Wednesday, October 4, 2017

WAFUGAJI NYUKI WATAKIWA KUANZISHA VIWANDA VIDOGO KUONGEZA THAMANI YA MAZAO YA NYUKI

Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe.Eng. Ramo Makani  amesema Wafugaji Nyuki wanayo fursa kubwa ya kujikita katika uanzishwaji wa viwanda vidogo vidogo vya kuchakata, kufungasha na kuongeza thamani mazao ya nyuki na kutengeneza vipodozi kutokana na mazao ya nyuki.

Mhandisi Makani  ameyasema hayo jana wakati alipozungumza na wafugaji wa nyuki na wananchi katika Maadhimisho ya Siku ya kutundika Mizinga ya Nyuki Kitaifa yaliyofanyika katika Kijiji cha Isengwa Wilaya ya Itilima Mkoani Simiyu, chini ya Kauli Mbiu “UFUGAJI NYUKI KIBIASHARA UNACHANGIA KATIKA UKUAJI WA VIWANDA”

Amesema Mazao ya Nyuki ni malighafi ya Viwanda mbalimbali vikiwemo viwanda vya vyakula vinavyotumia asali, viwanda vya dawa na vipodozi na viwanda vya utengenezaji vinavyotumia nta katika kuzalisha maturubai, dawa za kung’arisha viatu na bidhaa nyingine, hivyo wafugaji  wanao wajibu wa kuongeza uzalishaji wa mazao ya nyuki na ujuzi wa kuyaweka katika ubora na kuyaongezea thamani.

Aidha, ametoa wito kwa wafugaji wa nyuki kuungana katika vikundi vyenye usajili ili waweze kuzalisha asali kwa wingi na yenye kufanana, kwa kuwa ikiwa watazalisha kila mmoja kwa utaratibu wake, asali hiyo haiwezi kuchanganywa na itakuwa na ubora na sifa tofauti, lakini ikiwa wataungana na kuzalisha asali nyingi kwa pamoja wakaipima kwa viwango vya ubora unaotakiwa wataweza kupata soko.

Sanjali na hilo amesema Serikali itahakikisha inawaunganisha wafugaji nyuki na walaji wa ndani na nje na akabainisha kuwa kwa miaka zaidi ya 11 imekuwa na ushirikiano na soko la Ulaya ambapo sampuli za asali kutoka maeneo mbalimbali zimepelekwa Ulaya na taarifa za maabara zinathibitisha kuwa asali ya Tanzania ni salama kwa afya ya mlaji.

Aidha, amesema katika kuongeza uzalishaji wa mazao ya nyuki Serikali pia inaendelea kutoa elimu kwa wafugaji wa nyuki  kuachana na matumizi ya mizinga ya asili ambayo ni duni na inachukua nafasi kubwa wakati uzalishaji wake ni mdogo na kuwahamasisha kuanza kutumia mizinga ya kisasa.

“ Nawaagiza Mkurugenzi wa Misitu na Nyuki nchini na Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania kupitia jukwaa hili, kwamba mbuni njia rafiki ya kuweka msisitizo katika utoaji wa elimu, uhamasishaji na kupima mafanikio kila mwaka; taarifa ya utekelezaji wa maagizo haya itolewe mara kwa mara, taarifa ya kwanza baada ya agizo hili itolewe katika siku ya maadhimisho kama haya mwaka kesho 2018” aliagiza Naibu Waziri.

Katika hatua nyingine Mhe. Makani amepongeza juhudi zinazofanywa na Mradi wa LVEMP II katika kuboresha mazingira na kubainisha kuwa pamoja na kuhifadhi rasilimali za asili za Bonde la Ziwa Victoria ambayo husaidia kutunza vyanzo vya maji  na mazingira hayo yanafanywa kuwa mazingira bora kwa ufugaji nyuki, ambapo katika wilaya ya Itilima kuna vikundi 22 vyenye mizinga 2080 ya nyuki vinavyofadhiliwa na LVEMP.

Akitoa salamu za Mkoa kwa niaba ya Katibu Tawala Mkoa wa Simiyu, Ndg.Chele Ndaki amesema idadi ya wafugaji na mizinga ya nyuki imekuwa ikiongezeka kila mwaka ambapo kwa sasa kuna jumla ya vikundi 91 vyenye jumla ya mizinga 5824 na akaahidi kuwa mkoa utaendelea kusimamia uboreshaji wa mazingira ya ufugaji nyuki na kusimamia vikundi vinavyoanzishwa katika Halmashauri., ili wafugaji wanufaike na kujiimarisha kiuchumi.

Kwa upande wake Mwakilishi wa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania(TFS) Ndg.Herberth Haule amesema shughuli ya ufugaji wa nyuki  inasaidia katika uhifadhi wa mazingira na  kujenga uchumi kwa wananchi hususani vikundi vinavyojishughulisha na kazi hiyo.

Naye Mkurugenzi wa Misitu na Nyuki kutoka Wizara ya Maliasili na Utalii, Dkt.Ezekiel Mwakalukwa amesema Tanzania ni miongoni mwa nchi Tano za Afrika zinazoruhusiwa kuuza asali yake katika soko la Ulaya na nchi ya China.

