Tuesday, March 12, 2019

RC MTAKA: VIONGOZI TUTUMIE NGUVU NYINGI KUJIFUNZA KULIKO KUAMUA

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka ametoa wito kwa viongozi  kutumia nguvu nyingi kujifunza badala ya kutumia nguvu nyingi kuamua ili wanapofanya maamuzi waamue maamuzi yenye tija kwa maendeleo ya wananchi katika maeneo yao.


Mtaka amesema hayo Machi 11, 2019 Mjini Bariadi katika Mdahalo wa uongozi na maendeleo yenye tija kwa wote uliondaliwa na Taasisi ya Mwalimu Nyerere kwa viongozi wa Mkoa wa Simiyu,ambao uliwashirikisha viongozi ngazi ya Wilaya na Mkoa.

“Ni vizuri tukatumia nguvu nyingi kujifunza kuliko kuamua kwa sababu kama hutaki kujifunza unataka uamue utaamua hata usiyoyajua, inawezekanaje mtu anateuliwa leo kuwa Mkuu wa Mkoa, Wilaya au Mkurugenzi halafu unakuwa mtaalam wa kila kitu, kilimo wewe, afya wewe, elimu wewe ; unafikiri unaweza kutranform ( kufanya mabadiliko/mapinduzi ya) uchumi wa nani?” alisema Mtaka.
Aidha,  katika kumuenzi Mwalimu Nyerere amewaasa viongozi wenzake waliopewa dhamana na Mhe. Rais kuwatumikia wananchi  kushughulika na masuala yanayohusu maendeleo ya wananchi badala ya kujikita katika mambo yasiyo na tija ikiwemo ugomvi kati yao.

“Tumeaminiwa na Mhe. Rais tukapewa dhamana tuwatumikie Watanzania wenzetu tujishughulishe na masuala ya wananchi tuache mambo yasiyo na tija kwa wananchi; hivi kuna haja gani DC kugombana na DED au RC kugombana na RAS? Kwa nini tumsumbue Mhe. Rais badala ya kuongelea masuala ya maendeleo ya wananchi abaki kuzungumzia mambo ya ugomvi wa viongozi? Alihoji Mtaka

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa  Taasisi ya Mwalimu Nyerere, Bw. Joseph Butiku ametoa wito kwa viongozi kuheshimu Katibu ya Jamhuri ya Muungano waTanzania na kuishi katika misingi ya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere katika uongozi wao.

Aidha, Butiku ametoa rai kwa viongozi wote wa Serikali kutumia madaraka waliyopewa kwa maslahi ya wananchi na wahakikishe wanawafikia  wananchi mpaka ngazi za chini ili waweze kuwasaidia namna bora ya kutumia shughuli za uzalishaji  wanazozifanya hususani kilimo na mifugo kujikwamua kutoka katika umaskini.

Akitoa mada kwa viongozi wa Mkoa wa Simiyu, Mjumbe kutoka Taasisi ya  Mwalimu Nyerere Bw. Gallus Abed amesema katika kuwaletea maendeleo wananchi ni lazima viongozi wajiwekee malengo na kusimamia utekelezaji wa malengo hayo na kuhakikisha wanapima matokeo yake.

Nao baadhi ya Viongozi wa Mkoa wa Simiyu wakichangia hoja katika mdahalo wa uongozi na maendeleo yenye tija kwa wote wamezungumzia mchango wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere na namna wanavyomuenzi Mwalimu Nyerere katika utekelezaji wa shughuli zao za kuwaletea maendeleo wananchi.

“Tunaishukuru Taasisi ya Mwalimu Nyerere kwa namna ambavyo imeamua kutufikia na kuendelea kutuonyesha, kutukumbusha na kuturejesha ili tuishi maisha ya Mwalimu Nyerere ambaye amekuwa mfano wa kuigwa” Katibu Tawala Mkoa wa Simiyu, Bw. Jumanne Sagini.

“Serikali ya awamu ya tano imekuwa ikiyaishi maono ya Baba wa Taifa, Mwl.Julius Nyerere, kama unavyoona Mhe. Rais amekuwa akisema na sisi tunaona miradi mikubwa ya maendeleo inatekelezwa kwa fedha zetu za ndani” Mkuu wa Wilaya ya Busega, Mhe. Tano Mwera.

