ya Ziwa Mashariki (Simiyu, Mara na Shinyanga), wakifuatilia masuala mbalimbali wakati wa hafla  ufunguzi wa wa Kituo Kimoja cha Urasimishaji  na Uendelezaji  Biashara katika Halmashauri ya Mji wa Bariadi, iliyofanyika Julai 26, 2018.
Baadhi ya wafanyabiashara kutoka wa Makampuni sita ya Mjini Bariadi ambayo watu wake walipata mafunzo ya urasimishaji na uendelezaji biashara kutoka MKURABITA  wakifuatilia masuala mbalimbali wakati wa hafla  ufunguzi wa wa Kituo Kimoja cha Urasimishaji  na Uendelezaji  Biashara katika Halmashauri ya Mji wa Bariadi, iliyofanyika Julai 26, 2018.

Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga (mwenye suti ya rangi ya bluu bahari mbele) akiwaongoza Viongozi na wajumbe wa Bodi ya MKURABITA kwenda kwenye ufunguzi wa  ufunguzi  wa Kituo Kimoja cha Urasimishaji  na Uendelezaji  Biashara katika Halmashauri ya Mji wa Bariadi, uliofanyika Julai 26, 2018.
Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga (wa tano kulia) akiwa katika picha ya pamoja na wafanyabiashara kutoka wa Makampuni sita ya Mjini Bariadi ambayo watu wake walipata mafunzo ya urasimishaji na uendelezaji biashara kutoka MKURABITA , baada ya hafla ya ufunguzi wa Kituo Kimoja cha Urasimishaji  na Uendelezaji  Biashara katika Halmashauri ya Mji wa Bariadi, iliyofanyika Julai 26, 2018.


Baadhi ya Vijana waliopewa mafunzo na walipata mafunzo ya urasimishaji na uendelezaji biashara kutoka MKURABITA  wakifuatilia masuala mbalimbali wakati wa hafla  ufunguzi wa wa Kituo Kimoja cha Urasimishaji  na Uendelezaji  Biashara katika Halmashauri ya Mji wa Bariadi, iliyofanyika Julai 26, 2018.

Mwenyekiti Mstaafu wa Bodi ya MKURABITA  akizungumza na viongozi, katika hafla  ufunguzi wa wa Kituo Kimoja cha Urasimishaji  na Uendelezaji  Biashara katika Halmashauri ya Mji wa Bariadi, iliyofanyika  Julai 26, 2018.

 Katibu Tawala wa Mkoa, Bw. Jumanne Sagini akizungumza na viongozi na wafanyabiashara katika hafla  ufunguzi wa wa Kituo Kimoja cha Urasimishaji  na Uendelezaji  Biashara katika Halmashauri ya Mji wa Bariadi, iliyofanyika  Julai 26, 2018.
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi, Bw. Melkizedeck  Humbe akiwa siliha taarifa ya Kituo Kimoja cha Urasimishaji  na Uendelezaji  Biashara kilichofunguliwa rasmi katika Halmashauri ya Mji wa Bariadi, Julai 26, 2018.
Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga (kulia) akimpongeza Mwakilishi wa kampuni sita za Mjini Bariadi ambazo watu wake walipata mafunzo ya urasimishaji na uendelezaji biashara kutoka MKURABITA, Bw. Elimringi Lyimo  baada ya kusoma risala na kumkabidhi, katika hafla ya ufunguzi  wa Kituo Kimoja cha Urasimishaji  na Uendelezaji  Biashara katika Halmashauri ya Mji wa Bariadi iliyofanyika Julai 26, 2018.
Mratibu wa MKURABITA Bi. Seraphia Mgembe akizungumza na viongozi mbalimbali na wafanyabiashara katika hafla  ufunguzi wa wa Kituo Kimoja cha Urasimishaji  na Uendelezaji  Biashara katika Halmashauri ya Mji wa Bariadi, iliyofanyika  Julai 26, 2018.
Mkuu wa Wilaya ya Urambo, Mhe. Angelina Kwinga akizungumza na viongozi mbalimbali na wafanyabiashara katika hafla  ufunguzi wa wa Kituo Kimoja cha Urasimishaji  na Uendelezaji  Biashara katika Halmashauri ya Mji wa Bariadi, iliyofanyika  Julai 26, 2018.
Mtaalam kutoka Kampuni ya GOD TEC akitoa malezo juu ya manufaa ya Kituo cha Urasimishaji na uendelezaji biashara kwa viongozi mbalimbali waliofika katika hafla ya  ufunguzi wa wa Kituo Kimoja cha Urasimishaji  na Uendelezaji  Biashara katika Halmashauri ya Mji wa Bariadi, iliyofanyika  Julai 26, 2018.
Mwenyekiti wa Bodi ya MKURABITA Mhe. Daniel Ole Njoolay akizungumza viongozi mbalimbali na wafanyabiasha  katika hafla ya  ufunguzi wa wa Kituo Kimoja cha Urasimishaji  na Uendelezaji  Biashara katika Halmashauri ya Mji wa Bariadi, iliyofanyika  Julai 26, 2018.
Mwenyekiti wa Bodi ya MKURABITA Mhe. Daniel Ole Njoolay akizungumza viongozi mbalimbali na wafanyabiasha  katika hafla  ufunguzi wa wa Kituo Kimoja cha Urasimishaji  na Uendelezaji  Biashara katika Halmashauri ya Mji wa Bariadi, iliyofanyika  Julai 26, 2018.
Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga na viogozi wengine wakifurahia ufunguzi wa kituo Kimoja cha Urasimishaji  na Uendelezaji  Biashara katika Halmashauri ya Mji wa Bariadi, iliyofanyika  Julai 26, 2018.



0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!