Sunday, October 22, 2017

MABARAZA YA MADIWANI SIMIYU YARIDHIA HALMASHAURI ZIKOPE BILIONI 17.1 KUTEKELEZA MIRADI YA MAENDELEO

Mabaraza ya Madiwani katika Halmashauri ya Wilaya ya Busega na Meatu Mkoani Simiyu yameridhia Halmashauri hizo kukopa shilingi bilioni 17.1 kutoka Benki ya Maendeleo ya Kilimo (TADB), kwa ajili ya kutekeleza Miradi mikubwa miwili  ya Maendeleo.

Maridhiano hayo yamefikiwa katika Vikao vya dharura vya mabaraza ya madiwani vilivyofanyika kwa nyakati tofauti, ambapo Halmashauri ya Wilaya ya Busega imepanga kukopa shilingi bilioni 10.7 kwa ajili ya utekelezaji wa mradi wa Kilimo cha Umwagiliaji katika Bonde la Mwamanyili (eneo la ekari 2050)  na Meatu shilingi bilioni 6.4 kwa ajili ya upanuzi wa kiwanda cha maziwa(MEATU MILK).

 Akiwasilisha taarifa ya Maendeleo ya Mpango wa Kilimo cha Umwagiliaji Wilayani Busega, Afisa Mipango wa Wilaya hiyo Josephat Joseph, amesema hadi sasa kazi za upimaji wa mashamba na njia ya kupita bomba la maji, kupima udongo, kusanifu mfereji mkuu kwenye chanzo, sehemu ya kuchukulia maji, nyumba za pampu, mifereji ya kuingiza na kutolea maji,kuandaa michoro na gharama za mradi zimeshakamilika.

Aidha, amesema katika utekelezaji wa mradi huu Halmashauri ndiyo msimamizi mkuu wa mradi na itajenga miundombinu yote ya umwagiliaji, hivyo itaingia makubaliano na wakulima wa Mwamanyili kupitia umoja wao watakaounda katika kutekeleza shughuli za mradi.

Nao wakulima wa Bonde la Mwamanyili wamesema wameupokea mradi huo kwa mikono miwili na kwa sasa wamesitisha shughuli zote za Kilimo katika bonde hilo, ili kupisha shughuli nyingine za maandalizi ya ujenzi wa miundombinu ya mradi huo.

“ Tunawashukuru viongozi wetu kwa kutusaidia kupata mkopo wa kutekeleza mradi huu naupokea kwa mikono miwili tena natamani uanze haraka, sasa hivi hatutalima maeneo yetu tunapisha wataalam waendelee na shughuli za maandalizi ya mradi ili wakikamilisha tu tuanze ” alisema Joseph Mayala.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka amesema kutekelezwa kwa mradi huo, kutaiandikia historia wilaya ya BUSEGA  kwa kuwainua wananchi kiuchumi na kuondokana na aibu ya kuomba chakula cha msaada Serikalini, ambapo amesisitiza kuwa utakuwa mradi wa pekee ambao mnyororo wake wa thamani utaonekana kupitia mazao yatakayolimwa hususani mpunga.

Kwa upande wa Mradi wa Upanuzi wa Kiwanda cha Maziwa Meatu, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Meatu, Fabian Manoza amesema kuelekea upanuzi wa kiwanda hicho, Halmashauri imekusudia kuongeza idadi ya wafugaji wanaopeleka maziwa kiwandani kutoka 45 wa sasa na kufikia wafugaji 400 wakubwa ambao wanafuga ng’ombe wa kisasa.

Mikakati mingine ni kununua mtambo mpya wa kuchakata maziwa wenye uwezo wa kuchakata lita elfu 15,000 kwa siku, kununua Mitamba 1000 na kuandaa shamba la malisho lenye miundombinu muhimu pamoja na kuongeza soko la MEATU MILK kwa kuingia mikataba na mawakala na kuweka maduka katika baadhi ya miji mikubwa.