Nao wafugaji wa nyuki na wajasiriamali wa mazao ya nyuki wameiomba Serikali pamoja na wadau wengine kuwekeza katika viwanda vya kutengeneza vifungashio kwa kuwa suala hilo ni changamoto kwao ambayo  inawalazimu kuagiza vifungashio nje ya nchi kwa kutumia gharama kubwa.


Maadhimisho ya Siku ya Kutundika Mizinga ya Nyuki Kitaifa kwa mwaka 2017 yameadhimishwa kwa mara kwanza Mkoani Simiyu yakiwa ni maadhimisho ya tano kufanyika hapa nchini, ambapo kwa mara ya kwanza  yalifanyika mwaka 2013 Mkoani Singida.


Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe.Eng. Ramo Makani (Mb)(kulia)akitundika Mzinga katika Banda la Nyuki la Kikundi cha Wafugaji Nyuki cha Malela wakati wa Maadhimisho ya siku ya kutundika Mizinga ya Nyuki Kitaifa yaliyofanyika jana katika Kijiji cha Isengwa Wilaya ya Itilima Mkoani Simiyu.
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe.Eng. Ramo Makani (Mb)(kulia)akitundika Mzinga katika Banda la Nyuki la Kikundi cha Wafugaji Nyuki cha Malela wakati wa Maadhimisho ya siku ya kutundika Mizinga ya Nyuki Kitaifa yaliyofanyika jana katika Kijiji cha Isengwa Wilaya ya Itilima Mkoani Simiyu.
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe.Eng. Ramo Makani (Mb)akizungumza na wananchi wa Wilaya ya Itilima(hawapo pichani ) wakati wa Maadhimisho ya siku ya kutundika Mizinga ya Nyuki Kitaifa yaliyofanyika jana katika Kijiji cha Isengwa Wilayani humo katika  Mkoa Simiyu.
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe.Eng. Ramo Makani(Mb)(kulia) akizungumza na Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka ofisini kwake kabla ya kuhitimisha maadhimisho ya Siku ya kutundika Mizinga ya Nyuki yaliyofanyika Mkoani humo katika kijiji cha Isengwa Wilayani Itilima
Mkuu wa Wilaya ya Itilima, Mhe.Benson Kilangi akizungumza na wananchi wa wilayani hiyo (hawapo pichani ) wakati wa Maadhimisho ya siku ya kutundika Mizinga ya Nyuki Kitaifa yaliyofanyika jana katika Kijiji cha Isengwa Wilayani humo katika  Mkoa Simiyu.
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe.Eng. Ramo Makani(Mb) akizindua Manzuki (Shamba la Miti lenye Mizinga ya Nyuki) ya Kikundi cha Wafugaji nyuki cha Malela Wilayani Itilima wakati wa Maadhimisho ya siku ya kutundika Mizinga ya Nyuki Kitaifa yaliyofanyika jana katika Kijiji cha Isengwa Wilayani humo katika  Mkoa Simiyu.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka(kushoto) akimsikiliza Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe.Eng.Ramo Makani(Mb) (kulia) kabla ya kuanza safari kuelekea kwenye Maadhimisho ya Siku ya Kutundika Mizinga ya Nyuki Kitaifa yaliyofanyika katika Kijiji cha Isengwa Wilaya ya Itilima Mkoani humo.
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe.Eng. Ramo Makani (Mb)(wa pili kulia) akiwa na baadhi ya viongozi wa Wilaya ya Itilima na Mkoa wa Simiyu wakielekea eneo la ktundika Mizinga wakati wa Maadhimisho ya siku ya kutundika Mizingaya Nyuki  Kitaifa yaliyofanyika jana katika Kijiji cha Isengwa Wilayani Itilima katika  Mkoa Simiyu.
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe.Eng.Ramo Makani(Mb) akivishwa skafu na Vijana wa Skauti ya Wilaya ya Itilima ikiwa ni ishara ya kumkaribisha katika wa Maadhimisho ya siku ya kutundika Mizinga ya Nyuki Kitaifa yaliyofanyika jana katika Kijiji cha Isengwa Wilayani Itilima katika  Mkoa Simiyu
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe.Eng.Ramo Makani(Mb) (mwenye skafu) akiangalia mazao ya Nyuki alipotembelea Banda la maonesho la Kikundi cha Wafugaji Nyuki cha Malela wilayani Itilima, wakati wa Maadhimisho ya siku ya kutundika Mizinga ya Nyuki Kitaifa yaliyofanyika jana katika Kijiji cha Isengwa Wilayani humo katika  Mkoa Simiyu.
Baadhi ya wanachama wa Kikundi cha Wafugaji Nyuki cha Malela wakimuonesha Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe.Eng.Ramo Makani(Mb) moja ya tuzo waliyopata kutokana na uzalishaji wa asali bora, wakati wa Maadhimisho ya siku ya kutundika Mizinga ya Nyuki Kitaifa yaliyofanyika jana katika Kijiji cha Isengwa Wilayani Itilima katika  Mkoa Simiyu.
Kutoka kulia Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Simiyu, Mhe.Dkt. Titus Kamani, Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe.Eng.Ramo Makani(Mb) na Mkuu wa Wilaya ya Itilima, Mhe.Benson Kilangi wakizungumza jambo,   wakati wa Maadhimisho ya siku ya kutundika Mizinga ya Nyuki Kitaifa yaliyofanyika jana katika Kijiji cha Isengwa Wilayani Itilima katika  Mkoa Simiyu.
