Friday, March 15, 2019

MAAFISA ELIMU WAPEWA SIKU 37 KUKAMILISHA MABOMA

Maafisa elimu   na wakuu wa shule  zote za  sekondari Mkoani Simiyu wametakiwa kuhakikisha wanasimamia ukamilishaji wa ujenzi wa maboma ya vyumba vya madarasa kabla ya kufikia  Aprili 20,mwaka huu ili kuruhusu wanafunzi waliokosa nafasi ya kujiunga na kidato cha kwaka 2019 waweze kuanza masomo.


Wito huo umetolewa Machi 13, 2019 na Afisa Elimu wa Mkoa wa Simiyu, Mwl.Ernest Hinju wakati wa kikao cha kuweka mikakati madhubuti ya elimu Mkoani humo.

Hinju amesema kuwa maafisa elimu wote pamoja na wakuu wa shule za sekondari wanatakiwa kusimamia vema ujenzi wa maboma hayo ili yaweze kukamilika kwa wakati wakati na ubora unaotakiwa.

Ameongeza kuwa ni lazima ukamilishaji huo ,ukawa ndani ya muda uliokusudiwa kwani tayari Serikali imeshaziwezesha shule kiasi cha shilingi 12,500,000/= (kwa chumba kimoja) kwa ajili ya ukamilishaji wa majengo hayo kwa haraka.

Naye Edda Malick kiongozi wa Mpango wa kuinua Ubora wa Elimu Tanzania (EQUIP T) amesema kwa upande wao wameweza kukamilisha ujenzi wa maboma kwa asilimia 60.

Malick ameongeza kuwa wameweza kufikia asilimia hizo kutokana na jitihada na usimamizi madhubuti wa maafisa elimu na wakuu wa shule 
MWISHO



Afisa Elimu wa Mkoa wa Simiyu, Mwl.Ernest Hinju akizungumza na baadhi ya viongozi na watendaji wa idara ya Elimu ngazi ya Mkoa na Wilaya katika kikao kazi kilichofanyika Machi 13, 2019 Mjini Bariadi.
Kiongozi wa Mpango wa Kuinua Ubora wa Elimu Tanzania (EQUIP T) Mkoa wa Simiyu, Edda Malick akizungumza na baadhi ya viongozi na watendaji wa idara ya Elimu ngazi ya Mkoa na Wilaya katika kikao kazi kilichofanyika Machi 13, 2019 Mjini Bariadi.
Baadhi ya viongozi na watendaji wa idara ya Elimu ngazi ya Mkoa na Wilaya wakiwa katika kikao kazi kilichofanyika Machi 13, 2019 Mjini Bariadi.

0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!