Wafugaji wa Wilaya ya Meatu wamesema wameupokea mradi wa upanuzi wa kiwanda cha maziwa wilayani humo kwa furaha, kwani utawasaidia kuongeza upatikanaji wa soko la uhakika la maziwa.
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Meatu, Mhe.Pius Machungwa ametoa wito kwa wafugaji kukubali kubadilika na kuanza kufuga kisasa kulingana na jinsi wanavyoshauriwa na wataalam ili kuongeza tija.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka amesema Serikali mkoani humo imejipanga kutafuta  majawabu ya changamoto za wafugaji kwa kuwasaidia kufuga kisasa, ikiwa ni pamoja na kuwashauri kupima maeneo yao na kuyawekea miundombinu muhimu kama mabwawa, visima, majosho na mashamba ya malisho.

 “Kiwanda mnachokihitaji hapa kitatumia lita 15,000 kwa siku, mnapaswa kuweka mikakati mizuri ya ng’ombe wenu ili muwe na uhakika wa maziwa, nayazungumza haya ili kila mmoja aone umuhimu wa kiwanda; tuwasaidie wafugaji wafuge kisasa na kwa tija” alisema Mtaka.

Halmashauri ya Wilaya ya Busega na Meatu zinatarajia kupata Mkopo kutoka Benki ya Maendeleo ya Kilimo ambayo imekubali kutoa mikopo hiyo ili kuunga mkono juhudi za Viongozi na wananchi wa mkoa wa Simiyu katika kuleta maendeleo. 
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka (katikati) akizungumza na Madiwani na baadhi ya wafugaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Meatu(hawapo pichani)   katika kikao cha dharura cha Baraza la Madiwani, kilichofanyika Mjini Mwanhuzi kwa lengo la kujadili maombi ya mkopo kwa ajili upanuzi wa kiwanda cha maziwa wilayani humo.
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Meatu, Mhe.Pius Machungwa akifungua kikao dharura cha Baraza la Madiwani kilichofanyika Mjini Mwanhuzi kwa lengo la kujadili maombi ya mkopo kwa ajili upanuzi wa kiwanda cha maziwa wilayani humo.
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Busega, Mhe.Vumi Magoti(wa pili kulia)akizungumza na Madiwani na baadhi ya wakulima wa Busega(hawapo pichani) katika kikao cha dharura cha Baraza la Madiwani kilichofanyika Nyashimo kwa lengo la kujadili maombi ya mkopo kwa ajili kutekeleza Mradi wa Kilimo cha Umwagiliaji katika Bonde la Mwamanyili Wilayani humo
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Meatu, Ndg.Fabian Manoza akizungumza na Madiwani na baadhi ya wafugaji wa Halmashauri hiyo (hawapo pichani)  katika kikao cha dharura cha Baraza la Madiwani, kilichofanyika Mjini Mwanhuzi kwa lengo la kujadili maombi ya mkopo kwa ajili upanuzi wa kiwanda cha maziwa wilayani humo.
Mkuu wa Wilaya ya Meatu, Mhe.Dkt.Joseph Chilongani akizungumza na Madiwani na baadhi ya wafugaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Meatu (hawapo pichani)  katika kikao cha dharura cha Baraza la Madiwani, kilichofanyika Mjini Mwanhuzi kwa lengo la kujadili suala la maombi ya mkopo kwa ajili upanuzi wa kiwanda cha maziwa wilayani humo.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka (katikati) akizungumza na Madiwani na baadhi ya wakulima Bonde la Mwamanyili wa Halmashauri ya Wilaya ya Busega (hawapo pichani) katika kikao cha dharura cha Baraza la Madiwani, kilichofanyika Nyashimo kwa lengo la kujadili suala la maombi ya mkopo kwa ajili kutekeleza Mradi wa Kilimo cha Umwagiliaji katika Bonde la Mwamanyili Wilayani humo.
