Tuesday, May 10, 2016

WAKAZI WA ITILIMA WAISHUKURU LIFE MINISTRY KUWACHIMBIA KISIMA



Wakazi wa kijiji cha Ikindilo wilayani Itilima wamelishukuru Shirika la dini la Life Minisry kwa kuwatoa katika adha ya maji iliyokuwa ikiwakabili kwa kuwachimbia kisima kirefu chenye thamani ya shilingi milioni 50.

Akizungumza mara baada ya uzinduzi wa kisima hicho uliofanywa na Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony . J. Mtaka , mkazi wa kijiji cha Ikindilo bibi . Monica Malugu alisema kisima hicho kimewasadia kuondokana na ashida ya kufuata maji kwa mwendo mrefu.

“Nawashukuru sana wafadhili kwa kutukumbuka wana Ikindilo kwa kutuchimbia kisima hiki, tulikuwa tunafuata mbali yaani tulikuwa tunatembea zaidi ya masaa matatu. Tulikuwa tunaamka usiku kwenda kufuata maji  na wakati mwingine tukichelewa kurudi tunapigwa na waume zetu” alisema Bibi Monica.

Akitoa shukrani kwa niaba ya Serikali, Mkuu wa mkoa wa Simiyu amesema Serikali inatambua na kuthamini mchango wa mashirika ya dini katika maendeleo ya nchi ya Tanzania na watu wake na akaahidi kuulinda mradi huo na miradi mingine ya Life Ministry inayotekelezwa katika mkoa wa Simiyu.

Aidha, Mtaka alisema wafadhili kama hao wamekuwa wadau wakubwa wa maendeleo tangu uhuru hivyo  aliwahakikishia kuwa watapata ushirikiano wa kotosha kutoka kwa Viongozi wa Serikali ngazi ya kijiji hadi Mkoa pale watakapohitaji  kutekeleza miradi mingine ya maendeleo.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Life Ministry Tanzania Bw.Dismas Shekalaghe aliwataka wakazi wa Ikindilo kukilinda na kukitunza kisima hicho na miundombinu yake ili kiwanufaishe kwa kuwapa huduma  ya maji safi iliyo endelevu, ambapo walaihidi kukifanyia ukarabati kila baada ya mwaka mmoja.
Shirika la Life Ministry linafanya kazi katika nchi zaidi ya 198 duniani, Pamoja na kuchimba visima vitatu katika mkoa wa Simiyu wanatarajia  kuwasaidia wananchi  katika maeneo mengine,  hususani kilimo cha mboga mboga ili kuwakwamua katika umasikini.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka  (katikati) akikata utepe wakati wa uzinduzi wa kisima kilichochimbwa na shirika la dini la Life Ministry kwa ajili ya wakazi wa Ikindilo wilayani Itilima, kushoto kwake ni Mkurugenzi wa Shirika la Life Ministry Bw. Dismas Shekalaghe na kulia kwake ni Diwani wa kata ya Ikindilo, Mhe.Joseph Kulwa. Picha na Stella Kalinga


 Mkurugenzi wa Shirika la Life Ministry Bw. Dismas Shekalaghe (kulia) akizungumza na wananchi wa Ikindilo (hawapo pichani) kabla ya uzinduzi wa kisima cha maji, wa pili kulia Mkuu wa mkoa wa Simiyu akifatiwa na Mkuu waWilaya ya Itilima Mhe. Georgiina Bundala.



0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!