Mbunge wa Jimbo la Itilima Mhe.Njalu Silanga akizungumza wakati wa Maadhimisho ya siku ya kutundika Mizinga ya Nyuki Kitaifa yaliyofanyika jana katika Kijiji cha Isengwa Wilayani Itilima katika  Mkoa Simiyu.
Mwakilishi wa Katibu Tawala Mkoa wa Simiyu, Ndg.Chele Ndaki(kushoto) akiwasilisha taarifa ya Mkoa ya ufugaji Nyuki wakati wa Maadhimisho ya siku ya kutundika Mizinga ya Nyuki Kitaifa yaliyofanyika jana katika Kijiji cha Isengwa Wilayani Itilima katika  Mkoa Simiyu.
Mkurugenzi wa Misitu na Nyuki kutoka Wizara ya Maliasili na Utalii, Dkt. Ezekiel Mwakalukwa akitoa taarifa ya ufugaji nyuki, wakati wa Maadhimisho ya siku ya kutundika Mizinga ya Nyuki Kitaifa yaliyofanyika jana katika Kijiji cha Isengwa Wilayani Itilima katika  Mkoa Simiyu.
Baadhi ya Viongozi wa Mkoa wa Simiyu wakimsikiliza Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe.Eng. Ramo Makani(Mb) (hayupo pichani) alipokuwa akizungumza nao kabla ya kuanza safari ya kuelekea kwenye Maadhimisho ya Siku ya Kutundika Mizinga ya Nyuki Kitaifa yaliyofanyika katika Kijiji cha Isengwa Wilaya ya Itilima Mkoani humo.
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe.Eng. Ramo Makani(Mb) (mwenye skafu) akizungumza na wajasiriamali wa mazao ya nyuki kutoka Wilaya ya Bukombe Mkoani Geita, alipotembelea banda lao wakati wa Maadhimisho ya siku ya kutundika Mizinga ya Nyuki Kitaifa yaliyofanyika jana,  katika Kijiji cha Isengwa Wilayani Itilima katika  Mkoa Simiyu.
Baadhi ya Viongozi wa Mkoa wa Simiyu wakimsikiliza Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe.Eng. Ramo Makani(Mb) (hayupo pichani) wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Kutundika Mizinga ya Nyuki Kitaifa yaliyofanyika katika Kijiji cha Isengwa Wilaya ya Itilima Mkoani humo.
Baadhi ya wananchi wa Wilaya ya Itilima wakimsikiliza Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe.Eng. Ramo Makani(Mb) (hayupo pichani) wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Kutundika Mizinga ya Nyuki Kitaifa yaliyofanyika katika Kijiji cha Isengwa Wilayani humo  Mkoani Simiyu.
Baadhi ya wananchi wa Wilaya ya Itilima wakimsikiliza Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe.Eng. Ramo Makani(Mb) (hayupo pichani) wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Kutundika Mizinga ya Nyuki Kitaifa yaliyofanyika katika Kijiji cha Isengwa Wilayani humo  Mkoani Simiyu.
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe.Eng. Ramo Makani(wa nne kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya viongozi wa Mkoa wa Simiyu na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Itilima, wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Kutundika Mizinga ya Nyuki Kitaifa yaliyofanyika katika Kijiji cha Isengwa Wilaya ya Itilima Mkoani Simiyu.
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe.Eng. Ramo Makani(wa nne kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya viongozi wa Mkoa wa Simiyu na watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Itilima na Halmashauri jirani, wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Kutundika Mizinga ya Nyuki Kitaifa yaliyofanyika katika Kijiji cha Isengwa Wilaya ya Itilima Mkoani Simiyu.
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe.Eng. Ramo Makani(wa nne kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya viongozi wa Mkoa wa Simiyu na Wanachama wa Kikundi cha Wafugaji Nyuki cha Malela Wilaya ya Itilima, wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Kutundika Mizinga ya Nyuki Kitaifa yaliyofanyika katika Kijiji cha Isengwa Wilayani humo Mkoani Simiyu.
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe.Eng. Ramo Makani(wa nne kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya viongozi wa Mkoa wa Simiyu na baadhi ya wajasiriamali walioleta bidhaa zao za mazao ya nyuki, wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Kutundika Mizinga ya Nyuki Kitaifa yaliyofanyika katika Kijiji cha Isengwa Wilaya ya Itilima Mkoani Simiyu.

0 comments:

Post a Comment

Kumbukumbu za Blogu

Powered by Blogger.
Subscribe Via Email

Subscribe to our newsletter to get the latest updates to your inbox. ;-)

Your email address is safe with us!