Afisa Mipango kutoa Halmashauri ya Wilaya ya Busega, Ndg.Josephat Joseph akiwasilisha taarifa ya Maendeleo ya Mpango wa Kilimo cha Umwagiliaji katika Bonde la Mwamanyili kwa viongozi, madiwani na baadhi ya wakulima (hawapo pichani) katika kikao cha dharura cha baraza la madiwani kilichofanyika kwa lengo la kujadili maombi ya mkopo kwa ajili ya kutekeleza mradi huo wilayani Busega.
Madiwani  na baadhi ya Wafugaji  wa Halmashauri ya Wilaya ya Meatu wakifuatilia mjadala kuhusu suala la maombi ya Mkopo kwa ajili ya Upanuzi wa Kiwanda cha Maziwa Wilayani Meatu katika kikao cha dharura cha Baraza kilichofanyika Mjini Mwanhuzi.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka akizungumza na Viongozi wa Wilaya ya Meatu (baadhi hawapo pichani) alipotembelea eneo lililoandaliwa kwa ajili ya kuanzisha shamba la malisho ya mifugo wanaotarajiwa kununuliwa na Halmashauri hiyo kwa ajili ya kuwezesha  upatikanaji wa maziwa katika kiwanda cha maziwa wilayani humo.
Diwani wa Kata ya Mwamishali katika Halmashauri ya Wilaya ya Meatu Mhe.Christopher Ndamo akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kumalizika kwa kikao cha dharura cha Baraza la Madiwani, kilichofanyika kwa lengo la kujadili suala la maombi ya mkopo kwa ajili upanuzi wa kiwanda cha maziwa wilayani humo.
Diwani wa Kata ya Mwamanyili, Mhe.Charles Luyenze akichangia hoja katika kikao cha cha dharura cha Baraza la Madiwani kilichofanyika kwa lengo la kujadili suala la maombi ya mkopo kwa ajili ya kutekeleza Mradi wa Kilimo cha Umwagiliaji katika Bonde la Mwamanyili wilayani Busega.
Mmoja wa Wafugaji kutoka Wilaya ya Meatu, akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kumalizika kwa kikao cha dharura cha Baraza la Madiwani, kilichofanyika kwa lengo la kujadili suala la maombi ya mkopo kwa ajili upanuzi wa kiwanda cha maziwa wilayani humo.
Baadhi ya Watendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Busega wakifuatilia mjadala kuhusu suala la maombi ya Mkopo kwa ajili ya Utekelezaji wa Mradi wa Kilimo cha Umwagiliaji katika Bonde la Mwamanyili wilayani humo, katika cha dharura cha Baraza la Madiwani kilichofanyika hivi karibuni katika makao makuu ya wilaya hiyo Nyashimo.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka(katikati) akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa Wilaya ya Busega  (meza kuu)  na watendaji mbalimbali wa Wilaya hiyo baada ya kikao cha dharura cha Baraza la Madiwani kilichofanyika kwa lengo la kujadili suala la maombi ya mkopo kwa ajili ya kutekeleza Mradi wa Kilimo cha Umwagiliaji katika Bonde la Mwamanyili wilayani humo.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka(katikati) akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa Wilaya ya Busega  (meza kuu)  na madiwani wa Halmashauri hiyo baada ya kikao cha dharura cha Baraza la Madiwani kilichofanyika kwa lengo la kujadili suala la maombi ya mkopo kwa ajili ya kutekeleza Mradi wa Kilimo cha Umwagiliaji katika Bonde la Mwamanyili wilayani humo.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka(katikati) akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa Wilaya ya Busega  (meza kuu)  na baadhi ya wakulima baada ya kikao cha dharura cha Baraza la Madiwani kilichofanyika kwa lengo la kujadili suala la maombi ya mkopo kwa ajili ya kutekeleza Mradi wa Kilimo cha Umwagiliaji katika Bonde la Mwamanyili wilayani humo.

0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!