“Tunatekeleza fikra za Mwalimu Nyerere kwa kuanzia hasa  katika utekelezaji wa malengo yaliyoko katika Dira ya Maendeleo ya Taifa ya Miaka Mitano kwenye maeneo yetu” Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi, Bibi.Suzana Sabuni.
MWISHO
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka akifungua Mdahalo wa uongozi na maendeleo yenye tija kwa wote uliondaliwa na Taasisi hiyo kwa viongozi wa Mkoa wa Simiyu, ambao ulifanyika Machi 11, 2019 Mjini Bariadi.


Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere Joseph Butiku  (wa pili kushoto) akizungumza na viongozi wa Mkoa wa Simiyu, kabla ya kuanza Mdahalo wa uongozi na maendeleo yenye tija kwa wote uliondaliwa na Taasisi hiyo kwa viongozi wa Mkoa wa Simiyu, ambao ulifanyika Machi 11, 2019 Mjini Bariadi(kushoto) Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka.
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere, Joseph Butiku  akizungumza na baadhi ya viongozi wa Mkoa wa Simiyu, katika Mdahalo wa uongozi na maendeleo yenye tija kwa wote uliondaliwa na Taasisi hiyo kwa viongozi wa Mkoa wa Simiyu, ambao ulifanyika Machi 11, 2019 Mjini Bariadi.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka akiteta jambo na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere Joseph Butiku  katika Mdahalo wa uongozi na maendeleo yenye tija kwa wote uliondaliwa na Taasisi hiyo kwa viongozi wa Mkoa wa Simiyu, ambao ulifanyika Machi 11, 2019 Mjini Bariadi.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka akifungua Mdahalo wa uongozi na maendeleo yenye tija kwa wote uliondaliwa na Taasisi hiyo kwa viongozi wa Mkoa wa Simiyu, ambao ulifanyika Machi 11, 2019 Mjini Bariadi.




Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga akichangia hoja katika mdahalo wa uongozi na maendeleo yenye tija kwa wote uliondaliwa na Taasisi ya Mwalimu Nyerere kwa viongozi wa Mkoa wa Simiyu, ambao ulifanyika Machi 11, 2019 Mjini Bariadi.
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Meatu, Mhe. Pius Machungwa akichangia hoja katika mdahalo wa uongozi na maendeleo yenye tija kwa wote uliondaliwa na Taasisi ya Mwalimu Nyerere  kwa viongozi wa Mkoa wa Simiyu, ambao ulifanyika Machi 11, 2019 Mjini Bariadi.

Mkuu wa Wilaya ya Busega, Mhe. Tano Mwera akichangia hoja katika mdahalo wa uongozi na maendeleo yenye tija kwa wote uliondaliwa na Taasisi ya mwalimu Nyerere  kwa viongozi wa Mkoa wa Simiyu, ambao ulifanyika Machi 11, 2019 Mjini Bariadi

Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere Joseph Butiku (wa pili kulia) akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi wa Mkoa wa Simiyu mara baada ya ufunguzi wa mdahalo uliondaliwa wa uongozi na maendeleo yenye tija kwa wote na Taasisi hiyo kwa viongozi wa Mkoa wa Simiyu, ambao ulifanyika Machi 11, 2019 Mjini Bariadi.




Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi, Bi. Suzana Sabuni akichangia hoja katika mdahalo wa uongozi na maendeleo yenye tija kwa wote uliondaliwa na Taasisi ya Mwalimu Nyerere  kwa viongozi wa Mkoa wa Simiyu, ambao ulifanyika Machi 11, 2019 Mjini Bariadi.
Katibu Tawala Msaidizi anayeshughulikia Uchumi na Uzalishaji katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Dkt. Gamitwe Mahaza akichangia hoja katika mdahalo wa uongozi na maendeleo yenye tija kwa wote uliondaliwa na Taasisi hiyo kwa viongozi wa Mkoa wa Simiyu, ambao ulifanyika Machi 11, 2019 Mjini Bariadi.
Mkuu wa Kitengo cha Sheria katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Bibi. Mwanahamisi Kawega, akichangia hoja katika mdahalo wa uongozi na maendeleo yenye tija kwa wote uliondaliwa na Taasisi ya Mwalimu Nyerere kwa viongozi wa Mkoa wa Simiyu, ambao ulifanyika Machi 11, 2019 Mjini Bariadi.
Baadhi ya viongozi wa mkoa wa Simiyu wakiwa katika mdahalo wa uongozi na maendeleo yenye tija kwa wote maalum ulioandaliwa na Taasisi ya Mwalimu Nyerere ambao ulifanyika Machi 11, 2019 Mjini Bariadi.
Mkuu wa Wilaya ya Meatu, Dkt. Joseph Chilongani akichangia hoja katika mdahalo wa uongozi na maendeleo yenye tija kwa wote uliondaliwa na Taasisi ya Mwalimu Nyerere  kwa viongozi wa Mkoa wa Simiyu, ambao ulifanyika Machi 11, 2019 Mjini Bariadi.
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere Joseph Butiku (wa pili kulia) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya waandishi wa habari wa  Mkoa wa Simiyu mara baada ya ufunguzi wa mdahalo wa uongozi na maendeleo yenye tija kwa wote uliondaliwa na Taasisi hiyo kwa viongozi wa Mkoa wa Simiyu, ambao ulifanyika Machi 11, 2019 Mjini Bariadi.
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere Joseph Butiku (wa pili kulia) akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi wa Mkoa wa Simiyu mara baada ya ufunguzi wa mdahalo uliondaliwa na Taasisi hiyo kwa viongozi wa Mkoa wa Simiyu, ambao ulifanyika Machi 11, 2019 Mjini Bariadi.
Kutoka kushoto (mbele)Mkuu wa Wilaya ya Meatu, Mhe. Dkt. Joseph Chilongani, :- Mkuu wa Wilaya ya Busega, Mhe. Tano Mwera,Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga wakifuailia mdahalo uliondaliwa na Taasisi ya Mwalimu Nyerere  kwa viongozi wa Mkoa wa Simiyu, ambao ulifanyika Machi 11, 2019 Mjini Bariadi.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka akimweleza jambo Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere Joseph Butiku (kulia) ofisini kwake , mara baada ya kiongozi huyo kuwasili Mjini Bariadi, kwa ajili ya mdahalo uliondaliwa na Taasisi ya Mwalimu Nyerere  kwa viongozi wa Mkoa wa Simiyu, ambao ulifanyika Machi 11, 2019 Mjini Bariadi.
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere Joseph Butiku (kulia) akimweleza jambo Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka mara baada ya kiongozi huyo kuwasili Mjini Bariadi, kwa ajili ya mdahalo uliondaliwa na Taasisi ya Mwalimu Nyerere  kwa viongozi wa Mkoa wa Simiyu, ambao ulifanyika Machi 11, 2019 Mjini Bariadi.

Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere Joseph Butiku  (wa pili kushoto) akizungumza na viongozi wa Mkoa wa Simiyu, kabla ya kuanza Mdahalo uliondaliwa na Taasisi hiyo kwa viongozi wa Mkoa wa Simiyu, ambao ulifanyika Machi 11, 2019 Mjini Bariadi(kushoto) Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka.
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere Joseph Butiku  (wa nne kushoto) akizungumza na viongozi wa Mkoa wa Simiyu, kabla ya kuanza Mdahalo uliondaliwa na Taasisi hiyo kwa viongozi wa Mkoa wa Simiyu, ambao ulifanyika Machi 11, 2019 Mjini Bariadi.
 Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere Joseph Butiku  (wa nne kushoto) akizungumza na viongozi wa Mkoa wa Simiyu, kabla ya kuanza Mdahalo uliondaliwa na Taasisi hiyo kwa viongozi wa Mkoa wa Simiyu, ambao ulifanyika Machi 11, 2019 Mjini Bariadi.


Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka(kushoto) akizungumza na baadhi ya viongozi wa mkoa huo na baadhi ya Viongozi wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere ofisini kwake kabla ya kuanza Mdahalo uliondaliwa na Taasisi hiyo kwa viongozi wa Mkoa wa Simiyu, ambao ulifanyika Machi 11, 2019 Mjini Bariadi.

0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!